< 2 Wafalme 13 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wa Yoashi mwana wa Ahazia mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu alianza kutawala Israeli katika Samaria, naye akatawala miaka kumi na saba.
Im Jahre dreiundzwanzig der Jahre des Joasch, des Sohnes von Achasjahu, dem König von Judah, ward Jehoachas, der Sohn Jehus, König über Israel in Samaria, siebzehn Jahre.
2 Akafanya maovu machoni pa Bwana kwa kufuata dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, na wala hakuziacha.
Und er tat, was böse war in den Augen Jehovahs, und wandelte nach den Sünden Jerobeams, des Sohnes Nebats, der Israel sündigen machte, er wich nicht davon ab.
3 Kwa hiyo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli na kwa muda mrefu akawaweka chini ya utawala wa Hazaeli mfalme wa Aramu, na Ben-Hadadi mwanawe.
Und es entbrannte der Zorn Jehovahs wider Israel, und er gab sie in die Hand Chasaels, König von Aram, und in die Hand Ben-Hadads, des Sohnes von Chasael, alle Tage.
4 Ndipo Yehoahazi akamsihi Bwana rehema, naye Bwana akamsikiliza, kwa maana aliona jinsi mfalme wa Aramu alivyokuwa akiwatesa Israeli vikali.
Und Jehoachas flehte das Angesicht Jehovahs an, und Jehovah hörte auf ihn; denn er sah die Unterdrückung Israels, wie der König Aram sie unterdrückte.
5 Bwana akamtoa mwokozi kwa ajili ya Israeli, nao wakaokoka kutoka kwenye mamlaka ya Aramu. Hivyo Waisraeli wakaishi katika nyumba zao wenyewe kama ilivyokuwa hapo awali.
Und Jehovah gab Israel einen Retter, daß sie ausgingen aus Arams Hand und die Söhne Israels wohnten in ihren Zelten wie gestern und ehegestern.
6 Lakini hawakuziacha dhambi za nyumba ya Yeroboamu, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, bali wakaendelea kuzitenda. Nguzo ya Ashera pia iliendelea kusimama katika Samaria.
Doch wichen sie nicht ab von den Sünden des Hauses Jerobeams, der Israel sündigen machte, sie wandelten darinnen; und auch die Aschere blieb stehen in Samaria.
7 Hapakubaki kitu chochote katika jeshi la Yehoahazi isipokuwa wapanda farasi hamsini, magari kumi ya vita na askari wa miguu elfu kumi, kwa kuwa mfalme wa Aramu alikuwa amewaangamiza hao wengine na kuwafanya kama mavumbi wakati wa kupura nafaka.
Denn es verblieb dem Jehoachas nicht mehr Volkes als fünfzig Reiter und zehn Streitwagen und zehntausend Fußvolk; denn der König von Aram hatte sie zugrunde gerichtet, und sie gemacht, wie den Staub beim Dreschen.
8 Matukio mengine ya utawala wa Yehoahazi yote aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Und die übrigen Geschichten des Jehoachas, und alles, was er tat und seine Macht, ist es nicht geschrieben im Buche der Tagesgeschichte der Könige Israels?
9 Yehoahazi akalala pamoja na baba zake, akazikwa huko Samaria. Naye Yehoashi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Und Jehoachas entschlief zu seinen Vätern, und sie begruben ihn in Samaria, und Joasch, sein Sohn, ward König an seiner Stelle.
10 Katika mwaka wa thelathini na saba wa utawala wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yehoashi mwana wa Yehoahazi alianza kutawala Israeli huko Samaria, naye akatawala miaka kumi na sita.
Im Jahre siebenunddreißig der Jahre von Joasch, dem König Judahs, ward Jehoasch, Sohn des Jehoachas, König über Israel in Samaria sechzehn Jahre;
11 Alifanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi yoyote kati ya zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, bali aliendelea kuzitenda.
Und tat, was böse war in den Augen Jehovahs. Er wich nicht ab von all den Sünden Jerobeams, des Sohnes Nebats, der Israel sündigen machte; er wandelte darin.
12 Na kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, yote aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita yake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Und die übrige Geschichte des Joasch und alles, was er tat, und seine Macht, wie er mit Amazjah, dem Könige Judahs, stritt, ist es nicht geschrieben im Buche der Tagesgeschichte der Könige Israels?
13 Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli. Yeroboamu akawa mfalme baada yake.
Und Joasch entschlief zu seinen Vätern, und Jerobeam saß auf seinem Thron, Joasch aber ward begraben in Samaria bei den Königen von Israel.
14 Wakati huu, Elisha alikuwa anaumwa na ugonjwa ambao baadaye ulimuua. Yehoashi mfalme wa Israeli akashuka kwenda kumwona na kumlilia. Akalia, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya vita ya Israeli na wapanda farasi wake!”
Und Elischa ward krank an seiner Krankheit, an der er starb. Und Joasch, König von Israel, kam zu ihm herab und weinte vor ihm und sprach: Mein Vater, mein Vater! Streitwagen Israels und seine Reiter!
15 Elisha akasema, “Leta upinde na baadhi ya mishale,” naye mfalme akafanya hivyo.
Und Elischa sprach zu ihm: Nimm Bogen und Pfeile; und er nahm zu sich Bogen und Pfeile.
16 Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Shika upinde mikononi mwako.” Alipokwisha kuichukua, Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme.
Und er sprach zu dem Könige von Israel: Lege deine Hand auf den Bogen. Und er legte seine Hand an, und Elischa legte seine Hände auf des Königs Hände.
17 Elisha akasema, “Fungua dirisha la mashariki,” naye akalifungua. Elisha akasema, “Piga mshale!” Naye akapiga mshale. Elisha akasema, “Mshale wa ushindi wa Bwana, mshale wa ushindi juu ya Aramu! Utawaangamiza Waaramu kabisa huko Afeki.”
Und sprach: Öffne das Fenster gegen Morgen, und er öffnete es. Und Elischa sprach: Schieße! Und er schoß. Und er sprach: Ein Pfeil des Heils von Jehovah und ein Pfeil des Heils wider Aram, und du wirst Aram schlagen in Aphek bis zur Vollendung.
18 Kisha akasema, “Chukua mishale,” naye mfalme akaichukua. Elisha akamwambia, “Piga ardhi kwa hiyo mishale.” Akaipiga mara tatu, halafu akaacha.
Und er sprach: Nimm die Pfeile, und er nahm sie. Und er sprach zum König von Israel: Schlage auf die Erde, und er schlug dreimal und stand stille.
19 Mtu wa Mungu akamkasirikia na akasema, “Ungepiga chini mara tano au sita, ndipo ungeishinda Aramu na kuiangamiza kabisa. Lakini sasa utaishinda mara tatu tu.”
Und der Mann Gottes ward entrüstet über ihn und sprach: Hättest du fünf oder sechsmal geschlagen, dann hättest du Aram bis zur Vollendung geschlagen. Nun aber wirst du Aram dreimal schlagen.
20 Elisha akafa, nao wakamzika. Vikosi vya Wamoabu vilikuwa vinashambulia nchi kwa vita kila mwaka wakati wa vuli.
Und Elischa starb, und sie begruben ihn. Und es kamen Kriegshaufen der Moabiter ins Land mit dem kommenden Jahre.
21 Ikawa Waisraeli fulani walipokuwa wanamzika mtu, ghafula wakaona kikosi cha washambuliaji, basi wakaitupa ile maiti ya yule mtu ndani ya kaburi la Elisha. Wakati ile maiti ilipogusa mifupa ya Elisha, yule mtu akafufuka na kusimama kwa miguu yake.
Und es geschah, daß sie einen Mann begruben; und siehe da, sie sahen den Kriegshaufen und warfen den Mann in Elischas Grab, und der Mann kam hin und berührte die Gebeine Elischas und er ward lebendig und stand auf seinen Füßen.
22 Hazaeli mfalme wa Aramu aliwatesa Israeli wakati wote wa utawala wa Yehoahazi.
Und Chasael, König Arams, unterdrückte Israel alle Tage des Jehoachas.
23 Lakini Bwana akawarehemu na akawahurumia, akaonyesha kujishughulisha nao kwa sababu ya Agano lake na Abrahamu, Isaki na Yakobo. Hadi leo, hajawaangamiza wala kuwafukuza mbele zake.
Und Jehovah war ihnen gnädig, und erbarmte Sich ihrer, und wandte Sich ihnen zu um Seines Bundes willen mit Abraham, Isaak und Jakob, und war nicht willens, sie zu verderben, und warf sie nicht weg von Seinem Angesicht bis jetzt.
24 Hazaeli mfalme wa Shamu akafa, naye Ben-Hadadi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Und Chasael, König von Aram, starb, und Ben-Hadad, sein Sohn, ward König an seiner Stelle.
25 Kisha Yehoashi mwana wa Yehoahazi akateka tena kutoka kwa Ben-Hadadi mwana wa Hazaeli ile miji aliyokuwa ameitwaa kwa vita kutoka kwa baba yake Yehoahazi. Yehoashi alimshinda mara tatu, hivyo akaweza kuiteka tena ile miji ya Waisraeli.
Und Jehoasch, der Sohn des Jehoachas, kehrte um und nahm aus der Hand des Ben-Hadad, des Sohnes Chasaels, die Städte, die er dem Jehoachas, seinem Vater, im Streite aus der Hand genommen hatte. Dreimal schlug ihn Joasch, und nahm zurück die Städte Israels.

< 2 Wafalme 13 >