< 2 Wafalme 14 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
En la seconde année de Joas, fils de Joachaz, roi d’Israël, régna Amasias, fils de Joas, roi de Juda.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani, kutoka Yerusalemu.
Il avait vingt-cinq ans lorsqu’il commença à régner; et il régna vingt-neuf ans dans Jérusalem; le nom de sa mère était Joadan de Jérusalem.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kama Daudi baba yake alivyokuwa amefanya. Katika kila kitu alifuata mfano wa Yoashi baba yake.
Et il fit ce qui était droit devant le Seigneur, cependant non pas comme David, son père. Il fit selon tout ce que Joas son père avait fait;
4 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Si ce n’est seulement qu’il n’abolit point les hauts lieux, car le peuple sacrifiait encore et brûlait de l’encens sur les hauts lieux.
5 Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
Et lorsqu’il eut obtenu le royaume, il frappa de mort ses serviteurs qui avaient tué le roi, son père;
6 Hata hivyo, hakuwaua wana wa wale wauaji, sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose ambako Bwana aliamuru, “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
Mais les enfants de ceux qui avaient commis le meurtre, il ne les tua points selon ce qui est écrit au livre de la loi de Moïse, et comme a ordonné le Seigneur, disant: Des pères ne mourront pas pour des enfants, et des enfants ne mourront point pour des pères; mais chacun mourra pour son péché.
7 Ndiye aliwashinda Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi, na akauteka Sela katika vita, naye akauita Yoktheeli, jina ambalo mji huo unalo hadi leo.
Ce fut lui qui battit Edom dans la vallée des Salines, tuant dix mille hommes, et il prit le rocher dans cette bataille, et il l’appela du nom de Jectéhel, jusqu’au présent jour.
8 Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tuonane uso kwa uso.”
Alors Amasias envoya des messagers vers Joas, fils de Joachaz, fils de Jéhu, roi d’Israël, disant: Venez, et voyons-nous.
9 Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda: “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
Et Joas, roi d’Israël, envoya à son tour vers Amasias, roi de Juda, disant: Le chardon du Liban envoya vers le cèdre qui est au Liban, disant: Donnez votre fille à mon fils pour femme. Et les bêtes de la forêt qui sont au Liban passèrent, et foulèrent aux pieds le chardon.
10 Hakika umeishinda Edomu, na sasa unajivuna. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini unachokoza na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
Vous l’avez emporté sur Edom, en le battant, et votre cœur vous a élevé. Soyez content de cette gloire, et restez dans votre maison. Pourquoi provoquez-vous un malheur, pour que vous tombiez, vous et Juda avec vous?
11 Hata hivyo, Amazia hakusikia, hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
Mais Amasias ne l’écouta pas; et Joas, roi d’Israël, monta contre lui, et ils se virent, lui et Amasias, roi de Juda, à Bethsamès, ville de Juda.
12 Yuda ikashindwa na Israeli, na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
Et Juda fut vaincu par Israël, et ils s’enfuirent, chacun dans leurs tabernacles.
13 Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akaenda Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
Mais Joas, roi d’Israël, prit à Bethsamès, Amasias, roi de Juda, fils de Joas, fils d’Ochozias, et l’emmena à Jérusalem; et il perça le mur de Jérusalem, depuis la porte d’Ephraïm jusqu’à la porte de l’angle, espace de quatre cents coudées.
14 Akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina zote za jumba la mfalme. Akachukua pia mateka na akarudi Samaria.
Et il emporta tout l’or et l’argent, tous les vases qui furent trouvés dans la maison du Seigneur, et dans tous les trésors du roi, et les otages, et il retourna à Samarie.
15 Matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita vyake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Mais le reste des actions de Joas, et son courage avec lequel il combattit contre Amasias, roi de Juda, n’est-ce pas écrit dans le Livre des actions des jours des rois d’Israël?
16 Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli, naye Yeroboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Joas dormit avec ses pères, et fut enseveli à Samarie avec les rois d’Israël; et Jéroboam, son fils, régna en sa place.
17 Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
Mais Amasias, fils de Joas, roi de Juda, vécut quinze ans après que fut mort Joas, fils de Joachaz, roi d’Israël.
18 Matukio mengine ya utawala wa Amazia, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Mais le reste des actions d’Amasias n’est-il pas écrit dans le Livre des actions des jours des rois de Juda?
19 Wakafanya shauri baya dhidi ya Amazia huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi, nao wakamuulia huko.
Et il se fit une conspiration contre lui à Jérusalem; mais lui s’enfuit à Lachis. Et on envoya après lui à Lachis, et on le tua là.
20 Akarudishwa kwa farasi na akazikwa huko Yerusalemu pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi.
On transporta son cadavre sur les chevaux, et il fut enseseveli avec ses pères dans la cité de David.
21 Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, na kumfanya mfalme mahali pa baba yake Amazia.
Tout le peuple prit ensuite Azarias, âgé de seize ans, et ils l’établirent roi en la place de son père Amasias.
22 Ndiye aliijenga tena Elathi na kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
Ce fut lui qui bâtit Elath, et la rendit à Juda, après que le roi se fut endormi avec ses pères.
23 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala huko Samaria, naye akatawala kwa miaka arobaini na mmoja.
En la quinzième année d’Amasias, fils de Joas, roi de Juda, Jéroboam, fils de Joas, roi d’Israël, régna à Samarie, et il régna quarante-un ans;
24 Akafanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi hata moja ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
Et il fit le mal devant le Seigneur. Il ne s’écarta pas de tous les péchés de Jéroboam, fils de Nabath, qui fit pécher Israël.
25 Ndiye alirudishia mipaka ya Israeli kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bahari ya Araba, sawasawa na neno la Bwana, Mungu wa Israeli, lililosemwa kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-Heferi.
C’est lui qui rétablit les limites d’Israël depuis l’entrée d’Emath jusqu’à la mer du désert, selon la parole que le Seigneur Dieu d’Israël avait dite par son serviteur Jonas, le prophète, fils d’Amathi, qui était de Geth, qui est en Opher.
26 Bwana alikuwa ameona jinsi kila mmoja katika Israeli, awe mtumwa au aliye huru, alivyoteseka kwa uchungu; hapakuwepo na yeyote wa kuwasaidia.
Car le Seigneur vit l’affliction très amère d’Israël, et qu’ils étaient consumés jusqu’à ceux qui étaient renfermés dans la prison, et jusqu’aux derniers du peuple, et qu’il n’y avait personne qui secourût Israël.
27 Kwa kuwa Bwana alikuwa hajasema kuwa atafuta jina la Israeli chini ya mbingu, akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
Et le Seigneur ne dit pas qu’il effacerait le nom d’Israël de dessous le ciel; mais il les sauva par la main de Jéroboam, fils de Joas.
28 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, yote aliyoyafanya na mafanikio yake ya kijeshi, ikiwa ni pamoja na jinsi alivyorudisha Dameski na Hamathi kwa Israeli, ambayo ilikuwa mali ya Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Mais le reste des actions de Jéroboam, tout ce qu’il a fait, son courage avec lequel il combattit, et comment il rendit Damas et Emath à Juda en Israël, n’est-ce pas écrit dans le Livre des actions des jours des rois d’Israël?
29 Yeroboamu akalala pamoja na baba zake, wafalme wa Israeli. Naye Zekaria mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Jéroboam dormit avec ses pères, les rois d’Israël, et Zacharie, son fils, régna en sa place.

< 2 Wafalme 14 >