< 2 Wafalme 16 >

1 Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
En la dix-septième année du règne de Phacée, fils de Romélie, Achaz, fils de Joatham, devint roi de Juda.
2 Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana, Mungu wake.
Il avait vingt ans quand il monta sur le trône, et il régna seize ans à Jérusalem; il ne fit point ce qui est droit aux yeux du Seigneur son Dieu, aussi fidèlement que David, son aïeul.
3 Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na hata akamtoa mwanawe kafara katika moto, akifuata njia za machukizo za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli.
Et il marcha dans la voie des rois d'Israël; même il livra son fils aux flammes de Moloch, selon l'abomination des peuples que le Seigneur avait exterminés devant la face des fils d'Israël.
4 Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.
Et il immola des victimes sur les hauts lieux, sur les collines, et sous tout arbre touffu.
5 Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda.
Alors, Rasin, roi de Syrie, et Phacée, roi d'Israël, vinrent combattre sous les murs de Jérusalem; ils assiégèrent Achaz, mais ils ne purent prévaloir sur lui.
6 Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi, nao wanaishi huko mpaka leo.
En temps-là, Rasin reprit Elath pour la Syrie, il en chassa les Juifs, et des Iduméens y vinrent; et ils y sont demeurés jusqu'à nos jours.
7 Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli, ambao wananishambulia.”
Et Achaz envoya des messagers à Theglath-Phalasar, roi des Assyriens, disant: Moi et mon fils, nous sommes tes serviteurs; viens, sauve-moi des mains du roi de Syrie, et des mains du roi d'Israël, qui se sont levés contre moi.
8 Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme, na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru.
Achaz prit l'argent et l'or qui se trouva dans les trésors, soit du temple, soit du palais, et il en fit présent au roi d'Assyrie.
9 Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumuua Resini.
Et le roi des Assyriens l'écouta; il marcha sur Damas, la prit, la dépeupla, et mit à mort le roi Rasin.
10 Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaona madhabahu huko Dameski, naye akamtumia Uria kuhani mchoro wa hayo madhabahu, pamoja na maelezo ya mpango kamili wa ujenzi wake.
Et le roi Achaz alla dans Damas à la rencontre de Theglath-Phalasar; il vit un autel à Damas, et il envoya au prêtre Urie l'image de l'autel, ses proportions, sa structure.
11 Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski, na akamaliza ujenzi kabla ya Mfalme Ahazi kurudi.
Et le prêtre Urie bâtit un autel selon le modèle que le roi lui avait envoyé de Damas.
12 Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuona hayo madhabahu, akayasogelea na kutoa sadaka juu yake.
Puis, Achaz vit l'autel et il y monta;
13 Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hayo madhabahu.
Il fit son holocauste, son sacrifice et sa libation, et il répandit le sang de ses hosties pacifiques offertes sur l'autel
14 Mfalme Ahazi akayaondoa madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu la Bwana, yaliyokuwa yamesimama kati ya ingilio la Hekalu na hayo madhabahu mapya, naye akayaweka upande wa kaskazini mwa hayo madhabahu mapya.
D'airain qui était devant le Seigneur. Et il transporta cet autel de devant la façade du temple, du lieu entre l'autel et le temple, et il le dressa du même côté en tirant vers le nord.
15 Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa Uria kuhani: “Juu ya hayo madhabahu kubwa mapya, toa sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hayo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hayo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.”
Ensuite, le roi Achaz donna ses ordres au prêtre Urie, disant: Tu présenteras, sur le grand autel, l'holocauste du matin, les oblations du soir, l'holocauste du roi et son oblation, l'holocauste de tout le peuple, et son oblation et sa libation; tu répandras sur le même autel tout le sang de l'holocauste et tout le sang de toute autre victime, et l'autel d'airain le matin me sera réservé.
16 Naye Uria kuhani akafanya kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.
Et Urie le prêtre fit tout ce que lui avait prescrit le roi Achaz.
17 Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vilivyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia, na kuiweka kwenye kitako cha jiwe.
Le roi Achaz effaça les ciselures des bassins, il enleva les cuvettes qu'ils supportaient, et il ôta, pour la mettre sur une base de pierre, la mer qui reposait sur les bœufs d'airain.
18 Kwa heshima ya mfalme wa Ashuru, akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu, na akaondoa ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu la Bwana.
Et il construisit une base pour le trône dans le temple du Seigneur, et il transporta à l'intérieur la porte extérieure par laquelle le roi entrait dans le temple, à cause du roi des Assyriens.
19 Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Quant au reste de l'histoire du roi Achaz, n'est-il pas écrit au livre des Faits et gestes des rois de Juda?
20 Ahazi akalala na baba zake, naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Achaz s'endormit avec ses pères; il fut enseveli dans la ville de David, et son fils Ezéchias régna à sa place.

< 2 Wafalme 16 >