< 2 Wafalme 13 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wa Yoashi mwana wa Ahazia mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu alianza kutawala Israeli katika Samaria, naye akatawala miaka kumi na saba.
In the twenty-third year of Joash, the son of Ahaziah, king of Judah, Jehoahaz, the son of Jehu, became king over Israel in Samaria, ruling for seventeen years.
2 Akafanya maovu machoni pa Bwana kwa kufuata dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, na wala hakuziacha.
He did evil in the eyes of the Lord, copying the sins of Jeroboam, the son of Nebat, which he did and made Israel do; he did not keep himself from them.
3 Kwa hiyo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli na kwa muda mrefu akawaweka chini ya utawala wa Hazaeli mfalme wa Aramu, na Ben-Hadadi mwanawe.
So the wrath of the Lord was burning against Israel, and he gave them up into the power of Hazael, king of Aram, and into the power of Ben-hadad, the son of Hazael, again and again.
4 Ndipo Yehoahazi akamsihi Bwana rehema, naye Bwana akamsikiliza, kwa maana aliona jinsi mfalme wa Aramu alivyokuwa akiwatesa Israeli vikali.
Then Jehoahaz made prayer to the Lord, and the Lord gave ear to him, for he saw how cruelly Israel was crushed by the king of Aram.
5 Bwana akamtoa mwokozi kwa ajili ya Israeli, nao wakaokoka kutoka kwenye mamlaka ya Aramu. Hivyo Waisraeli wakaishi katika nyumba zao wenyewe kama ilivyokuwa hapo awali.
(And the Lord gave Israel a saviour, so that they became free from the hands of the Aramaeans; and the children of Israel were living in their tents as in the past.
6 Lakini hawakuziacha dhambi za nyumba ya Yeroboamu, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, bali wakaendelea kuzitenda. Nguzo ya Ashera pia iliendelea kusimama katika Samaria.
But still they did not give up the sin of Jeroboam, which he made Israel do, but went on with it; and there was an image of Asherah in Samaria.)
7 Hapakubaki kitu chochote katika jeshi la Yehoahazi isipokuwa wapanda farasi hamsini, magari kumi ya vita na askari wa miguu elfu kumi, kwa kuwa mfalme wa Aramu alikuwa amewaangamiza hao wengine na kuwafanya kama mavumbi wakati wa kupura nafaka.
For out of all his army, Jehoahaz had only fifty horsemen and ten carriages and ten thousand footmen; the king of Aram had given them up to destruction, crushing them like dust.
8 Matukio mengine ya utawala wa Yehoahazi yote aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Now the rest of the acts of Jehoahaz, and all he did, and his great power, are they not recorded in the book of the history of the kings of Israel?
9 Yehoahazi akalala pamoja na baba zake, akazikwa huko Samaria. Naye Yehoashi mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Jehoahaz went to rest with his fathers, and was put into the earth in Samaria; and Joash his son became king in his place.
10 Katika mwaka wa thelathini na saba wa utawala wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yehoashi mwana wa Yehoahazi alianza kutawala Israeli huko Samaria, naye akatawala miaka kumi na sita.
In the thirty-seventh year of the rule of Joash, king of Judah, Joash, the son of Jehoahaz, became king over Israel in Samaria, ruling for sixteen years.
11 Alifanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi yoyote kati ya zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, bali aliendelea kuzitenda.
He did evil in the eyes of the Lord, not turning away from the sin of Jeroboam, the son of Nebat, which he did and made Israel do, but he went on with it.
12 Na kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, yote aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita yake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Now the rest of the acts of Joash, and all he did, and the force with which he went to war against Amaziah, king of Judah, are they not recorded in the book of the history of the kings of Israel?
13 Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli. Yeroboamu akawa mfalme baada yake.
And Joash went to rest with his fathers and Jeroboam took his place as king; and Joash was put into the earth in Samaria with the kings of Israel.
14 Wakati huu, Elisha alikuwa anaumwa na ugonjwa ambao baadaye ulimuua. Yehoashi mfalme wa Israeli akashuka kwenda kumwona na kumlilia. Akalia, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya vita ya Israeli na wapanda farasi wake!”
Now Elisha became ill with the disease which was the cause of his death: and Joash, king of Israel, came down to him, and weeping over him said, My father, my father, the war-carriages of Israel and its horsemen!
15 Elisha akasema, “Leta upinde na baadhi ya mishale,” naye mfalme akafanya hivyo.
Then Elisha said to him, Take bow and arrows: and he took bow and arrows.
16 Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Shika upinde mikononi mwako.” Alipokwisha kuichukua, Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme.
And he said to the king of Israel, Put your hand on the bow: and he put his hand on it; and Elisha put his hands on the king's hands.
17 Elisha akasema, “Fungua dirisha la mashariki,” naye akalifungua. Elisha akasema, “Piga mshale!” Naye akapiga mshale. Elisha akasema, “Mshale wa ushindi wa Bwana, mshale wa ushindi juu ya Aramu! Utawaangamiza Waaramu kabisa huko Afeki.”
Then he said; Let the window be open to the east: and he got it open. Then Elisha said, Let the arrow go; and he let it go. And he said, The Lord's arrow of salvation, of salvation over Aram; for you will overcome the Aramaeans in Aphek and put an end to them.
18 Kisha akasema, “Chukua mishale,” naye mfalme akaichukua. Elisha akamwambia, “Piga ardhi kwa hiyo mishale.” Akaipiga mara tatu, halafu akaacha.
And he said, Take the arrows: and he took them. And he said to the king of Israel, Send them down into the earth; and he did so three times and no more.
19 Mtu wa Mungu akamkasirikia na akasema, “Ungepiga chini mara tano au sita, ndipo ungeishinda Aramu na kuiangamiza kabisa. Lakini sasa utaishinda mara tatu tu.”
Then the man of God was angry with him and said, If you had done it five or six times, then you would have overcome Aram completely; but now you will only overcome them three times.
20 Elisha akafa, nao wakamzika. Vikosi vya Wamoabu vilikuwa vinashambulia nchi kwa vita kila mwaka wakati wa vuli.
And death came to Elisha and they put his body into the earth. Now in the spring of the year, armed bands of Moabites frequently came, overrunning the land.
21 Ikawa Waisraeli fulani walipokuwa wanamzika mtu, ghafula wakaona kikosi cha washambuliaji, basi wakaitupa ile maiti ya yule mtu ndani ya kaburi la Elisha. Wakati ile maiti ilipogusa mifupa ya Elisha, yule mtu akafufuka na kusimama kwa miguu yake.
And while they were putting a dead man into the earth, they saw a band coming; and they put the man quickly into the place where Elisha's body was; and the dead man, on touching Elisha's bones, came to life again, and got up on his feet.
22 Hazaeli mfalme wa Aramu aliwatesa Israeli wakati wote wa utawala wa Yehoahazi.
And Israel was crushed under the power of Hazael, king of Aram, all the days of Jehoahaz.
23 Lakini Bwana akawarehemu na akawahurumia, akaonyesha kujishughulisha nao kwa sababu ya Agano lake na Abrahamu, Isaki na Yakobo. Hadi leo, hajawaangamiza wala kuwafukuza mbele zake.
But the Lord was kind to them and had pity on them, caring for them, because of his agreement with Abraham, Isaac, and Jacob; he would not put them to destruction or send them away from before his face till now.
24 Hazaeli mfalme wa Shamu akafa, naye Ben-Hadadi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Then Hazael, king of Aram, came to his end; and Ben-hadad his son became king in his place.
25 Kisha Yehoashi mwana wa Yehoahazi akateka tena kutoka kwa Ben-Hadadi mwana wa Hazaeli ile miji aliyokuwa ameitwaa kwa vita kutoka kwa baba yake Yehoahazi. Yehoashi alimshinda mara tatu, hivyo akaweza kuiteka tena ile miji ya Waisraeli.
And Jehoash, the son of Jehoahaz, took again from Ben-hadad, the son of Hazael, the towns which he had taken from Jehoahaz his father in war. Three times Jehoash overcame him and got back the towns of Israel.

< 2 Wafalme 13 >