< 2 Wafalme 11 >

1 Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme.
Or Athalie, mère d’Achazia, vit que son fils était mort, et elle se leva et fit périr toute la semence royale.
2 Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, aliyekuwa pia dada yake Ahazia, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala na kumficha humo ili Athalia asimwone; kwa hiyo hakuuawa.
Mais Jehoshéba, fille du roi Joram, sœur d’Achazia, prit Joas, fils d’Achazia, et le déroba du milieu des fils du roi qu’on mettait à mort [et le cacha], lui et sa nourrice, dans la chambre à coucher; et on le cacha de devant Athalie, et il ne fut pas mis à mort.
3 Alibaki amefichwa pamoja na yaya wake katika Hekalu la Bwana kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.
Et il fut caché six ans auprès d’elle dans la maison de l’Éternel. Et Athalie régna sur le pays.
4 Katika mwaka wa saba, Yehoyada akatumania wakuu wa vikundi vya mamia, na Wakari, na walinzi, nao wakaletwa kwake katika Hekalu la Bwana. Alifanya agano nao na kuwaapisha katika Hekalu la Bwana. Ndipo akawaonyesha mwana wa mfalme.
Et la septième année, Jehoïada envoya, et prit les chefs de centaines des gardes et des coureurs; et il les fit entrer vers lui dans la maison de l’Éternel, et fit un pacte avec eux et les fit jurer dans la maison de l’Éternel, et leur montra le fils du roi.
5 Akawaamuru akisema, “Hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Ninyi ambao mko makundi matatu mnaoingia zamu siku ya Sabato, theluthi yenu inayolinda jumba la kifalme,
Et il leur commanda, disant: C’est ici ce que vous ferez: un tiers d’entre vous qui entrez le [jour du] sabbat, fera la garde de la maison du roi;
6 theluthi nyingine Lango la Suri, na theluthi nyingine lango lililo nyuma ya walinzi, ambao hupeana zamu kulinda Hekalu,
et un tiers sera à la porte de Sur; et un tiers sera à la porte qui est derrière les coureurs; et vous veillerez à la garde de la maison, pour tenir à distance [tout étranger].
7 nanyi ambao mko katika makundi mengine mawili ambao kwa kawaida hupumzika Sabato, wote mtalinda Hekalu kwa ajili ya mfalme.
Et les deux tiers d’entre vous, tous ceux qui sortent le [jour du] sabbat, feront la garde de la maison de l’Éternel, auprès du roi.
8 Jipangeni kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha yake mkononi. Yeyote anayesogelea safu zenu lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”
Et vous entourerez le roi de tous côtés, chacun ses armes à la main; et celui qui entrera dans les rangs sera mis à mort; et soyez avec le roi quand il sortira et quand il entrera.
9 Wakuu wa vikosi vya mamia wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, nao wakaja kwa kuhani Yehoyada.
Et les chefs de centaines firent selon tout ce que Jehoïada, le sacrificateur, avait commandé; et ils prirent chacun ses hommes, ceux qui entraient le [jour du] sabbat et ceux qui sortaient le [jour du] sabbat; et ils vinrent auprès de Jehoïada, le sacrificateur.
10 Ndipo akawapa wale wakuu mikuki na ngao zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana.
Et le sacrificateur donna aux chefs de centaines les lances et les boucliers qui avaient appartenu au roi David, et qui étaient dans la maison de l’Éternel.
11 Wale walinzi, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, wakajipanga kumzunguka mfalme, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.
Et les coureurs se tinrent là, chacun ses armes à la main, depuis le côté droit de la maison jusqu’au côté gauche de la maison, vers l’autel et vers la maison, auprès du roi, tout autour.
12 Yehoyada akamtoa mwana wa mfalme na kumvika taji, akampa nakala ya agano, na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta, nao watu wakapiga makofi na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”
Et on fit sortir le fils du roi, et on mit sur lui la couronne et le témoignage; et ils le firent roi, et l’oignirent, et frappèrent des mains, et dirent: Vive le roi!
13 Athalia aliposikia kelele iliyofanywa na walinzi pamoja na watu, akawaendea watu pale penye Hekalu la Bwana.
Et Athalie entendit le cri des coureurs [et] du peuple, et elle entra vers le peuple dans la maison de l’Éternel.
14 Akaangalia, na tazama alikuwako mfalme, akiwa amesimama karibu na nguzo, kama ilivyokuwa desturi. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa pembeni mwa mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wakifurahi na kupiga tarumbeta. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kulia, “Uhaini! Uhaini!”
Et elle regarda, et voici, le roi se tenait sur l’estrade, suivant l’usage, et les chefs et les trompettes étaient auprès du roi, et tout le peuple du pays se réjouissait et sonnait des trompettes. Et Athalie déchira ses vêtements, et s’écria: Conspiration! Conspiration!
15 Kuhani Yehoyada akawaagiza majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Hatauawa ndani ya Hekalu la Bwana.”
Et Jehoïada, le sacrificateur, commanda aux chefs de centaines qui étaient préposés sur l’armée, et leur dit: Faites-la sortir en dehors des rangs, et celui qui la suivra mettez-le à mort par l’épée; car le sacrificateur dit: Qu’elle ne soit pas mise à mort dans la maison de l’Éternel.
16 Basi wakamkamata Athalia, na alipofika mahali ambapo farasi huingilia katika viwanja vya jumba la mfalme, wakamuulia hapo.
Et ils lui firent place; et elle alla par le chemin de l’entrée des chevaux dans la maison du roi, et là elle fut mise à mort.
17 Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Bwana na mfalme na watu kwamba watakuwa watu wa Bwana. Akafanya pia agano kati ya mfalme na watu.
Et Jehoïada fit une alliance entre l’Éternel et le roi et le peuple, qu’ils seraient le peuple de l’Éternel, – et entre le roi et le peuple.
18 Watu wote wa nchi wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu na sanamu, na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu. Kisha Yehoyada kuhani akawaweka walinzi kwenye Hekalu la Bwana.
Et tout le peuple du pays entra dans la maison de Baal, et ils la démolirent; ses autels et ses images, ils les brisèrent entièrement; et ils tuèrent devant les autels Matthan, sacrificateur de Baal. Et le sacrificateur établit des gardes sur la maison de l’Éternel.
19 Pamoja naye akawachukua majemadari wa mamia, Wakari, walinzi na watu wote wa nchi, nao kwa pamoja wakamteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana na kwenda kwenye jumba la mfalme, wakiingilia njia ya lango la walinzi. Ndipo mfalme akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi,
Et il prit les chefs de centaines, et les gardes, et les coureurs, et tout le peuple du pays, et ils firent descendre le roi de la maison de l’Éternel, et entrèrent dans la maison du roi par le chemin de la porte des coureurs; et il s’assit sur le trône des rois.
20 nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia, kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga nyumbani kwa mfalme.
Et tout le peuple du pays se réjouit, et la ville fut tranquille: et ils avaient mis à mort Athalie par l’épée, dans la maison du roi.
21 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala.
Joas était âgé de sept ans lorsqu’il commença de régner.

< 2 Wafalme 11 >