< 2 Wafalme 13 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wa Yoashi mwana wa Ahazia mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu alianza kutawala Israeli katika Samaria, naye akatawala miaka kumi na saba.
Uti tredje och tjugonde årena Joas, Ahasia sons, Juda Konungs, vardt Joahas, Jehu son, Konung öfver Israel i Samarien, sjutton år.
2 Akafanya maovu machoni pa Bwana kwa kufuata dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, na wala hakuziacha.
Och han gjorde det ondt var för Herranom, och vandrade efter Jerobeams synder, Nebats sons, hvilken Israel kom till att synda; och öfvergaf det icke.
3 Kwa hiyo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli na kwa muda mrefu akawaweka chini ya utawala wa Hazaeli mfalme wa Aramu, na Ben-Hadadi mwanawe.
Och Herrans vrede förgrymmade sig öfver Israel, och gaf dem under Hasaels hand, Konungens i Syrien, och i Benhadads, Hasaels sons, hand, i deras lifsdagar.
4 Ndipo Yehoahazi akamsihi Bwana rehema, naye Bwana akamsikiliza, kwa maana aliona jinsi mfalme wa Aramu alivyokuwa akiwatesa Israeli vikali.
Men Joahas bad Herrans ansigte, och Herren hörde honom; ty han såg på Israels jämmer, som Konungen i Syrien dem gjorde.
5 Bwana akamtoa mwokozi kwa ajili ya Israeli, nao wakaokoka kutoka kwenye mamlaka ya Aramu. Hivyo Waisraeli wakaishi katika nyumba zao wenyewe kama ilivyokuwa hapo awali.
Och Herren gaf Israel en frälsare, som dem förde utu de Syrers våld; så att Israels barn bodde uti sina hyddor, såsom tillförene.
6 Lakini hawakuziacha dhambi za nyumba ya Yeroboamu, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, bali wakaendelea kuzitenda. Nguzo ya Ashera pia iliendelea kusimama katika Samaria.
Dock öfvergåfvo de icke Jerobeams hus synder, hvilken Israel kom till att synda, utan vandrade derutinnan; och den lunden i Samarien blef ståndandes.
7 Hapakubaki kitu chochote katika jeshi la Yehoahazi isipokuwa wapanda farasi hamsini, magari kumi ya vita na askari wa miguu elfu kumi, kwa kuwa mfalme wa Aramu alikuwa amewaangamiza hao wengine na kuwafanya kama mavumbi wakati wa kupura nafaka.
Förty af Joahas folk var icke mer qvart blifvet, än femtio resenärer, tio vagnar, och tiotusend fotfolk; ty Konungen i Syrien hade slagit dem ihjäl, och gjort dem såsom tröskestoft.
8 Matukio mengine ya utawala wa Yehoahazi yote aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Hvad nu mer af Joahas sägandes är, och allt det han gjort hafver, och hans magt, si, det är skrifvet i Israels Konungars Chrönico.
9 Yehoahazi akalala pamoja na baba zake, akazikwa huko Samaria. Naye Yehoashi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Och Joahas afsomnade med sina fäder, och man begrof honom i Samarien; och hans son Joas vardt Konung i hans stad.
10 Katika mwaka wa thelathini na saba wa utawala wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yehoashi mwana wa Yehoahazi alianza kutawala Israeli huko Samaria, naye akatawala miaka kumi na sita.
Uti sjunde och tretionde årena Joas, Juda Konungs, vardt Joas, Joahas son, Konung öfver Israel i Samarien, sexton år;
11 Alifanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi yoyote kati ya zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, bali aliendelea kuzitenda.
Och gjorde det ondt var för Herranom, och öfvergaf icke alla Jerobeams, Nebats sons, synder, den Israel kom till att synda; utan vandrade derutinnan.
12 Na kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, yote aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita yake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Hvad nu mer af Joas sägandes är, och hvad han gjort hafver, och hans magt, huru han med Amazia, Juda Konung, stridt hafver, si, det är skrifvet uti Israels Konungars Chrönico.
13 Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli. Yeroboamu akawa mfalme baada yake.
Och Joas afsomnade med sina fader; och Jerobeam satt på hans stol. Men Joas vardt begrafven i Samarien när de Israels Konungar.
14 Wakati huu, Elisha alikuwa anaumwa na ugonjwa ambao baadaye ulimuua. Yehoashi mfalme wa Israeli akashuka kwenda kumwona na kumlilia. Akalia, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya vita ya Israeli na wapanda farasi wake!”
Då vardt Elisa krank, der han ock af död blef; och Joas, Israels Konung, kom ned till honom, och gret för honom, och sade: Min fader, min fader, Israels vagn, och hans resenärer.
15 Elisha akasema, “Leta upinde na baadhi ya mishale,” naye mfalme akafanya hivyo.
Elisa sade till honom: Tag bågan och pilarna. Och då han tog bågan och pilarna,
16 Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Shika upinde mikononi mwako.” Alipokwisha kuichukua, Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme.
Sade han till Israels Konung: Bänd bågan med dine hand. Och han bände med sine hand. Och Elisa lade sina hand på Konungens hand;
17 Elisha akasema, “Fungua dirisha la mashariki,” naye akalifungua. Elisha akasema, “Piga mshale!” Naye akapiga mshale. Elisha akasema, “Mshale wa ushindi wa Bwana, mshale wa ushindi juu ya Aramu! Utawaangamiza Waaramu kabisa huko Afeki.”
Och sade: Låt upp fenstret österut; och han lät det upp. Och Elisa sade: Skjut; och han sköt. Han sade: En salighetspil af Herranom, en salighetspil emot de Syrer; och du skall slå de Syrer i Aphek, tilldess de blifva ändade.
18 Kisha akasema, “Chukua mishale,” naye mfalme akaichukua. Elisha akamwambia, “Piga ardhi kwa hiyo mishale.” Akaipiga mara tatu, halafu akaacha.
Och han sade: Tag pilarna. Och då han tog dem, sade han till Israels Konung: Slå på jordena. Och han slog tre gånger, och höll upp.
19 Mtu wa Mungu akamkasirikia na akasema, “Ungepiga chini mara tano au sita, ndipo ungeishinda Aramu na kuiangamiza kabisa. Lakini sasa utaishinda mara tatu tu.”
Då vardt Guds mannen vred på honom, och sade: Hade du slagit fem eller sex gånger, så skulle du hafva slagit de Syrer, tilldess du hade gjort en ända på dem; men nu skall du slå dem tre gånger.
20 Elisha akafa, nao wakamzika. Vikosi vya Wamoabu vilikuwa vinashambulia nchi kwa vita kila mwaka wakati wa vuli.
Då nu Elisa var död, och man hade begrafvit honom, föllo de Moabiters krigsfolk in uti landet på samma året.
21 Ikawa Waisraeli fulani walipokuwa wanamzika mtu, ghafula wakaona kikosi cha washambuliaji, basi wakaitupa ile maiti ya yule mtu ndani ya kaburi la Elisha. Wakati ile maiti ilipogusa mifupa ya Elisha, yule mtu akafufuka na kusimama kwa miguu yake.
Och det begaf sig, att de begrofvo en man; och som de fingo se krigsfolket, kastade de mannen uti Elisa graf; och då han kom vid Elisa ben, vardt han lefvandes, och stod upp på sina fötter.
22 Hazaeli mfalme wa Aramu aliwatesa Israeli wakati wote wa utawala wa Yehoahazi.
Alltså tvingade nu Hasael, Konungen i Syrien, Israel, så länge Joahas lefde.
23 Lakini Bwana akawarehemu na akawahurumia, akaonyesha kujishughulisha nao kwa sababu ya Agano lake na Abrahamu, Isaki na Yakobo. Hadi leo, hajawaangamiza wala kuwafukuza mbele zake.
Men Herren gjorde nåd med dem, och förbarmade sig öfver dem, och vände sig till dem för sitt förbunds skull med Abraham, Isaac och Jacob, och ville, icke förderfva dem; och förkastade dem icke heller ifrå sitt ansigte allt härtill.
24 Hazaeli mfalme wa Shamu akafa, naye Ben-Hadadi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Och Hasael, Konungen i Syrien, blef död; och hans son Benhadad vardt Konung i hans stad.
25 Kisha Yehoashi mwana wa Yehoahazi akateka tena kutoka kwa Ben-Hadadi mwana wa Hazaeli ile miji aliyokuwa ameitwaa kwa vita kutoka kwa baba yake Yehoahazi. Yehoashi alimshinda mara tatu, hivyo akaweza kuiteka tena ile miji ya Waisraeli.
Men Joas vände om, och tog de städer igen utu Benhadads, Hasaels sons, hand, som han utu hans faders Joahas hand med strid tagit hade. Tre gånger slog Joas honom, och fick Israels städer igen.

< 2 Wafalme 13 >