< 2 Wafalme 14 >
1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
In year two of Joash [the] son of Jehoahaz [the] king of Israel he became king Amaziah [the] son of Joash [the] king of Judah.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani, kutoka Yerusalemu.
A son of twenty and five year[s] he was when became king he and twenty and nine year[s] he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his ([was] Jehoaddan *Q(K)*) from Jerusalem.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kama Daudi baba yake alivyokuwa amefanya. Katika kila kitu alifuata mfano wa Yoashi baba yake.
And he did the right in [the] eyes of Yahweh only not like David ancestor his according to all that he had done Joash father his he did.
4 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Only the high places not they were removed still the people [were] sacrificing and [were] making smoke at the high places.
5 Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
And it was just when it was secure the kingdom in hand his and he struck down servants his who had struck down the king father his.
6 Hata hivyo, hakuwaua wana wa wale wauaji, sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose ambako Bwana aliamuru, “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
And [the] sons of those [who] had struck down not he put to death according to [what] is written in [the] book of [the] law of Moses which he commanded Yahweh saying not they will be put to death fathers on sons and sons not they will be put to death on fathers that except each for own sin his (he will be put to death. *Q(K)*)
7 Ndiye aliwashinda Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi, na akauteka Sela katika vita, naye akauita Yoktheeli, jina ambalo mji huo unalo hadi leo.
He he struck down Edom in [the] Valley of (Salt *Q(K)*) ten thousand and he seized Sela in battle and he called name its Joktheel until the day this.
8 Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tuonane uso kwa uso.”
Then he sent Amaziah messengers to Jehoash [the] son of Jehoahaz [the] son of Jehu [the] king of Israel saying come! let us look at one another faces.
9 Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda: “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
And he sent Jehoash [the] king of Israel to Amaziah [the] king of Judah saying thornbush which [was] in Lebanon it sent to cedar which [was] in Lebanon saying give! daughter your to son my to a wife and it passed by [the] animal of the field which [was] in Lebanon and it trampled the thornbush.
10 Hakika umeishinda Edomu, na sasa unajivuna. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini unachokoza na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
Certainly you have struck down Edom and it has lifted you heart your be honored and remain at home your and why? will you engage in strife with harm and you will fall you and Judah with you.
11 Hata hivyo, Amazia hakusikia, hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
And not he listened Amaziah and he went up Jehoash [the] king of Israel and they looked at one another faces he and Amaziah [the] king of Judah at Beth Shemesh which [belonged] to Judah.
12 Yuda ikashindwa na Israeli, na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
And it was defeated Judah before Israel and they fled everyone (to tents his. *Q(K)*)
13 Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akaenda Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
And Amaziah [the] king of Judah [the] son of Jehoash [the] son of Ahaziah he seized Jehoash [the] king of Israel at Beth Shemesh (and he came *Q(K)*) Jerusalem and he made a breach in [the] wall of Jerusalem at [the] gate of Ephraim to [the] gate of the corner four hundred cubit[s].
14 Akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina zote za jumba la mfalme. Akachukua pia mateka na akarudi Samaria.
And he took all the gold and the silver and all the articles which were found [the] house of Yahweh and in [the] treasuries of [the] house of the king and [the] sons of the pledges and he returned Samaria towards.
15 Matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita vyake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
And [the] rest of [the] matters of Jehoash which he did and might his and which he waged war with Amaziah [the] king of Judah ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Israel.
16 Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli, naye Yeroboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
And he lay down Jehoash with ancestors his and he was buried in Samaria with [the] kings of Israel and he became king Jeroboam son his in place of him.
17 Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
And he lived Amaziah [the] son of Joash [the] king of Judah after [the] death of Jehoash [the] son of Jehoahaz [the] king of Israel fif-teen year[s].
18 Matukio mengine ya utawala wa Amazia, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
And [the] rest of [the] matters of Amaziah ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Judah.
19 Wakafanya shauri baya dhidi ya Amazia huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi, nao wakamuulia huko.
And people conspired on him a conspiracy in Jerusalem and he fled Lachish towards and they sent after him Lachish towards and they put to death him there.
20 Akarudishwa kwa farasi na akazikwa huko Yerusalemu pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi.
And they carried him on horses and he was buried in Jerusalem with ancestors his in [the] city of David.
21 Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, na kumfanya mfalme mahali pa baba yake Amazia.
And they took all [the] people of Judah Azariah and he [was] a son of six-teen year[s] and they made king him in place of father his Amaziah.
22 Ndiye aliijenga tena Elathi na kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
He he built Elath and he restored it to Judah after lay down the king with ancestors his.
23 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala huko Samaria, naye akatawala kwa miaka arobaini na mmoja.
In year fif-teen year of Amaziah [the] son of Joash [the] king of Judah he became king Jeroboam [the] son of Joash [the] king of Israel in Samaria forty and one year[s].
24 Akafanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi hata moja ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
And he did the evil in [the] eyes of Yahweh not he turned aside from all [the] sins of Jeroboam [the] son of Nebat which he caused to sin Israel.
25 Ndiye alirudishia mipaka ya Israeli kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bahari ya Araba, sawasawa na neno la Bwana, Mungu wa Israeli, lililosemwa kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-Heferi.
He he restored [the] border of Israel from Lebo Hamath to [the] sea of the Arabah according to [the] word of Yahweh [the] God of Israel which he spoke by [the] hand of servant his Jonah [the] son of Amittai the prophet who [was] from Gath Hepher.
26 Bwana alikuwa ameona jinsi kila mmoja katika Israeli, awe mtumwa au aliye huru, alivyoteseka kwa uchungu; hapakuwepo na yeyote wa kuwasaidia.
For he saw Yahweh [the] affliction of Israel rebellious very and there not [was] shut up and there not [was] freed and there not [was] a helper for Israel.
27 Kwa kuwa Bwana alikuwa hajasema kuwa atafuta jina la Israeli chini ya mbingu, akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
And not he had spoken Yahweh to wipe out [the] name of Israel from under the heavens and he delivered them by [the] hand of Jeroboam [the] son of Joash.
28 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, yote aliyoyafanya na mafanikio yake ya kijeshi, ikiwa ni pamoja na jinsi alivyorudisha Dameski na Hamathi kwa Israeli, ambayo ilikuwa mali ya Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
And [the] rest of [the] matters of Jeroboam and all that he did and might his which he waged war and which he restored Damascus and Hamath to Judah in Israel ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Israel.
29 Yeroboamu akalala pamoja na baba zake, wafalme wa Israeli. Naye Zekaria mwanawe akawa mfalme baada yake.
And he lay down Jeroboam with ancestors his with [the] kings of Israel and he became king Zechariah son his in place of him.