< 2 Wafalme 15 >

1 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
Israel lengpa Jeroboam ni na vaihom kum somni le sagi lhin chun, Amaziah chapa Uzziah chun Judah lenggam ah vai ahinhom pantan ahi.
2 Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
Ama leng ahung chan kum chun, ama kum somle gup alhingtan ahi, chuleh aman Jerusalem’ah kum somle nga sungin lengvai anahom in ahi. Anu chu Jerusalem ma kon Jecoliah ahi.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
Amahin apa bangin Pathen mitmu’n alunglhaina jeng ana bollin ahi.
4 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Ahinlah aman doiphung ho ana sumang dehpon chuleh mipihon kithoina gantha ana bollun hal namtui jong ana lhut’un ahi.
5 Bwana akampiga mfalme kwa ukoma mpaka siku aliyokufa, naye aliishi katika nyumba iliyotengwa peke yake. Yothamu mwana wa mfalme akawa msimamizi wa jumba la mfalme, na akawatawala watu wa nchi.
Pakaiyin lengpa chu anaphah sah in athini khogei jin aphah in ahi. Ama chu in chom’ah atum’in achangin ana chengin ahi. Lengpa chapa Jotham chu leng inpi ngahin anapangin ahi, hiti chun aman gamsung mite lah’a vai anahom in ahi.
6 Matukio mengine ya utawala wa Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Uzziah vaihom sunga thilsoh hole aman anatohdoh ho jouse chu Judah lengte thusim kijihlutna lekhabua aum in ahi.
7 Azaria akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika Mji wa Daudi, na Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Uzziah athiphat’in amachu David khopia apu apate kivuina munah ana kivuijin ahi. Achapa Jotham chun ama banin lengmun analo tan ahi.
8 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, naye akatawala miezi sita.
Judah lengpa Uzziah in Judah gam anapoh kum somthum le get lhinin Jeroboam ni na chapa Zechariah in Israel te chunga vai ana hom’in ahi. Aman Samaria ah lha gup vai anahom in ahi.
9 Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama baba zake walivyofanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Zechariah in apu apate bang bangin Pakai mitmu’n thilse jeng ana bollin, Nebat chapa Jeroboam min Israel te anachonset sah bangin ama jong hiche chonsetna ho akonin kile heiding ana nompon ahi.
10 Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya shauri baya dhidi ya Zekaria. Akamshambulia mbele ya watu, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Hijou chun Jabesh chapa Shallum chun Zechariah dounan lungthimse ana gongin mipi lah’a ana that in, ama leng ahung chang tan ahi.
11 Matukio mengine ya utawala wa Zekaria yameandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Zechariah vaihom sunga thilsoh ho jouse chu Israel lengte thusim kijihna lekhabua chun abon'in aum’in ahi.
12 Kwa hiyo neno la Bwana lililonenwa kwa Yehu likatimia, kwamba, “Wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
Pakaiyin Jehu kom’a anasei, “Nachilhah te khang li geija leng kachansah ding ahi,” tichu guilhun na ahi.
13 Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa thelathini na tisa wa Uzia mfalme wa Yuda, naye akatawala katika Samaria kwa mwezi mmoja.
Judah gam'a Uzziah in leng achan kal kum som thumle ko alhinin, Jebesh chapa Shallum hin Israel gamsung’a lengvai ana hom’in ahi.
14 Kisha Menahemu mwana wa Gadi akaenda kutoka Tirsa mpaka Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi huko Samaria, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Hijou chun Gadi chapa Menahem chu Tirzah a konin Samaria-ah agachen ama chu athat’in, lengmun ahin lotan ahi.
15 Matukio mengine ya utawala wa Shalumu, na mauaji aliyoyafanya, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Shallum vaihom sunga thilsoh ho chuleh alungthimse gonho pum chun, Israelte thusim kijih lutna lekhabua abonchan aum’in ahi.
16 Wakati ule, akianzia Tirsa, Menahemu alishambulia Tifsa na kila mtu ndani yake, na wale waliokuwa maeneo jirani, kwa sababu walikataa kufungua malango yao. Akaiangamiza Tifsa yote, na kuwapasua matumbo wanawake wote wenye mimba.
Hiche pat chun Menahem in Tappuah khopi leh avella gamho jouse, Tirzah geijin asumang hel in ahi, ajeh chu akhomite le akimvela mite, akhopi ho chu akoma ahin pehlut nomlou jeh’u ahi. Aman agamsung mite jouse chu athat gam’in chule numei gailai ho jong akhedoh sohkei jin ahi.
17 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, akatawala huko Samaria kwa miaka kumi.
Judah gam’ah Uzziah lengpan lengvai ana hom kal kum somthum le ko alhinin, Gadi chapa Menahem in Israel gam’ah lengvai ana hom’in ahi. Aman Samaria a hin kum som sungin lengvai ana hom’in ahi.
18 Akatenda maovu machoni pa Bwana. Katika wakati wa utawala wake wote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Ahin Menahem hin Pathen mitmu’n thilse jing anabol in ahi. Avaihom sunghin Nebat chapa Jeroboam min Israelte achonset sahna a kona kile heiding ana nompon ahi.
19 Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaishambulia Israeli. Menahemu mfalme wa Israeli akampa talanta elfu moja za fedha ili amsaidie na kumwezesha katika utawala wake.
Hijou chun Assyria mi Tiglath-pileser lengpan gamsung chu gal’in ahin nokhumtan ahi. Ahinla Menahem min athaneina a vai ahomjom jouna dingin ama chu dangka ton somthum le sagi anapen ahi.
20 Menahemu akatoza fedha hizi kwa nguvu kutoka kwa Israeli. Kila mtu tajiri alilazimika kuchanga shekeli hamsini za fedha ambazo alipewa mfalme wa Ashuru. Basi mfalme wa Ashuru akajiondoa na hakuendelea kuikalia nchi.
Menahem hin Israel mite lah’a ahaoho kom’ah sum namna in ala in, mikhat cheh chun Assyria lengpa hi dangka som nga cheh apeh diuvin thu apen ahi. Hiti chun Assyria lengpa chu Israel gam'a kon chun ahung kinungle tan ahi.
21 Matukio mengine ya utawala wa Menahemu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Menahem vaihom sunga thilsoh ho chuleh aman atoh ho jouse chu Israel lengte thusim kijihlutna lekhabua aum’in ahi.
22 Menahemu akalala pamoja na baba zake. Naye Pekahia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Menahem athiphat’in, achapa Pekahiah in leng mun ahinlo tan ahi.
23 Katika mwaka wa hamsini wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, akatawala miaka miwili.
Judah gam'a Uzziah in lengvai apoh kal kum som nga alhinin, Menahem chapa Pekahiah in Israel gam’ah lengvai ahin hompan in ahi.
24 Pekahia akafanya uovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Ahinlah Pekahiah chun Pakai mitmu’n thilse jing ana bollin, Nebat chapa Jeroboam in Israel te ana chonset sahna a kon chun kiheimang ding ana nompon ahi.
25 Mmoja wa maafisa wake wakuu, Peka mwana wa Remalia, akafanya shauri baya dhidi yake. Akachukua watu hamsini wa Gileadi pamoja naye, akamuua Pekahia, pamoja na Argobu na Aria, katika ngome ya jumba la kifalme huko Samaria. Kwa hiyo Peka akamuua Pekahia, naye akaingia mahali pake kuwa mfalme.
Hijou chun Remaliah chapa Pekah, Pekahiah sepai lamkaipa chun achung nga thilse ana gongin ahi. Aman Gilead akonin mi som nga leh Argob le Arieh toh akitho in Pekahiah chu Samria leng inpi ah chun ana that’un, hiti chun Pekah leng ahung chang tan ahi.
26 Matukio mengine ya utawala wa Pekahia na yote aliyoyafanya yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Pekahiah vaihom sunga thilsoh ho chuleh aman anatohho chu Israel lengte thusim kijihna lekhabua abonchan aum’in ahi.
27 Katika mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala miaka ishirini.
Judah gamsunga Uzziah lengpan alengvaipoh kum som nga le ni alhinin, Remaliah chapa Pekah in Israel te chungah lengvai ana hom panin ahi.
28 Akafanya maovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Pekah in Pakai mitmu’n thilse jeng anabollin, Nebat chapa Jeroboam min Israelte ana chonset sahna a kona kinnung heiding chu ana nompon ahi.
29 Wakati wa utawala wa Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alikuja na kuteka Iyoni, Abel-Beth-Maaka, Yanoa, Kedeshi na Hazori. Akateka miji ya Gileadi na Galilaya, pamoja na nchi yote ya Naftali, na kuwahamishia watu wote Ashuru.
Pekah vaihom sungin Assyria lengpa Tiglath-pileser in Israel ahin sat in Ijon khopi, Abel-beth-maacah, Janoah, Kedesh, leh Hazor khopi ho ana kilahtan ahi. Aman Gilead gam leh avel ho, Galilee chule Naphtali ho ajouvin chuleh mipiho chu Assyria gam’ah gal hing in ana kaimang tan ahi.
30 Kisha Hoshea mwana wa Ela akafanya shauri baya dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akamshambulia na kumuua, kisha akaingia mahali pake kuwa mfalme katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
Hijou chun Elah chapa Hoshea chun Pekah douna lungthim phalou ana gongin, ana that dohtan ahi. Aman Uzziah chapa Jotham vaihom kal kum somni lhinin Israel chunga lengvai anahom pantan ahi.
31 Matukio mengine ya utawala wa Peka na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Pekah vaihom sunga thilsoh ho, aman anatoh ho chu Israel lengte thusim kijihna lekhabua aum’in ahi.
32 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Uzia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
Pekah lengpan Israel gamsunga lengvai apoh kal kum ni lhinin, Uzziah chapa Jotham in Judah gam’ah lengvai anahom’in ahi.
33 Alikuwa na miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Aman lengvai ahinpoh chun ama kum somni le nga alhingtan ahi. Aman Jerusalem’ah kum somle gup sungin lengvai anahom in ahi. Anu min chu Zadok chanu Jerusha ahi.
34 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya.
Jotham hin Pakai mitmu’n thilpha jeng ana bollin, amahin apa Uzziah in bangin thil ijakai ana tongdoh sohkeijin ahi.
35 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko. Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana.
Ahinlah aman doiphung ho chu ana sumang pon chuleh mipiho chun hikoma chu kilhaina gantha le gimnamtui jong ana lhut’un ahi. Aman Pakai houin sahlam kelkot jong chu ana semphan ahi.
36 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Jotham vaihom sunga thilsoh jouse leh aman ana thilbol jouse Judah lengte thusimbua akijih lut soh keijin ahi.
37 (Katika siku hizo, Bwana akaanza kuwatuma Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia dhidi ya Yuda.)
Hiche nikholai chun, Pakaiyin Syria lengpa Rezin leh Israel lengpa Pekah chu Judah nokhum dingin ahin solpan tan ahi.
38 Yothamu akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi, mji wa baba zake. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Jotham athiphat’in David khopia apu apate kivuina munah ana vuikhom tauvin ahi. Akhelin achapa Ahaz chun lengvai ahinpo tan ahi.

< 2 Wafalme 15 >