< 2 Wafalme 12 >
1 Katika mwaka wa saba wa utawala wa Yehu, Yoashi alianza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka arobaini. Jina la mama yake aliitwa Sibia, kutoka Beer-Sheba.
В седмата година на Ииуя се възцари Иоас, и царува четиридесет години в Ерусалим; а името на майка му бе Савия, от Вирсавее.
2 Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa akimwelekeza.
И Иоас вършеше това, което бе право пред Господа, през всичкото време, когато го наставляваше свещеник Иодай.
3 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Обаче високите места не се отмъхнаха; людете още жертвуваха и кадяха по високите места.
4 Yoashi akawaambia makuhani, “Kusanyeni fedha zote ambazo zitaletwa kama sadaka takatifu kwenye Hekalu la Bwana, yaani fedha zilizokusanywa kama kodi, fedha zilizopokelewa kutokana na nadhiri za watu binafsi, na fedha zilizoletwa kwa hiari hekaluni.
А Иоас рече на свещениците: Всичките пари от посветените неща, които се внасят в Господния дом, и парите от всекиго, който преминава преброението, и парите от всукиго според оценката му, и всичките пари, които би дошло някому в сърцето да принесе в Господния дом,
5 Kila kuhani na apokee fedha kutoka kwa mmoja wa watunza hazina, nazo zitumike kukarabati uharibifu wowote unaoonekana katika Hekalu.”
свещениците нека ги вземат у себе си, всеки от познатия си, и нека поправят разваленото на дома, гдето се набери развалено.
6 Lakini ikawa kufikia mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Mfalme Yoashi, makuhani walikuwa bado hawajalikarabati Hekalu.
Но понеже до двадасат и тертата година на цар Иоаса свещениците не бяха поправяли разваленото на дома,
7 Kwa hiyo Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na makuhani wengine, akawauliza, “Kwa nini hamtengenezi uharibifu uliofanyika hekaluni? Msichukue fedha zaidi kutoka kwa watunza hazina wenu kwa ajili ya matumizi yenu, lakini kuanzia sasa ni lazima fedha yote itumike kwa ajili ya kukarabati Hekalu.”
затова цар Иоас повика свещеник Иодай и другите свещеници та им рече: Защо не поправихте разваленото на дома? Сега, прочее, не вземайте вече пари от познатите си, но дайте събраното за разваленото на дома.
8 Makuhani wakakubali kuwa hawatakusanya tena fedha kutoka kwa watu na kwamba hawatakarabati Hekalu wenyewe.
И свещениците склониха нито да вземат вече пари от людете, нито да бъдат отговорни за поправяне разваленото на дома.
9 Yehoyada kuhani akachukua kisanduku na akatoboa tundu kwenye kifuniko chake. Akakiweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia hekaluni mwa Bwana. Makuhani waliolinda ingilio wakaweka ndani ya kisanduku fedha zote ambazo zililetwa katika Hekalu la Bwana.
А свещеник Иодай взе един котвчег и като отвори дупка на капака му, тури го при олтара отдясно на входа в Господния дом; и свещениците, които пазеха вратата, туриха в него всичките пари, които се внасяха в Господния дом.
10 Kila mara walipoona kuwa kuna kiasi kikubwa cha fedha ndani ya kisanduku, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja, wakazihesabu fedha hizo zilizoletwa katika Hekalu la Bwana, na kuziweka katika mifuko.
И когато виждаха, че имаше много пари в ковчега, царският секретар и първосвещеникът отиваха та завързваха в мешци намерените в Господния дом пари, като ги брояха.
11 Wakiisha kuthibitisha kiasi cha hizo fedha, waliwapa watu walioteuliwa kusimamia kazi katika Hekalu. Kwa fedha hizo, wakawalipa wale watu waliofanya kazi katika Hekalu la Bwana: yaani, maseremala na wajenzi,
И даваха преброените пари в ръцете на ония, които вършеха делото, които надзираваха Господния дом; а те ги иждивяваха по дърводелците и строителите, които работеха в Господния дом,
12 waashi na wakata mawe. Walinunua mbao na mawe ya kuchongwa kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana, na kulipia gharama nyingine zote za kulitengeneza.
и по зидарите и по каменоделците, и за купеване на дървета и дялани камъни за поправяне разваленото на Господния дом, и за всяко иждивение за поправката на дома.
13 Fedha zilizoletwa kwenye Hekalu hazikutumiwa kutengenezea masinia ya fedha, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, tarumbeta wala vyombo vingine vyovyote vya dhahabu au fedha kwa ajili ya Hekalu la Bwana;
Но от парите, които се внасяха в Господния дом, не се направиха сребърни чаши, щипци, легени, тръби, нито какви да било златни съдове или сребърни съдове;
14 zililipwa kwa wafanyakazi, ambao walizitumia kwa kukarabati Hekalu.
но даваха ги на работниците, и поправяха с тях Господния дом.
15 Wao hawakudai kupewa hesabu ya fedha kutoka kwa wale waliowapa ili kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu walifanya kwa uaminifu wote.
Освен това, не търсеха сметка от човеците, на които даваха парите за да се разпределят на работниците, защото постъпваха честно.
16 Fedha zilizopatikana kutokana na sadaka za hatia na sadaka za dhambi hazikuletwa katika Hekalu la Bwana; zilikuwa mali ya makuhani.
Обаче, парите принасяни за преспътление и парите принасяне за грях, не се внасяха в Господния дом; те бяха за свещениците.
17 Wakati huu Hazaeli mfalme wa Aramu akapanda kuishambulia Gathi, akaiteka. Kisha akageuka ili kuishambulia Yerusalemu.
Тогава дойде сирийският цар Азаил та воюва против Гет и го превзе; и Азаил обърна лицето си за да дойде против Ерусалим.
18 Lakini Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vyombo vyote vitakatifu vilivyowekwa wakfu na baba zake, yaani Yehoshafati, Yehoramu na Ahazia, wafalme wa Yuda, zawadi ambazo yeye mwenyewe alikuwa ameziweka wakfu pamoja na dhahabu yote iliyokutwa katika hazina za Hekalu la Bwana na katika jumba la kifalme, akazipeleka kwa Hazaeli mfalme wa Aramu, ambaye hatimaye aliondoka Yerusalemu.
Затова Юдовият цер Иоас взе всичките посветени неща, които бащите му Иосафат, Иорам и Охозия, Юдовите царе, бяха посветили, и посветените от него неща, и всичкото злато, което се намери в съкровищата на Господния дом и на църската къща, та го прати на сирийския цар Азаил; и той се оттегли от Ерусалим.
19 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
А останалите дела на Иоаса, и всичко що извърши, не са ли написани в Книгота на летописите на Юдовите царе?
20 Maafisa wake wakafanya shauri baya dhidi yake, nao wakamuulia Yoashi huko Beth-Milo, kwenye barabara iteremkayo kuelekea Sila.
И слугите му се подигнаха и, като направиха заговор, убиха Иоаса в къщата Мило, в надолнището към Сила.
21 Maafisa waliomuua walikuwa Yozabadi mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri. Akafa na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi. Naye Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Защото слугите му Иозахар Семеатовият син, и Иозавад, Сомировият син, го поразиха, та умря; и погребаха го с бещите му в Давидовия град; и вместо него се възцари син му Амасия.