< 2 Wafalme 18 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Hoshea mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Hezekia mwana wa Ahazi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
and to be in/on/with year three to/for Hoshea son: child Elah king Israel to reign Hezekiah son: child Ahaz king Judah
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
son: aged twenty and five year to be in/on/with to reign he and twenty and nine year to reign in/on/with Jerusalem and name mother his Abi daughter Zechariah
3 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Daudi baba yake alivyofanya.
and to make: do [the] upright in/on/with eye: appearance LORD like/as all which to make: do David father his
4 Akapaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, akazivunja sanamu, akakatakata nguzo za Ashera. Akavunja vipande vipande ile nyoka ya shaba Mose aliyotengeneza, kwa kuwa hadi siku hizo wana wa Israeli walikuwa wanaifukizia uvumba (ilikuwa ikiitwa Nehushtani).
he/she/it to turn aside: remove [obj] [the] high place and to break [obj] [the] pillar and to cut: cut [obj] [the] Asherah and to crush serpent [the] bronze which to make Moses for till [the] day [the] they(masc.) to be son: descendant/people Israel to offer: offer to/for him and to call: call by to/for him Nehushtan
5 Hezekia aliweka tumaini lake kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Hapakuwepo na mfalme mwingine wa kufanana naye miongoni mwa wafalme wa Yuda, kabla yake au baada yake.
in/on/with LORD God Israel to trust and after him not to be like him in/on/with all king Judah and which to be to/for face: before his
6 Alishikamana na Bwana kwa bidii wala hakuacha kumfuata; alishika amri ambazo Bwana alikuwa amempa Mose.
and to cleave in/on/with LORD not to turn aside: depart from after him and to keep: obey commandment his which to command LORD [obj] Moses
7 Naye Bwana alikuwa pamoja naye, akafanikiwa katika kila alichokifanya. Aliasi dhidi ya mfalme wa Ashuru, wala hakumtumikia.
and to be LORD with him in/on/with all which to come out: come be prudent and to rebel in/on/with king Assyria and not to serve him
8 Kuanzia mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye ngome, aliwashinda Wafilisti, hadi kufikia Gaza na himaya yake yote.
he/she/it to smite [obj] Philistine till Gaza and [obj] border: area her from tower to watch till city fortification
9 Mwaka wa nne wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa saba wa Hoshea mwana wa Ela kutawala Israeli, Shalmanesa mfalme wa Ashuru alikwenda kuishambulia Samaria na kuuzunguka kwa majeshi.
and to be in/on/with year [the] fourth to/for king Hezekiah he/she/it [the] year [the] seventh to/for Hoshea son: child Elah king Israel to ascend: rise Shalmaneser king Assyria upon Samaria and to confine upon her
10 Baada ya miaka mitatu Waashuru wakautwaa. Kwa hiyo Samaria ulitekwa katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea mfalme wa Israeli.
and to capture her from end three year in/on/with year six to/for Hezekiah he/she/it year nine to/for Hoshea king Israel to capture Samaria
11 Mfalme wa Ashuru akawahamishia Waisraeli huko Ashuru na akawaweka Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
and to reveal: remove king Assyria [obj] Israel Assyria [to] and to lead them in/on/with Halah and in/on/with Habor river Gozan and city Mede
12 Hili lilitokea kwa sababu hawakumtii Bwana Mungu wao, lakini walikuwa wamevunja agano lake, yale yote ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwaamuru. Hawakuzisikiliza amri wala kuzitimiza.
upon which not to hear: obey in/on/with voice LORD God their and to pass: trespass [obj] covenant his [obj] all which to command Moses servant/slave LORD and not to hear: hear and not to make: do
13 Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
and in/on/with four ten year to/for king Hezekiah to ascend: rise Sennacherib king Assyria upon all city Judah [the] to gather/restrain/fortify and to capture them
14 Basi Hezekia mfalme wa Yuda akamtumia ujumbe mfalme wa Ashuru huko Lakishi akisema: “Nimefanya makosa. Ondoka katika nchi yangu, nami nitakulipa chochote unachokitaka kwangu.” Mfalme wa Ashuru akamtoza Hezekia mfalme wa Yuda talanta 300 za fedha, na talanta thelathini za dhahabu.
and to send: depart Hezekiah king Judah to(wards) king Assyria Lachish [to] to/for to say to sin to return: turn back from upon me [obj] which to give: pay upon me to lift: guilt and to set: take king Assyria upon Hezekiah king Judah three hundred talent silver: money and thirty talent gold
15 Basi Hezekia akampa fedha yote iliyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme.
and to give: give Hezekiah [obj] all [the] silver: money [the] to find house: temple LORD and in/on/with treasure house: home [the] king
16 Wakati huu Hezekia mfalme wa Yuda akabandua dhahabu yote iliyokuwa imefunika milango na miimo ya Hekalu la Bwana, akampa mfalme wa Ashuru.
in/on/with time [the] he/she/it to cut Hezekiah [obj] door temple LORD and [obj] [the] pillar which to overlay Hezekiah king Judah and to give: give them to/for king Assyria
17 Mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wake mkuu, na afisa wake mkuu, na jemadari wa jeshi, pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Wakaja Yerusalemu na kusimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
and to send: depart king Assyria [obj] Tartan and [obj] Rab-saris Rab-saris and [obj] Rabshakeh Rabshakeh from Lachish to(wards) [the] king Hezekiah in/on/with strength: soldiers heavy Jerusalem and to ascend: rise and to come (in): come Jerusalem and to ascend: rise and to come (in): come and to stand: stand in/on/with conduit [the] pool [the] high which in/on/with highway Field (of the Launderer) Washer's
18 Wakaagiza mfalme aitwe. Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la mfalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakawaendea.
and to call: call to to(wards) [the] king and to come out: come to(wards) them Eliakim son: child Hilkiah which upon [the] house: temple and Shebna [the] secretary and Joah son: child Asaph [the] to remember
19 Yule jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia: “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
and to say to(wards) them Rabshakeh Rabshakeh to say please to(wards) Hezekiah thus to say [the] king [the] great: large king Assyria what? [the] trust [the] this which to trust
20 Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
to say surely word lip: words counsel and might to/for battle now upon who? to trust for to rebel in/on/with me
21 Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
now behold to trust to/for you upon staff [the] branch: stem [the] to crush [the] this upon Egypt which to support man: anyone upon him and to come (in): come in/on/with palm his and to pierce her so Pharaoh king Egypt to/for all [the] to trust upon him
22 Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya katika Yerusalemu”?
and for to say [emph?] to(wards) me to(wards) LORD God our to trust not he/she/it which to turn aside: remove Hezekiah [obj] high place his and [obj] altar his and to say to/for Judah and to/for Jerusalem to/for face: before [the] altar [the] this to bow in/on/with Jerusalem
23 “‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
and now to pledge please with lord my with king Assyria and to give: give to/for you thousand horse if be able to/for to give: put to/for you to ride upon them
24 Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
and how? to return: turn back [obj] face governor one servant/slave lord my [the] small and to trust to/for you upon Egypt to/for chariot and to/for horseman
25 Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza mahali hapa pasipo neno kutoka kwa Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
now from beside LORD to ascend: rise upon [the] place [the] this to/for to ruin him LORD to say to(wards) me to ascend: rise upon [the] land: country/planet [the] this and to ruin her
26 Ndipo Eliakimu mwana wa Hilkia, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
and to say Eliakim son: child Hilkiah and Shebna and Joah to(wards) Rabshakeh Rabshakeh to speak: speak please to(wards) servant/slave your Aramaic for to hear: understand we and not to speak: speak with us Judahite in/on/with ear: hearing [the] people which upon [the] wall
27 Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
and to say to(wards) them Rabshakeh Rabshakeh upon lord your and to(wards) you to send: depart me lord my to/for to speak: speak [obj] [the] word [the] these not upon [the] human [the] to dwell upon [the] wall to/for to eat [obj] (filth their *Q(K)*) and to/for to drink [obj] (water foot their *Q(K)*) with you
28 Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni neno la mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
and to stand: stand Rabshakeh Rabshakeh and to call: call out in/on/with voice great: large Judahite and to speak: speak and to say to hear: hear word [the] king [the] great: large king Assyria
29 Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa mkononi mwangu.
thus to say [the] king not to deceive to/for you Hezekiah for not be able to/for to rescue [obj] you from hand: power his
30 Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
and not to trust [obj] you Hezekiah to(wards) LORD to/for to say to rescue to rescue us LORD and not to give: give [obj] [the] city [the] this in/on/with hand: power king Assyria
31 “Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
not to hear: hear to(wards) Hezekiah for thus to say king Assyria to make with me blessing and to come out: come to(wards) me and to eat man: anyone vine his and man: anyone fig his and to drink man: anyone water pit his
32 mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na mashamba ya mizabibu, nchi ya mizeituni na asali. Chagueni uzima, sio mauti! “Msimsikilize Hezekia, kwa kuwa anawapotosha asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’
till to come (in): come I and to take: take [obj] you to(wards) land: country/planet like/as land: country/planet your land: country/planet grain and new wine land: country/planet food: bread and vineyard land: country/planet olive oil and honey and to live and not to die and not to hear: hear to(wards) Hezekiah for to incite [obj] you to/for to say LORD to rescue us
33 Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
to rescue to rescue God [the] nation man: anyone [obj] land: country/planet his from hand: power king Assyria
34 Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu, Hena na Iva? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
where? God Hamath and Arpad where? God Sepharvaim Hena and Ivvah for to rescue [obj] Samaria from hand: power my
35 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
who? in/on/with all God [the] land: country/planet which to rescue [obj] land: country/planet their from hand: power my for to rescue LORD [obj] Jerusalem from hand: power my
36 Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
and be quiet [the] people and not to answer [obj] him word for commandment [the] king he/she/it to/for to say not to answer him
37 Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.
and to come (in): come Eliakim son: child Hilkiah which upon [the] house: temple and Shebna [the] secretary and Joah son: child Asaph [the] to remember to(wards) Hezekiah to tear garment and to tell to/for him word Rabshakeh Rabshakeh

< 2 Wafalme 18 >