< 2 Wafalme 15 >

1 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
In the seuenthe and twentithe yeer of Jeroboam, king of Israel, Azarie, sone of Amasie, kyng of Juda, regnede;
2 Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
he was of sixtene yeer, whanne he bigan to regne, and he regnede two and fifti yeer in Jerusalem; the name of his modir was Jecelia of Jerusalem.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
And he dide that, that was plesaunt bifor the Lord, bi alle thingis which Amasie, his fadir, hadde do;
4 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
netheles he distriede not hiy thingis; yit the puple made sacrifice, and brente encense in hiye thingis.
5 Bwana akampiga mfalme kwa ukoma mpaka siku aliyokufa, naye aliishi katika nyumba iliyotengwa peke yake. Yothamu mwana wa mfalme akawa msimamizi wa jumba la mfalme, na akawatawala watu wa nchi.
Forsothe the Lord smoot the kyng, and he was leprouse til in to the day of his deeth; and he dwellide in an hous freli bi hym silf. Sotheli Joathas, sone of the kyng, gouernde the palis, and demyde the puple of the lond.
6 Matukio mengine ya utawala wa Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Forsothe the residue of the wordis of Azarie, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Juda?
7 Azaria akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika Mji wa Daudi, na Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Azarie slepte with hise fadris; and thei birieden hym with hise eldre men in the citee of Dauid; and Joathas, his sone, regnede for hym.
8 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, naye akatawala miezi sita.
In the eiyte and threttithe yeer of Azarie, kyng of Juda, Zacharie, sone of Jeroboam, regnede on Israel in Samarie sixe monethis.
9 Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama baba zake walivyofanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
And he dide that, that was yuel bifor the Lord, as his fadris diden; he departide not fro the synnes of Jeroboam, sone of Nabath, that made Israel to do synne.
10 Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya shauri baya dhidi ya Zekaria. Akamshambulia mbele ya watu, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Forsothe Sellum, the sone of Jabes, conspiride ayens hym in Samarie; and Sellum smoot hym opynli, and killide hym, and regnede for hym.
11 Matukio mengine ya utawala wa Zekaria yameandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Sotheli the residue of the wordis of Zacharie, whethir these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel?
12 Kwa hiyo neno la Bwana lililonenwa kwa Yehu likatimia, kwamba, “Wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
Thilke is the word of the Lord, which he spak to Hieu, and seide, `Thi sones `til to the fourthe generacioun schulen sitte `of thee on the trone of Israel; and it was doon so.
13 Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa thelathini na tisa wa Uzia mfalme wa Yuda, naye akatawala katika Samaria kwa mwezi mmoja.
Sellum, sone of Jabes, regnede in the nynthe and thritty yeer of Azarie, kyng of Juda; sotheli he regnyde o monethe in Samarie.
14 Kisha Menahemu mwana wa Gadi akaenda kutoka Tirsa mpaka Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi huko Samaria, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
And Manaheu, the sone of Gaddi, styede fro Thersa, and cam in to Samarie; and he smoot Sellum, sone of Jabes, in Samarie, and killide hym, and regnede for hym.
15 Matukio mengine ya utawala wa Shalumu, na mauaji aliyoyafanya, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Sotheli the residue of wordis of Sellum, and his conspirasie, bi which he settide tresouns, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel.
16 Wakati ule, akianzia Tirsa, Menahemu alishambulia Tifsa na kila mtu ndani yake, na wale waliokuwa maeneo jirani, kwa sababu walikataa kufungua malango yao. Akaiangamiza Tifsa yote, na kuwapasua matumbo wanawake wote wenye mimba.
Thanne Manaheu smoot Capham, and alle men that weren thereynne, and the termes therof fro Thersa, for thei nolden opyn to hym; and he killide alle wymmen therof with child, and karf hem.
17 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, akatawala huko Samaria kwa miaka kumi.
In the nynthe and thrittithe yeer of Azarie, kyng of Juda, Manaheu, sone of Gaddi, regnede on Israel ten yeer in Samarie.
18 Akatenda maovu machoni pa Bwana. Katika wakati wa utawala wake wote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
And he dide that, that was yuel bifor the Lord; he departide not fro the synnes of Jeroboam, sone of Nabath, that made Israel to do synne.
19 Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaishambulia Israeli. Menahemu mfalme wa Israeli akampa talanta elfu moja za fedha ili amsaidie na kumwezesha katika utawala wake.
In alle the daies of hym Phul, the kyng of Assiries, cam in to Thersa. And Manaheu yaf to Phul a thousynde talentis of siluer, that he schulde be to hym in to help, and schulde make stidefast his rewme;
20 Menahemu akatoza fedha hizi kwa nguvu kutoka kwa Israeli. Kila mtu tajiri alilazimika kuchanga shekeli hamsini za fedha ambazo alipewa mfalme wa Ashuru. Basi mfalme wa Ashuru akajiondoa na hakuendelea kuikalia nchi.
and Manaheu settide taliage of siluer on Israel to alle myyti men and riche, that he schulde yyue to the kyng of Assiries; he settide fifti siclis of siluer bi alle men; and the king of Assiries turnede ayen, and dwellide not in Thersa.
21 Matukio mengine ya utawala wa Menahemu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Forsothe the residue of wordis of Manaheu, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not wrytun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel?
22 Menahemu akalala pamoja na baba zake. Naye Pekahia mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Manaheu slepte with hise fadris; and Phaceia, his sone, regnyde for hym.
23 Katika mwaka wa hamsini wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, akatawala miaka miwili.
In the fiftithe yeer of Azarie, kyng of Juda, Phaceia, sone of Manaheu, regnede on Israel in Samarie twei yeer.
24 Pekahia akafanya uovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
And he dide that, that was yuel bifor the Lord; he departide not fro the synnes of Jeroboam, sone of Nabath, that made Israel to do synne.
25 Mmoja wa maafisa wake wakuu, Peka mwana wa Remalia, akafanya shauri baya dhidi yake. Akachukua watu hamsini wa Gileadi pamoja naye, akamuua Pekahia, pamoja na Argobu na Aria, katika ngome ya jumba la kifalme huko Samaria. Kwa hiyo Peka akamuua Pekahia, naye akaingia mahali pake kuwa mfalme.
Forsothe Phacee, sone of Romelie, duyk of his oost, conspiride ayens hym, and smoot hym in Samarie, in the tour of the kyngis hous, bisidis Argob, and bisidis Arib; `and he smoot hym with fifti men of the sones of Galaditis; and Phacee killide hym, and regnede for hym.
26 Matukio mengine ya utawala wa Pekahia na yote aliyoyafanya yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Sotheli the residue of wordis of Phacee, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel?
27 Katika mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala miaka ishirini.
In the two and fiftithe yeer of Azarie, kyng of Juda, Phasee, sone of Romelie, regnyde in Samarie twenti yeer.
28 Akafanya maovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
And he dide that, that was yuel bifor the Lord; and he departide not fro the synnes of Jeroboam, sone of Nabath, that made Israel to do synne.
29 Wakati wa utawala wa Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alikuja na kuteka Iyoni, Abel-Beth-Maaka, Yanoa, Kedeshi na Hazori. Akateka miji ya Gileadi na Galilaya, pamoja na nchi yote ya Naftali, na kuwahamishia watu wote Ashuru.
In the daies of Phacee, kyng of Israel, Teglat Phalasar, kyng of Assur, cam, and took Aion, and Aibel, the hows of Maacha, and Janoe, and Cedes, and Asor, and Galaad, and Galilee, and al the lond of Neptalym; and translatide hem in to Assiriens.
30 Kisha Hoshea mwana wa Ela akafanya shauri baya dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akamshambulia na kumuua, kisha akaingia mahali pake kuwa mfalme katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
Forsothe Osee, sone of Hela, conspiride, and settide tresouns ayens Phasee, sone of Romelie, and smoot hym, and killide hym; and he regnyde for hym, in the twentithe yeer of Joathan, sone of Ozie.
31 Matukio mengine ya utawala wa Peka na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Forsothe the residue of wordis of Phacee, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel?
32 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Uzia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
In the secounde yeer of Phacee, sone of Romelie, kyng of Israel, Joathan, sone of Ozie, kyng of Juda, regnyde;
33 Alikuwa na miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
he was of fyue and twenti yeer, whanne he bigan to regne, and he regnede sixtene yeer in Jerusalem; the name of his modir was Jerusa, the douyter of Sadoch.
34 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya.
And he dide that, that was plesaunt bifor the Lord; he wrouyte bi alle thingis, whiche his fadir Ozie hadde do;
35 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko. Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana.
netheles he dide not awey hiy thingis; yit the puple made sacrifice, and brente incense in hiy thingis; he bildide the hiyeste yate of the hows of the Lord.
36 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Forsothe the residue of wordis of Joathan, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Juda?
37 (Katika siku hizo, Bwana akaanza kuwatuma Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia dhidi ya Yuda.)
In tho daies the Lord bigan to sende in to Juda Rasyn, the kyng of Sirie, and Phacee, the sone of Romelie.
38 Yothamu akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi, mji wa baba zake. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Joathan slepte with hise fadris, and was biried with hem in the citee of Dauid, his fadir; and Achaz, his sone, regnyde for hym.

< 2 Wafalme 15 >