< 2 Wafalme 14 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
No segundo ano de Joás, filho de Joaaz, rei de Israel, o Amazonas, filho de Joás, rei de Judá, começou a reinar.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani, kutoka Yerusalemu.
Ele tinha vinte e cinco anos quando começou a reinar; e reinou vinte e nove anos em Jerusalém. O nome de sua mãe era Jehoaddin de Jerusalém.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kama Daudi baba yake alivyokuwa amefanya. Katika kila kitu alifuata mfano wa Yoashi baba yake.
Ele fez o que era certo aos olhos de Iavé, mas não como Davi, seu pai. Ele fez de acordo com tudo o que Joás, seu pai, havia feito.
4 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
No entanto, os lugares altos não foram tirados. O povo ainda sacrificou e queimou incenso nos lugares altos.
5 Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
Assim que o reino foi estabelecido em suas mãos, ele matou seus servos que haviam matado o rei seu pai,
6 Hata hivyo, hakuwaua wana wa wale wauaji, sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose ambako Bwana aliamuru, “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
mas os filhos dos assassinos que ele não matou, de acordo com o que está escrito no livro da lei de Moisés, como mandou Javé, dizendo: “Os pais não serão mortos pelos filhos, nem os filhos serão mortos pelos pais; mas cada homem morrerá por seu próprio pecado”.
7 Ndiye aliwashinda Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi, na akauteka Sela katika vita, naye akauita Yoktheeli, jina ambalo mji huo unalo hadi leo.
Ele matou dez mil Edomitas no Vale do Sal, e tomou Sela pela guerra, e chamou seu nome de Joktheel, até hoje.
8 Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tuonane uso kwa uso.”
Então Amaziah enviou mensageiros a Jehoash, o filho de Jehoahaz, filho de Jeú, rei de Israel, dizendo: “Venham, vamos nos olhar na cara”.
9 Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda: “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
Jehoash o rei de Israel enviou ao Amazonas, rei de Judá, dizendo: “O cardo que estava no Líbano enviou ao cedro que estava no Líbano, dizendo: 'Dê sua filha a meu filho como esposa'. Então passou um animal selvagem que estava no Líbano, e pisoteou o cardo.
10 Hakika umeishinda Edomu, na sasa unajivuna. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini unachokoza na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
Você realmente atingiu Edom, e seu coração o levantou. Desfrute a glória disso, e fique em casa; pois por que você deveria se intrometer em seu mal, para que você caia, até mesmo você, e Judá com você”?
11 Hata hivyo, Amazia hakusikia, hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
Mas o Amaziah não quis ouvir. Então Jeoás, rei de Israel, subiu; e ele e o Amazias, rei de Judá, olharam um para o outro no rosto de Beth Shemesh, que pertence a Judá.
12 Yuda ikashindwa na Israeli, na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
Judá foi derrotado por Israel; e cada homem fugiu para sua tenda.
13 Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akaenda Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
Jeoás, rei de Israel, levou o Amazias, rei de Judá, filho de Jeoás, filho de Acazias, a Bete-Semes e veio a Jerusalém, depois derrubou o muro de Jerusalém desde a porta de Efraim até a porta da esquina, quatrocentos côvados.
14 Akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina zote za jumba la mfalme. Akachukua pia mateka na akarudi Samaria.
Ele levou todo o ouro e prata e todos os vasos que foram encontrados na casa de Iavé e nos tesouros da casa do rei, os reféns também, e voltou para Samaria.
15 Matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita vyake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Agora o resto dos atos de Jeoás que ele fez, e seu poder, e como ele lutou com o Amazonas, rei de Judá, não estão escritos no livro das crônicas dos reis de Israel?
16 Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli, naye Yeroboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Jeoás dormiu com seus pais, e foi enterrado em Samaria com os reis de Israel; e Jeroboão seu filho reinou em seu lugar.
17 Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
Amaziah, filho de Joás, rei de Judá, viveu após a morte de Jeoás, filho de Jeoacaz, rei de Israel, quinze anos.
18 Matukio mengine ya utawala wa Amazia, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Agora o resto dos atos do Amazonas, não estão escritos no livro das crônicas dos reis de Judá?
19 Wakafanya shauri baya dhidi ya Amazia huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi, nao wakamuulia huko.
Eles fizeram uma conspiração contra ele em Jerusalém, e ele fugiu para Laquis; mas mandaram atrás dele para Laquis e o mataram lá.
20 Akarudishwa kwa farasi na akazikwa huko Yerusalemu pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi.
Eles o trouxeram em cavalos, e ele foi enterrado em Jerusalém com seus pais, na cidade de Davi.
21 Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, na kumfanya mfalme mahali pa baba yake Amazia.
Todo o povo de Judá tomou Azarias, que tinha dezesseis anos de idade, e o fez rei no lugar de seu pai Amazonas.
22 Ndiye aliijenga tena Elathi na kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
Ele construiu Elath e o restituiu a Judá. Depois disso, o rei dormiu com seus pais.
23 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala huko Samaria, naye akatawala kwa miaka arobaini na mmoja.
No décimo quinto ano do Amazonas, filho de Joás, rei de Judá, Jeroboão, filho de Joás, rei de Israel, começou a reinar em Samaria por quarenta e um anos.
24 Akafanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi hata moja ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
Ele fez o que era mau aos olhos de Iavé. Ele não se afastou de todos os pecados de Jeroboão, filho de Nebate, com os quais ele fez Israel pecar.
25 Ndiye alirudishia mipaka ya Israeli kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bahari ya Araba, sawasawa na neno la Bwana, Mungu wa Israeli, lililosemwa kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-Heferi.
Ele restaurou a fronteira de Israel desde a entrada de Hamath até o mar de Arabah, segundo Javé, a palavra do Deus de Israel, que ele falou por seu servo Jonas, filho de Amitai, o profeta, que era de Gate Hepher.
26 Bwana alikuwa ameona jinsi kila mmoja katika Israeli, awe mtumwa au aliye huru, alivyoteseka kwa uchungu; hapakuwepo na yeyote wa kuwasaidia.
Para Javé viu a aflição de Israel, que era muito amarga para todos, escrava e livre; e não havia nenhum ajudante para Israel.
27 Kwa kuwa Bwana alikuwa hajasema kuwa atafuta jina la Israeli chini ya mbingu, akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
Javé não disse que apagaria o nome de Israel de debaixo do céu; mas ele os salvou pela mão de Jeroboão, o filho de Joás.
28 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, yote aliyoyafanya na mafanikio yake ya kijeshi, ikiwa ni pamoja na jinsi alivyorudisha Dameski na Hamathi kwa Israeli, ambayo ilikuwa mali ya Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Agora o resto dos atos de Jeroboão, e tudo o que ele fez, e seu poder, como ele lutou, e como ele recuperou Damasco, e Hamath, que tinha pertencido a Judá, para Israel, não estão escritos no livro das crônicas dos reis de Israel?
29 Yeroboamu akalala pamoja na baba zake, wafalme wa Israeli. Naye Zekaria mwanawe akawa mfalme baada yake.
Jeroboão dormiu com seus pais, mesmo com os reis de Israel; e Zacarias, seu filho, reinou em seu lugar.

< 2 Wafalme 14 >