< 2 Wafalme 12 >

1 Katika mwaka wa saba wa utawala wa Yehu, Yoashi alianza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka arobaini. Jina la mama yake aliitwa Sibia, kutoka Beer-Sheba.
In the seventh year of Jehu, Jehoash has reigned, and he has reigned forty years in Jerusalem, and the name of his mother [is] Zibiah of Beer-Sheba,
2 Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa akimwelekeza.
and Jehoash does that which is right in the eyes of YHWH all his days in which Jehoiada the priest directed him,
3 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
only, the high places have not been removed—the people are still sacrificing and making incense in high places.
4 Yoashi akawaambia makuhani, “Kusanyeni fedha zote ambazo zitaletwa kama sadaka takatifu kwenye Hekalu la Bwana, yaani fedha zilizokusanywa kama kodi, fedha zilizopokelewa kutokana na nadhiri za watu binafsi, na fedha zilizoletwa kwa hiari hekaluni.
And Jehoash says to the priests, “All the money of the sanctified things that is brought into the house of YHWH, the money of him who is passing over, the money of each of the souls—his valuation, all the money that goes up on the heart of a man to bring into the house of YHWH,
5 Kila kuhani na apokee fedha kutoka kwa mmoja wa watunza hazina, nazo zitumike kukarabati uharibifu wowote unaoonekana katika Hekalu.”
the priests take to themselves, each from his acquaintance, and they strengthen the breach of the house in all [places] there where a breach is found.”
6 Lakini ikawa kufikia mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Mfalme Yoashi, makuhani walikuwa bado hawajalikarabati Hekalu.
And it comes to pass, in the twenty-third year of King Jehoash, the priests have not strengthened the breach of the house,
7 Kwa hiyo Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na makuhani wengine, akawauliza, “Kwa nini hamtengenezi uharibifu uliofanyika hekaluni? Msichukue fedha zaidi kutoka kwa watunza hazina wenu kwa ajili ya matumizi yenu, lakini kuanzia sasa ni lazima fedha yote itumike kwa ajili ya kukarabati Hekalu.”
and King Jehoash calls to Jehoiada the priest, and to the priests, and says to them, “Why are you not strengthening the breach of the house? And now, receive no money from your acquaintances, but give it for the breach of the house.”
8 Makuhani wakakubali kuwa hawatakusanya tena fedha kutoka kwa watu na kwamba hawatakarabati Hekalu wenyewe.
And the priests do not consent to receive money from the people, nor to strengthen the breach of the house,
9 Yehoyada kuhani akachukua kisanduku na akatoboa tundu kwenye kifuniko chake. Akakiweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia hekaluni mwa Bwana. Makuhani waliolinda ingilio wakaweka ndani ya kisanduku fedha zote ambazo zililetwa katika Hekalu la Bwana.
and Jehoiada the priest takes a chest, and pierces a hole in its lid, and puts it near the altar, on the right side, as one comes into the house of YHWH, and the priests keeping the threshold have put all the money there that is brought into the house of YHWH.
10 Kila mara walipoona kuwa kuna kiasi kikubwa cha fedha ndani ya kisanduku, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja, wakazihesabu fedha hizo zilizoletwa katika Hekalu la Bwana, na kuziweka katika mifuko.
And it comes to pass, at their seeing that the money [is] abundant in the chest, that there goes up a scribe of the king, and of the high priest, and they bind [it] up, and count the money that is found [in] the house of YHWH,
11 Wakiisha kuthibitisha kiasi cha hizo fedha, waliwapa watu walioteuliwa kusimamia kazi katika Hekalu. Kwa fedha hizo, wakawalipa wale watu waliofanya kazi katika Hekalu la Bwana: yaani, maseremala na wajenzi,
and have given the weighed money into the hands of those doing the work, those inspecting the house of YHWH, and they bring it out to those working in the wood, and to builders who are working in the house of YHWH,
12 waashi na wakata mawe. Walinunua mbao na mawe ya kuchongwa kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana, na kulipia gharama nyingine zote za kulitengeneza.
and to those [repairing] the wall, and to hewers of stone, and to buy wood and hewn stones to strengthen the breach of the house of YHWH, and for all that goes out on the house, to strengthen it.
13 Fedha zilizoletwa kwenye Hekalu hazikutumiwa kutengenezea masinia ya fedha, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, tarumbeta wala vyombo vingine vyovyote vya dhahabu au fedha kwa ajili ya Hekalu la Bwana;
Only, there is not made for the house of YHWH basins of silver, snuffers, bowls, trumpets, any vessel of gold, and vessel of silver, out of the money that is brought into the house of YHWH;
14 zililipwa kwa wafanyakazi, ambao walizitumia kwa kukarabati Hekalu.
for they give it to those doing the work, and they have strengthened the house of YHWH with it,
15 Wao hawakudai kupewa hesabu ya fedha kutoka kwa wale waliowapa ili kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu walifanya kwa uaminifu wote.
and they do not reckon with the men into whose hand they give the money to give to those doing the work, for they are dealing in faithfulness.
16 Fedha zilizopatikana kutokana na sadaka za hatia na sadaka za dhambi hazikuletwa katika Hekalu la Bwana; zilikuwa mali ya makuhani.
The money of a trespass-offering and the money of sin-offerings is not brought into the house of YHWH—it is for the priests.
17 Wakati huu Hazaeli mfalme wa Aramu akapanda kuishambulia Gathi, akaiteka. Kisha akageuka ili kuishambulia Yerusalemu.
Then Hazael king of Aram goes up and fights against Gath, and captures it, and Hazael sets his face to go up against Jerusalem;
18 Lakini Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vyombo vyote vitakatifu vilivyowekwa wakfu na baba zake, yaani Yehoshafati, Yehoramu na Ahazia, wafalme wa Yuda, zawadi ambazo yeye mwenyewe alikuwa ameziweka wakfu pamoja na dhahabu yote iliyokutwa katika hazina za Hekalu la Bwana na katika jumba la kifalme, akazipeleka kwa Hazaeli mfalme wa Aramu, ambaye hatimaye aliondoka Yerusalemu.
and Jehoash king of Judah takes all the sanctified things that Jehoshaphat, and Jehoram, and Ahaziah, his fathers, kings of Judah, had sanctified, and his own sanctified things, and all the gold that is found in the treasures of the house of YHWH and of the house of the king, and sends [them] to Hazael king of Aram, and he goes up from off Jerusalem.
19 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
And the rest of the matters of Joash and all that he did, are they not written on the scroll of the Chronicles of the Kings of Judah?
20 Maafisa wake wakafanya shauri baya dhidi yake, nao wakamuulia Yoashi huko Beth-Milo, kwenye barabara iteremkayo kuelekea Sila.
And his servants rise, and make a conspiracy, and strike Joash in the house of Millo, that is going down to Silla.
21 Maafisa waliomuua walikuwa Yozabadi mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri. Akafa na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi. Naye Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Indeed, Jozachar son of Shimeath, and Jehozabad son of Shemer, his servants, have struck him, and he dies, and they bury him with his fathers in the City of David, and his son Amaziah reigns in his stead.

< 2 Wafalme 12 >