< 2 Wafalme 14 >
1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
En la seconde année de Joas, fils de Joachaz, roi d'Israël, commença le règne d'Amasias, fils de Joas, roi de Juda.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani, kutoka Yerusalemu.
Il avait alors vingt-cinq ans, et il en régna vingt-neuf en Jérusalem; le nom de sa mère était Joadim de Jérusalem.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kama Daudi baba yake alivyokuwa amefanya. Katika kila kitu alifuata mfano wa Yoashi baba yake.
Et il fit ce qui était droit aux yeux du Seigneur, mais non pas comme David, son aïeul. Il fit tout ce qu'avait fait Joas, son père.
4 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Il ne détruisit point les hauts lieux; le peuple offrit encore des sacrifices, et brûla de l'encens sur les hauts lieux.
5 Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
Quand la royauté fut affermie dans ses mains, il tua ceux de ses serviteurs qui avaient frappé son père.
6 Hata hivyo, hakuwaua wana wa wale wauaji, sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose ambako Bwana aliamuru, “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
Mais il ne fit pas périr les fils des meurtriers, se conformant à ce qui est écrit au livre de la loi de Moïse, et à l'ordonnance du Seigneur, disant: Les pères ne seront pas mis à mort à cause des fils, et les fils ne seront pas mis à mort à cause des pères; chacun mourra pour son péché.
7 Ndiye aliwashinda Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi, na akauteka Sela katika vita, naye akauita Yoktheeli, jina ambalo mji huo unalo hadi leo.
Ensuite, il tailla en pièces, dans la vallée des Sels, dix mille hommes de l'Idumée; et il prit, en cette guerre, le rocher auquel il donna le nom de Jéthoël, nom qui lui est resté jusqu'à nos jours.
8 Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tuonane uso kwa uso.”
Alors, Amasias envoya des messagers à Joas, fils de Joachaz, fils de Jéhu, roi d'Israël, disant: Viens, que nous nous voyions face à face.
9 Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda: “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
Mais Joas, roi d'Israël, fit répondre au roi de Juda: Le chardon du Liban envoya des gens au cèdre pour lui dire: Donne ta fille à mon fils pour femme; et les bêtes fauves du champ voisin passèrent, et elles foulèrent aux pieds le chardon.
10 Hakika umeishinda Edomu, na sasa unajivuna. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini unachokoza na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
Tu as battu l'Iduméen, et ton cœur s'est exalté; glorifie-toi tranquillement en ta demeure; à quoi bon me cherches-tu querelle pour ta perte? Tu tomberas, et avec toi Juda.
11 Hata hivyo, Amazia hakusikia, hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
Amasias ne l'écouta point; et Joas, roi d'Israël, partit, et ils se virent face à face à Bethsamys en Juda.
12 Yuda ikashindwa na Israeli, na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
Mais Juda tomba devant Israël, et chacun s'enfuit en sa demeure.
13 Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akaenda Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
Et Joas, roi d'Israël, fit prisonnier, à Bethsamys, Amasias, fils de Joas, fils d'Ochozias; il entra à Jérusalem, et il abattit le rempart depuis la porte d'Ephraïm jusqu'à la porte de l'angle, sur une longueur de quatre cents coudées.
14 Akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina zote za jumba la mfalme. Akachukua pia mateka na akarudi Samaria.
Il prit l'argent et l'or, et tous les ornements qu'il trouva soit dans le temple du Seigneur, soit dans le palais du roi; il se fit donner des otages, et il retourna en Samarie.
15 Matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita vyake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Quant au reste de l'histoire de Joas, et à ses combats avec Amasias, ne sont-ils pas écrits au livre des Faits et gestes des rois d'Israël?
16 Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli, naye Yeroboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Joas s'endormit avec ses pères; il fut enseveli à Samarie avec les rois d'Israël, et Jéroboam, son fils, régna à sa place.
17 Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
Amasias, fils de Joas, roi de Jérusalem, vécut encore quinze ans après la mort de Joas, fils de Joachaz, roi d'Israël.
18 Matukio mengine ya utawala wa Amazia, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Quant au reste de l'histoire d'Amasias, n'est-il pas écrit au livre des Faits et gestes des rois de Juda?
19 Wakafanya shauri baya dhidi ya Amazia huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi, nao wakamuulia huko.
Et il y eut un complot contre lui en Jérusalem; il se réfugia à Lachis, où les conjurés le poursuivirent, et ils le tuèrent dans cette ville.
20 Akarudishwa kwa farasi na akazikwa huko Yerusalemu pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi.
Puis, ils l'enlevèrent sur un char, et il fut enseveli à Jérusalem auprès de ses pères, dans la ville de David.
21 Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, na kumfanya mfalme mahali pa baba yake Amazia.
Et tout le peuple de Juda fit choix d'Azarias, alors âgé de seize ans, et ils le proclamèrent roi à la place d'Amasias son père.
22 Ndiye aliijenga tena Elathi na kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
Ce fut lui qui bâtit Elath, après l'avoir reprise pour Juda, lorsque le roi eut été déposé auprès de ses pères.
23 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala huko Samaria, naye akatawala kwa miaka arobaini na mmoja.
En la quinzième année du règne d'Amasias, fils de Joas, roi de Juda, Jéroboam, fils de Joas, roi d'Israël, commença un règne qui dura quarante et un ans.
24 Akafanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi hata moja ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
Et il fit le mal devant le Seigneur; il ne se retira pas des péchés où Jéroboam, fils de Nabat, avait fait tomber Israël.
25 Ndiye alirudishia mipaka ya Israeli kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bahari ya Araba, sawasawa na neno la Bwana, Mungu wa Israeli, lililosemwa kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-Heferi.
Ce fut lui qui rétablit les limites d'Israël, depuis l'entrée d'Emath jusqu'à la mer d'Araba, selon la parole que le Seigneur Dieu d'Israël avait fait connaître par son serviteur le prophète Jonas, fils d'Amatbi, de Gethchopher;
26 Bwana alikuwa ameona jinsi kila mmoja katika Israeli, awe mtumwa au aliye huru, alivyoteseka kwa uchungu; hapakuwepo na yeyote wa kuwasaidia.
Parce que le Seigneur avait vu l'abaissement bien triste d'Israël, son petit nombre, son asservissement, son indigence et son isolement; car il n'était personne qui secourût Israël.
27 Kwa kuwa Bwana alikuwa hajasema kuwa atafuta jina la Israeli chini ya mbingu, akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
Et le Seigneur dit qu'il ne voulait pas effacer sous les cieux la race d'Israël; mais il la sauva par les mains de Jéroboam, fils de Joas.
28 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, yote aliyoyafanya na mafanikio yake ya kijeshi, ikiwa ni pamoja na jinsi alivyorudisha Dameski na Hamathi kwa Israeli, ambayo ilikuwa mali ya Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Quant au reste de l'histoire de Jéroboam, et aux actions qu'il fit en sa puissance, et aux combats qui rendirent Damas et Emath de Juda à Israël, ne sont-ils pas écrits au livre des Faits et gestes des rois d'Israël?
29 Yeroboamu akalala pamoja na baba zake, wafalme wa Israeli. Naye Zekaria mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Jéroboam s'endormit avec ses pères, avec les rois d'Israël, et Zacharias, son fils, régna à sa place.