< 2 Wafalme 16 >

1 Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
W siedemnastym roku Pekacha, syna Remaliasza, Achaz, syn Jotama, króla Judy, [zaczął] królować.
2 Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana, Mungu wake.
Achaz miał dwadzieścia lat, kiedy zaczął królować, i królował szesnaście lat w Jerozolimie, ale nie czynił tego, co słuszne w oczach PANA, swego Boga, jak Dawid, jego ojciec;
3 Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na hata akamtoa mwanawe kafara katika moto, akifuata njia za machukizo za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli.
Lecz chodził drogami królów Izraela, a nawet swojego syna przeprowadził przez ogień według obrzydliwości pogan, których PAN wypędził sprzed oblicza synów Izraela.
4 Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.
Składał ofiary i palił kadzidło na wyżynach, na pagórkach i pod każdym zielonym drzewem.
5 Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda.
Wtedy Resin, król Syrii, i Pekach, syn Remaliasza, król Izraela, wyruszyli na wojnę przeciw Jerozolimie i oblegli Achaza, ale nie mogli go pokonać.
6 Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi, nao wanaishi huko mpaka leo.
W tym samym czasie Resin, król Syrii, przywrócił Syrii Elat i wypędził Żydów z Elat, a Syryjczycy przybyli do Elat i mieszkają tam aż do dziś.
7 Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli, ambao wananishambulia.”
Achaz więc wysłał posłańców do Tiglat-Pilesera, króla Asyrii, ze słowami: Jestem twoim sługą i twoim synem. Przyjdź i wybaw mnie z ręki króla Syrii i z ręki króla Izraela, którzy powstali przeciw mnie.
8 Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme, na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru.
Wtedy Achaz wziął srebro i złoto, które znajdowały się w domu PANA i w skarbcach domu królewskiego, i posłał [je jako] dar królowi Asyrii.
9 Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumuua Resini.
I król Asyrii wysłuchał go. Wyruszył bowiem król Asyrii przeciw Damaszkowi, zdobył go i uprowadził jego [mieszkańców] do Kir, a Resina zabił.
10 Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaona madhabahu huko Dameski, naye akamtumia Uria kuhani mchoro wa hayo madhabahu, pamoja na maelezo ya mpango kamili wa ujenzi wake.
Potem król Achaz udał się do Damaszku na spotkanie z Tiglat-Pilserem, królem Asyrii. Gdy zobaczył w Damaszku ołtarz, król Achaz posłał do kapłana Uriasza wzór tego ołtarza i cały plan jego budowy.
11 Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski, na akamaliza ujenzi kabla ya Mfalme Ahazi kurudi.
I kapłan Uriasz zbudował ołtarz dokładnie według tego, co król Achaz przesłał z Damaszku. Tak to uczynił kapłan Uriasz, zanim król Achaz wrócił z Damaszku.
12 Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuona hayo madhabahu, akayasogelea na kutoa sadaka juu yake.
A gdy król wrócił z Damaszku, zobaczył ołtarz, zbliżył się do niego i złożył na nim ofiary.
13 Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hayo madhabahu.
Spalił swoje całopalenie i ofiarę z pokarmów, wylał swoją ofiarę z płynów i pokropił ołtarz krwią swoich ofiar pojednawczych.
14 Mfalme Ahazi akayaondoa madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu la Bwana, yaliyokuwa yamesimama kati ya ingilio la Hekalu na hayo madhabahu mapya, naye akayaweka upande wa kaskazini mwa hayo madhabahu mapya.
Ołtarz zaś z brązu, który był przed PANEM, przeniósł z przedniej części domu, gdzie znajdował się między ołtarzem a domem PANA, i postawił go po północnej stronie ołtarza.
15 Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa Uria kuhani: “Juu ya hayo madhabahu kubwa mapya, toa sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hayo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hayo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.”
Król Achaz rozkazał też kapłanowi Uriaszowi: Na wielkim ołtarzu będziesz palił poranną ofiarę całopalną i wieczorną ofiarę z pokarmów, [a także] całopalną ofiarę króla i jego ofiarę z pokarmów oraz całopalną ofiarę całego ludu ziemi, ich ofiarę z pokarmów i ich ofiary z płynów. Będziesz też kropił na nim wszelką krwią całopalenia i wszelką krwią z ofiar [krwawych], ale ołtarz z brązu będzie dla mnie do szukania rady.
16 Naye Uria kuhani akafanya kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.
I kapłan Uriasz uczynił wszystko zgodnie z tym, jak rozkazał król Achaz.
17 Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vilivyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia, na kuiweka kwenye kitako cha jiwe.
Król Achaz odciął też listwy podstawek i wyjął z nich kadzie. Zdjął również morze sponad wołów z brązu, które pod nim były, a postawił je na posadzce kamiennej.
18 Kwa heshima ya mfalme wa Ashuru, akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu, na akaondoa ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu la Bwana.
Zadaszenie na szabat, które zbudowano w domu, oraz zewnętrzne wejście królewskie usunął z domu PANA ze względu na króla Asyrii.
19 Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
A pozostałe dzieje Achaza, które czynił, są zapisane w księdze kronik królów Judy.
20 Ahazi akalala na baba zake, naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.
I Achaz zasnął ze swymi ojcami, i został pogrzebany z nimi w mieście Dawida. A Ezechiasz, jego syn, królował w jego miejsce.

< 2 Wafalme 16 >