< 2 Wafalme 17 >

1 Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Ahazi mfalme wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, akatawala kwa miaka tisa.
No décimo segundo ano de Acaz, rei de Judá, Oséias, filho de Elá, começou a reinar em Samaria sobre Israel por nove anos.
2 Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini si kama wafalme wengine wa Israeli waliomtangulia.
Ele fez o que era mau aos olhos de Iavé, mas não como os reis de Israel que foram antes dele.
3 Mfalme Shalmanesa wa Ashuru akainuka dhidi ya Mfalme Hoshea, ambaye hapo mbeleni alikuwa mtumwa wake na kumlipa ushuru.
Shalmaneser, rei da Assíria, veio contra ele; e Oséias tornou-se seu servo, e lhe trouxe tributo.
4 Lakini mfalme wa Ashuru akagundua kuwa Hoshea alikuwa msaliti, kwa kuwa alikuwa ametuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri, naye hakuendelea kulipa ushuru kwa mfalme wa Ashuru tena kama alivyokuwa anafanya kila mwaka. Kwa hiyo Shalmanesa akamkamata na kumtia gerezani.
O rei da Assíria descobriu uma conspiração em Oséias; pois ele havia enviado mensageiros para So, rei do Egito, e não ofereceu nenhum tributo ao rei da Assíria, como ele havia feito ano após ano. Por isso, o rei da Assíria o apreendeu e o amarrou na prisão.
5 Mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akapigana dhidi ya Samaria na kuizunguka kwa majeshi miaka mitatu.
Então o rei da Assíria subiu por toda a terra, foi até Samaria, e a sitiou três anos.
6 Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaiteka Samaria na kuwahamishia Waisraeli huko Ashuru. Akawaweka huko Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
No nono ano de Oséias, o rei da Assíria tomou Samaria e levou Israel para a Assíria, e os colocou em Halah, e no Habor, o rio de Gozan, e nas cidades dos Medos.
7 Yote haya yalitokea kwa sababu Waisraeli walikuwa wametenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wao, ambaye alikuwa amewapandisha kutoka Misri akiwatoa chini ya utawala wa nguvu wa Farao mfalme wa Misri. Waliabudu miungu mingine
Foi assim porque os filhos de Israel tinham pecado contra Javé seu Deus, que os tirou da terra do Egito sob a mão do Faraó, rei do Egito, e temeram outros deuses,
8 na kufuata desturi za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao, pamoja na desturi ambazo wafalme wa Israeli walizileta.
e andaram nos estatutos das nações que Javé expulsou de diante dos filhos de Israel, e dos reis de Israel, que eles fizeram.
9 Waisraeli wakafanya vitu kwa siri dhidi ya Bwana Mungu wao, ambavyo havikuwa sawa. Kuanzia kwenye mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye maboma walijijengea wenyewe mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji yao yote.
Os filhos de Israel fizeram secretamente coisas que não eram corretas contra Javé seu Deus; e construíram lugares altos para si mesmos em todas as suas cidades, desde a torre dos guardas até a cidade fortificada;
10 Wakaweka mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda.
e ergueram para si mesmos pilares e varas de Asera em cada colina alta e debaixo de cada árvore verde;
11 Wakafukiza uvumba kila mahali palipoinuka, kama yalivyofanya yale mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao. Wakafanya mambo maovu ambayo yalimghadhibisha Bwana.
e lá queimaram incenso em todos os lugares altos, como as nações que Javé levou antes deles; e fizeram coisas más para provocar Javé à ira;
12 Wakaabudu sanamu, ingawa Bwana alikuwa amesema, “Msifanye mambo haya.”
e serviram ídolos, dos quais Javé lhes disse: “Não fareis isto”.”
13 Bwana akawaonya Israeli na Yuda kupitia kwa manabii na waonaji wake wote: “Acheni njia zenu mbaya. Shikeni amri na maagizo yangu, kufuatana na sheria yangu yote niliyowaagiza baba zenu kuitii ambayo niliileta kwenu kupitia kwa watumishi wangu manabii.”
No entanto, Javé testemunhou a Israel e a Judá, por cada profeta e por cada vidente, dizendo: “Convertei-vos de vossos maus caminhos, e guardai meus mandamentos e meus estatutos, de acordo com toda a lei que ordenei a vossos pais, e que vos enviei por meus servos, os profetas”.
14 Lakini hawakusikiliza, walikuwa na shingo ngumu kama baba zao, ambao hawakumtegemea Bwana Mungu wao.
Notwithstanding, eles não quiseram ouvir, mas endureceram seu pescoço como o pescoço de seus pais que não acreditavam em Yahweh, seu Deus.
15 Walizikataa amri zake, na agano alilokuwa amelifanya na baba zao, na maonyo aliyokuwa amewapa. Wakafuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai. Wakayaiga mataifa yaliyowazunguka, ingawa Bwana alikuwa amewaonya akiwaambia, “Msifanye kama wanavyofanya,” nao wakafanya mambo ambayo Bwana alikuwa amewakataza wasifanye.
Rejeitaram seus estatutos e seu pacto que ele fez com seus pais, e seus testemunhos que ele lhes testemunhou; e seguiram a vaidade, e tornaram-se vaidosos, e seguiram as nações que estavam ao seu redor, sobre as quais Javé lhes ordenara que não fizessem como eles.
16 Wakayaacha maagizo yote ya Bwana Mungu wao na kujitengenezea sanamu mbili, walizozisubu katika sura ya ndama na nguzo ya Ashera. Wakasujudia mianga yote ya angani, na wakamtumikia Baali.
Eles abandonaram todos os mandamentos de Iavé seu Deus, e fizeram imagens fundidas para si mesmos, mesmo dois bezerros, e fizeram um Asherah, e adoraram todo o exército do céu, e serviram Baal.
17 Wakawatoa kafara wana wao na mabinti zao katika moto. Wakafanya uaguzi na uchawi, nao wakajiuza wenyewe katika kutenda uovu machoni pa Bwana, wakamghadhibisha.
Eles fizeram seus filhos e suas filhas passarem pelo fogo, usaram adivinhações e encantamentos, e venderam-se para fazer o que era mau aos olhos de Iavé, para provocá-lo à raiva.
18 Basi Bwana akawakasirikia sana Israeli na kuwaondoa kwenye uwepo wake. Ni kabila la Yuda tu lililobaki;
Portanto, Javé ficou muito zangado com Israel, e os tirou de sua vista. Não havia mais ninguém além da tribo de Judá apenas.
19 na hata hivyo nao Yuda hawakuzishika amri za Bwana Mungu wao. Wakafuata desturi ambazo Israeli walikuwa wamezianzisha.
Também Judá não guardou os mandamentos de Javé seu Deus, mas caminhou nos estatutos de Israel que eles fizeram.
20 Kwa hiyo Bwana aliwakataa watu wote wa Israeli; akawatesa na kuwaachia katika mikono ya wateka nyara hadi alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake.
Javé rejeitou toda a descendência de Israel, afligiu-os e os entregou nas mãos de invasores, até que os expulsou de sua vista.
21 Alipokwisha kuwatenga Israeli mbali na nyumba ya Daudi, wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme wao. Yeroboamu akawashawishi Israeli waache kumfuata Bwana na akawasababisha kutenda dhambi kuu.
Pois ele arrancou Israel da casa de Davi; e eles fizeram de Jeroboão o filho de Nebate rei; e Jeroboão expulsou Israel de seguir a Iavé, e os fez pecar um grande pecado.
22 Nao Israeli wakadumu katika dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati, nao hawakuziacha
Os filhos de Israel caminharam em todos os pecados de Jeroboão que ele fez; não se afastaram deles
23 hadi Bwana alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake, kama vile alivyokuwa ameonya kupitia watumishi wake wote manabii. Hivyo watu wa Israeli wakaondolewa kutoka nchi yao kwenda uhamishoni Ashuru, nao wako huko mpaka sasa.
até que Javé tirou Israel de sua vista, como ele disse por todos os seus servos, os profetas. Então Israel foi levado de sua própria terra para a Assíria até os dias de hoje.
24 Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli, Kutha, Ava, Hamathi na Sefarvaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria badala ya Waisraeli. Wakaimiliki Samaria na kuishi katika miji yake.
O rei da Assíria trouxe pessoas da Babilônia, de Cuthah, de Avva, e de Hamath e Sefarvaim, e as colocou nas cidades de Samaria ao invés das crianças de Israel; e elas possuíam Samaria e viviam em suas cidades.
25 Wakati walianza kuishi humo, hawakumwabudu Bwana, kwa hiyo akatuma simba miongoni mwao, wakawaua baadhi ya watu.
Então foi, no início de sua residência lá, que eles não temiam Yahweh. Portanto, Javé enviou leões entre eles, o que matou alguns deles.
26 Habari ikapelekwa kwa mfalme wa Ashuru, kusema: “Watu uliowahamisha na kuwaweka katika miji ya Samaria hawajui kile Mungu wa nchi hiyo anachokitaka. Ametuma simba miongoni mwao, ambao wanawaua, kwa sababu watu hawajui anachokitaka.”
Portanto, eles falaram ao rei da Assíria, dizendo: “As nações que vocês levaram e colocaram nas cidades de Samaria não conhecem a lei do deus da terra”. Por isso ele enviou leões entre eles; e eis que os matam, porque não conhecem a lei do deus da terra”.
27 Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru hivi: “Mtwae mmoja wa makuhani uliowachukua mateka kutoka Samaria ili arudi kuishi humo na awafundishe watu kile ambacho Mungu wa nchi anataka.”
Então o rei da Assíria ordenou, dizendo: “Levai ali um dos sacerdotes que de lá trouxestes; e deixai-o ir e habitar ali, e deixai-o ensinar-lhes a lei do deus da terra”.
28 Basi mmoja wa makuhani ambaye alikuwa amepelekwa uhamishoni kutoka Samaria akaja kuishi Betheli na kuwafundisha jinsi ya kumwabudu Bwana.
Então um dos sacerdotes que eles haviam levado de Samaria veio e viveu em Betel, e lhes ensinou como deveriam temer a Iavé.
29 Hata hivyo, kila kikundi cha taifa lililoletwa Samaria kilitengeneza miungu yao wenyewe katika miji kadhaa mahali walipoishi, nao wakaiweka mahali pa ibada za miungu ambapo watu wa Samaria walikuwa wametengeneza katika mahali pa juu.
However cada nação fez seus próprios deuses e os colocou nas casas dos lugares altos que os samaritanos tinham feito, cada nação em suas cidades em que viviam.
30 Watu kutoka Babeli wakamtengeneza Sukoth-Benothi kuwa mungu wao, watu kutoka Kutha wakamtengeneza Nergali, na watu kutoka Hamathi wakamtengeneza Ashima;
Os homens da Babilônia fizeram Succoth Benoth, e os homens de Cuth fizeram Nergal, e os homens de Hamath fizeram Ashima,
31 Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki, nao Wasefarvi wakachoma watoto wao kama kafara kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.
e os Avvitas fizeram Nibhaz e Tartak; e os Sefarvitas queimaram seus filhos no fogo a Adrammelech e Anammelech, os deuses de Sefarvaim.
32 Walimwabudu Bwana, lakini pia waliteua aina zote za watu wao ili kuwawakilisha kama makuhani katika mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu pa ibada.
Então eles temiam Yahweh, e também fizeram entre si sacerdotes dos altos lugares para si, que se sacrificaram por eles nas casas dos altos lugares.
33 Walimwabudu Bwana, lakini pia waliitumikia miungu yao kulingana na desturi za mataifa walikotoka.
Eles temiam a Iavé, e também serviam a seus próprios deuses, depois dos caminhos das nações das quais haviam sido transportados.
34 Mpaka leo wanashikilia desturi zao za zamani. Hawamwabudu Bwana wala kuzishika hukumu na maagizo, sheria na amri ambazo Bwana aliwapa uzao wa Yakobo, ambaye alimwita Israeli.
Até hoje, eles fazem o que faziam antes. Eles não temem a Javé, e não seguem os estatutos, ou as ordenanças, ou a lei, ou o mandamento que Javé ordenou aos filhos de Jacó, a quem deu o nome de Israel;
35 Wakati Bwana alipofanya Agano na Waisraeli, aliwaamuru akisema: “Msiiabudu miungu mingine yoyote wala kuisujudia, wala kuitumikia wala kuitolea dhabihu.
com quem Javé fez um pacto e os ordenou, dizendo: “Não temereis outros deuses, nem vos inclinareis diante deles, nem os servireis, nem lhes sacrificareis”;
36 Bali imewapasa kumwabudu Bwana aliyewapandisha kutoka Misri kwa uwezo wake mkuu na kwa mkono wake ulionyooshwa. Kwake yeye mtasujudu na kwake yeye mtatoa dhabihu.
mas temereis a Javé, que vos tirou da terra do Egito com grande poder e com um braço estendido, e vos inclinareis diante dele, e lhe sacrificareis”.
37 Imewapasa daima kuwa waangalifu kutunza hukumu na maagizo, sheria na amri alizowaandikia. Msiabudu miungu mingine.
Os estatutos e as ordenanças, e a lei e o mandamento que ele escreveu para vós, observareis para fazer sempre mais. Não temerás outros deuses.
38 Msisahau agano nililofanya nanyi, wala msiabudu miungu mingine.
Não vos esquecereis do pacto que fiz convosco. Não temerás os outros deuses.
39 Bali, mtamwabudu Bwana Mungu wenu, kwani yeye ndiye atakayewakomboa kutoka mikononi mwa adui zenu wote.”
Mas temerás a Javé teu Deus, e ele te livrará da mão de todos os teus inimigos”.
40 Hata hivyo hawakusikiliza, lakini waliendelea na desturi zao za awali.
Entretanto, eles não ouviram, mas fizeram o que fizeram antes.
41 Hata wakati watu hawa walipokuwa wanamwabudu Bwana, walikuwa bado wakitumikia sanamu zao. Mpaka leo watoto wao na watoto wa watoto wao wanaendelea kufanya kama baba zao walivyofanya.
Então estas nações temiam Yahweh, e também serviram suas imagens gravadas. Seus filhos fizeram o mesmo, assim como os filhos de seus filhos. Eles fazem como seus pais fizeram até hoje.

< 2 Wafalme 17 >