< 2 Wafalme 15 >

1 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
No vigésimo sétimo ano de Jeroboão, rei de Israel, começou a reinar Azarias, filho de Amazonas, rei de Judá.
2 Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
Ele tinha dezesseis anos quando começou a reinar, e reinou cinqüenta e dois anos em Jerusalém. O nome de sua mãe era Jecoliah de Jerusalém.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
Ele fez o que era certo aos olhos de Javé, de acordo com tudo o que seu pai, Amazias, havia feito.
4 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
No entanto, os lugares altos não foram tirados. O povo ainda sacrificava e queimava incenso nos lugares altos.
5 Bwana akampiga mfalme kwa ukoma mpaka siku aliyokufa, naye aliishi katika nyumba iliyotengwa peke yake. Yothamu mwana wa mfalme akawa msimamizi wa jumba la mfalme, na akawatawala watu wa nchi.
Yahweh atingiu o rei, de modo que ele foi um leproso até o dia de sua morte, e viveu em uma casa separada. Jotham, o filho do rei, estava sobre a casa, julgando o povo da terra.
6 Matukio mengine ya utawala wa Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Agora o resto dos atos de Azarias, e tudo o que ele fez, não estão escritos no livro das crônicas dos reis de Judá?
7 Azaria akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika Mji wa Daudi, na Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Azarias dormiu com seus pais; e eles o enterraram com seus pais na cidade de David; e Jotham seu filho reinou em seu lugar.
8 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, naye akatawala miezi sita.
No trigésimo oitavo ano de Azarias, rei de Judá, Zacarias, filho de Jeroboão, reinou sobre Israel em Samaria durante seis meses.
9 Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama baba zake walivyofanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Ele fez o que era mau aos olhos de Iavé, como seus pais haviam feito. Ele não se afastou dos pecados de Jeroboão, o filho de Nebat, com os quais fez Israel pecar.
10 Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya shauri baya dhidi ya Zekaria. Akamshambulia mbele ya watu, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Shallum, o filho de Jabesh, conspirou contra ele, golpeou-o diante do povo e o matou, e reinou em seu lugar.
11 Matukio mengine ya utawala wa Zekaria yameandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Agora o resto dos atos de Zacarias, eis que estão escritos no livro das crônicas dos reis de Israel.
12 Kwa hiyo neno la Bwana lililonenwa kwa Yehu likatimia, kwamba, “Wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
Esta foi a palavra de Javé que ele falou a Jeú, dizendo: “Seus filhos à quarta geração sentar-se-ão no trono de Israel”. E assim aconteceu.
13 Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa thelathini na tisa wa Uzia mfalme wa Yuda, naye akatawala katika Samaria kwa mwezi mmoja.
Shallum, filho de Jabesh, começou a reinar no trigésimo nono ano de Uzziah, rei de Judá, e reinou por um mês em Samaria.
14 Kisha Menahemu mwana wa Gadi akaenda kutoka Tirsa mpaka Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi huko Samaria, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Menahem o filho de Gadi subiu de Tirzah, veio para Samaria, atingiu Shallum o filho de Jabesh em Samaria, matou-o, e reinou em seu lugar.
15 Matukio mengine ya utawala wa Shalumu, na mauaji aliyoyafanya, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Agora o resto dos atos de Shallum, e sua conspiração que ele fez, eis que estão escritos no livro das crônicas dos reis de Israel.
16 Wakati ule, akianzia Tirsa, Menahemu alishambulia Tifsa na kila mtu ndani yake, na wale waliokuwa maeneo jirani, kwa sababu walikataa kufungua malango yao. Akaiangamiza Tifsa yote, na kuwapasua matumbo wanawake wote wenye mimba.
Então Menahem atacou Tiphsah e todos os que estavam nele e em suas áreas de fronteira, de Tirzah. Ele o atacou porque eles não lhe abriram as portas, e ele arrancou todas as mulheres que estavam com crianças.
17 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, akatawala huko Samaria kwa miaka kumi.
No ano trinta e nove de Azaria, rei de Judá, Menahem, filho de Gadi, começou a reinar sobre Israel por dez anos em Samaria.
18 Akatenda maovu machoni pa Bwana. Katika wakati wa utawala wake wote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Ele fez o que era mau aos olhos de Iavé. Ele não se afastou todos os seus dias dos pecados de Jeroboão, filho de Nebat, com os quais fez Israel pecar.
19 Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaishambulia Israeli. Menahemu mfalme wa Israeli akampa talanta elfu moja za fedha ili amsaidie na kumwezesha katika utawala wake.
Pul, o rei da Assíria, veio contra a terra, e Menahem deu a Pul mil talentos de prata, para que sua mão pudesse estar com ele para confirmar o reino em sua mão.
20 Menahemu akatoza fedha hizi kwa nguvu kutoka kwa Israeli. Kila mtu tajiri alilazimika kuchanga shekeli hamsini za fedha ambazo alipewa mfalme wa Ashuru. Basi mfalme wa Ashuru akajiondoa na hakuendelea kuikalia nchi.
Menahem exigiu o dinheiro de Israel, mesmo de todos os homens poderosos e ricos, de cada homem cinqüenta siclos de prata, para dar ao rei da Assíria. Assim, o rei da Assíria voltou atrás, e não ficou lá na terra.
21 Matukio mengine ya utawala wa Menahemu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Agora o resto dos atos de Menahem, e tudo o que ele fez, não estão escritos no livro das crônicas dos reis de Israel?
22 Menahemu akalala pamoja na baba zake. Naye Pekahia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Menahem dormiu com seus pais, e Pekahiah, seu filho, reinou em seu lugar.
23 Katika mwaka wa hamsini wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, akatawala miaka miwili.
No quinquagésimo ano de Azarias, rei de Judá, Pekahiah, filho de Menahem, começou a reinar sobre Israel em Samaria por dois anos.
24 Pekahia akafanya uovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Ele fez o que era mau aos olhos de Iavé. Ele não se afastou dos pecados de Jeroboão, filho de Nebate, com os quais ele fez Israel pecar.
25 Mmoja wa maafisa wake wakuu, Peka mwana wa Remalia, akafanya shauri baya dhidi yake. Akachukua watu hamsini wa Gileadi pamoja naye, akamuua Pekahia, pamoja na Argobu na Aria, katika ngome ya jumba la kifalme huko Samaria. Kwa hiyo Peka akamuua Pekahia, naye akaingia mahali pake kuwa mfalme.
Pekah, o filho de Remalias, seu capitão, conspirou contra ele e o atacou em Samaria, na fortaleza da casa do rei, com Argob e Arieh; e com ele estavam cinqüenta homens dos gileaditas. Ele o matou, e reinou em seu lugar.
26 Matukio mengine ya utawala wa Pekahia na yote aliyoyafanya yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Agora o resto dos atos de Pekahiah, e tudo o que ele fez, eis que estão escritos no livro das crônicas dos reis de Israel.
27 Katika mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala miaka ishirini.
No quinquagésimo segundo ano de Azarias, rei de Judá, Pekah, filho de Remalias, começou a reinar sobre Israel em Samaria por vinte anos.
28 Akafanya maovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Ele fez o que era mau aos olhos de Iavé. Ele não se afastou dos pecados de Jeroboão, filho de Nebate, com os quais ele fez Israel pecar.
29 Wakati wa utawala wa Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alikuja na kuteka Iyoni, Abel-Beth-Maaka, Yanoa, Kedeshi na Hazori. Akateka miji ya Gileadi na Galilaya, pamoja na nchi yote ya Naftali, na kuwahamishia watu wote Ashuru.
Nos dias de Pekah, rei de Israel, Tiglate Pileser, rei da Assíria, veio e levou Ijon, Abel Beth Maacah, Janoah, Kedesh, Hazor, Gilead e Galileia, todas as terras de Naftali; e levou-as cativas para a Assíria.
30 Kisha Hoshea mwana wa Ela akafanya shauri baya dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akamshambulia na kumuua, kisha akaingia mahali pake kuwa mfalme katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
Hoshea, filho de Elá, fez uma conspiração contra Pekah, filho de Remalias, atacou-o, matou-o e reinou em seu lugar, no vigésimo ano de Jotão, filho de Uzias.
31 Matukio mengine ya utawala wa Peka na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Agora o resto dos atos de Pekah, e tudo o que ele fez, eis que estão escritos no livro das crônicas dos reis de Israel.
32 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Uzia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
No segundo ano de Pekah, filho de Remalias, rei de Israel, Jotham, filho de Uzziah, rei de Judá, começou a reinar.
33 Alikuwa na miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Ele tinha vinte e cinco anos quando começou a reinar, e reinou dezesseis anos em Jerusalém. O nome de sua mãe era Jerusha, filha de Zadoque.
34 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya.
Ele fez o que era certo aos olhos de Iavé. Ele fez de acordo com tudo o que seu pai Uzziah havia feito.
35 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko. Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana.
No entanto, os lugares altos não foram tirados. O povo ainda sacrificou e queimou incenso nos lugares altos. Ele construiu o portão superior da casa de Yahweh.
36 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Agora o resto dos atos de Jotham, e tudo o que ele fez, não estão escritos no livro das crônicas dos reis de Judá?
37 (Katika siku hizo, Bwana akaanza kuwatuma Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia dhidi ya Yuda.)
Naqueles dias, Javé começou a enviar Rezin, o rei da Síria, e Pekah, o filho de Remalias, contra Judá.
38 Yothamu akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi, mji wa baba zake. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Jotham dormiu com seus pais, e foi enterrado com seus pais na cidade de seu pai David; e Ahaz, seu filho, reinou em seu lugar.

< 2 Wafalme 15 >