< 2 Wafalme 14 >
1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
Amasías, hijo de Joás, llegó a ser rey de Judá en el segundo año del reinado de Joás, hijo de Joacaz, rey de Israel.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani, kutoka Yerusalemu.
Tenía veinticinco años cuando llegó a ser rey, y reinó en Jerusalén durante veintinueve años. Su madre se llamaba Joadán de Jerusalén.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kama Daudi baba yake alivyokuwa amefanya. Katika kila kitu alifuata mfano wa Yoashi baba yake.
Hizo lo que era correcto a los ojos del Señor, pero no de la misma manera que su antepasado David. Hizo todo como lo había hecho su padre Joás.
4 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Pero los altares paganos no fueron destruidos. El pueblo seguía sacrificando y presentando holocaustos en esos lugares.
5 Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
Una vez que estuvo seguro en el trono, ejecutó a los funcionarios que habían asesinado a su padre el rey.
6 Hata hivyo, hakuwaua wana wa wale wauaji, sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose ambako Bwana aliamuru, “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
Pero no ejecutó a los hijos de los asesinos, siguiendo el mandato del Señor en la ley de Moisés: “Los padres no deben morir por los pecados de sus hijos, ni los hijos deben morir por los pecados de sus padres. Cada uno debe morir por su propio pecado”.
7 Ndiye aliwashinda Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi, na akauteka Sela katika vita, naye akauita Yoktheeli, jina ambalo mji huo unalo hadi leo.
Amasías mató a diez mil edomitas en el Valle de la Sal. Atacó y capturó Sela y la rebautizó como Joktheel, que es como se llama hasta hoy.
8 Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tuonane uso kwa uso.”
Amasías envió mensajeros al rey de Israel, Joás, hijo de Joacaz, hijo de Jehú, diciéndole: “Luchemos, cara a cara!”
9 Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda: “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
Joás, rey de Israel, respondió a Amasías, rey de Judá: “En el Líbano, un cardo envió un mensaje a un cedro, diciendo: ‘Dale tu hija como esposa a mi hijo’. Pero pasó un animal salvaje del Líbano y pisoteó el cardo.
10 Hakika umeishinda Edomu, na sasa unajivuna. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini unachokoza na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
Puede que hayas derrotado a Edom. Ahora te has vuelto arrogante. Quédate en casa y disfruta de tu victoria. ¿Por qué provocar problemas que te harán caer a ti, y a Judá contigo?”
11 Hata hivyo, Amazia hakusikia, hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
Pero Amasías se negó a escuchar, así que Joás, rey de Israel, vino a atacarlo. Él y Amasías, rey de Judá, se encontraron cara a cara en Bet Semes, en Judá.
12 Yuda ikashindwa na Israeli, na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
El ejército de Judá fue derrotado por Israel y huyó a su casa.
13 Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akaenda Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
Joás, rey de Israel, capturó a Amasías, rey de Judá, hijo de Joás, hijo de Ocozías, en Bet Semes. Entonces Joás atacó Jerusalén y derribó la muralla de la ciudad desde la puerta de Efraín hasta la puerta de la Esquina, de unos cuatrocientos codos de longitud.
14 Akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina zote za jumba la mfalme. Akachukua pia mateka na akarudi Samaria.
Se llevó todo el oro y la plata, y todos los objetos que se encontraban en el Templo del Señor y en los tesoros del palacio real, y también algunos rehenes. Luego regresó a Samaria.
15 Matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita vyake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
El resto de lo que sucedió en el reinado de Joás, todo lo que hizo y sus grandes logros y su guerra con Amasías, rey de Judá, están registrados en el Libro de las Crónicas de los Reyes de Israel.
16 Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli, naye Yeroboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Joás murió y fue enterrado en Samaria con los reyes de Israel. Su hijo Jeroboam le sucedió como rey.
17 Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
Amasías, hijo de Joás, rey de Judá, vivió quince años más después de la muerte de Joás, hijo de Joacaz, rey de Israel.
18 Matukio mengine ya utawala wa Amazia, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
El resto de los acontecimientos que ocurrieron en el reinado de Amasías están registrados en el Libro de las Crónicas de los Reyes de Judá.
19 Wakafanya shauri baya dhidi ya Amazia huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi, nao wakamuulia huko.
Una conspiración contra Amasías tuvo lugar en Jerusalén, y él huyó a Laquis. Pero se enviaron hombres tras él y lo asesinaron allí.
20 Akarudishwa kwa farasi na akazikwa huko Yerusalemu pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi.
Lo trajeron de vuelta a caballo y lo enterraron en Jerusalén con sus antepasados en la Ciudad de David.
21 Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, na kumfanya mfalme mahali pa baba yake Amazia.
Entonces todo el pueblo de Judá nombró rey al hijo de Amasías, Azarías, para que reemplazara a su padre. Azarías tenía dieciséis años.
22 Ndiye aliijenga tena Elathi na kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
Azarías reconquistó Elat para Judá y la reconstruyó después de la muerte de su padre.
23 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala huko Samaria, naye akatawala kwa miaka arobaini na mmoja.
Jeroboam, hijo de Joás, llegó a ser rey de Israel en el año quince del reinado de Amasías, hijo de Joás, rey de Judá. Reinó en Samaria durante cuarenta y un años.
24 Akafanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi hata moja ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
Hizo lo malo a los ojos del Señor y no puso fin a todos los pecados que Jeroboam, hijo de Nabat, había hecho cometer a Israel.
25 Ndiye alirudishia mipaka ya Israeli kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bahari ya Araba, sawasawa na neno la Bwana, Mungu wa Israeli, lililosemwa kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-Heferi.
Restituyó la frontera de Israel a donde estaba, desde Lebó-Jamat hasta el Mar de la Arabá, como el Señor, el Dios de Israel, había dicho por medio de su siervo Jonás, hijo de Amitai, el profeta, que venía de Gat-Jefer.
26 Bwana alikuwa ameona jinsi kila mmoja katika Israeli, awe mtumwa au aliye huru, alivyoteseka kwa uchungu; hapakuwepo na yeyote wa kuwasaidia.
El Señor había visto lo mucho que estaban sufriendo los israelitas, tanto los esclavos como los libres. Nadie estaba allí para ayudar a Israel.
27 Kwa kuwa Bwana alikuwa hajasema kuwa atafuta jina la Israeli chini ya mbingu, akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
Sin embargo, como el Señor había dicho que no eliminaría a Israel, lo salvó por medio de Jeroboam, hijo de Joás.
28 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, yote aliyoyafanya na mafanikio yake ya kijeshi, ikiwa ni pamoja na jinsi alivyorudisha Dameski na Hamathi kwa Israeli, ambayo ilikuwa mali ya Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
El resto de lo que sucedió en el reinado de Jeroboam, todo lo que hizo, sus grandes logros y las batallas que libró, y cómo recuperó para Israel tanto Damasco como Jamat, están registrados en el Libro de las Crónicas de los Reyes de Israel.
29 Yeroboamu akalala pamoja na baba zake, wafalme wa Israeli. Naye Zekaria mwanawe akawa mfalme baada yake.
Jeroboam murió y fue enterrado con los reyes de Israel. Su hijo Zacarías le sucedió como rey.