< 2 Wafalme 15 >

1 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
Israel manghai Jeroboam kah kum kul kum rhih dongah Judah manghai Amaziah capa Azariah te manghai van.
2 Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
Anih te kum hlai rhuk a lo ca vaengah manghai coeng tih Jerusalem ah sawmnga kum nit manghai. A manu ming tah Jerusalem lamkah Jekoliah ni.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
A napa Amaziah loh a cungkuem a saii vanbangla BOEIPA mikhmuh ah a thuem ni a. saii van.
4 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Tedae hmuensang te a khoe moenih. Hmuensang ah pilnam a nawn tih a phum pueng.
5 Bwana akampiga mfalme kwa ukoma mpaka siku aliyokufa, naye aliishi katika nyumba iliyotengwa peke yake. Yothamu mwana wa mfalme akawa msimamizi wa jumba la mfalme, na akawatawala watu wa nchi.
BOEIPA loh manghai te a ben dongah a dueknah hnin duela pahuk. Te dongah im hloeh la om tih im ah manghai capa Jotham loh khohmuen pilnam te lai a tloek pah.
6 Matukio mengine ya utawala wa Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Azariah kah ol noi neh a cungkuem a saii te Judah manghai rhoek kah khokhuen olka cabu dongah a daek moenih a?
7 Azaria akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika Mji wa Daudi, na Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Azariah te a napa rhoek taengla a khoem uh vaengah anih te David khopuei kah a napa taengah a up uh. Te phoeiah a capa Jotham te anih yueng la manghai.
8 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, naye akatawala miezi sita.
Judah manghai Azariah kah a kum sawmthum kum rhet vaengah Samaria kah Israel te Jeroboam capa Zekhariah loh hla rhuk a manghai thil.
9 Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama baba zake walivyofanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
A napa rhoek kah a saii bangla BOEIPA mik ah boethae ni a. saii. Israel aka tholh sak Nebat capa Jeroboam kah tholhnah lamloh a nong moenih.
10 Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya shauri baya dhidi ya Zekaria. Akamshambulia mbele ya watu, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Jabesh capa Shallum loh anih te a taeng tih pilnam mikhmuh ah anih te a ngawn. Anih te a ngawn van nen tah anih yuengla manghai.
11 Matukio mengine ya utawala wa Zekaria yameandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Zekhariah kah ol noi khaw Israel manghai rhoek kah khokhuen olka cabu dongah a daek uh coeng ne.
12 Kwa hiyo neno la Bwana lililonenwa kwa Yehu likatimia, kwamba, “Wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
Jehu taengah BOEIPA ol a thui pah bangla, “Nang lamkah a khong li ca hil tah Israel ngolkhoel dongah ngol ni,” a ti nah te thoeng tangloeng coeng.
13 Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa thelathini na tisa wa Uzia mfalme wa Yuda, naye akatawala katika Samaria kwa mwezi mmoja.
Judah manghai Uzziah kah kum sawmthum kum ko vaengah Jabesh capa Shallum manghai tih Samaria ah hla khat hnin khat manghai.
14 Kisha Menahemu mwana wa Gadi akaenda kutoka Tirsa mpaka Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi huko Samaria, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Te phoeiah tah Tirzah lamkah Gadi capa Menahem te cet tih Samaria la pawk. Te vaengah Samaria kah Jabesh capa Shallum te a ngawn tih anih a duek sak phoeiah tah anih yueng la manghai.
15 Matukio mengine ya utawala wa Shalumu, na mauaji aliyoyafanya, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Shallum kah ol noi khaw, lairhui loh anih a ven te khaw Israel manghai rhoek kah khokhuen olka cabu dongah a daek uh coeng he.
16 Wakati ule, akianzia Tirsa, Menahemu alishambulia Tifsa na kila mtu ndani yake, na wale waliokuwa maeneo jirani, kwa sababu walikataa kufungua malango yao. Akaiangamiza Tifsa yote, na kuwapasua matumbo wanawake wote wenye mimba.
Tiphsah Menahem neh a khuikah boeih khaw, Tirzah lamloh a khorhi te khaw a tloek. Thoh a ong pah pawt dongah bungvawn boeih te khaw a ngawn tih a bung a boe pah.
17 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, akatawala huko Samaria kwa miaka kumi.
Judah manghai Azariah kah a kum sawmthum kum ko vaengah Samaria kah Gadi capa Menahem loh Israel te kum rha a manghai thil.
18 Akatenda maovu machoni pa Bwana. Katika wakati wa utawala wake wote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Amah tue khuiah tah BOEIPA mikhmuh ah boethae a saii tih Israel aka tholh sak Nebat capa Jeroboam kah tholhnah lamloh a nong moenih.
19 Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaishambulia Israeli. Menahemu mfalme wa Israeli akampa talanta elfu moja za fedha ili amsaidie na kumwezesha katika utawala wake.
Assyria manghai Pul loh khohmuen a muk vaengah anih neh kut at la om ham khaw, amah kut ah ram duel ham khaw Menahem loh Pul taengah tangka talent thawng khat a paek.
20 Menahemu akatoza fedha hizi kwa nguvu kutoka kwa Israeli. Kila mtu tajiri alilazimika kuchanga shekeli hamsini za fedha ambazo alipewa mfalme wa Ashuru. Basi mfalme wa Ashuru akajiondoa na hakuendelea kuikalia nchi.
Menahem loh tangka te Israel taeng lamkah khaw, tatthai hlangrhalh boeih taeng lamkah khaw a khuen. Assyria manghai taengah a paek ham te hlang khat ah tangka shekel sawmnga a coi pah daengah Assyria manghai te khoe uh tih khohmuen ah khosa pawh.
21 Matukio mengine ya utawala wa Menahemu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Menahem kah ol noi neh a saii boeih te Israel manghai rhoek kah khokhuen olka cabu dongah a daek uh moenih a?
22 Menahemu akalala pamoja na baba zake. Naye Pekahia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Menahem te a napa rhoek taengla a khoem uh neh a capa Pekahiah te anih yueng la manghai.
23 Katika mwaka wa hamsini wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, akatawala miaka miwili.
Judah manghai Azariah kah kum sawmnga kum vaengah Menahem capa Pekahiah tah Samaria ah Israel kum nit a manghai thil.
24 Pekahia akafanya uovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
BOEIPA mikhmuh ah boethae a saii tih Israel aka tholh sak Nebat capa Jeroboam kah tholhnah lamloh a nong moenih.
25 Mmoja wa maafisa wake wakuu, Peka mwana wa Remalia, akafanya shauri baya dhidi yake. Akachukua watu hamsini wa Gileadi pamoja naye, akamuua Pekahia, pamoja na Argobu na Aria, katika ngome ya jumba la kifalme huko Samaria. Kwa hiyo Peka akamuua Pekahia, naye akaingia mahali pake kuwa mfalme.
Anih te a rhalboei Remaliah capa Pekah loh a taeng. Te dongah anih te Argob neh, Arieh neh, a taengkah Giladi ca rhoek lamkah hlang sawmnga loh Samaria kah manghai manghai im, impuei ah a ngawn. Anih te a duek sak phoeiah tah a yueng la amah tloep manghai.
26 Matukio mengine ya utawala wa Pekahia na yote aliyoyafanya yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Pekahiah kah ol noi neh a saii boeih te Israel manghai rhoek kah khokhuen olka cabu dongah a daek uh coeng he.
27 Katika mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala miaka ishirini.
Judah manghai Azariah kah kum sawmnga kum nit dongah Remaliah capa Pekah loh Samaria ah Israel kum kul a manghai thil.
28 Akafanya maovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
BOEIPA mikhmuh ah boethae a saii tih Israel aka tholh sak Nebat capa Jeroboam kah tholhnah lamloh a nong moenih.
29 Wakati wa utawala wa Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alikuja na kuteka Iyoni, Abel-Beth-Maaka, Yanoa, Kedeshi na Hazori. Akateka miji ya Gileadi na Galilaya, pamoja na nchi yote ya Naftali, na kuwahamishia watu wote Ashuru.
Israel manghai Pekah tue vaengah Assyria manghai Tiglathpileser loh a paan tih Ijon, Abel, Janoah, Kedesh neh Hazor, Gilead, Galilee neh Naphtali khohmuen pum te a loh pah. Te phoeiah amih te Assyria la a poelyoe.
30 Kisha Hoshea mwana wa Ela akafanya shauri baya dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akamshambulia na kumuua, kisha akaingia mahali pake kuwa mfalme katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
Elah capa Hosea loh Remaliah capa Pekah te lairhui a sui thil. Pekah te a ngawn tih a duek sak phoeiah tah Uzziah capa Jotham kah a kum kul vaengah Pekah yueng la manghai.
31 Matukio mengine ya utawala wa Peka na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Pekah kah ol noi neh a saii boeih te Israel manghai rhoek kah khokhuen olka cabu dongah a daek uh coeng he.
32 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Uzia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
Israel manghai Remaliah capa Pekah kah a kum bae dongah Judah manghai Uzziah capa Jotham manghai van.
33 Alikuwa na miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Anih te kum kul kum nga a lo ca vaengah manghai tih Jerusalem ah kum hlai rhuk manghai. A manu ming tah Zadok canu Jerusha ni.
34 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya.
BOEIPA mikhmuh ah a thuem ni a. saii. A cungkuem dongah a napa Uzziah kah a saii bangla a saii.
35 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko. Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana.
Te cakhaw hmuensang te a khoe moenih. Hmuensang ah pilnam a nawn tih a phum pueng. Anih loh BOEIPA im kah imhman vongka te a saii.
36 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Jotham kah ol noi neh a bi saii te Judah manghai rhoek kah khokhuen olka cabu dongah a daek uh moenih a?
37 (Katika siku hizo, Bwana akaanza kuwatuma Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia dhidi ya Yuda.)
Te vaeng tue ah ana tong tih BOEIPA loh Judah taengla Aram manghai Rezin neh Remaliah capa Pekah te a tueih coeng.
38 Yothamu akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi, mji wa baba zake. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Jotham te a napa rhoek taengla a khoem uh vaengah a napa David khopuei kah a napa rhoek taengah a up. Te phoeiah a capa Ahaz te anih yueng la manghai.

< 2 Wafalme 15 >