< 2 Wafalme 17 >
1 Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Ahazi mfalme wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, akatawala kwa miaka tisa.
En la douzième année du règne d'Achaz, en Juda, Osée, fils d'Ela, commença en Samarie, sur Israël, un règne de neuf ans.
2 Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini si kama wafalme wengine wa Israeli waliomtangulia.
Et il fit le mal aux yeux du Seigneur, mais non comme les rois d'Israël qui avaient existé avant lui.
3 Mfalme Shalmanesa wa Ashuru akainuka dhidi ya Mfalme Hoshea, ambaye hapo mbeleni alikuwa mtumwa wake na kumlipa ushuru.
Salmanasar, roi des Assyriens, marcha contre lui; Osée lui fut asservi, et il lui paya un tribut.
4 Lakini mfalme wa Ashuru akagundua kuwa Hoshea alikuwa msaliti, kwa kuwa alikuwa ametuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri, naye hakuendelea kulipa ushuru kwa mfalme wa Ashuru tena kama alivyokuwa anafanya kila mwaka. Kwa hiyo Shalmanesa akamkamata na kumtia gerezani.
Ensuite, Salmanasar trouva en Osée une iniquité, en ce qu'il avait envoyé des messagers à Ségor, roi d'Égypte, et n'avait point payé cette année-là le tribut au roi des Assyriens; et celui-ci l'assiégea et le jeta, enchaîné, dans une prison.
5 Mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akapigana dhidi ya Samaria na kuizunguka kwa majeshi miaka mitatu.
Puis, il parcourut toute la terre d'Israël, et monta à Samarie, qu'il assiégea trois ans.
6 Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaiteka Samaria na kuwahamishia Waisraeli huko Ashuru. Akawaweka huko Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
Ce fut en la neuvième année du règne d'Osée, que Salmanasar prit Samarie, et transporta Israël en Assyrie, où il l'établit en Hala, en Habor, sur le fleuve Gozan, et sur les montagnes des Mèdes.
7 Yote haya yalitokea kwa sababu Waisraeli walikuwa wametenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wao, ambaye alikuwa amewapandisha kutoka Misri akiwatoa chini ya utawala wa nguvu wa Farao mfalme wa Misri. Waliabudu miungu mingine
Et cela arriva, parce que les fils d'Israël avaient péché contre le Seigneur leur Dieu, qui les avait tirés de l'Égypte, et délivrés des mains du roi Pharaon; parce qu'ils avaient craint d'autres dieux.
8 na kufuata desturi za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao, pamoja na desturi ambazo wafalme wa Israeli walizileta.
Car ils avaient marché dans les voies des nations que le Seigneur avait exterminées devant les fils d'Israël, et dans celles des rois d'Israël qui avaient fait de tels péchés,
9 Waisraeli wakafanya vitu kwa siri dhidi ya Bwana Mungu wao, ambavyo havikuwa sawa. Kuanzia kwenye mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye maboma walijijengea wenyewe mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji yao yote.
Et dans celles des enfants d'Israël, adonnés à des coutumes qui n'étaient point selon le Seigneur leur Dieu; ils s'étaient bâti des hauts lieux en toutes les villes, depuis les tours des guetteurs jusqu'aux cités entourées de remparts.
10 Wakaweka mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda.
Et ils s'étaient dressé des colonnes dans des bois sacrés sur toutes les hautes collines, et sous tous les arbres touffus.
11 Wakafukiza uvumba kila mahali palipoinuka, kama yalivyofanya yale mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao. Wakafanya mambo maovu ambayo yalimghadhibisha Bwana.
Et ils avaient fait des sacrifices sur tous les hauts lieux, comme les nations que le Seigneur avait expulsées de devant leur face; ils avaient formé de honteuses associations, ils avaient gravé des images pour irriter le Seigneur.
12 Wakaabudu sanamu, ingawa Bwana alikuwa amesema, “Msifanye mambo haya.”
Et ils avaient servi des idoles au sujet desquelles le Seigneur leur avait dit: Ne faites point cette offense au Seigneur.
13 Bwana akawaonya Israeli na Yuda kupitia kwa manabii na waonaji wake wote: “Acheni njia zenu mbaya. Shikeni amri na maagizo yangu, kufuatana na sheria yangu yote niliyowaagiza baba zenu kuitii ambayo niliileta kwenu kupitia kwa watumishi wangu manabii.”
Cependant, le Seigneur protestait en Israël et en Juda par la bouche de tous ses voyants et de tous ses prophètes, disant: Détournez-vous de vos mauvaises voies, observez mes commandements et mes préceptes; suivez en toutes choses la loi que j'ai donnée à vos pères, et tout ce que je leur ai mandé par mes serviteurs les prophètes.
14 Lakini hawakusikiliza, walikuwa na shingo ngumu kama baba zao, ambao hawakumtegemea Bwana Mungu wao.
Mais ils ne l'écoutaient point; ils s'endurcissaient le cœur plus que ne l'avaient fait leurs pères.
15 Walizikataa amri zake, na agano alilokuwa amelifanya na baba zao, na maonyo aliyokuwa amewapa. Wakafuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai. Wakayaiga mataifa yaliyowazunguka, ingawa Bwana alikuwa amewaonya akiwaambia, “Msifanye kama wanavyofanya,” nao wakafanya mambo ambayo Bwana alikuwa amewakataza wasifanye.
Ils ne gardaient aucun des témoignages que portait le Seigneur; ils marchaient à la suite des vanités, étant vains eux-mêmes; à la suite des nations qui les entouraient, au sujet desquelles le Seigneur leur avait dit: Ne faites pas comme elles.
16 Wakayaacha maagizo yote ya Bwana Mungu wao na kujitengenezea sanamu mbili, walizozisubu katika sura ya ndama na nguzo ya Ashera. Wakasujudia mianga yote ya angani, na wakamtumikia Baali.
Ils abandonnaient les commandements du Seigneur leur Dieu; ils s'étaient fait deux génisses jetées en fonte; ils plantaient des bois sacrés; ils adoraient toute l'armée du ciel, et ils servaient Baal.
17 Wakawatoa kafara wana wao na mabinti zao katika moto. Wakafanya uaguzi na uchawi, nao wakajiuza wenyewe katika kutenda uovu machoni pa Bwana, wakamghadhibisha.
Et ils faisaient passer dans la flamme de Moloch leurs fils et leurs filles; ils usaient de la divination et des présages, et ils s'attachaient à faire le mal aux yeux du Seigneur et à l'irriter.
18 Basi Bwana akawakasirikia sana Israeli na kuwaondoa kwenye uwepo wake. Ni kabila la Yuda tu lililobaki;
Et le Seigneur conçut un grand courroux contre Israël; il le rejeta de devant sa face, et il ne resta que la seule tribu de Juda.
19 na hata hivyo nao Yuda hawakuzishika amri za Bwana Mungu wao. Wakafuata desturi ambazo Israeli walikuwa wamezianzisha.
Et Juda lui-même n'observa point les commandements du Seigneur son Dieu; il marcha dans les voies d'Israël, et il répudia le Seigneur.
20 Kwa hiyo Bwana aliwakataa watu wote wa Israeli; akawatesa na kuwaachia katika mikono ya wateka nyara hadi alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake.
Et le Seigneur se courrouça contre toute la race d'Israël; il les ébranla, il les livra à tous ceux qui vinrent les piller, jusqu'à ce. qu'il les rejetât de devant sa face.
21 Alipokwisha kuwatenga Israeli mbali na nyumba ya Daudi, wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme wao. Yeroboamu akawashawishi Israeli waache kumfuata Bwana na akawasababisha kutenda dhambi kuu.
Il le fit surtout parce qu'Israël ayant rejeté la maison de David, et s'étant donné pour roi Jéroboam, fils de Nabat, Jéroboam entraîna Israël hors des voies du Seigneur, et lui fit commettre un grand péché.
22 Nao Israeli wakadumu katika dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati, nao hawakuziacha
Car, les fils d'Israël tombèrent tous dans le péché de Jéroboam, et ils ne s'en retirèrent point,
23 hadi Bwana alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake, kama vile alivyokuwa ameonya kupitia watumishi wake wote manabii. Hivyo watu wa Israeli wakaondolewa kutoka nchi yao kwenda uhamishoni Ashuru, nao wako huko mpaka sasa.
Jusqu'à ce que le Seigneur eût expulsé Israël de devant sa face, comme il l'en avait menacé par la voix de tous ses serviteurs les prophètes. Et Israël fut emmené en la terre des Assyriens, où il est encore de nos jours.
24 Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli, Kutha, Ava, Hamathi na Sefarvaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria badala ya Waisraeli. Wakaimiliki Samaria na kuishi katika miji yake.
Ensuite, le roi des Assyriens amena des hommes de Babylone, de Chuth, d'Aïa, d'Emath, de Sepharvaïm, et il les établit en Samarie à la place des fils d'Israël; ils se partagèrent son territoire, et ils demeurèrent dans ses villes.
25 Wakati walianza kuishi humo, hawakumwabudu Bwana, kwa hiyo akatuma simba miongoni mwao, wakawaua baadhi ya watu.
Dans les premiers temps de leur séjour, ils ne craignaient point le Seigneur, et le Seigneur envoya contre eux des lions qui en tuèrent quelques- uns.
26 Habari ikapelekwa kwa mfalme wa Ashuru, kusema: “Watu uliowahamisha na kuwaweka katika miji ya Samaria hawajui kile Mungu wa nchi hiyo anachokitaka. Ametuma simba miongoni mwao, ambao wanawaua, kwa sababu watu hawajui anachokitaka.”
Ils le firent savoir au roi des Assyriens, disant: Les nations que tu as transportées et assises dans les villes de Samarie, ne connaissaient point les jugements du Dieu de cette terre; et il a envoyé contre eux des lions; et voilà que ces lions les tuent, parce qu'ils ne savent pas les jugements du Dieu de cette terre.
27 Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru hivi: “Mtwae mmoja wa makuhani uliowachukua mateka kutoka Samaria ili arudi kuishi humo na awafundishe watu kile ambacho Mungu wa nchi anataka.”
Et le roi des Assyriens donna ses ordres, disant: Emmenez d'ici des gens, qu'ils partent, qu'ils demeurent avec vous; ils vous éclaireront sur les jugements du Dieu de cette terre.
28 Basi mmoja wa makuhani ambaye alikuwa amepelekwa uhamishoni kutoka Samaria akaja kuishi Betheli na kuwafundisha jinsi ya kumwabudu Bwana.
Et ils emmenèrent un des prêtres qu'on avait transportés de Samarie; il s'établit à Béthel; il les éclaira, et il leur apprit comme ils devaient craindre le Seigneur.
29 Hata hivyo, kila kikundi cha taifa lililoletwa Samaria kilitengeneza miungu yao wenyewe katika miji kadhaa mahali walipoishi, nao wakaiweka mahali pa ibada za miungu ambapo watu wa Samaria walikuwa wametengeneza katika mahali pa juu.
Mais, chaque nation fabriqua ses dieux; on les plaça dans les temples des hauts lieux que les Samaritains avaient construits; chaque nation eut les siens dans les villes qu'elle habitait.
30 Watu kutoka Babeli wakamtengeneza Sukoth-Benothi kuwa mungu wao, watu kutoka Kutha wakamtengeneza Nergali, na watu kutoka Hamathi wakamtengeneza Ashima;
Ceux de Babylone avaient fabriqué Soccoth-Benith; ceux de Chuth, Ergel; ceux d'Emath, Asimath;
31 Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki, nao Wasefarvi wakachoma watoto wao kama kafara kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.
Les Evéens fabriquèrent Eblazer et Tharthac; ceux de Sepharvaïm firent le mal quand ils brûlèrent leurs fils dans les flammes d'Adra-Moloch et d'Ana- Moloch, leurs dieux.
32 Walimwabudu Bwana, lakini pia waliteua aina zote za watu wao ili kuwawakilisha kama makuhani katika mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu pa ibada.
Ils craignaient le Seigneur; mais ils avaient établi leurs abominations dans les temples des hauts lieux qu'avaient construits les Samaritains, chacun dans la ville que sa nation habitait; ils craignaient le Seigneur; mais ils avaient institué pour eux des prêtres des hauts lieux, et ils sacrifiaient dans les temples des hauts lieux.
33 Walimwabudu Bwana, lakini pia waliitumikia miungu yao kulingana na desturi za mataifa walikotoka.
Ils craignaient le Seigneur, mais ils servirent leurs dieux selon l'usage des nations dont ils avaient été tirés.
34 Mpaka leo wanashikilia desturi zao za zamani. Hawamwabudu Bwana wala kuzishika hukumu na maagizo, sheria na amri ambazo Bwana aliwapa uzao wa Yakobo, ambaye alimwita Israeli.
Jusqu'à ce jour, ils ont agi selon leurs usages; les mêmes gens craignent le Seigneur et agissent selon leurs mœurs, selon leurs usages, et en même temps selon la loi et les préceptes que le Seigneur a donnés aux fils de Jacob, qu'il a appelé aussi Israël;
35 Wakati Bwana alipofanya Agano na Waisraeli, aliwaamuru akisema: “Msiiabudu miungu mingine yoyote wala kuisujudia, wala kuitumikia wala kuitolea dhabihu.
Avec qui le Seigneur fit jadis alliance, disant: Vous ne craindrez point d'autres dieux, vous ne les adorerez pas, vous ne les servirez point, vous ne leur ferez point de sacrifices.
36 Bali imewapasa kumwabudu Bwana aliyewapandisha kutoka Misri kwa uwezo wake mkuu na kwa mkono wake ulionyooshwa. Kwake yeye mtasujudu na kwake yeye mtatoa dhabihu.
Vous ne craindrez, vous n'adorerez, vous n'honorerez par des sacrifices que le Seigneur qui vous a ramenés d'Égypte par sa toute-puissance, et par son bras très-haut.
37 Imewapasa daima kuwa waangalifu kutunza hukumu na maagizo, sheria na amri alizowaandikia. Msiabudu miungu mingine.
Vous observerez toujours les ordonnances, les jugements, la loi et les commandements qu'il a écrits, pour que vous les pratiquiez; vous ne craindrez point d'autres dieux.
38 Msisahau agano nililofanya nanyi, wala msiabudu miungu mingine.
Et vous n'abandonnerez point l'alliance qu'il a faite avec vous, et vous ne craindrez point d'autres dieux;
39 Bali, mtamwabudu Bwana Mungu wenu, kwani yeye ndiye atakayewakomboa kutoka mikononi mwa adui zenu wote.”
Vous ne craindrez que le Seigneur votre Dieu, et il vous délivrera de tous vos ennemis;
40 Hata hivyo hawakusikiliza, lakini waliendelea na desturi zao za awali.
Vous ne suivrez point les pratiques que suivent les Gentils.
41 Hata wakati watu hawa walipokuwa wanamwabudu Bwana, walikuwa bado wakitumikia sanamu zao. Mpaka leo watoto wao na watoto wa watoto wao wanaendelea kufanya kama baba zao walivyofanya.
Ces nations nouvelles craignaient donc le Seigneur, et elles servaient leurs idoles; et leurs fils, et les fils de leurs fils, ont fait comme leurs pères jusqu'à nos jours.