< 2 Wafalme 18 >
1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Hoshea mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Hezekia mwana wa Ahazi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
Uti tredje årena Hosea, Ela sons, Israels Konungs, vardt Hiskia Konung, Ahas son, Juda Konungs;
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
Och var fem och tjugu åra gammal, då han vardt Konung, och regerade nio och tjugu år i Jerusalem; hans moder het Abi, Zacharia dotter.
3 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Daudi baba yake alivyofanya.
Och han gjorde det godt var för Herranom, såsom hans fader David.
4 Akapaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, akazivunja sanamu, akakatakata nguzo za Ashera. Akavunja vipande vipande ile nyoka ya shaba Mose aliyotengeneza, kwa kuwa hadi siku hizo wana wa Israeli walikuwa wanaifukizia uvumba (ilikuwa ikiitwa Nehushtani).
Han lade bort de höjder, och bröt omkull stodarna, och utrotade lundarna, och slog sönder den kopparormen, som Mose gjort hade; ty allt intill den tiden hade Israels barn rökt för honom, och han kallade honom Nehusthan.
5 Hezekia aliweka tumaini lake kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Hapakuwepo na mfalme mwingine wa kufanana naye miongoni mwa wafalme wa Yuda, kabla yake au baada yake.
Han förtröste på Herran Israels Gud, så att ingen hans like var efter honom, ej heller för honom, ibland alla Juda Konungar.
6 Alishikamana na Bwana kwa bidii wala hakuacha kumfuata; alishika amri ambazo Bwana alikuwa amempa Mose.
Han höll sig intill Herran, och trädde icke ifrå honom, och höll hans bud, som Herren hade budit Mose.
7 Naye Bwana alikuwa pamoja naye, akafanikiwa katika kila alichokifanya. Aliasi dhidi ya mfalme wa Ashuru, wala hakumtumikia.
Och Herren var med honom, och hvart han utdrog, handlade han visliga. Dertill föll han af ifrå Konungen i Assyrien, och var honom icke underdånig.
8 Kuanzia mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye ngome, aliwashinda Wafilisti, hadi kufikia Gaza na himaya yake yote.
Han slog ock de Philisteer, allt intill Gasa, och deras gränsor, både slott och fasta städer.
9 Mwaka wa nne wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa saba wa Hoshea mwana wa Ela kutawala Israeli, Shalmanesa mfalme wa Ashuru alikwenda kuishambulia Samaria na kuuzunguka kwa majeshi.
Uti fjerde årena Hiskia, Juda Konungs, det var sjunde året Hosea, Ela sons, Israels Konungs, då drog Salmanasser, Konungen i Assyrien, upp emot Samarien, och belade det;
10 Baada ya miaka mitatu Waashuru wakautwaa. Kwa hiyo Samaria ulitekwa katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea mfalme wa Israeli.
Och vann det efter tre år, uti sjette Hiskia åre, det är, uti nionde årena Hosea, Israels Konungs, så vardt Samarien vunnet.
11 Mfalme wa Ashuru akawahamishia Waisraeli huko Ashuru na akawaweka Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
Och Konungen af Assyrien förde Israel bort till Assyrien, och satte dem i Halah och Habor, vid den älfven Gosan, och uti de Meders städer;
12 Hili lilitokea kwa sababu hawakumtii Bwana Mungu wao, lakini walikuwa wamevunja agano lake, yale yote ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwaamuru. Hawakuzisikiliza amri wala kuzitimiza.
Derföre, att de icke lydt hade Herrans sins Guds röst, och hade öfverträdt hans förbund; och allt det Mose Herrans tjenare budit hade, det hade de intet lydt, eller gjort.
13 Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
Men uti fjortonde årena Konungs Hiskia, drog upp Sanherib, Konungen i Assyrien, emot alla fasta städer i Juda, och tog dem in.
14 Basi Hezekia mfalme wa Yuda akamtumia ujumbe mfalme wa Ashuru huko Lakishi akisema: “Nimefanya makosa. Ondoka katika nchi yangu, nami nitakulipa chochote unachokitaka kwangu.” Mfalme wa Ashuru akamtoza Hezekia mfalme wa Yuda talanta 300 za fedha, na talanta thelathini za dhahabu.
Då sände Hiskia, Juda Konung, till Konungen af Assyrien i Lachis, och lät säga honom: Jag hafver syndat, vänd om ifrå mig; hvad du lägger mig uppå, det vill jag draga. Så lade Konungen af Assyrien på Hiskia, Juda Konung, trehundrad centener silfver, och tretio centener guld.
15 Basi Hezekia akampa fedha yote iliyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme.
Alltså gaf Hiskia ut allt det silfver, som i Herrans hus, och i Konungshusets drätsel funnet vardt.
16 Wakati huu Hezekia mfalme wa Yuda akabandua dhahabu yote iliyokuwa imefunika milango na miimo ya Hekalu la Bwana, akampa mfalme wa Ashuru.
På den samma tiden slog Hiskia, Juda Konung, sönder dörrarna af Herrans tempel, och de skifvor, som han sjelf hade låtit bedraga dem med, och fick dem Konungenom af Assyrien.
17 Mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wake mkuu, na afisa wake mkuu, na jemadari wa jeshi, pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Wakaja Yerusalemu na kusimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
Och Konungen af Assyrien sände Tharthan, och öfversta kamereraren, och RabSake ifrå Lachis, till Konung Hiskia med stora magt till Jerusalem, och de drogo upp; och då de kommo, höllo de vid vattugrafvena af öfversta dammen, som ligger vid den vägen på valkareåkrenom;
18 Wakaagiza mfalme aitwe. Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la mfalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakawaendea.
Och de kallade Konungen. Då kom ut till dem Eliakim, Hilkia son, hofmästaren, och Sebna skrifvaren, och Joah, Asaphs son, cancelleren.
19 Yule jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia: “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
Och RabSake sade till dem: Käre, säger Konung Hiskia: Så säger den store Konungen, Konungen af Assyrien: Hvad är detta för en tröst, der du förlåter dig uppå?
20 Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
Menar du, att du hafver ännu råd och magt till att strida? Hvaruppå förlåter då du dig nu, att du äst affallen ifrå mig?
21 Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
Si, förlåter du dig uppå den sönderbråkade rörstafven Egypten? Hvilken som stöder sig vid honom, honom varder han gångandes upp i handena, och genomstinger henne; alltså är Pharao, Konungen i Egypten, allom dem som förlåta sig på honom.
22 Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya katika Yerusalemu”?
Om I ock viljen säga till mig: Vi förlåte oss på Herran vår Gud; är icke han den, hvilkens höjder och altare Hiskia hafver aflagt, och sagt till Juda och Jerusalem: För detta altaret, som i Jerusalem är, skolen I tillbedja?
23 “‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
Så gör nu samman en hop minom herra, Konungenom af Assyrien, så vill jag få dig tutusend hästar; lät se, om du kan åstadkomma dem, som deruppå rida måga.
24 Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
Huru vill du då blifva ståndandes för en den minsta höfdingan, mins herras underdåna, om du förlåter dig uppå Egypten, för vagnars och resenärars skull?
25 Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza mahali hapa pasipo neno kutoka kwa Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
Menar du, att jag utan Herrans vilja är hit uppdragen, till att förderfva denna staden? Herren hafver mig det befallt: Drag upp i detta landet, och förderfva det.
26 Ndipo Eliakimu mwana wa Hilkia, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
Då sade Eliakim, Hilkia son, och Sebna, och Joah, till RabSake: Tala med dina tjenare på Syrisko, ty vi förstå det, och tala icke med oss på Judisko, för folkens öron, som på muren är.
27 Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
Men RabSake sade till dem: Hafver nu min herre sändt mig till din herra, eller till dig, att jag dessa orden säga skulle? Ja, till de män som sitta på muren, att de skulle äta sin egen träck med eder, och dricka sitt piss.
28 Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni neno la mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
Alltså stod RabSake, och ropade med höga röst på Judisko, talade, och sade: Hörer den stora Konungens röst, Konungens af Assyrien.
29 Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa mkononi mwangu.
Detta säger Konungen: Låter icke Hiskia bedraga eder; ty han förmår icke fria eder utu mine hand;
30 Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
Och låter icke Hiskia förtrösta eder på Herran, så att han säger: Herren skall fria oss, och denne stad skall icke gifven varda i Konungens händer af Assyrien.
31 “Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
Hörer icke Hiskia; ty så säger Konungen af Assyrien: Görer mig till vilja, och kommer ut till mig, så skall hvar och en äta af sitt vinträ, och af sitt fikonaträ, och dricka af sin brunn:
32 mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na mashamba ya mizabibu, nchi ya mizeituni na asali. Chagueni uzima, sio mauti! “Msimsikilize Hezekia, kwa kuwa anawapotosha asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’
Intilldess jag kommer, och hemtar eder uti ett land, det edro lande likt är, der korn, must, bröd, vingårdar, oljoträ, olja och hannog uti är, så fån I lefva, och icke dö; hörer intet Hiskia, ty han förförer eder, då han säger: Herren varder oss hjelpandes.
33 Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
Hafva ock Hedningarnas gudar hvar och en hulpit sitt land ifrå Konungens hand i Assyrien?
34 Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu, Hena na Iva? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
Hvar äro de gudar i Hamath och Arphad? Hvar äro de gudar i Sepharvaim, Hena och Iva? Hafva de ock hulpit Samarien utu mine hand?
35 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
Hvar är en gud ibland alla lands gudar, som sitt land friat hafver utu mina hand, att Herren nu skall fria Jerusalem utu mina hand?
36 Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
Då tigde folket, och svarade honom intet; ty Konungen hade budit, och sagt: Svarer honom intet.
37 Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.
Så kom då Eliakim, Hilkia son, hofmästaren, och Sebna skrifvaren, och Joah, Asaphs son, cancelleren, till Hiskia med rifven kläder, och gåfvo honom tillkänna RabSake ord.