< 2 Wafalme 19 >

1 Mfalme Hezekia aliposikia haya, akararua nguo zake na kuvaa nguo ya gunia, naye akaenda katika Hekalu la Bwana.
And whanne kyng Ezechie hadde herd these thingis, he to-rente his clothis, and was hilid with a sak; and he entride in to the hous of the Lord.
2 Akawatuma Eliakimu msimamizi wa nyumba ya mfalme, Shebna mwandishi, na viongozi wa makuhani, wote wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa nabii Isaya mwana wa Amozi.
And he sente Eliachym, souereyn of the hous, and Sobna, scryueyn, and elde men of the preestis, hilid with sackis, to Ysaie, the prophete, sone of Amos.
3 Wakamwambia, “Hili ndilo asemalo Hezekia: Siku hii ni siku ya dhiki, ya kukaripiwa na ya aibu, kama wakati watoto wanapofikia karibu kuzaliwa na kumbe hakuna nguvu ya kuwazaa.
Whiche seiden, Ezechie seith these thingis, This dai is a dai of tribulacioun, and of blamyng, and of blasfemye; sones camen `til to the childberyng, and the `traueler of childe hath not strengthis.
4 Yamkini Bwana, Mungu wako atayasikia maneno ya jemadari wa jeshi, ambaye bwana wake, mfalme wa Ashuru, amemtuma kumdhihaki Mungu aliye hai, tena kwamba atamkemea kwa maneno ambayo Bwana, Mungu wako ameyasikia. Kwa hiyo omba kwa ajili ya mabaki ambao bado wako.”
If perauenture thi Lord God here alle the wordis of Rabsaces, whom the kyng of Assiryens, his lord sente, that he schulde dispise the Lord lyuynge, and repreue bi wordis, whiche thi Lord God herde; and make thou preier for these relikis, that ben foundun.
5 Maafisa wa Mfalme Hezekia walipofika kwa Isaya,
Therfor the seruauntis of kyng Ezechie camen to Isaie;
6 Isaya akawaambia, “Mwambieni bwana wenu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Usiogope kwa hayo uliyoyasikia, yale maneno ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru wamenitukana nayo.
and Isaie seide to hem, Seie ye these thingis to youre lord, The Lord seith these thingis, Nyle thou drede of the face of wordis whiche thou herdist, bi whiche the children of the kyng of Assiriens blasfemeden me.
7 Sikiliza! Nitatia roho fulani ndani yake ili atakaposikia taarifa fulani, atarudi nchi yake mwenyewe, nami huko nitafanya auawe kwa upanga.’”
Lo! Y schal sende to hym a spirit, and he schal here a messanger, and he schal turne ayen in to his lond; and Y schal caste hym doun bi swerd in his owne lond.
8 Jemadari wa jeshi aliposikia kwamba mfalme wa Ashuru ameondoka Lakishi, alirudi, akamkuta mfalme akipigana na Libna.
Therfor Rabsaces turnede ayen, and foond the kyng of Assiriens fiytynge ayens Lobna; for he hadde herd, that the kyng hadde go awei fro Lachis.
9 Basi Senakeribu akapata taarifa kwamba Tirhaka, Mkushi mfalme wa Misri, alikuwa anaenda kupigana naye. Basi akatuma tena wajumbe kwa Hezekia na neno hili:
And whanne he hadde herd of Theracha, kyng of Ethiope, `men seyynge, Lo! he yede out, that he fiyte ayens thee; that he schulde go ayens `that kyng, he sente messangeris to Ezechie,
10 “Mwambieni Hezekia mfalme wa Yuda: Usikubali huyo Mungu unayemtumainia akudanganye wakati anaposema, ‘Yerusalemu haitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.’
and seide, Seie ye these thingis to Ezechie, kyng of Juda, Thi Lord God, in whom thou hast trist, disseyue not thee, nether seie thou, Jerusalem schal not be `bitakun in to the hondis of the kyng of Assiriens;
11 Hakika umesikia yale ambayo wafalme wa Ashuru wametenda kwa nchi zote, wakiwaangamiza kabisa. Je, wewe utaokolewa?
for thou thi silf herdist what thingis the kyngis of Assiriens diden in alle londis, hou thei wastiden tho; whether therfor thou aloone maist be delyuered?
12 Je, miungu ya mataifa ambayo yaliangamizwa na baba zangu iliweza kuwaokoa, hiyo miungu ya Gozani, Harani, Resefu, na ya watu wa Edeni waliokuwa Telasari?
Whether the goddis of hethene men delyueriden alle men whiche my fadris distrieden, that is, Gozam, and Aran, and Reseph, and the sones of Eden, that weren in Thelassar?
13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, mfalme wa mji wa Sefarvaimu, au wa Hena au wa Iva?”
Where is the kyng of Emath, and the kyng of Arphat? and the kyng of the cytee of Sepharuaym, of Ana, and of Aua?
14 Hezekia akapokea barua kutoka kwa wale wajumbe, naye akaisoma. Kisha akapanda katika Hekalu la Bwana, akaikunjua mbele za Bwana.
Therfor whanne Ezechie hadde take the lettris fro the hond of messangeris, and hadde red tho, he stiede in to the hows of the Lord, and spredde abrood tho bifor the Lord;
15 Naye Hezekia akamwomba Bwana akisema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, uketiye juu ya kiti cha enzi kati ya makerubi, wewe peke yako ndiwe Mungu juu ya falme zote za dunia. Wewe umeumba mbingu na nchi.
and preiede in his siyt, and seide, Lord God of Israel, that sittist on cherubym, thou art God aloone of alle kyngis of erthe; thou madist heuene and erthe.
16 Tega sikio, Ee Bwana, usikie; fungua macho yako, Ee Bwana, uone; sikiliza maneno ambayo Senakeribu ametuma kumtukana Mungu aliye hai.
Bowe thin eere, and here; opyn thin iyen, Lord, and se; and here alle the wordis of Senacherib, which sente, that he schulde dispise `to vs `God lyuynge.
17 “Ni kweli, Ee Bwana, kwamba wafalme wa Ashuru wameyaangamiza mataifa haya na nchi zao.
Verili, Lord, the kynges of Assiriens distrieden hethene men, and the londis of alle men,
18 Wameitupa miungu yao kwenye moto na kuiangamiza, kwa kuwa haikuwa miungu, bali miti na mawe tu iliyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
and senten the goddis of hem in to fier; for thei weren not goddis, but werkis of `hondis of men, of tre and stoon; and thei losten `tho goddis.
19 Sasa basi, Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe kutoka mkononi mwake, ili falme zote duniani zipate kujua kwamba wewe peke yako, Ee Bwana, ndiwe Mungu.”
Now therfor, oure Lord God, make vs saaf fro the hond of hem, that alle rewmes of erthe wite that thou art the Lord God aloone.
20 Kisha Isaya mwana wa Amozi akapeleka ujumbe kwa Hezekia, akasema: “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nimesikia maombi yako kuhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru.
Forsothe Isaie, sone of Amos, sente to Ezechie, and seide, The Lord God of Israel seith these thingis, Y haue herd tho thingis, whiche thou preidist me on Sennacherib, king of Assiriens.
21 Hili ndilo neno ambalo Bwana amelisema dhidi yake: “‘Bikira Binti Sayuni anakudharau na kukudhihaki. Binti Yerusalemu anatikisa kichwa chake unapokimbia.
This is the word, which the Lord spak of hym, Thou virgyn douytir of Syon, he dispiside thee, and scornyde thee; thou douyter of Jerusalem, he mouyde his heed aftir thi bak.
22 Ni nani uliyemtukana na kumkufuru? Ni nani uliyeinua sauti yako dhidi yake, na kumwinulia macho yako kwa kiburi? Ni dhidi ya yule Aliye Mtakatifu wa Israeli!
Sennacherib, whom `dispisidist thou, and whom `blasfemedist thou? Ayens whom hast thou reisid thi vois, and hast reisid thin iyen an hiye? Ayens the hooli of Israel.
23 Kupitia kwa wajumbe wako umelundika matukano juu ya Bwana. Nawe umesema, “Kwa magari yangu mengi ya vita, nimepanda juu ya vilele vya milima, vilele vya juu sana katika Lebanoni. Nami nimeiangusha mierezi yake mirefu, misunobari yake iliyo bora sana. Nimefikia sehemu zake zilizo mbali sana, misitu yake iliyo mizuri sana.
Bi the hond of thi seruauntis thou dispisidist the Lord, and seidist, In the multitude of my charys Y stiede in to the hiye thingis of hillis, in the hiynesse of Liban, and kittide doun the hiye cedris therof, and the chosyn beechis therof; and Y entride `til to the termes therof,
24 Nimechimba visima katika nchi za kigeni na kunywa maji yake. Kwa nyayo za miguu yangu nimekausha vijito vyote vya Misri.”
and Y kittide doun the forest of Carmele therof; and Y drank alien watris, and Y made drie with the steppis of `the feet of myn `alle watris closid.
25 “‘Je, hujasikia? Zamani sana niliamuru hili. Siku za kale nilipanga hili; sasa nimelifanya litokee, kwamba umegeuza miji yenye ngome kuwa malundo ya mawe.
Whether thou herdist not, what Y made at the bigynnyng? Fro elde daies Y made it, and now Y haue brouyt forth; and strengthid citees of fiyteris schulen be in to fallyng of hillis.
26 Watu wa miji hiyo wameishiwa nguvu, wanavunjika mioyo na kuaibishwa. Wao ni kama mimea katika shamba, kama machipukizi mororo ya kijani, kama majani yachipuayo juu ya paa la nyumba, ambayo hukauka kabla ya kukua.
And thei that sitten meke of hond in tho, trembliden togidere, and ben schent; thei ben maad as the hei of the feeld, and as grene eerbe of roouys, which is dried, bifor that it cam to ripenesse.
27 “‘Lakini ninajua mahali ukaapo, kutoka kwako na kuingia kwako, na jinsi unavyoghadhibika dhidi yangu.
And Y bifor knew thi dwellyng, and thi goyng out, and thin entryng, and thi weie, and thi woodnesse ayens me.
28 Kwa sababu unaghadhibika dhidi yangu, na ufidhuli wako umefika masikioni mwangu, nitaweka ndoana yangu puani mwako na hatamu yangu kinywani mwako, nami nitakufanya urudi kwa njia ile uliyoijia.’
Thou were wood ayens me, and thi pride stide in to myn eeris; therfor Y schal putte a cercle in thi nosethirlis, and a bernacle in thi lippis, and Y schal lede thee ayen in to the weie bi which thou camest.
29 “Hii ndiyo itakuwa ishara kwako, ee Hezekia: “Mwaka huu utakula kile kiotacho chenyewe, na mwaka wa pili utakula kutoka machipukizi yake. Lakini katika mwaka wa tatu, panda na uvune, panda mashamba ya mizabibu na ule matunda yake.
Forsothe, Ezechie, this schal be a signe `to thee; ete thou in this yeer that, that thou fyndist; forsothe in the secounde yeer tho thingis, that growen bi her owne wille; sotheli in the thridde yeer sowe ye, and repe ye, plaunte ye vyneris, and ete the fruytis of tho.
30 Mara nyingine tena mabaki ya nyumba ya Yuda wataeneza mizizi chini na kuzaa matunda juu.
And what euer thing schal be residue of the hows of Juda, it schal sende root dounward, and schal make fruyt vpward.
31 Kwa kuwa kutoka Yerusalemu watakuja mabaki, na kutoka Mlima Sayuni kundi la walionusurika. Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote ndio utatimiza jambo hili.
For relikis schulen go out of Jerusalem, and that, that schal be sauyd, `schal go out of the hil of Syon; the feruent loue of the Lord of oostis schal do this.
32 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme wa Ashuru: “Hataingia katika mji huu wala hatapiga mshale hapa. Hatakuja mbele yake akiwa na ngao, wala kupanga majeshi kuuzingira.
Wherfor the Lord seith these thingis of the kyng of Assiriens, He schal not entre in to this citee, nethir he schal sende an arowe in to it, nether scheeld shal occupie it, nether strengthing, ethir bisegyng, schal cumpasse it.
33 Kwa njia ile aliyoijia, ndiyo atakayorudi; hataingia katika mji huu, asema Bwana.
He schal turne ayen bi the weie `bi which he cam, and he schal not entre in to this citee, seith the Lord;
34 Nitaulinda mji huu na kuuokoa, kwa ajili yangu mwenyewe, na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”
and Y schal defende this citee, and Y schal saue it for me, and for Dauid, my seruaunt.
35 Usiku ule, malaika wa Bwana akaenda, akawaua wanajeshi 185,000 katika kambi ya Waashuru. Wenzao walipoamka asubuhi yake, walikuta maiti kila mahali!
Therfor it was don, in that niyt the aungel of the Lord cam, and smoot in the castels of Assiryens an hundrid foure score and fyue thousynde. And whanne Sennacherib hadde rise eerli, he siy alle bodies of deed men; and he departide, and yede awei.
36 Basi Senakeribu mfalme wa Ashuru akavunja kambi na kuondoka. Akarudi Ninawi na kukaa huko.
And Sennacherib, the kyng of Assiriens, turnede ayen, and dwellide in Nynyue.
37 Siku moja, alipokuwa akiabudu katika hekalu la mungu wake Nisroki, wanawe Adrameleki na Shareza wakamuua kwa upanga, nao wakakimbilia nchi ya Ararati. Naye Esar-Hadoni mwanawe akawa mfalme badala yake.
And whanne he worschipide in the temple Nestrach his god, Adramelech and Sirasar, his sones, killide hym with swerd; and thei fledden in to the lond of Armenyes; and Asaradon, his sone, regnyde for hym.

< 2 Wafalme 19 >