< 2 Wafalme 19 >

1 Mfalme Hezekia aliposikia haya, akararua nguo zake na kuvaa nguo ya gunia, naye akaenda katika Hekalu la Bwana.
Yuda hina bagade Hesegaia da ilia sia: ne iasu nababeba: le, e da ea abula gadelale, eboboi abula salawane, Hina Gode Ea Debolo diasuga asi.
2 Akawatuma Eliakimu msimamizi wa nyumba ya mfalme, Shebna mwandishi, na viongozi wa makuhani, wote wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa nabii Isaya mwana wa Amozi.
E da Ilaiagime (hina bagade diasu ouligisu dunu), Siebena (hina bagade diasuga esalebe fi ilia sia: dedene legesu dunu) amola asigilai gobele salasu dunu amo huluane balofede dunu Aisaia (A: imose egefe) ema asunasi. Ilia amola da eboboi abula salawene asi.
3 Wakamwambia, “Hili ndilo asemalo Hezekia: Siku hii ni siku ya dhiki, ya kukaripiwa na ya aibu, kama wakati watoto wanapofikia karibu kuzaliwa na kumbe hakuna nguvu ya kuwazaa.
Hesegaia da adola ahoasu dunuma Aisaiama amane sia: sima: ne sia: i, “Wali eso da se nabasu eso bagadedafa! Ninia da se iasu naba amola gogosiasu da ninima doaga: i. Ninia da uda ilia mano lalelegemu gadenesea, gasa hameba: le, mano lamu hamedei, ninia da amo agoai ba: sa.
4 Yamkini Bwana, Mungu wako atayasikia maneno ya jemadari wa jeshi, ambaye bwana wake, mfalme wa Ashuru, amemtuma kumdhihaki Mungu aliye hai, tena kwamba atamkemea kwa maneno ambayo Bwana, Mungu wako ameyasikia. Kwa hiyo omba kwa ajili ya mabaki ambao bado wako.”
Asilia hina bagade da ea afoha ouligisu dunu amo Hina Godema gademusa: asunasi dagoi. Dia Hina Gode da amo gadesu sia: nabalu, amo gadesu sia: su dunuma se dabe imunu da defea. Amaiba: le, ninia dunu da hame bogoi esalebe, amo fidima: ne, dia Godema sia: ne gadoma.”
5 Maafisa wa Mfalme Hezekia walipofika kwa Isaya,
Aisaia da hina bagade Hesegaia ea sia: si, nababeba: le,
6 Isaya akawaambia, “Mwambieni bwana wenu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Usiogope kwa hayo uliyoyasikia, yale maneno ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru wamenitukana nayo.
e da ema bu dabe adole ima: ne amane sia: si, “Hina Gode da dima amane sia: sa, ‘Asilia dunu da dili beda: ma: ne, Na da dili gaga: mu da hamedei sia: sa. Be ilia gasa fili sia: beba: le, mae beda: ma!
7 Sikiliza! Nitatia roho fulani ndani yake ili atakaposikia taarifa fulani, atarudi nchi yake mwenyewe, nami huko nitafanya auawe kwa upanga.’”
Na, Hina Gode da hamobeba: le, Asilia hina bagade da beda: ma: ne udigili sia: nababeba: le, hi sogega buhagimu. Amola Na da hamobeba: le, e da amogawi medole legei ba: mu.’”
8 Jemadari wa jeshi aliposikia kwamba mfalme wa Ashuru ameondoka Lakishi, alirudi, akamkuta mfalme akipigana na Libna.
Asilia dadi gagui ouligisu dunu afae, da Asilia hina bagade amo La: igisi moilai bai bagade fisili, eno gadenene moilai Libina amoma doagala: musa: asi, amo nababeba: le, amogawi ema fada: i sia: sia: musa: asi.
9 Basi Senakeribu akapata taarifa kwamba Tirhaka, Mkushi mfalme wa Misri, alikuwa anaenda kupigana naye. Basi akatuma tena wajumbe kwa Hezekia na neno hili:
Amola Asilia dunu da sia: amane sia: si nabi, Idioubia hina bagade da Idibidi dadi gagui dunu wa: i amo bisili, Asilia hina bagade ema doagala: musa: mana, amane sia: be nabi. Asilia hina bagade da amo sia: nababeba: le, e da Yuda hina bagade Hesegaiama meloa amane dedene iasi,
10 “Mwambieni Hezekia mfalme wa Yuda: Usikubali huyo Mungu unayemtumainia akudanganye wakati anaposema, ‘Yerusalemu haitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.’
“Dilia ‘gode’ amo da dilia dafawaneyale dawa: sa, dilima ogogole, na da dili hame hasalimu sia: sa. Be amo ogogosu sia: mae nabima!
11 Hakika umesikia yale ambayo wafalme wa Ashuru wametenda kwa nchi zote, wakiwaangamiza kabisa. Je, wewe utaokolewa?
Dilia da sia: nabi, amo Asilia hina bagade da soge fi gugunufinisimusa: sia: sea, e da dafawane gugunufinisimu. Dilia da hobeale gaga: su ba: mu, mae dawa: ma!
12 Je, miungu ya mataifa ambayo yaliangamizwa na baba zangu iliweza kuwaokoa, hiyo miungu ya Gozani, Harani, Resefu, na ya watu wa Edeni waliokuwa Telasari?
Na aowalali ilia da Gousa: ne, Halane, amola Lisefe moilai huluane gugunufinisi. Amola Bede Idini fi dunu Dila: sa moilai ganodini esala, huluane medole legei. Ilia ‘gode’ da amo huluane gaga: mu hamedei ba: i.
13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, mfalme wa mji wa Sefarvaimu, au wa Hena au wa Iva?”
Moilai Ha: ima: de amola Aba: de, Sefafa: ime, Hina, amola Ifai, ilia hina bagade ili da habila: ?”
14 Hezekia akapokea barua kutoka kwa wale wajumbe, naye akaisoma. Kisha akapanda katika Hekalu la Bwana, akaikunjua mbele za Bwana.
Yuda hina bagade Hesegaia da amo meloa dedei sia: adola ahoasu dunuma lale, idi. Amalalu, e da Debolo Diasuga asili, meloa amo Hina Gode Ea midadi ligisili,
15 Naye Hezekia akamwomba Bwana akisema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, uketiye juu ya kiti cha enzi kati ya makerubi, wewe peke yako ndiwe Mungu juu ya falme zote za dunia. Wewe umeumba mbingu na nchi.
amane sia: ne gadoi, “Isala: ili fi ilia Hina Gode! Di da Dia fisu da: iya, amo ougia hamoi liligi gadodili esalebe. Disu da Godedafa amola Di da fifi asi gala huluanedafa ouligisa. Disu da osobo bagade amola mu hahamoi.
16 Tega sikio, Ee Bwana, usikie; fungua macho yako, Ee Bwana, uone; sikiliza maneno ambayo Senakeribu ametuma kumtukana Mungu aliye hai.
Wali Hina Gode! Hou da ninima doaga: i ba: ma! Sena: gelibi da Di, Esalebe Godedafa, amo Dima gadele sia: be nabima!
17 “Ni kweli, Ee Bwana, kwamba wafalme wa Ashuru wameyaangamiza mataifa haya na nchi zao.
Hina Gode! Ninia huluane dawa: ! Asilia hina bagade ilia da fifi asi gala bagohame gugunufinisi dagoi, amola ilia soge wadela: lesi.
18 Wameitupa miungu yao kwenye moto na kuiangamiza, kwa kuwa haikuwa miungu, bali miti na mawe tu iliyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
Ilia da amo dunu fi ilia ‘gode’ huluane laluga ulagi. (Be amo ‘gode’ ilia da ‘gode’dafa hame - ilia da osobo bagade dunu ilia loboga ifa amola gelega hamoi liligi fawane).
19 Sasa basi, Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe kutoka mkononi mwake, ili falme zote duniani zipate kujua kwamba wewe peke yako, Ee Bwana, ndiwe Mungu.”
Amaiba: le, wali ninia Hina Gode! Osobo bagade fifi asi gala huluanedafa, ilia da Di, Hina Gode da Godedafa, amo ilia dawa: ma: ne, Asilia dunu da nini mae hasalima: ne, nini gaga: ma!”
20 Kisha Isaya mwana wa Amozi akapeleka ujumbe kwa Hezekia, akasema: “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nimesikia maombi yako kuhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru.
Amalalu, Aisaia da hina bagade Hesegaiama, Hina Gode da ema ea sia: ne gadosu amane adole ima: ne amo sia: amane sia: si,
21 Hili ndilo neno ambalo Bwana amelisema dhidi yake: “‘Bikira Binti Sayuni anakudharau na kukudhihaki. Binti Yerusalemu anatikisa kichwa chake unapokimbia.
“Hina Gode da amane sia: i dagoi, ‘Sena: galibi di! Yelusaleme moilai bai bagade da diba: le oufesega: sa.
22 Ni nani uliyemtukana na kumkufuru? Ni nani uliyeinua sauti yako dhidi yake, na kumwinulia macho yako kwa kiburi? Ni dhidi ya yule Aliye Mtakatifu wa Israeli!
Di da Na, Isala: ili ilia Hadigidafa Hina Gode, Nama mae nodone, gadele sia: beba: le, di da nowa dunula: ?
23 Kupitia kwa wajumbe wako umelundika matukano juu ya Bwana. Nawe umesema, “Kwa magari yangu mengi ya vita, nimepanda juu ya vilele vya milima, vilele vya juu sana katika Lebanoni. Nami nimeiangusha mierezi yake mirefu, misunobari yake iliyo bora sana. Nimefikia sehemu zake zilizo mbali sana, misitu yake iliyo mizuri sana.
Di da dia adola ahoasu dunu Nama hidale, di amola dia ‘sa: liode’ fila heda: i dunu da baligili heda: i Lebanone goumi huluane hasali dagoi, amo Nama hidale sia: musa: asunasi. Di da baligili heda: i dolo ifa amola ‘saibala: se’ ifa noga: idafa abusa: le, iwiladafa amoga doaga: i, amo Nama hidale sia: i.
24 Nimechimba visima katika nchi za kigeni na kunywa maji yake. Kwa nyayo za miguu yangu nimekausha vijito vyote vya Misri.”
Di da eno hidale, amo di da hano si dogone, ga fi dunu ilia soge ganodini hano dili mai, amola dia dadi gagui dunu da osa: giba: le, Naile Hano da hafoga: i dagoi ba: i, amo huluane di hidale sia: i.
25 “‘Je, hujasikia? Zamani sana niliamuru hili. Siku za kale nilipanga hili; sasa nimelifanya litokee, kwamba umegeuza miji yenye ngome kuwa malundo ya mawe.
Amo hou Na da hemonega ilegei, amo di da hame nabibala: ? Amola wali Na ilegei hou Na da hamoi dagoi. Di da gagili sali moilai bagohame gugunufinisiba: le, ilia da isu ligisisu agoai ba: sa. Be amo hamoma: ne, Nisu fawane da dima gasa defele i.
26 Watu wa miji hiyo wameishiwa nguvu, wanavunjika mioyo na kuaibishwa. Wao ni kama mimea katika shamba, kama machipukizi mororo ya kijani, kama majani yachipuayo juu ya paa la nyumba, ambayo hukauka kabla ya kukua.
Dunu amogawi esalu da gasa hamedafa ba: i. Ilia da bagadewane beda: i amola gasa hameba: le, sidi agoai dialebe ba: i. Ilia da gisi, logo bega: o diasu da: iya gadodili lelebe, amo da gia: i bagade fo, gusudili mabe amoga fabe, amo defele ba: i.
27 “‘Lakini ninajua mahali ukaapo, kutoka kwako na kuingia kwako, na jinsi unavyoghadhibika dhidi yangu.
Be dia hou huluanedafa Na dawa: ! Dia hamobe amola dia habidili ahoabe, amo huluane Na dawa: Na da dia Nama nimi bagade ougi hou Na dawa:
28 Kwa sababu unaghadhibika dhidi yangu, na ufidhuli wako umefika masikioni mwangu, nitaweka ndoana yangu puani mwako na hatamu yangu kinywani mwako, nami nitakufanya urudi kwa njia ile uliyoijia.’
Na da dia ougi bagade hou amola gasa fi bagade hou amo sia: ne iasu, Na da lai dagoi. Amaiba: le, Na da wali dia mi ma: goga mi gala: mu, amola dia lafi ganodini gula misimu. Amola amoga, Na da di logo di misi amoga di buhagima: ne sesemu.”
29 “Hii ndiyo itakuwa ishara kwako, ee Hezekia: “Mwaka huu utakula kile kiotacho chenyewe, na mwaka wa pili utakula kutoka machipukizi yake. Lakini katika mwaka wa tatu, panda na uvune, panda mashamba ya mizabibu na ule matunda yake.
Amalalu, Aisaia da hina bagade Hesegaiama amane sia: i, “Na da dima hobea misunu hou da dafawane doaga: mu, amo dawa: digima: ne olelesu dima imunu. Wali ode amola aya ode, dilia da udigili sogega heda: i gala: ine fawane manu. Be ode aduna baligili eno amoga, dilia da gala: ine bugili, gamimu amola waini efe sagai bugili, waini fage manu.
30 Mara nyingine tena mabaki ya nyumba ya Yuda wataeneza mizizi chini na kuzaa matunda juu.
Yuda soge ganodini, dunu amo da hame bogoi esalebe ba: sea, ilia da bugi amo da difi osobo gududafa sa: i, amola fage noga: le legei, amo defele ba: mu.
31 Kwa kuwa kutoka Yerusalemu watakuja mabaki, na kutoka Mlima Sayuni kundi la walionusurika. Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote ndio utatimiza jambo hili.
Yelusaleme moilai bai bagadega amola Saione Goumia dunu hame bogoi, esalebe ba: mu. Bai Hina Gode da amo hou doaga: ma: ne, dafawane ilegei dagoi.
32 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme wa Ashuru: “Hataingia katika mji huu wala hatapiga mshale hapa. Hatakuja mbele yake akiwa na ngao, wala kupanga majeshi kuuzingira.
Amola Hina Gode da Asilia hina bagade ema misunu hou olelema: ne, amane sia: sa, ‘E da Yelusaleme hamedafa golili sa: imu. E da amoga dadi afae hamedafa gala: mu. Dadi gagui dunu da da: igene gaga: su liligi gaguiwane da, Yelusaleme gadenena hame misunu. Ilia da amoma doagala: musa: , osobo gasa: le lelegela hame heda: mu.
33 Kwa njia ile aliyoijia, ndiyo atakayorudi; hataingia katika mji huu, asema Bwana.
Asilia hina bagade da moilai ganodini mae golili sa: ili, hi misi logoga buhagimu. Bai Na, Hina Gode da amo sia: i dagoi.
34 Nitaulinda mji huu na kuuokoa, kwa ajili yangu mwenyewe, na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”
Dunu da Nama nodoma: ne amola Na da Na hawa: hamosu dunu Da: ibidima dafawane ilegele sia: beba: le, Na da amo moilai gaga: mu.”
35 Usiku ule, malaika wa Bwana akaenda, akawaua wanajeshi 185,000 katika kambi ya Waashuru. Wenzao walipoamka asubuhi yake, walikuta maiti kila mahali!
Amo gasia, Hina Gode Ea a: igele dunu da Asilia ha wa: i fisisu amoga asili, Asilia dadi gagui dunu 185,000 agoane medole legei. Golale, hahabe, ilia huluane da osoboga bogogia: i dialebe ba: i.
36 Basi Senakeribu mfalme wa Ashuru akavunja kambi na kuondoka. Akarudi Ninawi na kukaa huko.
Amalalu, Asili hina bagade Sena: galibi da Yuda soge fi doagala: lalu yolesili, Ninife moilai bagadega buhagi.
37 Siku moja, alipokuwa akiabudu katika hekalu la mungu wake Nisroki, wanawe Adrameleki na Shareza wakamuua kwa upanga, nao wakakimbilia nchi ya Ararati. Naye Esar-Hadoni mwanawe akawa mfalme badala yake.
Eso afaega, e da ea ogogosu ‘gode’ Miseloge ea debolo diasua ema nodone sia: ne gadolaloba, egefe aduna amo A: dala: melege amola Sialisa da elea gegesu gobiheiga, Sena: galibi fane legele, Elala: de sogega hobea: i. Sena: galibi egefe eno, amo Isaha: done, da e bagia Asilia hina bagade hamoi.

< 2 Wafalme 19 >