< 2 Wafalme 12 >

1 Katika mwaka wa saba wa utawala wa Yehu, Yoashi alianza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka arobaini. Jina la mama yake aliitwa Sibia, kutoka Beer-Sheba.
Ce fut la septième année de Jéhu que Joas devint roi, et il régna quarante ans à Jérusalem. Or le nom de sa mère était Tsibia de Béerséba.
2 Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa akimwelekeza.
Et Joas pratiqua ce qui est droit aux yeux de l'Éternel, aussi longtemps qu'il eut les directions du Prêtre Jehojada.
3 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Seulement les tertres ne disparurent pas; le peuple offrait encore des victimes et de l'encens sur les tertres.
4 Yoashi akawaambia makuhani, “Kusanyeni fedha zote ambazo zitaletwa kama sadaka takatifu kwenye Hekalu la Bwana, yaani fedha zilizokusanywa kama kodi, fedha zilizopokelewa kutokana na nadhiri za watu binafsi, na fedha zilizoletwa kwa hiari hekaluni.
Et Joas dit aux Prêtres: Tout l'argent consacré qui est apporté au temple de l'Éternel, argent ayant cours, l'argent pour la vie payé par chacun d'après son estimation, tout l'argent que le cœur suggère à quelqu'un d'apporter au temple de l'Éternel,
5 Kila kuhani na apokee fedha kutoka kwa mmoja wa watunza hazina, nazo zitumike kukarabati uharibifu wowote unaoonekana katika Hekalu.”
que les Prêtres le retirent chacun de ses relations et l'emploient à réparer les brèches du temple partout où il s'y trouvera une brèche.
6 Lakini ikawa kufikia mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Mfalme Yoashi, makuhani walikuwa bado hawajalikarabati Hekalu.
Et il arriva que, la vingt-troisième année du roi Joas, les Prêtres n'avaient point réparé les brèches du temple.
7 Kwa hiyo Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na makuhani wengine, akawauliza, “Kwa nini hamtengenezi uharibifu uliofanyika hekaluni? Msichukue fedha zaidi kutoka kwa watunza hazina wenu kwa ajili ya matumizi yenu, lakini kuanzia sasa ni lazima fedha yote itumike kwa ajili ya kukarabati Hekalu.”
Alors le roi Joas manda le Prêtre Jehojada et les Prêtres et leur dit: Pourquoi ne réparez-vous pas les brèches du temple? Eh bien! donc vous n'avez plus à retirer d'argent de vos relations, car vous devez l'affecter aux brèches du temple.
8 Makuhani wakakubali kuwa hawatakusanya tena fedha kutoka kwa watu na kwamba hawatakarabati Hekalu wenyewe.
Et les Prêtres consentirent à ne plus retirer l'argent du peuple et à ne pas réparer les brèches du temple.
9 Yehoyada kuhani akachukua kisanduku na akatoboa tundu kwenye kifuniko chake. Akakiweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia hekaluni mwa Bwana. Makuhani waliolinda ingilio wakaweka ndani ya kisanduku fedha zote ambazo zililetwa katika Hekalu la Bwana.
Et le Prêtre Jehojada prit un coffre au couvercle duquel il perça un trou et qu'il plaça à côté de l'autel à droite; quelqu'un entrait-il au temple de l'Éternel, les Prêtres, gardes du seuil, y jetaient tout l'argent apporté au temple de l'Éternel.
10 Kila mara walipoona kuwa kuna kiasi kikubwa cha fedha ndani ya kisanduku, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja, wakazihesabu fedha hizo zilizoletwa katika Hekalu la Bwana, na kuziweka katika mifuko.
Et quand ils virent il qu'il y avait beaucoup d'argent dans le coffre, le Secrétaire du roi et le Grand Prêtre vinrent, et ils en firent des rouleaux, et comptèrent cet argent qui se trouvait dans le temple de l'Éternel.
11 Wakiisha kuthibitisha kiasi cha hizo fedha, waliwapa watu walioteuliwa kusimamia kazi katika Hekalu. Kwa fedha hizo, wakawalipa wale watu waliofanya kazi katika Hekalu la Bwana: yaani, maseremala na wajenzi,
Et ils remirent l'argent, pesé, entre les mains des entrepreneurs de l'ouvrage employés au temple de l'Éternel, et ceux-ci en payèrent les charpentiers et architectes occupés au temple de l'Éternel
12 waashi na wakata mawe. Walinunua mbao na mawe ya kuchongwa kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana, na kulipia gharama nyingine zote za kulitengeneza.
et les maçons et tailleurs de pierre, et les achats de bois et de pierre de taille pour la réparation des brèches du temple de l'Éternel, et toutes les dépenses faites au temple pour la restauration.
13 Fedha zilizoletwa kwenye Hekalu hazikutumiwa kutengenezea masinia ya fedha, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, tarumbeta wala vyombo vingine vyovyote vya dhahabu au fedha kwa ajili ya Hekalu la Bwana;
Cependant pour le temple de l'Éternel on ne fit ni bassins d'argent, ni couteaux, ni jattes, ni trompettes, ni vaisselle quelconque d'or et d'argent, avec l'argent entré au temple de l'Éternel,
14 zililipwa kwa wafanyakazi, ambao walizitumia kwa kukarabati Hekalu.
mais on l'employa à payer ceux qui firent l'ouvrage, et qui l'appliquèrent à la restauration du temple de l'Éternel.
15 Wao hawakudai kupewa hesabu ya fedha kutoka kwa wale waliowapa ili kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu walifanya kwa uaminifu wote.
Et l'on ne compta point avec les hommes entre les mains desquels on avait remis l'argent pour en payer les ouvriers, car c'est avec bonne foi qu'ils agissaient.
16 Fedha zilizopatikana kutokana na sadaka za hatia na sadaka za dhambi hazikuletwa katika Hekalu la Bwana; zilikuwa mali ya makuhani.
L'amende pour délit et l'amende pour péché
17 Wakati huu Hazaeli mfalme wa Aramu akapanda kuishambulia Gathi, akaiteka. Kisha akageuka ili kuishambulia Yerusalemu.
n'entrèrent point dans le temple de l'Éternel; elles furent pour les Prêtres.
18 Lakini Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vyombo vyote vitakatifu vilivyowekwa wakfu na baba zake, yaani Yehoshafati, Yehoramu na Ahazia, wafalme wa Yuda, zawadi ambazo yeye mwenyewe alikuwa ameziweka wakfu pamoja na dhahabu yote iliyokutwa katika hazina za Hekalu la Bwana na katika jumba la kifalme, akazipeleka kwa Hazaeli mfalme wa Aramu, ambaye hatimaye aliondoka Yerusalemu.
C'est alors que Hazaël, roi de Syrie, s'avança et vint attaquer Gath dont il s'empara. Et Hazaël ayant résolu de marcher sur Jérusalem, Joas, roi de Juda, prit toutes les choses consacrées qu'avaient consacrées Josaphat et Joram et Achazia, ses pères, rois de Juda, et ce qu'il avait consacré lui-même et tout l'or qui se trouvait dans les trésors du temple de l'Éternel et du palais royal, et envoya le tout à Hazaël, roi de Syrie. Et Hazaël s'éloigna de Jérusalem.
19 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Le reste des actes de Joas et toutes ses entreprises sont d'ailleurs consignés dans le livre des annales des rois de Juda.
20 Maafisa wake wakafanya shauri baya dhidi yake, nao wakamuulia Yoashi huko Beth-Milo, kwenye barabara iteremkayo kuelekea Sila.
Et ses serviteurs se levèrent et formèrent une conjuration et frappèrent Joas à Beth-Millo, qui descend à Silla.
21 Maafisa waliomuua walikuwa Yozabadi mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri. Akafa na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi. Naye Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Jozachar, fils de Simeath, et Jozabad, fils de Somer, ses serviteurs, lui portèrent les coups dont il mourut; et ils lui donnèrent la sépulture à côté de ses pères dans la ville de David. Et Amatsia, son fils, régna en sa place.

< 2 Wafalme 12 >