< 2 Wafalme 14 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
La deuxième année de Joas, fils de Joachaz, roi d'Israël, Amatsia, fils de Joas, roi de Juda, devint roi.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani, kutoka Yerusalemu.
Il avait vingt-cinq ans à son avènement et il régna vingt-neuf ans à Jérusalem. Or, le nom de sa mère était Joadan de Jérusalem.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kama Daudi baba yake alivyokuwa amefanya. Katika kila kitu alifuata mfano wa Yoashi baba yake.
Et il fit ce qui est droit aux yeux de l'Éternel, toutefois pas à l'égal de David, son père: il agit entièrement comme avait agi Joas, son père.
4 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Seulement les tertres ne disparurent pas; le peuple offrait encore des victimes et de l'encens sur les tertres.
5 Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
Et lorsque la royauté fut affermie dans sa main, il fit main basse sur ceux de ses serviteurs qui avaient fait main basse sur le roi, son père;
6 Hata hivyo, hakuwaua wana wa wale wauaji, sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose ambako Bwana aliamuru, “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
mais les fils des meurtriers, il ne les mit pas à mort, aux termes du livre de la Loi de Moïse et de ce que l'Éternel avait prescrit en disant: Les pères ne subiront pas la mort pour les fils, ni les fils pour les pères, mais chacun subira la mort pour son péché.
7 Ndiye aliwashinda Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi, na akauteka Sela katika vita, naye akauita Yoktheeli, jina ambalo mji huo unalo hadi leo.
Il battit les Edomites dans la Vallée du sel, dix mille hommes, et prit Séla dans la guerre et l'appela du nom de Jockthéel qu'elle porte encore aujourd'hui.
8 Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tuonane uso kwa uso.”
C'est alors qu'Amatsia envoya des messagers à Joas, fils de Joachaz, fils de Jéhu, roi d'Israël, pour dire: Viens! il faut que nous nous voyions en face.
9 Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda: “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
Alors Joas, roi d'Israël, députa vers Amatsia, roi de Juda, avec cette réponse: L'épine du Liban fit-porter au Cèdre du Liban ce message: Donne ta fille en mariage à mon fils. Alors les bêtes sauvages du Liban passèrent sur l'épine et l'écrasèrent.
10 Hakika umeishinda Edomu, na sasa unajivuna. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini unachokoza na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
Tu as bien battu les Edomites, et ton cœur t'a exalté: sois glorieux! mais reste chez toi! Pourquoi veux-tu te mettre aux prises avec le malheur pour succomber, toi et Juda avec toi?
11 Hata hivyo, Amazia hakusikia, hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
Mais Amatsia n'écouta point, et Joas, roi d'Israël, s'avança, et ils se trouvèrent en présence, lui et Amatsia, roi de Juda, à Bethsémès, qui est à Juda.
12 Yuda ikashindwa na Israeli, na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
Mais Juda fut défait par Israël, et chacun s'enfuit dans sa tente:
13 Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akaenda Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
et Amatsia, roi de Juda, fils de Joas, fils d'Achazia, fut fait prisonnier à Bethsémès par Joas, roi d'Israël, qui vint à Jérusalem et fit une brèche au mur de Jérusalem à la porte d'Ephraïm jusqu'à la porte de l'angle, espace de quatre cents coudées,
14 Akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina zote za jumba la mfalme. Akachukua pia mateka na akarudi Samaria.
et il enleva la totalité de l'or et de l'argent et la totalité de la vaisselle, qui se trouva dans le temple de l'Éternel et dans les trésors du palais royal, et les otages et regagna Samarie.
15 Matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita vyake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Le reste des actes de Joas, ses entreprises et ses exploits et la guerre qu'il soutint contre Amatsia, roi de Juda, sont d'ailleurs consignés dans le livre des annales des rois d'Israël.
16 Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli, naye Yeroboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Joas reposa avec ses pères et reçut la sépulture à Samarie à côté des rois d'Israël, et Jéroboam, son fils, devint roi en sa place.
17 Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
Et Amatsia, fils de Joas, roi de Juda, survécut quinze ans après la mort de Joas, fils de Joachaz, roi d'Israël.
18 Matukio mengine ya utawala wa Amazia, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Le reste des actes d'Amatsia est d'ailleurs consigné dans le livre des annales des rois de Juda.
19 Wakafanya shauri baya dhidi ya Amazia huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi, nao wakamuulia huko.
Et l'on forma contre lui une conjuration dans Jérusalem, et il s'enfuit à Lachis et ils firent courir après lui à Lachis, et lui donnèrent la mort là.
20 Akarudishwa kwa farasi na akazikwa huko Yerusalemu pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi.
Et on le chargea sur les chevaux, et il reçut la sépulture dans Jérusalem à côté de ses pères dans la ville de David.
21 Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, na kumfanya mfalme mahali pa baba yake Amazia.
Alors tout le peuple de Juda prit Azaria, lequel avait seize ans, et l'établit roi en la place de son père, Amatsia.
22 Ndiye aliijenga tena Elathi na kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
C'est lui qui rebâtit Élath, l'ayant reconquise à Juda, après que le roi fut couché à côté de ses pères.
23 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala huko Samaria, naye akatawala kwa miaka arobaini na mmoja.
La quinzième année d'Amatsia, fils de Joas, roi de Juda, Jéroboam, fils de Joas, roi d'Israël, devint roi à Samarie pour quarante-un ans.
24 Akafanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi hata moja ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
Et il fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel; il ne se départit d'aucun des péchés de Jéroboam, fils de Nebat, qui avait entraîné Israël à pécher.
25 Ndiye alirudishia mipaka ya Israeli kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bahari ya Araba, sawasawa na neno la Bwana, Mungu wa Israeli, lililosemwa kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-Heferi.
Il rétablit les frontières d'Israël à partir de Hamath jusqu'à la Mer de la Plaine, selon la parole de l'Éternel, Dieu d'Israël, qu'il avait prononcée par l'organe de son serviteur Jonas, fils d'Amittaï, le prophète, originaire de Gath-Hépher.
26 Bwana alikuwa ameona jinsi kila mmoja katika Israeli, awe mtumwa au aliye huru, alivyoteseka kwa uchungu; hapakuwepo na yeyote wa kuwasaidia.
Car l'Éternel voyait la misère d'Israël, bien rebelle tout y étant à bout, mineurs et émancipés, et nul ne délivrant Israël;
27 Kwa kuwa Bwana alikuwa hajasema kuwa atafuta jina la Israeli chini ya mbingu, akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
et l'Éternel n'avait point parlé d'effacer le nom d'Israël de dessous les cieux, et Il leur vint en aide par le moyen de Jéroboam, fils de Joas.
28 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, yote aliyoyafanya na mafanikio yake ya kijeshi, ikiwa ni pamoja na jinsi alivyorudisha Dameski na Hamathi kwa Israeli, ambayo ilikuwa mali ya Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Le reste des actes de Jéroboam et toutes ses entreprises et ses exploits, ses guerres, et le recouvrement de Damas et de Hamath, [jadis] à Juda, par Israël, sont d'ailleurs consignés dans le livre des annales des rois d'Israël.
29 Yeroboamu akalala pamoja na baba zake, wafalme wa Israeli. Naye Zekaria mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Jéroboam reposa avec ses pères, avec les rois d'Israël, et Zacharie, son fils, devint roi en sa place.

< 2 Wafalme 14 >