< 2 Wafalme 15 >
1 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
La vingt-septième année de Jéroboam, roi d'Israël, Azaria, fils d'Amatsia, roi de Juda, commença à régner.
2 Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
Il avait seize ans lorsqu'il devint roi, et il régna cinquante-deux ans à Jérusalem. Le nom de sa mère était Jecolia, de Jérusalem.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
Il fit ce qui est droit aux yeux de l'Éternel, selon tout ce qu'avait fait son père Amatsia.
4 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Cependant, les hauts lieux ne furent pas supprimés. Le peuple continuait à offrir des sacrifices et à brûler des parfums sur les hauts lieux.
5 Bwana akampiga mfalme kwa ukoma mpaka siku aliyokufa, naye aliishi katika nyumba iliyotengwa peke yake. Yothamu mwana wa mfalme akawa msimamizi wa jumba la mfalme, na akawatawala watu wa nchi.
Yahvé frappa le roi, de sorte qu'il fut lépreux jusqu'au jour de sa mort et qu'il vécut dans une maison séparée. Jotham, fils du roi, était à la tête de la maison et jugeait le peuple du pays.
6 Matukio mengine ya utawala wa Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Le reste des actes d'Azaria et tout ce qu'il a fait, n'est-ce pas écrit dans le livre des Chroniques des rois de Juda?
7 Azaria akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika Mji wa Daudi, na Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Azaria se coucha avec ses pères, et on l'enterra avec ses pères dans la ville de David; et Jotham, son fils, régna à sa place.
8 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, naye akatawala miezi sita.
La trente-huitième année d'Azaria, roi de Juda, Zacharie, fils de Jéroboam, régna sur Israël à Samarie pendant six mois.
9 Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama baba zake walivyofanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Il fit ce qui est mal aux yeux de Yahvé, comme avaient fait ses pères. Il ne se détourna pas des péchés de Jéroboam, fils de Nebath, par lesquels il avait fait pécher Israël.
10 Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya shauri baya dhidi ya Zekaria. Akamshambulia mbele ya watu, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Shallum, fils de Jabesh, conspira contre lui, le frappa devant le peuple, le tua, et régna à sa place.
11 Matukio mengine ya utawala wa Zekaria yameandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Le reste des actes de Zacharie, voici, ils sont écrits dans le livre des chroniques des rois d'Israël.
12 Kwa hiyo neno la Bwana lililonenwa kwa Yehu likatimia, kwamba, “Wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
Telle fut la parole que Yahvé adressa à Jéhu, en disant: « Tes fils jusqu'à la quatrième génération s'assiéront sur le trône d'Israël. » Ainsi s'accomplit ce qui suit.
13 Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa thelathini na tisa wa Uzia mfalme wa Yuda, naye akatawala katika Samaria kwa mwezi mmoja.
Schallum, fils de Jabesh, régna la trente-neuvième année d'Ozias, roi de Juda, et il régna un mois à Samarie.
14 Kisha Menahemu mwana wa Gadi akaenda kutoka Tirsa mpaka Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi huko Samaria, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Menahem, fils de Gadi, monta de Thirtsa, vint à Samarie, frappa Shallum, fils de Jabesh, à Samarie, le tua, et régna à sa place.
15 Matukio mengine ya utawala wa Shalumu, na mauaji aliyoyafanya, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Le reste des actes de Shallum, et la conspiration qu'il a formée, sont écrits dans le livre des Chroniques des rois d'Israël.
16 Wakati ule, akianzia Tirsa, Menahemu alishambulia Tifsa na kila mtu ndani yake, na wale waliokuwa maeneo jirani, kwa sababu walikataa kufungua malango yao. Akaiangamiza Tifsa yote, na kuwapasua matumbo wanawake wote wenye mimba.
Alors Menahem attaqua Tiphsah et tous ceux qui s'y trouvaient, ainsi que les régions limitrophes, depuis Tirza. Il l'attaqua parce qu'ils ne lui avaient pas ouvert leurs portes, et il déchira toutes leurs femmes enceintes.
17 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, akatawala huko Samaria kwa miaka kumi.
La trente-neuvième année d'Azaria, roi de Juda, Menahem, fils de Gadi, régna sur Israël pendant dix ans à Samarie.
18 Akatenda maovu machoni pa Bwana. Katika wakati wa utawala wake wote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Il fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel. Il ne se détourna pas pendant toute sa vie des péchés de Jéroboam, fils de Nebat, par lesquels il avait fait pécher Israël.
19 Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaishambulia Israeli. Menahemu mfalme wa Israeli akampa talanta elfu moja za fedha ili amsaidie na kumwezesha katika utawala wake.
Pul, roi d'Assyrie, vint contre le pays, et Menahem donna à Pul mille talents d'argent, afin que sa main soit avec lui pour confirmer le royaume entre ses mains.
20 Menahemu akatoza fedha hizi kwa nguvu kutoka kwa Israeli. Kila mtu tajiri alilazimika kuchanga shekeli hamsini za fedha ambazo alipewa mfalme wa Ashuru. Basi mfalme wa Ashuru akajiondoa na hakuendelea kuikalia nchi.
Menahem exigea d'Israël, de tous les hommes riches et puissants, cinquante sicles d'argent chacun, pour les donner au roi d'Assyrie. Et le roi d'Assyrie s'en retourna, et ne resta pas dans le pays.
21 Matukio mengine ya utawala wa Menahemu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Le reste des actes de Menahem, et tout ce qu'il a fait, n'est-ce pas écrit dans le livre des Chroniques des rois d'Israël?
22 Menahemu akalala pamoja na baba zake. Naye Pekahia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Menahem se coucha avec ses pères, et Pekahiah, son fils, régna à sa place.
23 Katika mwaka wa hamsini wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, akatawala miaka miwili.
La cinquantième année d'Azaria, roi de Juda, Pekahia, fils de Menahem, régna sur Israël à Samarie pendant deux ans.
24 Pekahia akafanya uovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Il fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel. Il ne se détourna pas des péchés de Jéroboam, fils de Nebat, par lesquels il avait fait pécher Israël.
25 Mmoja wa maafisa wake wakuu, Peka mwana wa Remalia, akafanya shauri baya dhidi yake. Akachukua watu hamsini wa Gileadi pamoja naye, akamuua Pekahia, pamoja na Argobu na Aria, katika ngome ya jumba la kifalme huko Samaria. Kwa hiyo Peka akamuua Pekahia, naye akaingia mahali pake kuwa mfalme.
Pékah, fils de Remalia, son chef, conspira contre lui et l'attaqua à Samarie, dans la forteresse de la maison du roi, avec Argob et Arieh; il avait avec lui cinquante hommes des Galaadites. Il le tua, et régna à sa place.
26 Matukio mengine ya utawala wa Pekahia na yote aliyoyafanya yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Le reste des actes de Pékahia, et tout ce qu'il a fait, voici, cela est écrit dans le livre des chroniques des rois d'Israël.
27 Katika mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala miaka ishirini.
La cinquante-deuxième année d'Azaria, roi de Juda, Pékah, fils de Remalia, régna sur Israël à Samarie pendant vingt ans.
28 Akafanya maovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Il fit ce qui est mal aux yeux de Yahvé. Il ne se détourna pas des péchés de Jéroboam, fils de Nebat, par lesquels il avait fait pécher Israël.
29 Wakati wa utawala wa Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alikuja na kuteka Iyoni, Abel-Beth-Maaka, Yanoa, Kedeshi na Hazori. Akateka miji ya Gileadi na Galilaya, pamoja na nchi yote ya Naftali, na kuwahamishia watu wote Ashuru.
Du temps de Pékah, roi d'Israël, Tiglath Pileser, roi d'Assyrie, vint et prit Ijon, Abel Beth Maaca, Janoah, Kedesh, Hatsor, Galaad et Galilée, tout le pays de Nephtali, et il les emmena captifs en Assyrie.
30 Kisha Hoshea mwana wa Ela akafanya shauri baya dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akamshambulia na kumuua, kisha akaingia mahali pake kuwa mfalme katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
Hosée, fils d'Éla, forma une conspiration contre Pékah, fils de Remalia, l'attaqua, le tua et régna à sa place, la vingtième année de Jotham, fils d'Ozias.
31 Matukio mengine ya utawala wa Peka na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Le reste des actes de Pékach, et tout ce qu'il a fait, est écrit dans le livre des Chroniques des rois d'Israël.
32 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Uzia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
La deuxième année de Pékah, fils de Remalia, roi d'Israël, Jotham, fils d'Ozias, roi de Juda, commença à régner.
33 Alikuwa na miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Il avait vingt-cinq ans lorsqu'il devint roi, et il régna seize ans à Jérusalem. Le nom de sa mère était Jérusha, fille de Tsadok.
34 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya.
Il fit ce qui est droit aux yeux de l'Éternel. Il fit tout ce que son père Ozias avait fait.
35 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko. Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana.
Cependant, les hauts lieux ne furent pas supprimés. Le peuple continuait à offrir des sacrifices et à brûler des parfums sur les hauts lieux. Il construisit la porte supérieure de la maison de Yahvé.
36 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Le reste des actes de Jotham, et tout ce qu'il a fait, n'est-il pas écrit dans le livre des chroniques des rois de Juda?
37 (Katika siku hizo, Bwana akaanza kuwatuma Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia dhidi ya Yuda.)
En ces jours-là, Yahvé commença à envoyer contre Juda Rezin, roi de Syrie, et Pékah, fils de Remalia.
38 Yothamu akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi, mji wa baba zake. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Jotham se coucha avec ses pères et fut enterré avec ses pères dans la ville de David, son père, et Achaz, son fils, régna à sa place.