< 2 Wafalme 15 >

1 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
V sedemindvajsetem letu Izraelovega kralja Jerobeáma je začel kraljevati Azarjá, sin Judovega kralja Amacjája.
2 Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
Šestnajst let je bil star, ko je začel kraljevati in v Jeruzalemu je kraljeval dvainpetdeset let. Ime njegove matere je bilo Jehólja iz Jeruzalema.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
Delal je to, kar je bilo pravilno v Gospodovih očeh, glede na vse, kar je delal njegov oče Amacjá,
4 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
razen, da niso bili odstranjeni visoki kraji. Ljudstvo je na visokih krajih še vedno žrtvovalo in zažigalo kadilo.
5 Bwana akampiga mfalme kwa ukoma mpaka siku aliyokufa, naye aliishi katika nyumba iliyotengwa peke yake. Yothamu mwana wa mfalme akawa msimamizi wa jumba la mfalme, na akawatawala watu wa nchi.
Gospod je udaril kralja, tako da je bil gobavec do dneva svoje smrti in prebival v posebni hiši. Kraljev sin Jotám pa je bil nad hišo in sodil ljudstvu dežele.
6 Matukio mengine ya utawala wa Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Ostala Azarjájeva dela in vse, kar je storil, mar niso zapisana v kroniški knjigi Judovih kraljev?
7 Azaria akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika Mji wa Daudi, na Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Tako je Azarjá zaspal s svojimi očeti in v Davidovem mestu so ga pokopali z njegovimi očeti in namesto njega je zakraljeval njegov sin Jotám.
8 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, naye akatawala miezi sita.
V osemintridesetem letu Judovega kralja Azarjá je Jerobeámov sin Zaharija šest mesecev kraljeval nad Izraelom v Samariji.
9 Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama baba zake walivyofanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Počel je to, kar je bilo zlo v Gospodovih očeh, kakor so počeli njegovi očetje. Ni se oddvojil od grehov Nebátovega sina Jerobeáma, ki je Izraela pripravil, da greši.
10 Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya shauri baya dhidi ya Zekaria. Akamshambulia mbele ya watu, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Jabéšov sin Šalúm se je zoper njega zarotil, ga udaril vpričo ljudstva, ga usmrtil in zakraljeval namesto njega.
11 Matukio mengine ya utawala wa Zekaria yameandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Ostala Zaharijeva dela, glej, zapisana so v kroniški knjigi Izraelovih kraljev.
12 Kwa hiyo neno la Bwana lililonenwa kwa Yehu likatimia, kwamba, “Wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
To je bila beseda od Gospoda, ki jo je govoril Jehúju, rekoč: »Tvoji sinovi bodo sedeli na Izraelovem prestolu do četrtega rodu.« In tako se je zgodilo.
13 Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa thelathini na tisa wa Uzia mfalme wa Yuda, naye akatawala katika Samaria kwa mwezi mmoja.
Jabéšov sin Šalúm je začel kraljevati v devetintridesetem letu Judovega kralja Uzíjaha, in cel mesec je kraljeval v Samariji.
14 Kisha Menahemu mwana wa Gadi akaenda kutoka Tirsa mpaka Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi huko Samaria, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Kajti Gadíjev sin Menahém je iz Tirce odšel gor, prišel v Samarijo in v Samariji udaril Jabéševega sina Šalúma, ga umoril in zakraljeval namesto njega.
15 Matukio mengine ya utawala wa Shalumu, na mauaji aliyoyafanya, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Ostala Šalúmova dela in njegova zarota, ki jo je storil, glej, zapisana so v kroniški knjigi Izraelovih kraljev.
16 Wakati ule, akianzia Tirsa, Menahemu alishambulia Tifsa na kila mtu ndani yake, na wale waliokuwa maeneo jirani, kwa sababu walikataa kufungua malango yao. Akaiangamiza Tifsa yote, na kuwapasua matumbo wanawake wote wenye mimba.
Potem je Menahém udaril Tifsáha in vse, ki so bili v njem in njegove pokrajine od Tirce, ker se niso odprli k njemu, zato ga je udaril, in vse ženske, ki so bile v njem, ki so bile z otrokom, je razparal.
17 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, akatawala huko Samaria kwa miaka kumi.
V devetintridesetem letu Judovega kralja Azarjája je nad Izraelom začel kraljevati Gadíjev sin Menahém in v Samariji je kraljeval deset let.
18 Akatenda maovu machoni pa Bwana. Katika wakati wa utawala wake wote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Počel je to, kar je bilo zlo v Gospodovih očeh. Vse svoje dni se ni oddvojil od grehov Nebátovega sina Jerobeáma, ki je Izraela pripravil, da greši.
19 Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaishambulia Israeli. Menahemu mfalme wa Israeli akampa talanta elfu moja za fedha ili amsaidie na kumwezesha katika utawala wake.
Zoper deželo je prišel asirski kralj Pul in Menahém je dal Pulu tisoč talentov srebra, da bi bila njegova roka lahko z njim, da potrdi kraljestvo v njegovi roki.
20 Menahemu akatoza fedha hizi kwa nguvu kutoka kwa Israeli. Kila mtu tajiri alilazimika kuchanga shekeli hamsini za fedha ambazo alipewa mfalme wa Ashuru. Basi mfalme wa Ashuru akajiondoa na hakuendelea kuikalia nchi.
Menahém je od Izraela zahteval denar od vseh mogočnih mož obilja, od vsakega moža petdeset šeklov srebra, da jih dá asirskemu kralju. Tako se je kralj Asirije obrnil nazaj in ni ostal v deželi.
21 Matukio mengine ya utawala wa Menahemu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Ostala Menahémova dela in vse, kar je storil, mar niso zapisana v kroniški knjigi Izraelovih kraljev?
22 Menahemu akalala pamoja na baba zake. Naye Pekahia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Menahém je zaspal s svojimi očeti in namesto njega je zakraljeval njegov sin Pekahjá.
23 Katika mwaka wa hamsini wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, akatawala miaka miwili.
V petdesetem letu Judovega kralja Azarjája je nad Izraelom v Samariji začel kraljevati Menahémov sin Pekahjá in kraljeval je dve leti.
24 Pekahia akafanya uovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Počel je to, kar je bilo zlo v Gospodovih očeh; ni se oddvojil od grehov Nebátovega sina Jerobeáma, ki je Izraela pripravil, da greši.
25 Mmoja wa maafisa wake wakuu, Peka mwana wa Remalia, akafanya shauri baya dhidi yake. Akachukua watu hamsini wa Gileadi pamoja naye, akamuua Pekahia, pamoja na Argobu na Aria, katika ngome ya jumba la kifalme huko Samaria. Kwa hiyo Peka akamuua Pekahia, naye akaingia mahali pake kuwa mfalme.
Toda njegov poveljnik, Remaljájev sin Pékah, se je zarotil zoper njega in ga udaril v Samariji, v palači kraljeve hiše z Argóbom in Arjéjem in z njim petdeset mož izmed Gileádcev, ga ubil in zakraljeval namesto njega.
26 Matukio mengine ya utawala wa Pekahia na yote aliyoyafanya yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Ostala Pekahjájeva dela in vse, kar je storil, glej, ta so zapisana v kroniški knjigi Izraelovih kraljev.
27 Katika mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala miaka ishirini.
V dvainpetdesetem letu Judovega kralja Azarjá je nad Izraelom v Samariji začel kraljevati Remaljájev sin Pékah in kraljeval je dvajset let.
28 Akafanya maovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Počel je to, kar je bilo zlo v Gospodovih očeh. Ni se oddvojil od grehov Nebátovega sina Jerobeáma, ki je Izraela pripravil, da greši.
29 Wakati wa utawala wa Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alikuja na kuteka Iyoni, Abel-Beth-Maaka, Yanoa, Kedeshi na Hazori. Akateka miji ya Gileadi na Galilaya, pamoja na nchi yote ya Naftali, na kuwahamishia watu wote Ashuru.
V dneh Izraelovega kralja Pékaha je prišel asirski kralj Tiglát Piléser in zavzel Ijón, Abél Bet Maáho, Janóah, Kedeš, Hacór, Gileád in Galilejo, vso Neftálijevo deželo in jih ujete odvedel v Asirijo.
30 Kisha Hoshea mwana wa Ela akafanya shauri baya dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akamshambulia na kumuua, kisha akaingia mahali pake kuwa mfalme katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
Elájev sin Hošéa se je zarotil zoper Remaljájevega sina Pékaha, ga udaril, usmrtil in namesto njega zakraljeval v dvajsetem letu Uzíjahovega sina Jotáma.
31 Matukio mengine ya utawala wa Peka na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Ostala Pékahova dela in vse, kar je storil, glej, ta so zapisana v kroniški knjigi Izraelovih kraljev.
32 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Uzia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
V drugem letu Remaljájevega sina Pékaha, Izraelovega kralja, je začel kraljevati Jotám, sin Judovega kralja Uzíjaha.
33 Alikuwa na miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Petindvajset let je bil star, ko je začel kraljevati in v Jeruzalemu je kraljeval šestnajst let. Ime njegove matere je bilo Jerúša, Cadókova hči.
34 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya.
Delal je, kar je bilo pravilno v Gospodovih očeh. Storil je glede na vse, kar je storil njegov oče Uzíjah.
35 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko. Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana.
Vendar visoki kraji niso bili odstranjeni. Ljudstvo je še vedno žrtvovalo in na visokih krajih zažigalo kadilo. Zgradil je višja velika vrata Gospodove hiše.
36 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Torej preostala izmed Jotámovih dejanj in vse, kar je storil, mar niso zapisana v kroniški knjigi Judovih kraljev?
37 (Katika siku hizo, Bwana akaanza kuwatuma Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia dhidi ya Yuda.)
V tistih dneh je Gospod zoper Juda začel pošiljati sirskega kralja Recína in Remaljájevega sina Pékaha.
38 Yothamu akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi, mji wa baba zake. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Jotám je zaspal s svojimi očeti in bil s svojimi očeti pokopan v mestu svojega očeta Davida in namesto njega je zakraljeval njegov sin Aház.

< 2 Wafalme 15 >