< 2 Wafalme 11 >

1 Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme.
Now, when, Athaliah, mother of Ahaziah, saw that her son was dead, she arose and destroyed all the seed royal.
2 Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, aliyekuwa pia dada yake Ahazia, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala na kumficha humo ili Athalia asimwone; kwa hiyo hakuuawa.
But Jehosheba daughter of King Joram, sister of Ahaziah, took Joash son of Ahaziah, and stole him from among the king’s sons that were being slain—him and his nurse, into the bedchamber, —so she hid him from the face of Athaliah, that he was not slain.
3 Alibaki amefichwa pamoja na yaya wake katika Hekalu la Bwana kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.
And he was with her, in the house of Yahweh, hiding himself, six years, —while, Athaliah, was reigning over the land.
4 Katika mwaka wa saba, Yehoyada akatumania wakuu wa vikundi vya mamia, na Wakari, na walinzi, nao wakaletwa kwake katika Hekalu la Bwana. Alifanya agano nao na kuwaapisha katika Hekalu la Bwana. Ndipo akawaonyesha mwana wa mfalme.
But, in the seventh year, Jehoiada sent and took the captains over hundreds, of the Carian body-guard, and of the runners, and brought them unto him, in the house of Yahweh, —and, when he had solemnised a Covenant with them, and put them on oath, in the house of Yahweh, then shewed he them the king’s son;
5 Akawaamuru akisema, “Hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Ninyi ambao mko makundi matatu mnaoingia zamu siku ya Sabato, theluthi yenu inayolinda jumba la kifalme,
and commanded them, saying—This, is the thing which ye must do, —A third part of you, will be coming in on the sabbath, and keeping the watch of the house of the king;
6 theluthi nyingine Lango la Suri, na theluthi nyingine lango lililo nyuma ya walinzi, ambao hupeana zamu kulinda Hekalu,
and, a third, in the side-gate; and, a third, in the gate behind the runners, —so shall ye keep the watch of the house, by turns.
7 nanyi ambao mko katika makundi mengine mawili ambao kwa kawaida hupumzika Sabato, wote mtalinda Hekalu kwa ajili ya mfalme.
And, two parts of you, are all that are going out on the sabbath, —so shall ye keep the watch of the house of Yahweh, as touching the king.
8 Jipangeni kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha yake mkononi. Yeyote anayesogelea safu zenu lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”
Thus shall ye encompass the king round about, every man with his weapons in his hand, and, he that cometh within the ranks, let him be slain, —so be ye with the king, when he cometh out and when he goeth in.
9 Wakuu wa vikosi vya mamia wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, nao wakaja kwa kuhani Yehoyada.
And the captains of hundreds did according to all that Jehoiada the priest commanded, and they took every man his men who were coming in on the sabbath, with them who were going out on the sabbath, —and came unto Jehoiada the priest.
10 Ndipo akawapa wale wakuu mikuki na ngao zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana.
And the priest gave unto the captains of hundreds the spears and the shields which belonged to King David, —which were in the house of Yahweh.
11 Wale walinzi, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, wakajipanga kumzunguka mfalme, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.
And the runners stood, every man with his weapons in his hand, from the right corner of the house, as far as the left corner of the house, by the altar and the house, —near the king, round about.
12 Yehoyada akamtoa mwana wa mfalme na kumvika taji, akampa nakala ya agano, na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta, nao watu wakapiga makofi na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”
Then brought he forth the king’s son, and set upon him the crown, and the testimony, and they made him king, and anointed him, —and clapped their hands, and said—May the king live!
13 Athalia aliposikia kelele iliyofanywa na walinzi pamoja na watu, akawaendea watu pale penye Hekalu la Bwana.
And, when Athaliah heard the noise of the runners, the people, then came she in unto the people, in the house of Yahweh,
14 Akaangalia, na tazama alikuwako mfalme, akiwa amesimama karibu na nguzo, kama ilivyokuwa desturi. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa pembeni mwa mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wakifurahi na kupiga tarumbeta. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kulia, “Uhaini! Uhaini!”
and looked, and lo! the king, standing by the pillar, as the custom was, and the captains and the trumpeters, by the king, and, all the people of the land, rejoicing, and blowing with trumpets, —so Athaliah rent her garments, and cried out—Conspiracy! conspiracy!
15 Kuhani Yehoyada akawaagiza majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Hatauawa ndani ya Hekalu la Bwana.”
And Jehoiada the priest commanded the captains of hundreds—officers of the force, and said unto them—Take her forth into the inside of the ranks, and, he that cometh in after her, [ye are] to slay with the sword. For the priest said, Let her not be slain, in the house of Yahweh.
16 Basi wakamkamata Athalia, na alipofika mahali ambapo farasi huingilia katika viwanja vya jumba la mfalme, wakamuulia hapo.
So they made way for her, and she entered the road by which the horses approached the house of the king, and was slain there.
17 Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Bwana na mfalme na watu kwamba watakuwa watu wa Bwana. Akafanya pia agano kati ya mfalme na watu.
And Jehoiada solemnised a covenant between Yahweh, and the king, and the people, that they should become a people unto Yahweh, —also between the king and the people.
18 Watu wote wa nchi wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu na sanamu, na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu. Kisha Yehoyada kuhani akawaweka walinzi kwenye Hekalu la Bwana.
And all the people of the land entered the house of Baal, and brake it down, his altars and his images, brake they in pieces, utterly, and, Mattan the priest of Baal, they slew before the altars, —and the priest appointed officers over the house of Yahweh.
19 Pamoja naye akawachukua majemadari wa mamia, Wakari, walinzi na watu wote wa nchi, nao kwa pamoja wakamteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana na kwenda kwenye jumba la mfalme, wakiingilia njia ya lango la walinzi. Ndipo mfalme akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi,
And he took the captains of hundreds and the Carian bodyguard, and the runners, and all the people of the land, and they brought down the king out of the house of Yahweh, and they came, by way of the gate of the runners, into the house of the king, —and he took his seat on the throne of the kings;
20 nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia, kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga nyumbani kwa mfalme.
and all the people of the land rejoiced, and, the city, had rest, —when they had put, Athaliah, to death with the sword, in the house of the king.
21 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala.
Seven years old, was Jehoash, when he began to reign.

< 2 Wafalme 11 >