< 2 Wafalme 16 >

1 Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
In yac aksingoul itkosr ke pacl Tokosra Pekah wen natul Remaliah, el leum in Israel, Ahaz wen natul Jotham, el tokosrala lun Judah
2 Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana, Mungu wake.
ke el yac longoul, ac el leum in Jerusalem ke yac singoul onkosr. El tiana fahsr tukun srikasrak wo lun Tokosra David papa matu tumal, a el fahsr tukun ma su tia akinsewowoye LEUM GOD lal,
3 Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na hata akamtoa mwanawe kafara katika moto, akifuata njia za machukizo za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli.
ac el fahsr tukun ouiya koluk ma tokosra Israel elos oru. El sifacna kisakunla pac wen se natul in mwe kisa firir nu sin ma sruloala, ac etai lumah koluk lun mwet su LEUM GOD El tuh lusla liki acn inge ke pacl se mwet Israel elos utyak nu we.
4 Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.
Ahaz el orek kisa ac akosak mwe keng ke nien alu lun mwet pegan, su oan fin inging uh ac ye sak lul nukewa.
5 Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda.
Tokosra Resin lun Syria ac Tokosra Pekah lun Israel eltal mweuni acn Jerusalem, ac kuhlusya acn we, tuh tiana ku in kutangulla Ahaz.
6 Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi, nao wanaishi huko mpaka leo.
(In pacl sac pacna tokosra lun Edom el sifilpa eisla siti Elath, ac lusla mwet Judea su muta we. Mwet Edom elos oakwuki in siti Elath ac elos srakna muta we.)
7 Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli, ambao wananishambulia.”
Ahaz el supwala mwet nu yorol Tiglath Pileser, Tokosra Fulat lun Assyria, ac fahk kas inge: “Nga mwet kulansap oaru lom. Fahsru moliyula liki tokosra lun Syria ac Israel su mweun lainyu.”
8 Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme, na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru.
Ahaz el eis gold ac silver liki Tempul ac liki nien fil mwe kasrup inkul sin tokosra, ac supwala in mwe lung nu sin Tokosra Fulat sac.
9 Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumuua Resini.
Tiglath Pileser el illa wi mwet mweun lal in oana siyuk lal Ahaz. El mweuni ac sruokya acn Damascus, na el unilya Tokosra Rezin, ac usla mwet Damascus nu Kir in mwet sruoh we.
10 Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaona madhabahu huko Dameski, naye akamtumia Uria kuhani mchoro wa hayo madhabahu, pamoja na maelezo ya mpango kamili wa ujenzi wake.
Ke Tokosra Ahaz el som nu Damascus in osun nu sel Tokosra Fulat Tiglath Pileser, el tuh liye loang se we, na el sruloala luman loang se inge, ac srikeya ip srisrik nukewa kac, ac supwala nu sel Uriah, mwet tol.
11 Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski, na akamaliza ujenzi kabla ya Mfalme Ahazi kurudi.
Ouinge Uriah el musaela sie loang oana luman loang sac, ac aksafyela meet liki Ahaz el foloko.
12 Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuona hayo madhabahu, akayasogelea na kutoa sadaka juu yake.
Ke Ahaz el foloko liki acn Damascus el liye lah loang sac safla tari,
13 Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hayo madhabahu.
na el esukak mwe kisa firir ac mwe kisa wheat fin loang sac, ac el okoaung pac mwe kisa wain oayapa srah ke mwe kisa in akinsewowo nu fac.
14 Mfalme Ahazi akayaondoa madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu la Bwana, yaliyokuwa yamesimama kati ya ingilio la Hekalu na hayo madhabahu mapya, naye akayaweka upande wa kaskazini mwa hayo madhabahu mapya.
Loang bronze se ma kisakinyukla tari nu sin LEUM GOD ah oan inmasrlon loang sasu sac ac Tempul. Ouinge Ahaz el moklela nu layen epang in loang sasu se lal ah.
15 Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa Uria kuhani: “Juu ya hayo madhabahu kubwa mapya, toa sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hayo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hayo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.”
Na el sapkin nu sel Uriah ac fahk, “Orekmakin loang lulap se luk inge in orek mwe kisa firir ke lotutang, ac mwe kisa wheat ke ekela, oayapa nu ke mwe kisa firir ac mwe kisa wheat lun tokosra ac lun mwet uh, ac nu ke mwe kisa wain. Okoaung srahn kosro kisakinyukla nukewa nu fac. Tusruktu likiya loang bronze sac ngan orekmakin nu ke alyalu luk sifacna.”
16 Naye Uria kuhani akafanya kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.
Na Uriah el oru oana ma tokosra el sapkin.
17 Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vilivyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia, na kuiweka kwenye kitako cha jiwe.
Tokosra Ahaz el tuleya mwe wiwa ma orekla ke bronze su orekmakinyuk in Tempul, ac eisla pesin nukewa ma oan fac. El oayapa eisla tacng bronze se ma oan fintukun cow mukul bronze singoul lukwa, ac oakiya fin pwelung se orekla ke eot.
18 Kwa heshima ya mfalme wa Ashuru, akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu, na akaondoa ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu la Bwana.
In akinsewowoye Tokosra Fulat lun Assyria, Ahaz el oayapa moklela nien tu se ma oan in Tempul su ma nu ke tron lun tokosra, ac kaliya nien utyak se lal tokosra nu in Tempul.
19 Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Ma nukewa saya ma Tokosra Ahaz el orala, simla oasr in [Sramsram Matu Ke Tokosra Lun Judah].
20 Ahazi akalala na baba zake, naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Ahaz el misa ac pukpuki inkulyuk lun tokosra in Siti sel David, ac Hezekiah wen natul, el aolul in tokosra.

< 2 Wafalme 16 >