< 2 Wafalme 11 >

1 Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme.
Forsothe Athalie, modir of Ocozie, siy hir sone deed, and sche roos, and killide al the seed of the kyng.
2 Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, aliyekuwa pia dada yake Ahazia, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala na kumficha humo ili Athalia asimwone; kwa hiyo hakuuawa.
Sotheli Josaba, douyter of kyng Joram, the sistir of Ocozie, took Joas, sone of Ocozie, and stal him fro the myddis of the sones of the kyng, that weren slayn; and sche took the nursche of hym fro the hows of thre stagis; and sche hidde hym fro the face of Athalie, that he were not slayn.
3 Alibaki amefichwa pamoja na yaya wake katika Hekalu la Bwana kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.
And he was with hir in the hows of the Lord priueli sixe yeer. Forsothe Athalia regnede on the lond sixe yeer.
4 Katika mwaka wa saba, Yehoyada akatumania wakuu wa vikundi vya mamia, na Wakari, na walinzi, nao wakaletwa kwake katika Hekalu la Bwana. Alifanya agano nao na kuwaapisha katika Hekalu la Bwana. Ndipo akawaonyesha mwana wa mfalme.
Forsothe in the seuenthe yeer Joiada sente, and took centuriouns, and knyytis, and brouyte to hym in to the temple of the Lord; and couenauntide with hem boond of pees, and he made hem to swere in the temple of the Lord, and schewide to hem the sone of the kyng.
5 Akawaamuru akisema, “Hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Ninyi ambao mko makundi matatu mnaoingia zamu siku ya Sabato, theluthi yenu inayolinda jumba la kifalme,
And he comaundide to hem, and seide, This is the word, which ye owen to do;
6 theluthi nyingine Lango la Suri, na theluthi nyingine lango lililo nyuma ya walinzi, ambao hupeana zamu kulinda Hekalu,
the thridde part of you entre in the sabat, and kepe the wakyngis of the `hows of the kyng; sothely the thridde part be at the yate of Seir; and the thridde part be at the yate which is bihynde the dwellyng place of the makeris of scheeldis; and ye schulen kepe the wakyngis of the hows of Messa.
7 nanyi ambao mko katika makundi mengine mawili ambao kwa kawaida hupumzika Sabato, wote mtalinda Hekalu kwa ajili ya mfalme.
Forsothe twei partis of you alle goynge out in the sabat, kepe ye the wakyngis of the hows of the Lord aboute the kyng.
8 Jipangeni kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha yake mkononi. Yeyote anayesogelea safu zenu lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”
And ye schulen cumpasse hym, and ye schulen haue armeris in youre hondis; forsothe if ony man entrith in to the closyng of the temple, be he slayn; and ye schulen be with the kyng goynge in and goynge out.
9 Wakuu wa vikosi vya mamia wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, nao wakaja kwa kuhani Yehoyada.
And the centuriouns diden bi alle thingis whiche Joiada, the preest, hadde comaundid to hem; and alle takynge her men that entriden to the sabat, with hem that yeden out fro the sabat, camen to Joiada, the preest.
10 Ndipo akawapa wale wakuu mikuki na ngao zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana.
Which yaf to hem speris, and armeris of kyng Dauid, that weren in the hows of the Lord.
11 Wale walinzi, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, wakajipanga kumzunguka mfalme, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.
And alle stoden hauynge armeris in her hond, fro the riyt side of the temple `til to the left side of the auter and of the hows, aboute the kyng.
12 Yehoyada akamtoa mwana wa mfalme na kumvika taji, akampa nakala ya agano, na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta, nao watu wakapiga makofi na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”
And he brouyte forth the sone of the kyng, and puttide on hym a diademe, and witnessyng; and thei maden hym kyng, and anoyntiden hym; and thei beeten with the hoond, and seiden, The kyng lyue!
13 Athalia aliposikia kelele iliyofanywa na walinzi pamoja na watu, akawaendea watu pale penye Hekalu la Bwana.
Forsothe Athalia herde the vois of the puple rennynge, and sche entride to the cumpenyes in to the temple of the Lord,
14 Akaangalia, na tazama alikuwako mfalme, akiwa amesimama karibu na nguzo, kama ilivyokuwa desturi. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa pembeni mwa mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wakifurahi na kupiga tarumbeta. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kulia, “Uhaini! Uhaini!”
and sche siy the kyng stondynge on the trone bi custom, and syngeris, and cumpenyes nyy hym, and al the puple of the lond beynge glad, and syngynge with trumpis. And sche to-rente hir clothis, and criede, `Swerynge togidere! swerynge togidere! ether tresoun.
15 Kuhani Yehoyada akawaagiza majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Hatauawa ndani ya Hekalu la Bwana.”
Forsothe Joiada comaundide to the centuriouns, that weren on the oost, and seide to hem, Lede ye hir out of the closyngis of the temple; and who euer sueth hir, be smytun with swerd. Forsothe the preest seide, Be sche not slayn in the temple of the Lord.
16 Basi wakamkamata Athalia, na alipofika mahali ambapo farasi huingilia katika viwanja vya jumba la mfalme, wakamuulia hapo.
And thei puttiden hondis on hir, and hurliden hir bi the weie of the entryng of horsis bisidis the paleis; and sche was slayn there.
17 Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Bwana na mfalme na watu kwamba watakuwa watu wa Bwana. Akafanya pia agano kati ya mfalme na watu.
Therfor Joiada made boond of pees bitwixe the Lord and the kyng, and bitwixe the puple, that it schulde be the puple of the Lord; and bitwixe the kyng and the puple.
18 Watu wote wa nchi wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu na sanamu, na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu. Kisha Yehoyada kuhani akawaweka walinzi kwenye Hekalu la Bwana.
Al the puple of the lond entride in to the temple of Baal; and thei distrieden the auteris of hym, and al tobraken strongli the ymagis; and thei killiden bifore the auter Mathan, the preest of Baal. And the preest settide kepyngis in the hows of the Lord; and he took centuriouns, and the legiouns of Cerethi and Pherethi, and al the puple of the lond.
19 Pamoja naye akawachukua majemadari wa mamia, Wakari, walinzi na watu wote wa nchi, nao kwa pamoja wakamteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana na kwenda kwenye jumba la mfalme, wakiingilia njia ya lango la walinzi. Ndipo mfalme akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi,
And thei ledden forth the kyng fro the hows of the Lord; and thei camen bi the weie of the yate of makeris of scheldis in to the paleis; and he sat on the trone of kyngis.
20 nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia, kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga nyumbani kwa mfalme.
And al the puple of the lond was glad, and the citee restide. Forsothe Athalia was slayn bi swerd in the hows of the kyng.
21 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala.
And Joas was of seuen yeer, whanne he bigan to regne.

< 2 Wafalme 11 >