< 2 Wafalme 13 >
1 Katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wa Yoashi mwana wa Ahazia mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu alianza kutawala Israeli katika Samaria, naye akatawala miaka kumi na saba.
No vigésimo terceiro ano de Joás, filho de Acazias, rei de Judá, Jeoacaz, filho de Jeú, começou a reinar sobre Israel em Samaria por dezessete anos.
2 Akafanya maovu machoni pa Bwana kwa kufuata dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, na wala hakuziacha.
Ele fez o que era mau aos olhos de Iavé, e seguiu os pecados de Jeroboão, filho de Nebate, com os quais ele fez Israel pecar. Ele não se afastou dele.
3 Kwa hiyo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli na kwa muda mrefu akawaweka chini ya utawala wa Hazaeli mfalme wa Aramu, na Ben-Hadadi mwanawe.
A raiva de Javé queimou contra Israel, e ele os entregou na mão de Hazael, rei da Síria, e na mão de Benhadad, filho de Hazael, continuamente.
4 Ndipo Yehoahazi akamsihi Bwana rehema, naye Bwana akamsikiliza, kwa maana aliona jinsi mfalme wa Aramu alivyokuwa akiwatesa Israeli vikali.
Jehoahaz implorou a Javé, e Javé o ouviu; pois ele viu a opressão de Israel, como o rei da Síria os oprimiu.
5 Bwana akamtoa mwokozi kwa ajili ya Israeli, nao wakaokoka kutoka kwenye mamlaka ya Aramu. Hivyo Waisraeli wakaishi katika nyumba zao wenyewe kama ilivyokuwa hapo awali.
(Javé deu a Israel um salvador, para que eles saíssem de debaixo da mão dos sírios; e os filhos de Israel viviam em suas tendas como antes.
6 Lakini hawakuziacha dhambi za nyumba ya Yeroboamu, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, bali wakaendelea kuzitenda. Nguzo ya Ashera pia iliendelea kusimama katika Samaria.
No entanto eles não se afastaram dos pecados da casa de Jeroboão, com os quais ele fez Israel pecar, mas andou neles; e os Asherah também permaneceram em Samaria).
7 Hapakubaki kitu chochote katika jeshi la Yehoahazi isipokuwa wapanda farasi hamsini, magari kumi ya vita na askari wa miguu elfu kumi, kwa kuwa mfalme wa Aramu alikuwa amewaangamiza hao wengine na kuwafanya kama mavumbi wakati wa kupura nafaka.
Pois ele não deixou a Jehoahaz do povo mais de cinqüenta cavaleiros, dez carros e dez mil homens de pé; pois o rei da Síria os destruiu e os fez como o pó da debulha.
8 Matukio mengine ya utawala wa Yehoahazi yote aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Agora o resto dos atos de Jeoacaz, e tudo o que ele fez, e seu poder, não estão escritos no livro das crônicas dos reis de Israel?
9 Yehoahazi akalala pamoja na baba zake, akazikwa huko Samaria. Naye Yehoashi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Jehoahaz dormiu com seus pais; e eles o enterraram em Samaria; e Joás, seu filho, reinou em seu lugar.
10 Katika mwaka wa thelathini na saba wa utawala wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yehoashi mwana wa Yehoahazi alianza kutawala Israeli huko Samaria, naye akatawala miaka kumi na sita.
No trigésimo sétimo ano de Joás, rei de Judá, Jeoás, filho de Jeoacaz, começou a reinar sobre Israel em Samaria por dezesseis anos.
11 Alifanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi yoyote kati ya zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, bali aliendelea kuzitenda.
Ele fez o que era mau aos olhos de Iavé. Ele não se afastou de todos os pecados de Jeroboão, filho de Nebate, com os quais ele fez Israel pecar; mas ele andou neles.
12 Na kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, yote aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita yake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Agora o resto dos atos de Joás, e tudo o que ele fez, e sua força com que lutou contra o Amazonas, rei de Judá, não estão escritos no livro das crônicas dos reis de Israel?
13 Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli. Yeroboamu akawa mfalme baada yake.
Joás dormiu com seus pais; e Jeroboão sentou-se em seu trono. Joás foi enterrado em Samaria com os reis de Israel.
14 Wakati huu, Elisha alikuwa anaumwa na ugonjwa ambao baadaye ulimuua. Yehoashi mfalme wa Israeli akashuka kwenda kumwona na kumlilia. Akalia, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya vita ya Israeli na wapanda farasi wake!”
Now Eliseu adoeceu com a doença da qual morreu; e Joás, o rei de Israel, desceu até ele, chorou sobre ele e disse: “Meu pai, meu pai, os carros de Israel e seus cavaleiros”!
15 Elisha akasema, “Leta upinde na baadhi ya mishale,” naye mfalme akafanya hivyo.
Elisha lhe disse: “Pegue o arco e flechas”; e ele pegou arco e flechas para si mesmo.
16 Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Shika upinde mikononi mwako.” Alipokwisha kuichukua, Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme.
Ele disse ao rei de Israel: “Ponha sua mão sobre o arco”; e ele colocou sua mão sobre ele. Eliseu pôs suas mãos sobre as mãos do rei.
17 Elisha akasema, “Fungua dirisha la mashariki,” naye akalifungua. Elisha akasema, “Piga mshale!” Naye akapiga mshale. Elisha akasema, “Mshale wa ushindi wa Bwana, mshale wa ushindi juu ya Aramu! Utawaangamiza Waaramu kabisa huko Afeki.”
Ele disse: “Abra a janela para o leste”; e ele a abriu. Então Eliseu disse: “Atire!” e ele atirou. Ele disse: “A flecha da vitória de Javé, até mesmo a flecha da vitória sobre a Síria; pois vocês atingirão os sírios em Afek até que os tenham consumido”.
18 Kisha akasema, “Chukua mishale,” naye mfalme akaichukua. Elisha akamwambia, “Piga ardhi kwa hiyo mishale.” Akaipiga mara tatu, halafu akaacha.
Ele disse: “Pegue as flechas”; e ele as pegou. Ele disse ao rei de Israel: “Atinja o chão”; e ele bateu três vezes, e parou.
19 Mtu wa Mungu akamkasirikia na akasema, “Ungepiga chini mara tano au sita, ndipo ungeishinda Aramu na kuiangamiza kabisa. Lakini sasa utaishinda mara tatu tu.”
O homem de Deus ficou bravo com ele, e disse: “Você deveria ter atingido cinco ou seis vezes. Então você teria atingido a Síria até que a tivesse consumido, mas agora você terá atingido a Síria apenas três vezes”.
20 Elisha akafa, nao wakamzika. Vikosi vya Wamoabu vilikuwa vinashambulia nchi kwa vita kila mwaka wakati wa vuli.
Elisha morreu, e eles o enterraram. Agora, as bandas dos moabitas invadiram a terra na chegada do ano.
21 Ikawa Waisraeli fulani walipokuwa wanamzika mtu, ghafula wakaona kikosi cha washambuliaji, basi wakaitupa ile maiti ya yule mtu ndani ya kaburi la Elisha. Wakati ile maiti ilipogusa mifupa ya Elisha, yule mtu akafufuka na kusimama kwa miguu yake.
Quando estavam enterrando um homem, eis que viram um bando de saqueadores; e jogaram o homem na tumba de Elisha. Assim que o homem tocou os ossos de Elisha, ele reviveu, e se levantou de pé.
22 Hazaeli mfalme wa Aramu aliwatesa Israeli wakati wote wa utawala wa Yehoahazi.
Hazael, rei da Síria, oprimiu Israel durante todos os dias de Jehoahaz.
23 Lakini Bwana akawarehemu na akawahurumia, akaonyesha kujishughulisha nao kwa sababu ya Agano lake na Abrahamu, Isaki na Yakobo. Hadi leo, hajawaangamiza wala kuwafukuza mbele zake.
Mas Javé foi gentil com eles, e teve compaixão deles, e os favoreceu por causa de sua aliança com Abraão, Isaac e Jacó, e não os quis destruir e ainda não os expulsou de sua presença.
24 Hazaeli mfalme wa Shamu akafa, naye Ben-Hadadi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Hazael, rei da Síria, morreu; e Benhadad, seu filho, reinou em seu lugar.
25 Kisha Yehoashi mwana wa Yehoahazi akateka tena kutoka kwa Ben-Hadadi mwana wa Hazaeli ile miji aliyokuwa ameitwaa kwa vita kutoka kwa baba yake Yehoahazi. Yehoashi alimshinda mara tatu, hivyo akaweza kuiteka tena ile miji ya Waisraeli.
Jehoash, filho de Jehoahaz, tirou novamente da mão de Benhadad, filho de Hazael, as cidades que ele havia tirado da mão de Jehoahaz, seu pai, pela guerra. Joás o golpeou três vezes, e recuperou as cidades de Israel.