< 2 Wafalme 16 >

1 Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
The seuenteenth yeere of Pekah the sonne of Remaliah, Ahaz the sonne of Iotham King of Iudah began to reigne.
2 Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana, Mungu wake.
Twentie yeere olde was Ahaz, when hee began to reigne, and he reigned sixteene yeere in Ierusalem, and did not vprightly in the sight of the Lord his God, like Dauid his father:
3 Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na hata akamtoa mwanawe kafara katika moto, akifuata njia za machukizo za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli.
But walked in the way of ye kings of Israel, yea, and made his sonne to go through the fire, after the abominations of the heathen, whom the Lord had cast out before the children of Israel.
4 Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.
Also he offred and burnt incense in the hie places and on the hilles, and vnder euery greene tree.
5 Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda.
Then Rezin king of Aram and Pekah sonne of Remaliah King of Israel came vp to Ierusalem to fight: and they besieged Ahaz, but could not ouercome him.
6 Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi, nao wanaishi huko mpaka leo.
At the same time Rezin king of Aram restored Elath to Aram, and droue the Iewes from Elath: so the Aramites came to Elath, and dwelt there vnto this day.
7 Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli, ambao wananishambulia.”
Then Ahaz sent messengers to Tiglath Pileser king of Asshur, saying, I am thy seruant and thy sonne: come vp, and deliuer me out of the hand of the king of Aram, and out of the hand of the King of Israel which rise vp against me.
8 Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme, na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru.
And Ahaz tooke the siluer and the golde that was found in the house of the Lord, and in the treasures of the Kings house, and sent a present vnto the King of Asshur.
9 Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumuua Resini.
And the King of Asshur consented vnto him: and the King of Asshur went vp against Damascus. and when he had taken it, he caryed the people away to Kir, and slew Rezin.
10 Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaona madhabahu huko Dameski, naye akamtumia Uria kuhani mchoro wa hayo madhabahu, pamoja na maelezo ya mpango kamili wa ujenzi wake.
And King Ahaz went vnto Damascus to meete Tiglath Pileser King of Asshur: and when King Ahaz sawe the altar that was at Damascus, he sent to Vriiah the Priest the paterne of the altar, and the facion of it, and all the workemanship thereof.
11 Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski, na akamaliza ujenzi kabla ya Mfalme Ahazi kurudi.
And Vriiah the Priest made an altar in al poyntes like to that which King Ahaz had sent from Damascus, so did Vriiah the Priest against King Ahaz came from Damascus.
12 Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuona hayo madhabahu, akayasogelea na kutoa sadaka juu yake.
So when the King was come from Damascus, the King sawe the altar: and the King drewe neere to the altar and offered thereon.
13 Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hayo madhabahu.
And hee burnt his burnt offering, and his meate offring, and powred his drinke offring, and sprinkled the blood of his peace offrings besides the altar,
14 Mfalme Ahazi akayaondoa madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu la Bwana, yaliyokuwa yamesimama kati ya ingilio la Hekalu na hayo madhabahu mapya, naye akayaweka upande wa kaskazini mwa hayo madhabahu mapya.
And set it by the brasen altar which was before the Lord, and brought it in farther before the house betweene the altar and the house of the Lord, and set it on the North side of the altar.
15 Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa Uria kuhani: “Juu ya hayo madhabahu kubwa mapya, toa sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hayo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hayo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.”
And King Ahaz commanded Vriiah the Priest, and sayde, Vpon the great altar set on fire in the morning the burnt offring, and in the euen the meate offring, and the Kings burnt offring and his meate offering, with the burnt offring of all the people of the lande, and their meate offring, and their drinke offrings: and powre thereby all the blood of the burnt offring, and all the blood of the sacrifice, and the brasen altar shalbe for me to inquire of God.
16 Naye Uria kuhani akafanya kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.
And Vriiah the Priest did according to all that King Ahaz had commanded.
17 Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vilivyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia, na kuiweka kwenye kitako cha jiwe.
And King Ahaz brake the borders of the bases, and tooke the caldrons from off them, and tooke downe the sea from the brasen oxen that were vnder it, and put it vpon a pauement of stones.
18 Kwa heshima ya mfalme wa Ashuru, akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu, na akaondoa ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu la Bwana.
And the vaile for the Sabbath (that they had made in the house) and the Kings entrie without turned he to the house of the Lord, because of the King of Asshur.
19 Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Concerning the rest of the actes of Ahaz, which he did, are they not written in the booke of the Chronicles of the Kings of Iudah?
20 Ahazi akalala na baba zake, naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Ahaz slept with his fathers, and was buryed with his fathers in the citie of Dauid, and Hezekiah his sonne reigned in his steade.

< 2 Wafalme 16 >