< 2 Wafalme 12 >
1 Katika mwaka wa saba wa utawala wa Yehu, Yoashi alianza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka arobaini. Jina la mama yake aliitwa Sibia, kutoka Beer-Sheba.
Isala: ili hina bagade Yihiu da Isala: ili soge ode fesuale ouligilalu, Youa: se da muni Yuda hina bagade hamoi. E da Yelusaleme moilai bai bagade ganodini esala, ode 40agoanega Yuda fi ouligilalu. Ea ame da Biasiba moilai uda galu, ea dio amo Sibia.
2 Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa akimwelekeza.
Youa: se ea esalusu huluane amoga, Hina Gode hahawane ba: ma: ne hou hamonanusu. Bai gobele salasu dunu Yihoida da hou noga: idafa ema olelei.
3 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Be e da Gode Ea hou hame lalegagui dunu ilia ogogosu ‘gode’ma nodone sia: ne gadosu sogebi, amo hame wadela: lesi, amola amogawi Yuda fi dunu mogili da ohe amola gabusiga: manoma gobele sasalilalu.
4 Yoashi akawaambia makuhani, “Kusanyeni fedha zote ambazo zitaletwa kama sadaka takatifu kwenye Hekalu la Bwana, yaani fedha zilizokusanywa kama kodi, fedha zilizopokelewa kutokana na nadhiri za watu binafsi, na fedha zilizoletwa kwa hiari hekaluni.
Youa: se da gobele salasu dunu ili ema misa: ne sia: ne, ilia da muni amo da Debolo diasuga gobele salimusa: lai, amola hahawane udigili iasu muni, amo huluane momagele lelegema: ne sia: i.
5 Kila kuhani na apokee fedha kutoka kwa mmoja wa watunza hazina, nazo zitumike kukarabati uharibifu wowote unaoonekana katika Hekalu.”
Gobele salasu dunu afae afae ilia da muni ouligisu dunu ilia muni ilima i amoga lale, ilia da Debolo liligi wadela: lesi amo ba: sea, bu hahamoma: ne, Youa: se ea sia: i.
6 Lakini ikawa kufikia mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Mfalme Yoashi, makuhani walikuwa bado hawajalikarabati Hekalu.
Be Youa: se ea ouligibi ode23 agoane da doaga: loba, gobele salasu dunu ilia da bu hame hahamobeba: le, Debolo Diasu da hame hahamoi dialebe ba: i.
7 Kwa hiyo Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na makuhani wengine, akawauliza, “Kwa nini hamtengenezi uharibifu uliofanyika hekaluni? Msichukue fedha zaidi kutoka kwa watunza hazina wenu kwa ajili ya matumizi yenu, lakini kuanzia sasa ni lazima fedha yote itumike kwa ajili ya kukarabati Hekalu.”
Amaiba: le, Youa: se da Yihoida amola gobele salasu dunu huluane ema misa: ne sia: ne, amola ilima amane adole ba: i, “Dilia da abuliba: le Debolo Diasu bu hame hahamosala: ? Wali weganini, dilia muni lai amo mae modalegema! Dilia amo muni noga: le ouligima: ne, ouligisu dunuma ima.”
8 Makuhani wakakubali kuwa hawatakusanya tena fedha kutoka kwa watu na kwamba hawatakarabati Hekalu wenyewe.
Gobele salasu dunu ilia da amane hamoma: ne sia: i, amola ilila: da Debolo Diasu bu hame hahamomu sia: i.
9 Yehoyada kuhani akachukua kisanduku na akatoboa tundu kwenye kifuniko chake. Akakiweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia hekaluni mwa Bwana. Makuhani waliolinda ingilio wakaweka ndani ya kisanduku fedha zote ambazo zililetwa katika Hekalu la Bwana.
Amalalu, Yihoida da gagili lale, ga: lu da: iya gelabo doasili, gagili oloda bega: ligisi. Amo gagili da Debolo Diasu ea logo holei heda: su lobodafadini dialebe ba: i. Debolo Diasu logo holeiga gobele salasu hawa: hamosu dunu da, dunu amo da nodone sia: ne gadomusa: misi, ilia muni lale, gagili ganodini salasu.
10 Kila mara walipoona kuwa kuna kiasi kikubwa cha fedha ndani ya kisanduku, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja, wakazihesabu fedha hizo zilizoletwa katika Hekalu la Bwana, na kuziweka katika mifuko.
Ilia da amo gagili ganodini muni bagade ba: loba, hina bagade ea sia: dedesu dunu amola Gobele Salasu Hina dunu ela da misini, silifa fage lai amo idili, amola ea dioi defei ba: su.
11 Wakiisha kuthibitisha kiasi cha hizo fedha, waliwapa watu walioteuliwa kusimamia kazi katika Hekalu. Kwa fedha hizo, wakawalipa wale watu waliofanya kazi katika Hekalu la Bwana: yaani, maseremala na wajenzi,
12 waashi na wakata mawe. Walinunua mbao na mawe ya kuchongwa kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana, na kulipia gharama nyingine zote za kulitengeneza.
Ilia da amo muni ea idi defele dedene, ilia amo muni Debolo Diasu hawa: hamosu ouligisu dunu ilima iasu. Amo dunu ilia da diasu gagusu dunu, gele goudasu dunu amola gele dadamusu dunu, ilima iasu. Amola ilia da ifa gaga: i, amola gele gadelalesa: i, amo bu hahamoma: ne, amola eno hawa: hamoma: ne, amo dabe iasu.
13 Fedha zilizoletwa kwenye Hekalu hazikutumiwa kutengenezea masinia ya fedha, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, tarumbeta wala vyombo vingine vyovyote vya dhahabu au fedha kwa ajili ya Hekalu la Bwana;
Be amo muniga ilia da silifa faigelei, ofodo, dalabede, gamali gesosu liligi, amola eno silifa o gouli liligi huluane, amo hahamobe dunu iligili muni hame iasu.
14 zililipwa kwa wafanyakazi, ambao walizitumia kwa kukarabati Hekalu.
Muni huluanedafa da Debolo Diasu wadela: i buga: le hawa: hamosu dunu, iligili bidi imunusa: amola amo gagumu liligi fawane amo muniga lidisu.
15 Wao hawakudai kupewa hesabu ya fedha kutoka kwa wale waliowapa ili kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu walifanya kwa uaminifu wote.
Amo hawa: hamosu dunu ilia da moloidafa dunu. Amaiba: le, ilia da amo muni ea asi hou dedene legele hogomu hamedei ba: i.
16 Fedha zilizopatikana kutokana na sadaka za hatia na sadaka za dhambi hazikuletwa katika Hekalu la Bwana; zilikuwa mali ya makuhani.
Be muni amo Yuda dunu da wadela: i hou dabe gobele salasu iasu hamoma: ne i, amo da gagili ganodini hame salasu. Bai amo muni da gobele salasu dunu ilia: galu.
17 Wakati huu Hazaeli mfalme wa Aramu akapanda kuishambulia Gathi, akaiteka. Kisha akageuka ili kuishambulia Yerusalemu.
Amogalu, Silia hina bagade Ha: sa: iele da Ga: de moilai bai bagade doagala: le, hasali. Amalu, e da Yelusaleme doagala: musa: ilegei.
18 Lakini Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vyombo vyote vitakatifu vilivyowekwa wakfu na baba zake, yaani Yehoshafati, Yehoramu na Ahazia, wafalme wa Yuda, zawadi ambazo yeye mwenyewe alikuwa ameziweka wakfu pamoja na dhahabu yote iliyokutwa katika hazina za Hekalu la Bwana na katika jumba la kifalme, akazipeleka kwa Hazaeli mfalme wa Aramu, ambaye hatimaye aliondoka Yerusalemu.
Yuda hina bagade Youa: se da iasu liligi huluane amo e bisili hina bagade Yihosiafa: de amola Yihoula: me amola A: ihasaia ilia Hina Godema imunusa: ilegei, amola hisu iasu, amola gouli huluane Debolo Diasu amola hina bagade diasu ganodini dialu, amo huluane lale, hina bagade Ha: sa: iele ema iasi. Amalalu, Ha: sa: iele da ea dadi gagui wa: i, amo Yelusaleme fisili, masa: ne sia: i.
19 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Hina bagade Youa: se ea hamoi eno huluane da “Yuda hina bagade Ilia Hamonanu Meloa” amo ganodini dedene legei.
20 Maafisa wake wakafanya shauri baya dhidi yake, nao wakamuulia Yoashi huko Beth-Milo, kwenye barabara iteremkayo kuelekea Sila.
21 Maafisa waliomuua walikuwa Yozabadi mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri. Akafa na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi. Naye Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Hina bagade Youa: se ea eagene ouligisu dunu ilia da e medomusa: wamo sia: hahamoi. Ouligisu dunu aduna, amo Yosaga (Simia: de egefe) amola Yihosaba: de (Siouma egefe) ela da Sila sogega ahoasu logoa, diasu amo da osobo gasa: le lelegela heda: i Yelusaleme gusudili dialu, amo diasua Youa: se fane legei. Ilia da Youa: se amo hina bagade uli dogosu sogebi, Da: ibidi Moilai Bai Bagade ganodini, uli dogone sali. Youa: se egefe A: masaia da e bagia hina bagade hamoi.