< 2 Wafalme 18 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Hoshea mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Hezekia mwana wa Ahazi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
I Elas Søns, Kong Hosea af Israels, tredje Regeringsår blev Ezekias, Akaz's Søn, Konge over Juda.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
Han var fem og tyve År gammel, da han blev Konge, og han herskede ni og tyve År i Jerusalem. Hans Moder hed Abi og var en Datter af Zekarja.
3 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Daudi baba yake alivyofanya.
Han gjorde, hvad der var ret i HERRENs Øjne, ganske som hans Fader David.
4 Akapaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, akazivunja sanamu, akakatakata nguzo za Ashera. Akavunja vipande vipande ile nyoka ya shaba Mose aliyotengeneza, kwa kuwa hadi siku hizo wana wa Israeli walikuwa wanaifukizia uvumba (ilikuwa ikiitwa Nehushtani).
Han skaffede Offerhøjene bort, sønderbrød Stenstøtterne, omhuggede Asjerastøtten og knuste Kobberslangen, som Moses havde lavet; thi indtil den Tid havde Israeliterne tændt Offerild for den, og man kaldte den Nehusjtan.
5 Hezekia aliweka tumaini lake kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Hapakuwepo na mfalme mwingine wa kufanana naye miongoni mwa wafalme wa Yuda, kabla yake au baada yake.
Til HERREN, Israels Gud, satte han sin Lid, og hverken før eller siden fandtes hans Lige blandt alle Judas Konger.
6 Alishikamana na Bwana kwa bidii wala hakuacha kumfuata; alishika amri ambazo Bwana alikuwa amempa Mose.
Han holdt fast ved HERREN og veg ikke fra ham, og han overholdt de Bud, HERREN havde givet Moses.
7 Naye Bwana alikuwa pamoja naye, akafanikiwa katika kila alichokifanya. Aliasi dhidi ya mfalme wa Ashuru, wala hakumtumikia.
Og HERREN var med ham; i alt, hvad han tog sig for, havde han Lykken med sig. Han gjorde Oprør mod Assyrerkongen og vilde ikke stå under ham.
8 Kuanzia mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye ngome, aliwashinda Wafilisti, hadi kufikia Gaza na himaya yake yote.
Han slog Filisterne lige til Gaza og dets Omegn, både Vagttårnene og de befæstede Byer.
9 Mwaka wa nne wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa saba wa Hoshea mwana wa Ela kutawala Israeli, Shalmanesa mfalme wa Ashuru alikwenda kuishambulia Samaria na kuuzunguka kwa majeshi.
I Kong Ezekias's fjerde, Elas Søns, Kong Hosea af Israels, syvende Regeringsår, drog Assyrer kongen Salmanassar op mod Sa maria, belejrede
10 Baada ya miaka mitatu Waashuru wakautwaa. Kwa hiyo Samaria ulitekwa katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea mfalme wa Israeli.
og indtog det. Efter tre Års Forløb, i Ezekias's sjette, Kong Hosea af Israels niende Regeringsår, blev Samaria indtaget.
11 Mfalme wa Ashuru akawahamishia Waisraeli huko Ashuru na akawaweka Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
Og Assyrerkongen førte Israel i Landflygtighed til Assyrien og lod dem bosætte sig i Hala, ved Habor, Gozans Flod, og i Mediens Byer,
12 Hili lilitokea kwa sababu hawakumtii Bwana Mungu wao, lakini walikuwa wamevunja agano lake, yale yote ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwaamuru. Hawakuzisikiliza amri wala kuzitimiza.
til Straf for at de ikke havde adlydt HERREN deres Guds Røst, men overtrådt hans Pagt, alt hvad HERRENs Tjener Moses havde påbudt; de hørte ikke derpå og gjorde ikke derefter.
13 Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
I Kong Ezekias's fjortende Regeringsår drog Assyrerkongen Sankerib op mod alle Judas befæstede Byer og indtog dem.
14 Basi Hezekia mfalme wa Yuda akamtumia ujumbe mfalme wa Ashuru huko Lakishi akisema: “Nimefanya makosa. Ondoka katika nchi yangu, nami nitakulipa chochote unachokitaka kwangu.” Mfalme wa Ashuru akamtoza Hezekia mfalme wa Yuda talanta 300 za fedha, na talanta thelathini za dhahabu.
Da sendte Kong Ezekias af Juda Bud til Assyrerkongen i Lakisj og lod sige: "Jeg har forbrudt mig; drag bort fra mig igen! Hvad du pålægger mig, vil jeg tage på mig!" Da pålagde Assyrerkongen Kong Ezekias af Juda at udrede 300 Talenter Sølv og 300 talenter Guld;
15 Basi Hezekia akampa fedha yote iliyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme.
og Ezekias udleverede alt det Sølv, der var i HERRENs Hus og i Skatkamrene i Kongens Palads.
16 Wakati huu Hezekia mfalme wa Yuda akabandua dhahabu yote iliyokuwa imefunika milango na miimo ya Hekalu la Bwana, akampa mfalme wa Ashuru.
Ved den Lejlighed plyndrede Ezekias Dørene i HERRENs Helligdom og Pillerne for det Guld, han selv havde overtrukket dem med, og udleverede det til Assyrerkongen.
17 Mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wake mkuu, na afisa wake mkuu, na jemadari wa jeshi, pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Wakaja Yerusalemu na kusimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
Assyrerkongen sendte så Tartan, Rabsaris og Rabsjake med en anselig Styrke fra Lakisj til Kong Ezekias i Jerusalem, og de drog op og kom til Jerusalem og gjorde Holdt ved Øvredammens Vandledning, ved Vejen til Blegepladsen.
18 Wakaagiza mfalme aitwe. Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la mfalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakawaendea.
Da de krævede at få Kongen i Tale, gik Paladsøversten Eljakim, Hilkijas Søn, Statsskriveren Sjebna og Kansleren Joa, Asafs Søn, ud til dem.
19 Yule jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia: “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
Rabsjake sagde til dem: "Sig til Ezekias: Således siger Storkongen, Assyrerkongen: Hvad er det for en Fortrøstning, du hengiver dig til?
20 Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
Du mener vel, at et blot og bart Ord er det samme som Plan og Styrke i Krig? Og til hvem sætter du egentlig din Lid, siden du gør Oprør imod mig?
21 Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
Se nu, du sætter din Lid til Ægypten, denne brudte Rørkæp, som river Sår i Hånden på den, der støtter sig til den! Thi således går det alle dem, der sætter deres Lid til Farao, Ægyptens Konge.
22 Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya katika Yerusalemu”?
Men vil I sige til mig: Det er HERREN vor Gud, vi sætter vor Lid til! er det så ikke ham, hvis Offerhøje og Altre Ezekias skaffede bort, da han sagde til Juda og Jerusalem: Foran dette Alter, i Jerusalem skal I tilbede!
23 “‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
Og nu, indgå et Væddemål med min Herre, Assyrerkongen: Jeg giver dig to Gange tusind Heste, hvis du kan stille Ryttere til dem!
24 Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
Hvorledes vil du afslå et Angreb af en eneste Statholder, en af min Herres ringeste Tjenere? Og du sætter din Lid til Ægypten, til Vogne og Heste?
25 Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza mahali hapa pasipo neno kutoka kwa Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
Mon det desuden er uden HERRENs Vilje, at jeg er draget op mod dette Sted for at ødelægge det? Det var HERREN selv, der sagde til mig: Drag op mod dette Land og ødelæg det!"
26 Ndipo Eliakimu mwana wa Hilkia, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
Men Eljakim, Hilkijas Søn, Sjebna og Joa sagde til Rabsjake: "Tal dog Aramaisk til dine Trælle, det forstår vi godt; tal ikke Judæisk til os, medens Folkene på Muren hører på det!"
27 Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
Men Habsjake svarede dem: "Er det til din Herre og dig, min Herre har sendt mig med disse Ord? Er det ikke til de Mænd, der sidder på Muren hos eder og æder deres eget Skarn og drikker deres eget Vand!"
28 Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni neno la mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
Og Rabsjake trådte hen og råbte med høj Røst på Judæisk: "Hør Storkongens, Assyrerkongens, Ord!
29 Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa mkononi mwangu.
Således siger Kongen: Lad ikke Ezekias vildlede eder, thi han er ikke i Stand til at frelse eder af min Hånd!
30 Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
Og lad ikke Ezekias forlede eder til at sætte eders Lid til HERREN, når han siger: HERREN skal sikkert frelse os, og denne By skal ikke overgives i Assyrerkongens Hånd!
31 “Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
Hør ikke på Ezekias; thi således - siger Assyrerkongen: Vil I slutte Fred med mig og overgive eder til mig, så skal enhver af eder spise af sin Vinstok og sit Figentræ og drikke af sin Brønd,
32 mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na mashamba ya mizabibu, nchi ya mizeituni na asali. Chagueni uzima, sio mauti! “Msimsikilize Hezekia, kwa kuwa anawapotosha asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’
indtil jeg kommer og tager eder med til et Land, der ligner eders, et Land med Korn og Most, et Land med Brød og Vingårde, et Land med Oliventræer og Honning; så skal I leve og ikke dø. Hør derfor ikke på Ezekias, når han vil forføre eder og siger: HERREN vil frelse os!
33 Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
Mon nogen af Folkeslagenes Guder har kunnet frelse sit Land af Assyrerkongens Hånd?
34 Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu, Hena na Iva? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
Hvor er Hamats og Arpads Guder, hvor er Sefarvajims, Henas og Ivvas Guder? Hvor er Landet Samarias Guder? Mon de frelste Samaria af min Hånd?
35 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
Hvor er der blandt alle Landes Guder nogen, der har frelst sit Land af min Hånd? Mon da HERREN skulde kunne frelse Jerusalem?"
36 Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
Men de tav og svarede ham ikke et Ord, thi Kongens Bud lød på, at de ikke måtte svare ham.
37 Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.
Derpå gik Paladsøversten Eljakim, Hilkijas Søn, Statsskriveren Sjebna og Kansleren Joa, Asafs Søn, med sønderrevne Klæder til Ezekias og meddelte ham, hvad Rabsjake havde sagt.

< 2 Wafalme 18 >