< 2 Wafalme 15 >
1 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
La vingt-septième année de Jéroboam, roi d'Israël, Azaria, fils d'Amatsia, roi de Juda, devint roi.
2 Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
Il avait seize ans à son avènement, et il régna cinquante-deux ans à Jérusalem. Or, le nom de sa mère était Jecholia de Jérusalem.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
Et il fit ce qui est droit aux yeux de l'Éternel tout comme avait fait Amatsia, son père.
4 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Seulement les tertres ne disparurent pas, le peuple offrait encore des victimes et de l'encens sur les tertres.
5 Bwana akampiga mfalme kwa ukoma mpaka siku aliyokufa, naye aliishi katika nyumba iliyotengwa peke yake. Yothamu mwana wa mfalme akawa msimamizi wa jumba la mfalme, na akawatawala watu wa nchi.
Et l'Éternel infligea une plaie au roi, qui fut lépreux jusqu'au jour de sa mort et demeura dans une infirmerie. Cependant Jotham, fils du roi, était préposé sur la Maison, rendant la justice au peuple du pays.
6 Matukio mengine ya utawala wa Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Le reste des actes d'Azaria et toutes ses entreprises sont d'ailleurs consignés dans le livre des annales des rois de Juda.
7 Azaria akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika Mji wa Daudi, na Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Azaria reposa avec ses pères et on lui donna la sépulture avec ses pères dans la ville de David, et Jotham, son fils, devint roi en sa place.
8 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, naye akatawala miezi sita.
Là trente-huitième année d'Azaria, roi de Juda, Zacharie, fils de Jéroboam, devint roi d'Israël à Samarie pour six mois.
9 Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama baba zake walivyofanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Et il fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel comme avaient fait ses pères; il ne se départit point des péchés de Jéroboam, fils de Nebat, qui avait entraîné Israël à pécher.
10 Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya shauri baya dhidi ya Zekaria. Akamshambulia mbele ya watu, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Et Sallum, fils de Jabès, conspira contre lui et fit main basse sur lui publiquement, et le tua et devint roi en sa place.
11 Matukio mengine ya utawala wa Zekaria yameandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Le reste des actes de Zacharie est d'ailleurs consigné dans le livre des annales des rois d'Israël.
12 Kwa hiyo neno la Bwana lililonenwa kwa Yehu likatimia, kwamba, “Wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
C'est la parole de l'Éternel qu'il avait dite à Jéhu en ces termes: Tu auras des fils de la quatrième génération assis au trône d'Israël, et il en fut ainsi.
13 Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa thelathini na tisa wa Uzia mfalme wa Yuda, naye akatawala katika Samaria kwa mwezi mmoja.
Sallum, fils de Jabès, devint roi la trente-neuvième année d'Hozias, roi de Juda, et régna un mois de temps à Samarie.
14 Kisha Menahemu mwana wa Gadi akaenda kutoka Tirsa mpaka Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi huko Samaria, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Et Menahem, fils de Gadi, s'avança de Thirtsa, et entra dans Samarie, et fit main basse sur Sallum, fils de Jabès, dans Samarie, et lui donna la mort et devint roi en sa place.
15 Matukio mengine ya utawala wa Shalumu, na mauaji aliyoyafanya, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Le reste des actes de Sallum, et sa conjuration qu'il avait formée, sont d'ailleurs consignés dans le livre des annales des rois d'Israël.
16 Wakati ule, akianzia Tirsa, Menahemu alishambulia Tifsa na kila mtu ndani yake, na wale waliokuwa maeneo jirani, kwa sababu walikataa kufungua malango yao. Akaiangamiza Tifsa yote, na kuwapasua matumbo wanawake wote wenye mimba.
C'est alors que Menahem fit main basse sur Thiphsach et sur tous ceux qui y étaient, et sur tout son territoire à partir de Thirtsa; ce fut parce qu'on ne lui ouvrit pas qu'il porta ce coup; il y éventra toutes les femmes enceintes.
17 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, akatawala huko Samaria kwa miaka kumi.
La trente-neuvième année d'Azaria, roi de Juda, Menahem, fils de Gadi, devint roi d'Israël, pour dix ans à Samarie.
18 Akatenda maovu machoni pa Bwana. Katika wakati wa utawala wake wote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Et il fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel; il ne se départit point des péchés de Jéroboam, fils de Nebat, auxquels celui-ci avait entraîné Israël, toute sa vie durant.
19 Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaishambulia Israeli. Menahemu mfalme wa Israeli akampa talanta elfu moja za fedha ili amsaidie na kumwezesha katika utawala wake.
Phul, roi d'Assyrie, fit invasion dans le pays, et Ménahem donna à Phul mille talents d'argent afin qu'il lui prêtât la main pour assurer la royauté dans sa propre main.
20 Menahemu akatoza fedha hizi kwa nguvu kutoka kwa Israeli. Kila mtu tajiri alilazimika kuchanga shekeli hamsini za fedha ambazo alipewa mfalme wa Ashuru. Basi mfalme wa Ashuru akajiondoa na hakuendelea kuikalia nchi.
Et Menahem tira cette somme à payer au roi d'Assyrie, sur les Israélites, tous les gens à moyens, à raison de cinquante sicles d'argent par individu. Puis le roi d'Assyrie rebroussa sans séjourner alors dans le pays.
21 Matukio mengine ya utawala wa Menahemu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Le reste des actes de Menahem et toutes ses entreprises sont d'ailleurs consignés dans le livre des annales des rois d'Israël.
22 Menahemu akalala pamoja na baba zake. Naye Pekahia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Menahem reposa avec ses pères, et Pekachia, son fils, devint roi à sa place.
23 Katika mwaka wa hamsini wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, akatawala miaka miwili.
La cinquantième année d'Azaria roi de Juda, Pekachia, fils de Menahem, devint roi d'Israël à Samarie, pour deux ans.
24 Pekahia akafanya uovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Et il fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel; il ne se départit point des péchés de Jéroboam, fils de Nebat, auxquels celui-ci avait entraîné Israël.
25 Mmoja wa maafisa wake wakuu, Peka mwana wa Remalia, akafanya shauri baya dhidi yake. Akachukua watu hamsini wa Gileadi pamoja naye, akamuua Pekahia, pamoja na Argobu na Aria, katika ngome ya jumba la kifalme huko Samaria. Kwa hiyo Peka akamuua Pekahia, naye akaingia mahali pake kuwa mfalme.
Et Pékach, fils de Remalia, son aide-de-camp, conspira contre lui et lui porta le coup dans Samarie au donjon du palais royal, en même temps qu'à Argob et à Ariè; or il se trouvait avec lui cinquante hommes d'entre les fils des Galaadites; c'est ainsi qu'il lui donna la mort et devint roi en sa place.
26 Matukio mengine ya utawala wa Pekahia na yote aliyoyafanya yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Le reste des actes de Pekachia et toutes ses entreprises sont d'ailleurs consignés dans le livre des annales des rois d'Israël.
27 Katika mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala miaka ishirini.
La cinquante-deuxième année d'Azaria roi de Juda, Pékach, fils de Remalia, devint roi d'Israël à Samarie pour vingt ans.
28 Akafanya maovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Et il fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel; il ne se départit point des péchés de Jéroboam, fils de Nebat, auxquels celui-ci avait entraîné Israël.
29 Wakati wa utawala wa Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alikuja na kuteka Iyoni, Abel-Beth-Maaka, Yanoa, Kedeshi na Hazori. Akateka miji ya Gileadi na Galilaya, pamoja na nchi yote ya Naftali, na kuwahamishia watu wote Ashuru.
Au temps de Pékach, roi d'Israël, Thiglath-Piléser, roi d'Assyrie, vint et prit Ijon et Abel-Beth-Maacha et Janoha et Kédès et Hatsor et Galaad et la Galilée, tout le territoire de Nephthali, et il les emmena captifs en Assyrie.
30 Kisha Hoshea mwana wa Ela akafanya shauri baya dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akamshambulia na kumuua, kisha akaingia mahali pake kuwa mfalme katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
Et Hosée, fils d'Éla, forma une conspiration contre Pékach, fils de Remalia, et fit main basse sur lui et lui donna la mort et devint roi en sa place la vingtième année de Jotham, fils d'Hozias.
31 Matukio mengine ya utawala wa Peka na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Le reste des actes de Pékach et toutes ses entreprises, sont d'ailleurs consignés dans le livre des annales des rois d'Israël.
32 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Uzia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
La seconde année de Pékach, fils de Remalia, roi d'Israël, Jotham, fils d'Hozias, roi de Juda, devint roi.
33 Alikuwa na miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Il avait vingt-cinq ans à son avènement et il régna seize ans à Jérusalem. Or le nom de sa mère était Jérusa, fille de Tsadoc.
34 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya.
Et il fit ce qui est droit aux yeux de l'Éternel; il agit en tout comme avait agi Hozias, son père.
35 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko. Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana.
Seulement les tertres ne disparurent pas; le peuple offrait encore des victimes et de l'encens sur les tertres. Il construisit la porte supérieure du temple de l'Éternel.
36 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Le reste des actes, de Jotham et toutes ses entreprises sont d'ailleurs consignés dans le livre des annales des rois de Juda.
37 (Katika siku hizo, Bwana akaanza kuwatuma Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia dhidi ya Yuda.)
Dans ce même temps l'Éternel commença à envoyer contre Juda, Retsin, roi de Syrie, et Pékach, fils de Remalia.
38 Yothamu akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi, mji wa baba zake. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Jotham reposa avec ses pères et reçut la sépulture avec ses pères dans la ville de David, son père, et Achaz, son fils, devint roi en sa place.