< 2 Wafalme 14 >
1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
Jehoasa, Joakasa dēla, Israēla ķēniņa, otrā gadā Amacīja, Joasa, Jūda ķēniņa, dēls palika par ķēniņu.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani, kutoka Yerusalemu.
Divdesmit pieci gadus viņš bija vecs, kad palika par ķēniņu, un valdīja divdesmit deviņus gadus Jeruzālemē, un viņa mātei bija vārds Joadane no Jeruzālemes.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kama Daudi baba yake alivyokuwa amefanya. Katika kila kitu alifuata mfano wa Yoashi baba yake.
Un viņš darīja, kas Tam Kungam labi patika, tomēr ne tā kā viņa tēvs Dāvids, bet kā viņa tēvs Joas, tā viņš darīja.
4 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Tikai kalnu altāri netapa nopostīti; tie ļaudis upurēja un kvēpināja vēl uz kalniem.
5 Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
Un kad viņš bija stiprinājies savā valstībā, tad tas nokāva savus kalpus, kas viņa tēvu, to ķēniņu, bija nokāvuši.
6 Hata hivyo, hakuwaua wana wa wale wauaji, sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose ambako Bwana aliamuru, “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
Bet to slepkavu bērnus viņš nenokāva, kā rakstīts ir Mozus bauslības grāmatā, kur Tas Kungs pavēlējis sacīdams: tēviem nebūs tapt nokautiem par bērniem, un bērniem nebūs tapt nokautiem par tēviem, bet ikkatram būs tapt nokautam par saviem paša grēkiem.
7 Ndiye aliwashinda Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi, na akauteka Sela katika vita, naye akauita Yoktheeli, jina ambalo mji huo unalo hadi leo.
Viņš kāva Edomiešus sāls ielejā desmit tūkstošus un uzņēma Selu kaujā, un nosauca viņas vārdu Jokteēli līdz šai dienai.
8 Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tuonane uso kwa uso.”
Tad Amacīja sūtīja vēstnešus pie Jehoasa, Joakasa dēla, Jeūs dēla dēla, Israēla ķēniņa, un lika sacīt: nāc, skatīsimies acīs.
9 Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda: “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
Bet Jehoas, Israēla ķēniņš, sūtīja pie Amacījas, Jūda ķēniņa, un lika sacīt: Lībanus ērkšķu krūms sūtīja pie Lībanus ciedru koka, sacīdams: dod savu meitu manam dēlam par sievu. Bet Lībanus lauka zvēri gāja pāri un samina to ērkšķu krūmu.
10 Hakika umeishinda Edomu, na sasa unajivuna. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini unachokoza na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
Tu gan Edomu esi kāvis, - tāpēc tava sirds lepojās. Paturi to godu un paliec mājās, kāpēc tu gribi dzīties pēc nelaimes, ka tu krīti un Jūda līdz ar tevi?
11 Hata hivyo, Amazia hakusikia, hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
Bet Amacīja neklausīja. Tad Jehoas, Israēla ķēniņš, nāca un Amacīja, Jūda ķēniņš, saskatījās acīs pie BetŠemesas Jūda zemē.
12 Yuda ikashindwa na Israeli, na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
Un Jūda tapa sakauts no Israēla un tie bēga ikkatrs savā dzīvoklī.
13 Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akaenda Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
Un Jehoas, Israēla ķēniņš, sagūstīja Amacīju, Joasa dēlu, Ahazijas dēla dēlu, Jūda ķēniņu pie BetŠemesas, un nonāca Jeruzālemē un nolauzīja Jeruzālemes mūrus četrsimt olektis no Efraīma vārtiem līdz Stūra vārtiem.
14 Akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina zote za jumba la mfalme. Akachukua pia mateka na akarudi Samaria.
Un viņš ņēma visu zeltu un sudrabu un visus rīkus, kas atradās Tā Kunga namā un tā ķēniņa nama mantās, un bērnus ķīlām, un griezās atpakaļ uz Samariju.
15 Matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita vyake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Un kas vēl par Jehoasu stāstāms, ko viņš darījis, un viņa spēks, un kā viņš karojis ar Amacīju, Jūda ķēniņu, tas ir rakstīts Israēla ķēniņu laiku grāmatā.
16 Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli, naye Yeroboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Un Jehoas aizmiga saviem tēviem pakaļ un tapa aprakts Samarijā pie Israēla ķēniņiem, un Jerobeams, viņa dēls, palika par ķēniņu viņa vietā.
17 Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
Bet Amacīja, Joasa, Jūda ķēniņa, dēls, dzīvoja piecpadsmit gadus, kad Jehoas, Joakasa, Israēla ķēniņa, dēls, bija nomiris.
18 Matukio mengine ya utawala wa Amazia, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Un kas vēl par Amacīju stāstāms, tas ir rakstīts Jūda ķēniņu laiku grāmatā.
19 Wakafanya shauri baya dhidi ya Amazia huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi, nao wakamuulia huko.
Un dumpis cēlās pret viņu Jeruzālemē. Bet viņš bēga uz Laķisu, un viņam sūtīja pakaļ uz Laķisu un viņu tur nokāva.
20 Akarudishwa kwa farasi na akazikwa huko Yerusalemu pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi.
Un viņu atveda uz zirgiem un apraka Jeruzālemē pie viņa tēviem Dāvida pilī.
21 Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, na kumfanya mfalme mahali pa baba yake Amazia.
Un visi Jūda ļaudis ņēma Azariju, kas bija sešpadsmit gadus vecs, un to cēla par ķēniņu viņa tēva Amacījas vietā.
22 Ndiye aliijenga tena Elathi na kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
Tas uztaisīja Elatu un atdabūja to atkal pie Jūda pēc tam, kad ķēniņš bija aizmidzis pakaļ saviem tēviem.
23 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala huko Samaria, naye akatawala kwa miaka arobaini na mmoja.
Amacījas, Joasa dēla, Jūda ķēniņa, piecpadsmitā gadā Jerobeams, Jehoasa dēls, palika par ķēniņu pār Israēli Samarijā un valdīja četrdesmit un vienu gadu.
24 Akafanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi hata moja ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
Un viņš darīja, kas Tam Kungam nepatika; viņš neatstājās no visiem Jerobeama, Nebata dēla, grēkiem, kas Israēli bija pavedis uz grēkiem.
25 Ndiye alirudishia mipaka ya Israeli kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bahari ya Araba, sawasawa na neno la Bwana, Mungu wa Israeli, lililosemwa kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-Heferi.
Viņš atdabūja Israēla robežu no tās vietas, kur iet uz Hamatu, līdz klajuma jūrai, pēc Tā Kunga, Israēla Dieva, vārda, ko Viņš bija runājis caur Savu kalpu, pravieti Jonu, Amitajus dēlu, kas bija no GatEveras.
26 Bwana alikuwa ameona jinsi kila mmoja katika Israeli, awe mtumwa au aliye huru, alivyoteseka kwa uchungu; hapakuwepo na yeyote wa kuwasaidia.
Jo Tas Kungs uzlūkoja, ka Israēla bēdas bija ļoti rūgtas, un arī neviena vairs nebija ne maza ne liela, un ka Israēlim palīga nebija.
27 Kwa kuwa Bwana alikuwa hajasema kuwa atafuta jina la Israeli chini ya mbingu, akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
Un Tas Kungs nebija runājis, ka Israēla vārdu gribot izdeldēt apakš debesīm, bet Viņš tos atpestīja caur Jerobeama, Jehoasa dēla, roku.
28 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, yote aliyoyafanya na mafanikio yake ya kijeshi, ikiwa ni pamoja na jinsi alivyorudisha Dameski na Hamathi kwa Israeli, ambayo ilikuwa mali ya Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Un kas vēl par Jerobeamu stāstāms un viss, ko viņš darījis, un viņa spēks, kā viņš karojis un kā viņš Damasku un Hamatu atkal atdabūjis no Jūda pie Israēla, tas ir rakstīts Israēla ķēniņu laiku grāmatā.
29 Yeroboamu akalala pamoja na baba zake, wafalme wa Israeli. Naye Zekaria mwanawe akawa mfalme baada yake.
Un Jerobeams aizmiga pakaļ saviem tēviem Israēla ķēniņiem. Un viņa dēls Zaharija palika par ķēniņu viņa vietā.