< 2 Wafalme 15 >

1 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
В двадесет и седмата година на Израилевия цар Еровоама, се възцари Азария, син на Юдовия цар Амасия.
2 Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
Той беше шестнадест години на възраст когато се възцари, и царува петдесет и две години в Ерусалим; и името на майка му бе Ехолия, от Ерусалим.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
Той върши това, което бе право пред Господа, напълно според както беше сторил баща му Амасия.
4 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Но високите места не се отмахнаха; людете още жертвуваха и кадяха по високите места.
5 Bwana akampiga mfalme kwa ukoma mpaka siku aliyokufa, naye aliishi katika nyumba iliyotengwa peke yake. Yothamu mwana wa mfalme akawa msimamizi wa jumba la mfalme, na akawatawala watu wa nchi.
Но Господ порази царя, така щото той остана прокажен до деня на смъртта си, та живееше в отделна къща. А царският син Иотам бе домовладетел, и съдеше людете на земята.
6 Matukio mengine ya utawala wa Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
А останалите дела на Азария, и всичко що извърши, не са ли написани в Книгата на летописите на Юдовите царе?
7 Azaria akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika Mji wa Daudi, na Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
И Азария заспа с бащите си, и погребаха го с бащите му в Давидовия град; и вместо него се възцари син му Иотам.
8 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, naye akatawala miezi sita.
В тридесет и осмата година на Юдовия цар Азария, се възцари над Израиля в Самария Захария Еровоамовия син, и царува шест месеца.
9 Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama baba zake walivyofanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Той върши зло пред Господа, както сториха бащите му; не се остави от греховете на Еровоама Наватовия син, с които направи Изралия да греши.
10 Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya shauri baya dhidi ya Zekaria. Akamshambulia mbele ya watu, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
А Салум, Явисовият син, направи заговор против него, и порази го пред людете и го уби; и вместо него сам се възцари.
11 Matukio mengine ya utawala wa Zekaria yameandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
А останалите дела на Захария, ето, написани са в Книгата на летописите на Израилевите царе.
12 Kwa hiyo neno la Bwana lililonenwa kwa Yehu likatimia, kwamba, “Wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
Това беше изпълнение на словото, което Господ говори на Ииуя като рече: Твоите синове ще седят на Израилевия престол до четвъртото поколение. Така и стана.
13 Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa thelathini na tisa wa Uzia mfalme wa Yuda, naye akatawala katika Samaria kwa mwezi mmoja.
Салум, Явисовият син, се възцари в тридесет и деветата година на Юдовия цар Озия, и царува един месец в Самария.
14 Kisha Menahemu mwana wa Gadi akaenda kutoka Tirsa mpaka Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi huko Samaria, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Защото Манаим, Гадииният син, като излезе от Терса, дойде в Самария, и като порази Самума, Ависовия син в Самария и го уби, сам се възцари вместо него.
15 Matukio mengine ya utawala wa Shalumu, na mauaji aliyoyafanya, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
А останалите дела на Салума, и заговорът, който направи, ето, написани са в Книгата на летописите на Израилевите царе.
16 Wakati ule, akianzia Tirsa, Menahemu alishambulia Tifsa na kila mtu ndani yake, na wale waliokuwa maeneo jirani, kwa sababu walikataa kufungua malango yao. Akaiangamiza Tifsa yote, na kuwapasua matumbo wanawake wote wenye mimba.
Тогава Манаим порази Тапса и всичко що ме в нея, и околностите й, от Терса. Порази я понеже не му отвориха; и разпра всички бременни жени в нея.
17 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, akatawala huko Samaria kwa miaka kumi.
В тридесет и деветата година на Юдовият цар Азария, се възцари над Израиля Манаим, Гадииният син, и царува десет години в Самария.
18 Akatenda maovu machoni pa Bwana. Katika wakati wa utawala wake wote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Той върши зло пред Господа; през целия си живот не се оставяше от греховете на Еровоама, Наватовия син, с които направи Израиля да греши.
19 Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaishambulia Israeli. Menahemu mfalme wa Israeli akampa talanta elfu moja za fedha ili amsaidie na kumwezesha katika utawala wake.
Тогава асирийският цар Фул дойде против земята; а Манаим даде на Фула хиляда таланта сребро, за да му помогне да закрепи царството в ръката си.
20 Menahemu akatoza fedha hizi kwa nguvu kutoka kwa Israeli. Kila mtu tajiri alilazimika kuchanga shekeli hamsini za fedha ambazo alipewa mfalme wa Ashuru. Basi mfalme wa Ashuru akajiondoa na hakuendelea kuikalia nchi.
И Манаим с несилие събра среброто от Израиля, от всичките големи богаташи по петдесет сребърни сикли, за да даде на асирийския цар. И така асирийският цар се върна, и не остана там в земята.
21 Matukio mengine ya utawala wa Menahemu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
А останалите дела на Манаима, и всичко що извърши, не са ли написани в Книгата на летописите на Израилевите царе?
22 Menahemu akalala pamoja na baba zake. Naye Pekahia mwanawe akawa mfalme baada yake.
И Манаим заспа с бащите си; и вместо него се възцари син му Факия.
23 Katika mwaka wa hamsini wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, akatawala miaka miwili.
В петдесетата година на Юдовия цар Азария, се възцари над Израиля в Самария Факия, Манаимовият син, и царува две години.
24 Pekahia akafanya uovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Той върши зло пред Господа; не се остави от греховете на Еровоама, Наватовия син, с които направи Израиля да греши.
25 Mmoja wa maafisa wake wakuu, Peka mwana wa Remalia, akafanya shauri baya dhidi yake. Akachukua watu hamsini wa Gileadi pamoja naye, akamuua Pekahia, pamoja na Argobu na Aria, katika ngome ya jumba la kifalme huko Samaria. Kwa hiyo Peka akamuua Pekahia, naye akaingia mahali pake kuwa mfalme.
И полководецът му Факей, Ромелиевият син, направи заговор против него та го порази в Самария, във вътрешната царска къща, с Аргова и Арие, като имаше със себе си и петдесет мъже от галаадците; и уби го та сам се възцари вместо него.
26 Matukio mengine ya utawala wa Pekahia na yote aliyoyafanya yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
А останалите дела на Факия, и всичко що извърши, ето, написани са в Книгата на летописите на Израилевите царе.
27 Katika mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala miaka ishirini.
В петдесет и втората година на Юдовия цар Азария, се възцари над Израиля в Самария Факей, Ромеловият син, и царува двадесет години.
28 Akafanya maovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Той върши зло пред Господа; не се остави от греховете на Еровоама, Наватовия син, с които направи Израиля да греши.
29 Wakati wa utawala wa Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alikuja na kuteka Iyoni, Abel-Beth-Maaka, Yanoa, Kedeshi na Hazori. Akateka miji ya Gileadi na Galilaya, pamoja na nchi yote ya Naftali, na kuwahamishia watu wote Ashuru.
В дните на Израилевия цар Факей, дойде асирийският царТеглат-феласар та превзе Иион, Авел-вет-мааха, Янох, Кадес, Асор, Галаад и Галилея цялата Нефталимова земя, и заведе жителите им пленници в Асирия.
30 Kisha Hoshea mwana wa Ela akafanya shauri baya dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akamshambulia na kumuua, kisha akaingia mahali pake kuwa mfalme katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
А Осия, син на Ила, направи заговор против Факея Ромелиевия син и като го порази, уби го, и сам се възцари вместо него в двадесетата година на Иотама, Озиевия син.
31 Matukio mengine ya utawala wa Peka na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
А останалите дела на Факея, и всичко що извърши, ето написани са в Книгата на летописите на Израилевите царе.
32 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Uzia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
Във втората година на Израилевия цар Факей, Ромелиевия син, се възцари Иотам, син на Юдовия цар Озия.
33 Alikuwa na miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Той беше двадесет и пет години на възраст, когато се възцари и царува шестнадесет години в Ерусалим; а името на майка му бе Еруса Садокова дъщеря.
34 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya.
Той върши това, което бе право пред Господа; постъпваше съвсем както бе направил баща му Озия.
35 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko. Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana.
Но високите места не се отмахнаха; людете още жертвуваха и кадяха по високите места. Той построи горната порта на Господния дом.
36 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
А останалите дела на Иотама, и всичко що извърши, не са ли написани в Книгата на летописите на Юдовите царе?
37 (Katika siku hizo, Bwana akaanza kuwatuma Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia dhidi ya Yuda.)
В онова време Господ почна да праща против Юда сирийския цар Расин и Факея, Ромелиевия син.
38 Yothamu akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi, mji wa baba zake. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
А Иотам заспа с бащите си и биде погребан с бъщите си в града на баща си Давида; и вместо него се възцари син ме Ахаз.

< 2 Wafalme 15 >