< 2 Wafalme 12 >

1 Katika mwaka wa saba wa utawala wa Yehu, Yoashi alianza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka arobaini. Jina la mama yake aliitwa Sibia, kutoka Beer-Sheba.
Jehu a bawinae kum 7 navah, Jehoash teh siangpahrang lah ao. Jerusalem vah kum 40 touh a uk, a manu min teh Zibiah Beersheba kho e tami doeh.
2 Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa akimwelekeza.
Vaihma, Jehoiada ni Jehoash a pâtu nathung pueng teh BAWIPA mithmu vah, hawinae hah ouk a sak.
3 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Hatei hmuenrasang lah puen kalawn hoeh. Hmuenrasang dawk tami moikapap ni Cathut thuengnae hmuitui a sawi awh.
4 Yoashi akawaambia makuhani, “Kusanyeni fedha zote ambazo zitaletwa kama sadaka takatifu kwenye Hekalu la Bwana, yaani fedha zilizokusanywa kama kodi, fedha zilizopokelewa kutokana na nadhiri za watu binafsi, na fedha zilizoletwa kwa hiari hekaluni.
Jehoash ni vaihmanaw koe BAWIPA im vah kâenkhai e hno kathoung ratangnae, hnopainaw pueng, milu touk tangcoungnaw koe kacetnaw pueng hanelah, khoe lah kaawm e kâratangnae hnonaw hoi bangpatet e tami ni BAWIPA im vah a ceikhai teh a pasoung awh e naw hah,
5 Kila kuhani na apokee fedha kutoka kwa mmoja wa watunza hazina, nazo zitumike kukarabati uharibifu wowote unaoonekana katika Hekalu.”
vaihmanaw ni, amamae a uk awh e thungup lat van naseh. Bawkim a rawknae hmuen tangkuem koe rem awh naseh atipouh.
6 Lakini ikawa kufikia mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Mfalme Yoashi, makuhani walikuwa bado hawajalikarabati Hekalu.
Hatei siangpahrang Jehoash teh kum 23 touh a bawi nakunghai vaihmanaw ni bawkim ka rawk e naw heh pathoup kalawn awh hoeh.
7 Kwa hiyo Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na makuhani wengine, akawauliza, “Kwa nini hamtengenezi uharibifu uliofanyika hekaluni? Msichukue fedha zaidi kutoka kwa watunza hazina wenu kwa ajili ya matumizi yenu, lakini kuanzia sasa ni lazima fedha yote itumike kwa ajili ya kukarabati Hekalu.”
Hottelah siangpahrang Jehoash ni vaihma Jehoiada hoi vaihma alouknaw hah a kaw teh, ahnimouh koe, bangkongmaw bawkim ka rawk e hmuennaw hah na pathoup awh hoeh. Atu hoi teh, na uknae thung e tami koe e tangka lat awh hanh lawih. Bawkim ka rawk e pathoup nahanlah poe awh lawih telah a ti.
8 Makuhani wakakubali kuwa hawatakusanya tena fedha kutoka kwa watu na kwamba hawatakarabati Hekalu wenyewe.
Vaihmanaw ni hai ayânaw koe tangka toung laipalah, bawkim ka rawk e hai pathoup hoeh hanelah a hnâbo awh.
9 Yehoyada kuhani akachukua kisanduku na akatoboa tundu kwenye kifuniko chake. Akakiweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia hekaluni mwa Bwana. Makuhani waliolinda ingilio wakaweka ndani ya kisanduku fedha zote ambazo zililetwa katika Hekalu la Bwana.
Hot patetlah, vaihma Jehoiada ni thingkongca a la teh, a khuem hah a paawng. BAWIPA im kâennaw aranglah thuengnae khoungroe teng vah a tâ teh a sin awh e tangkanaw pueng hah, takhang ka ring e vaihma ni paloupalou a ta pouh.
10 Kila mara walipoona kuwa kuna kiasi kikubwa cha fedha ndani ya kisanduku, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja, wakazihesabu fedha hizo zilizoletwa katika Hekalu la Bwana, na kuziweka katika mifuko.
Hahoi teh hettelah doeh. Thingkong dawk tangka apap toe tie a panue awh toteh, siangpahrang e cakathutkung hoi vaihma kacue ni, a ceikhai teh BAWIPA im vah tangka kaawm e pueng a touk awh.
11 Wakiisha kuthibitisha kiasi cha hizo fedha, waliwapa watu walioteuliwa kusimamia kazi katika Hekalu. Kwa fedha hizo, wakawalipa wale watu waliofanya kazi katika Hekalu la Bwana: yaani, maseremala na wajenzi,
A touk awh e tangka teh thaw katawknaw, BAWIPA im kasakkungnaw, imsakkathoumnaw e kut phu, talung kadeinaw hoiyah talung katâcawtsaknaw e kut phu hoi,
12 waashi na wakata mawe. Walinunua mbao na mawe ya kuchongwa kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana, na kulipia gharama nyingine zote za kulitengeneza.
Bawipa e Bawkim ka rawk e naw pathoup nahanlah thing hoi talung kuennae hoi im a rawknae koe, a pankinae hmuen pueng koe a hno awh.
13 Fedha zilizoletwa kwenye Hekalu hazikutumiwa kutengenezea masinia ya fedha, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, tarumbeta wala vyombo vingine vyovyote vya dhahabu au fedha kwa ajili ya Hekalu la Bwana;
Hatei BAWIPA imthungkhu tangka a sin awh hoi BAWIPA im hanlah, ngun, rahum, hoi hmai paduenae hoi Ailo ka dung hoi mongka hoi suihlaamnaw, ngunhlaamnaw hah hote tangka hoi sak hoeh.
14 zililipwa kwa wafanyakazi, ambao walizitumia kwa kukarabati Hekalu.
Hatei, thaw katawkkungnaw ouk a poe awh teh BAWIPA e im pathoup nahanlah a hno awh.
15 Wao hawakudai kupewa hesabu ya fedha kutoka kwa wale waliowapa ili kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu walifanya kwa uaminifu wote.
Thaw katawkkungnaw, poe hanlah tangka a kuem sak awh e naw hoi kuekluek parei pouh hoeh toe. Bangkongtetpawiteh, yuemkamculah a tawk awh.
16 Fedha zilizopatikana kutokana na sadaka za hatia na sadaka za dhambi hazikuletwa katika Hekalu la Bwana; zilikuwa mali ya makuhani.
Kâtapoe thuengnae tangka hoi yon thuengnae tangka teh BAWIPA im dawk kâen sak a hoeh. Hot teh vaihmanaw e ham doeh.
17 Wakati huu Hazaeli mfalme wa Aramu akapanda kuishambulia Gathi, akaiteka. Kisha akageuka ili kuishambulia Yerusalemu.
Siria siangpahrang Hazael ni, Gath a tuk. Be a la hnukkhu Hazael teh Jerusalem ban hanlah a noe.
18 Lakini Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vyombo vyote vitakatifu vilivyowekwa wakfu na baba zake, yaani Yehoshafati, Yehoramu na Ahazia, wafalme wa Yuda, zawadi ambazo yeye mwenyewe alikuwa ameziweka wakfu pamoja na dhahabu yote iliyokutwa katika hazina za Hekalu la Bwana na katika jumba la kifalme, akazipeleka kwa Hazaeli mfalme wa Aramu, ambaye hatimaye aliondoka Yerusalemu.
Judah siangpahrang Jehoash ni a na pa hoi Jehoshaphat hoi Jehoram hoi Ahaziah tinaw ni ouk a poe awh e kathounge hnonaw pueng, amamouh ni thoung sak awh e hnonaw hoi BAWIPA im kaawmnaw pueng hoi siangpahrang im vah kaawm, suinaw pueng a la awh teh, Siria siangpahrang Hazael a patawn awh. Hahoi teh Jerusalem a kamlang takhai awh.
19 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Hot patetlah, Joash a tawksaknae naw thung dawk e kaawm rae naw, a sakyoe e naw pueng teh Judah siangpahrang setouknae cauk dawkvah koung thut lah ao nahoehmaw.
20 Maafisa wake wakafanya shauri baya dhidi yake, nao wakamuulia Yoashi huko Beth-Milo, kwenye barabara iteremkayo kuelekea Sila.
Hahoi a taminaw a thaw awh teh a kâcoun awh. Joash teh Silla lah ceinae lam, Millo im vah, a hem awh teh a thei awh.
21 Maafisa waliomuua walikuwa Yozabadi mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri. Akafa na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi. Naye Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
A san Shimeath capa Jozakhar koevah, Devit khopui dawk a pakawp awh teh a capa Amaziah teh a yueng lah a bawi.

< 2 Wafalme 12 >