< 2 Wafalme 15 >
1 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
Amy taom-paha roapolo-fito’ ambi’ Iarovame mpanjaka’ Israeley, ty niorota’ i Azarià ana’ i Amatsià mpanjaka’ Iehodà nifehe.
2 Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
Ni-folo-taoñ’eneñ’ amby re te niorotse nifeleke, le nifehe limampolo taoñe ro’ amby e Ierosalaime ao; Iekoliae nte-Ierosalaime, ty tahinan-drene’e.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
Nitolon-kavantañañe am-pivazohoa’ Iehovà re, hambañe amo hene fitoloñan-drae’e Amatsiào.
4 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Fe mboe tsy nafahañe o toets’ aboo; nitolom-panao soroñe naho nañoro tsotse amo toets-aboo avao ondatio.
5 Bwana akampiga mfalme kwa ukoma mpaka siku aliyokufa, naye aliishi katika nyumba iliyotengwa peke yake. Yothamu mwana wa mfalme akawa msimamizi wa jumba la mfalme, na akawatawala watu wa nchi.
Linama’ Iehovà haangamae i mpanjakay ampara’ ty andro nihomaha’e vaho nimoneñe añ’ akiba navìke ao. Iotame, ana’ i mpanjakay, ty nifehe’ i anjombay, naho nizaka ondati’ i taneio.
6 Matukio mengine ya utawala wa Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Ty ila’ o fitoloña’ i Azariào, o nanoe’e iabio; tsy fa sinokitse amy bokem-pamoliliañe o mpanjaka’ Iehodaoy hao?
7 Azaria akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika Mji wa Daudi, na Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Nitrao-pirotse aman-droae’e t’i Azarià, le nalenteke aman-droae’e an-drova’ i Davide ao; le nandimbe aze nifehe t’Iotame ana’e.
8 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, naye akatawala miezi sita.
Amy taom-paha-telopolo-valo’ ambi’ i Azarià mpanjaka’ Iehoday, te nifeleke Israele t’i Zekarià ana’ Iarovame enem-bolañe e Somerone ao.
9 Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama baba zake walivyofanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Nanao raty am-pivazohoa’ Iehovà re, manahak’ an-droae’e, tsy nisitaha’e o hakeo nampanaña’ Iarovame ana’ i Nebate tàhiñe Israeleo.
10 Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya shauri baya dhidi ya Zekaria. Akamshambulia mbele ya watu, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Nikinia aze t’i Salome, ana’ Iabese le zinevo’e añatrefa’ ondatio, vaho vinono’e, le nandimbe aze nifeleke.
11 Matukio mengine ya utawala wa Zekaria yameandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Aa ty ila’ o fitoloña’ i Zekariào, oniño t’ie sinokitse amy bokem-pamoliliañe o mpanjaka’ Israeleoy.
12 Kwa hiyo neno la Bwana lililonenwa kwa Yehu likatimia, kwamba, “Wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
Le niheneke ty nitsarae’ Iehovà am’ Ieho ami’ty hoe; O ana’o pak’ an-tariratse fah’ efatseo ty hiambesatse amy fiambesa’ Israeley, le izay ty ie.
13 Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa thelathini na tisa wa Uzia mfalme wa Yuda, naye akatawala katika Samaria kwa mwezi mmoja.
Niorotse nifehe amy taom-paha-telo-polo-sive’ ambi’ i Ozià mpanjaka’ Iehodaiy t’i Salome ana’ Iabese le nifeleke volan-draike do’e e Somerone ao.
14 Kisha Menahemu mwana wa Gadi akaenda kutoka Tirsa mpaka Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi huko Samaria, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Nionjoñe boak’e Tirtsà t’i Menakeme ana’ i Gadý, le nivotrake e Somerone eo, naho zinevo’e t’i Salome, ana’ Iabese, e Somerone ao naho vinono’e vaho nandimbe aze nifeleke.
15 Matukio mengine ya utawala wa Shalumu, na mauaji aliyoyafanya, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Aa naho o fitoloña’ i Salome ila’eo, i kilily nanoe’ey, oniño t’ie sinokitse amy bokem-pamoliliañe o mpanjaka’ Israeleoy.
16 Wakati ule, akianzia Tirsa, Menahemu alishambulia Tifsa na kila mtu ndani yake, na wale waliokuwa maeneo jirani, kwa sababu walikataa kufungua malango yao. Akaiangamiza Tifsa yote, na kuwapasua matumbo wanawake wote wenye mimba.
Zinevo’ i Menakeme amy zao ty Tifsà, ze tama’e ao iaby naho o mañohok’ azeo pake Tirtsà; amy t’ie tsy nisokafe’ iereo; aa le linafa’e vaho niriate’e iaby ze rakemba nivesatse ao.
17 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, akatawala huko Samaria kwa miaka kumi.
Amy taom-paha-telopolo-sive’ ambi’ i Azarià mpanjaka’ Iehodày ty niorota’ i Menakeme ana’ i Gadý nifeleke Israele, le nifehe folo taoñe e Somerone ao.
18 Akatenda maovu machoni pa Bwana. Katika wakati wa utawala wake wote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Nanao raty am-pivazohoa’ Iehovà re, le tsy napo’e amo hene andro’eo o hakeo nampanaña’ Iarovame ana’ i Nebate tahiñe Israeleo.
19 Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaishambulia Israeli. Menahemu mfalme wa Israeli akampa talanta elfu moja za fedha ili amsaidie na kumwezesha katika utawala wake.
Naname i taney t’i Pole mpanjaka’ i Asore, le natolo’ i Menakeme amy Pole ty talenta volafoty arivo soa te ho ama’e ty fità’e hamentea’e i fifeheañey.
20 Menahemu akatoza fedha hizi kwa nguvu kutoka kwa Israeli. Kila mtu tajiri alilazimika kuchanga shekeli hamsini za fedha ambazo alipewa mfalme wa Ashuru. Basi mfalme wa Ashuru akajiondoa na hakuendelea kuikalia nchi.
Sinaze’ i Menakeme drala t’Israele, boak’ amo fanalolahy mpañalealeo, songa hakare’ ondatio ty sekele limampolo hatolotse amy mpanjaka’ i Asorey, vaho nibalik’ añe i mpanjaka’ i Asorey le tsy nitambatse amy taney.
21 Matukio mengine ya utawala wa Menahemu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Aa naho o fitoloña’ i Menakeme ila’eo, ze hene nanoe’e, tsy fa sinokitse amy bokem-pamoliliañe o mpanjaka’ Israeleoy hao?
22 Menahemu akalala pamoja na baba zake. Naye Pekahia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Nitrao-piròtse aman-droae’e ao t’i Menakeme, le nandimbe aze nifehe t’i Pekaià, ana’e.
23 Katika mwaka wa hamsini wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, akatawala miaka miwili.
Amy taom-paha-limampolo’ i Azarià mpanjaka’ Iehoday, te niorotse nifehe Israele e Somerone ao t’i Pekaià ana’ i Menaheme; le nifeleke roe taoñe.
24 Pekahia akafanya uovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Nanao ze raty am-pivazohoa’ Iehovà re; tsy nisitaha’e o tahi’ Iarovame ana’ i Nebate nampanaña’e hakeo Israeleo.
25 Mmoja wa maafisa wake wakuu, Peka mwana wa Remalia, akafanya shauri baya dhidi yake. Akachukua watu hamsini wa Gileadi pamoja naye, akamuua Pekahia, pamoja na Argobu na Aria, katika ngome ya jumba la kifalme huko Samaria. Kwa hiyo Peka akamuua Pekahia, naye akaingia mahali pake kuwa mfalme.
Nikinia aze amy zao t’i Pekà ana’ i Remalià, sorotà’e, le nanjevoñ’ aze e Somerone, amy fitalakesañ’ abo’ i anjomba’ i mpanjakaiy ao, rekets’ i Argobe naho i Ariè vaho ondaty limampolo nte-Gilade nindre ama’eo; vinono’e, vaho nandimbe aze nifehe.
26 Matukio mengine ya utawala wa Pekahia na yote aliyoyafanya yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Aa naho o fitoloña’ i Pekaià ila’eo, o hene nanoe’eo, tsy fa sinokitse amy bokem-pamoliliañe o mpanjaka’ Israeleoy hao?
27 Katika mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala miaka ishirini.
Amy taom-paha-limampolo-ro’ ambi’ i Azarià, mpanjaka’ Iehodày, le niorotse nifehe e Israele e Somerone ao t’i Pekà ana’ i Remalià vaho nifeleke roapolo taoñe.
28 Akafanya maovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Nanao haratiañe am-pivazohoa’ Iehovà, tsy nisitaha’e o tahi’ Iarovame ana’ i Nebate, nampanaña’e hakeo Israeleo.
29 Wakati wa utawala wa Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alikuja na kuteka Iyoni, Abel-Beth-Maaka, Yanoa, Kedeshi na Hazori. Akateka miji ya Gileadi na Galilaya, pamoja na nchi yote ya Naftali, na kuwahamishia watu wote Ashuru.
Tañ’ andro’ i Pekà mpanjaka’ Israele, ty nanamea’ i Tiglate-pilèsere mpanjaka’ i Asore, le tinava’e t’Iione, i Abel-bete-maakà, Ianoà, i Kedese, i Kazore, i Gilade naho ze hene tane Naftalý vaho nendese’e an-drohy mb’e Asore añe.
30 Kisha Hoshea mwana wa Ela akafanya shauri baya dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akamshambulia na kumuua, kisha akaingia mahali pake kuwa mfalme katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
Kinilili’ i Hoseà, ana’ i Elà t’i Pekà, ana’ i Remalià, le linafa’e naho vinono’e vaho nandimbe aze nifehe amy taom-paha-roapolo’ Iotame ana’ i Oziày.
31 Matukio mengine ya utawala wa Peka na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Aa naho o fitoloña’ i Pekà ila’eo, o nanoe’eo, oniño t’ie misokitse amy bokem-pamoliliañe o mpanjaka’ Israeleoy.
32 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Uzia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
Amy tom-paharoe’ i Pekà, ana’ i Remalià, mpanjaka’ Israeley, te niorotse nifehe e Iehodà t’Iotame ana’ i Ozià.
33 Alikuwa na miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Roapolo taoñe lime amby re te niorotse nifeleke, le nifehe folo taoñe eneñ’ amby e Ierosalaime ao, Ierosoae ana’ i Tsadoke, ty tahinan-drene’e.
34 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya.
Nanao ty havantañañe am-pihaino’ Iehovà re, hene norihe’e ty satan-drae’e Ozià.
35 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko. Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana.
Fe tsy nafahañe añe o toets’ aboo; mbe nanao soroñe naho nañenga ey ondatio. Namboare’e ty lalambei’ ambone’ i anjomba’ Iehovày.
36 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Aa naho o fitoloña’ Iotame ila’eo, ze hene nanoe’e, tsy fa sinokitse amy bokem-pamoliliañe o mpanjaka’ Iehodàoy hao?
37 (Katika siku hizo, Bwana akaanza kuwatuma Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia dhidi ya Yuda.)
Namototse nañirake i Retsine mpanjaka’ i Arame naho i Pekà ana’ i Remalià, haname Iehodà t’Iehovà henane zay.
38 Yothamu akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi, mji wa baba zake. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Nitrao-piròtse aman-droae’e t’Iotame le nalentek’ aman-droae’e an-drova’ i Davide ao; vaho nandimbe aze nifehe t’i Ahkaze ana’e.