< 2 Wafalme 10 >

1 Wakati huu katika Samaria walikuwepo wana sabini wa nyumba ya Ahabu. Kwa hiyo Yehu akaandika barua na kuzituma Samaria: kwa maafisa wa Yezreeli, kwa wazee, na kwa walezi wa watoto wa Ahabu. Akasema,
A Ahav imaše sedamdeset sinova u Samariji; i Juj napisa knjigu i posla je u Samariju ka glavarima Jezraelskim, starješinama i hraniteljima Ahavovijem, i reèe:
2 “Mara tu barua hii itakapokufikia, kwa kuwa wana wa bwana wako wapo pamoja nawe, nawe una magari ya vita na farasi, mji wenye ngome na silaha,
Kako ova knjiga doðe k vama, u kojih su sinovi gospodara vašega i kola i konji i grad tvrdi i oružje,
3 mchague mwenye uwezo zaidi kati ya wana wa bwana wako, na umweke juu ya kiti cha enzi cha baba yake. Kisha upigane kwa ajili ya nyumba ya bwana wako.”
Gledajte koji je najbolji i najvještiji izmeðu sinova gospodara vašega, te ga posadite na prijesto oca njegova, i bijte se za dom gospodara svoga.
4 Lakini wakaogopa sana na kusema, “Ikiwa wafalme wawili hawakuweza kupambana na Yehu, sisi tutawezaje?”
Ali se oni vrlo uplašiše i rekoše: eto, dva cara ne odolješe mu, a kako æemo mu mi odoljeti?
5 Basi msimamizi wa jumba la mfalme, mtawala wa mji, na wazee na walezi wakatuma ujumbe huu kwa Yehu: “Sisi tu watumishi wako, na tutafanya kila kitu utakachosema. Hatutamteuwa mtu yeyote kuwa mfalme. Wewe fanya uonalo kuwa ni bora.”
I koji bijaše nad domom, i koji bijaše nad gradom, i starješine i hranitelji poslaše k Juju govoreæi: mi smo sluge tvoje, èiniæemo sve što nam kažeš; neæemo nikoga postavljati carem; èini što ti je volja.
6 Kisha Yehu akawaandikia barua ya pili, akisema, “Ikiwa ninyi mko upande wangu na mtanitii mimi, twaeni vichwa vya wana wa bwana wenu, na mnijie huku Yezreeli kesho wakati kama huu.” Wakati huo wana sabini wa mfalme walikuwa wakiishi pamoja na viongozi wa mji wa Samaria, waliokuwa wakiwalea.
I on im napisa drugu knjigu govoreæi: ako ste moji i slušate mene, uzmite glave svijeh sinova gospodara svojega i doðite k meni sjutra u ovo doba u Jezrael. A sinovi carevi, sedamdeset ljudi, bijahu kod najznatnijih graðana, koji ih hranjahu.
7 Hiyo barua ilipowafikia, watu hawa wakawachukua wale wana sabini wa mfalme na kuwachinja wote. Wakaweka vichwa vyao ndani ya makapu na kumpelekea Yehu huko Yezreeli.
I kad im doðe ova knjiga, uzeše sinove careve i poklaše, sedamdeset ljudi, i metnuvši glave njihove u kotarice poslaše mu u Jezrael.
8 Mjumbe alipofika, akamwambia Yehu, “Wameleta vichwa vya wana wa mfalme.” Ndipo Yehu akaagiza, “Viwekeni malundo mawili katika ingilio la lango la mji mpaka asubuhi.”
I doðe glasnik, koji mu javi govoreæi: donesoše glave sinova carevijeh. A on reèe: složite ih u dvije gomile na vratima, neka stoje do sjutra.
9 Asubuhi yake, Yehu akatoka nje. Akasimama mbele ya watu wote na akasema, “Hamna hatia. Ni mimi niliyefanya shauri baya dhidi ya bwana wangu na kumuua, lakini ni nani aliyewaua wote hawa?
A ujutru izašav stade i reèe svemu narodu: vi nijeste krivi; eto, ja se podigoh na gospodara svojega i ubih ga; ali ko pobi sve ove?
10 Fahamuni basi kwamba, hakuna neno ambalo Bwana amesema dhidi ya nyumba ya Ahabu ambalo halitatimia. Bwana amefanya lile aliloahidi kupitia mtumishi wake Eliya.”
Vidite sada da nije izostala nijedna rijeè Gospodnja koju reèe Gospod za dom Ahavov, nego je Gospod uèinio što je govorio preko sluge svojega Ilije.
11 Hivyo Yehu akaua kila mtu huko Yezreeli aliyekuwa amebaki wa nyumba ya Ahabu, ikiwa ni pamoja na wakuu wake, rafiki zake wa karibu, na makuhani wake. Hakuacha yeyote anusurike.
Potom pobi Juj sve koji bijahu ostali od doma Ahavova u Jezraelu i sve vlastelje njegove i prijatelje njegove i sveštenike njegove, da ne osta nijedan.
12 Kisha Yehu akaondoka kuelekea Samaria. Alipokuwa njiani karibu na nyumba ya kukatia manyoya ya kondoo, yaani, Beth-Ekedi ya wachunga kondoo,
Potom se podiže i poðe da ide u Samariju; i kad bijaše kod kolibe pastirske na putu,
13 Yehu akakutana na watu wa jamaa ya Ahazia mfalme wa Yuda, akauliza, “Ninyi ni nani?” Wao wakasema, “Sisi ni jamaa ya Ahazia, nasi tumeshuka kuwasalimu jamaa ya mfalme na ya mama malkia.”
Naðe Juj braæu Ohozije cara Judina, i reèe: ko ste? Oni rekoše: mi smo braæa Ohozijina i idemo da pozdravimo sinove careve i sinove carièine.
14 Yehu akaagiza, “Wakamateni wakiwa hai!” Kwa hiyo wakawachukua wakiwa hai, watu arobaini na wawili, na kuwachinja kando ya kisima cha Beth-Ekedi. Hakuacha yeyote anusurike.
Tada reèe: pohvatajte ih žive. I pohvataše ih žive i poklaše ih na studencu kod kolibe pastirske, njih èetrdeset, i ne ostavi nijednoga od njih.
15 Baada ya kuondoka hapo, alimkuta Yehonadabu mwana wa Rekabu, aliyekuwa akienda kumlaki. Yehu akamsalimu na kusema, “Je, moyo wako ni mnyofu kwangu kama moyo wangu ulivyo kwako?” Yehonadabu akajibu, “Ndiyo.” Yehu akasema, “Kama ndivyo, nipe mkono wako.” Yeye akampa mkono, naye Yehu akampandisha kwenye gari lake la vita.
Potom otišav odande naðe Jonadava sina Rihavova, koji ga srete. A on ga pozdravi i reèe mu: je li srce tvoje pravo kao što je moje srce prema tvome? A Jonadav odgovori: jest. Ako jest, odgovori Juj, daj mi ruku. I dade mu ruku; a on ga uze k sebi u kola.
16 Yehu akasema, “Twende pamoja ukaone wivu wangu kwa ajili ya Bwana.” Hivyo wakasafiri pamoja kwenye gari lake.
I reèe: hajde sa mnom, i vidi moju revnost za Gospoda. I odvezoše ga na njegovijem kolima.
17 Yehu alipofika Samaria, akawaua wale wote waliokuwa wamesalia wa jamaa ya Ahabu, akawaangamiza, sawasawa na neno la Bwana alilosema kupitia Eliya.
I kad doðe u Samariju, pobi sve što bješe ostalo od doma Ahavova u Samariji dokle ga ne istrijebi po rijeèi koju Gospod reèe Iliji.
18 Kisha Yehu akawaleta watu wote pamoja na kuwaambia, “Ahabu alimtumikia Baali kidogo. Lakini Yehu atamtumikia zaidi.
Potom sabra Juj sav narod i reèe mu: Ahav je malo služio Valu, Juj æe mu služiti više.
19 Sasa waiteni manabii wote wa Baali, watumishi wake wote na makuhani wake wote. Hakikisheni kwamba hakuna hata mmoja atakayekosekana, kwa sababu ninakwenda kutoa kafara kubwa sana kwa Baali. Yeyote atakayeshindwa kuja hataendelea kuishi.” Lakini Yehu alifanya hivyo kwa hila ili apate kuwaangamiza watumishi wote wa Baali.
Zato dozovite mi sve proroke Valove, sve sluge njegove i sve sveštenike njegove, nijedan da ne izostane, jer veliku žrtvu hoæu da prinesem Valu; ko ne doðe, poginuæe. A Juj èinjaše tako iz prijevare hoteæi pobiti sluge Valove.
20 Yehu akasema, “Itisheni kusanyiko kwa heshima ya Baali.” Basi wakatangaza jambo hilo.
I reèe Juj: svetkujte svetkovinu Valu. I oglasiše je.
21 Kisha Yehu akapeleka ujumbe katika Israeli yote, nao watumishi wote wa Baali wakaja, hakuna hata mmoja ambaye hakufika. Wakasongana ndani ya hekalu la Baali hadi likajaa tangu mlango hadi mwisho wake.
I posla Juj po svemu Izrailju, te doðoše sve sluge Valove, i ne izosta nijedan da ne doðe; i uðoše u kuæu Valovu, i napuni se kuæa Valova od kraja do kraja.
22 Naye Yehu akamwambia yule aliyekuwa mtunza chumba cha mavazi, “Leta majoho kwa ajili ya watumishi wote wa Baali.” Basi akawaletea majoho.
Tada reèe onomu koji bijaše nad riznicom: iznesi haljine svijem slugama Valovijem. I iznese im haljine.
23 Kisha Yehu na Yehonadabu mwana wa Rekabu wakaingia ndani ya hekalu la Baali. Yehu akawaambia watumishi wa Baali, “Tazameni kila mahali mhakikishe kwamba hakuna hata mtumishi mmoja wa Bwana aliye hapa pamoja nanyi, ila ni watumishi wa Baali tu.”
Zatijem uðe Juj s Jonadavom sinom Rihavovijem u kuæu Valovu, i reèe slugama Valovijem: promotrite i vidite da nije tu s vama koji sluga Gospodnji, nego same sluge Valove.
24 Kwa hiyo wakaingia ndani ili kutoa kafara na sadaka ya kuteketezwa. Wakati huu, Yehu alikuwa amewaweka watu wake themanini akiwa amewapa onyo kwamba, “Ikiwa mmoja wenu atamwachia mtu yeyote ninayemweka mikononi mwake atoroke, itakuwa uhai wako kwa uhai wake.”
I tako uðoše da prinesu prinose i žrtve paljenice, a Juj namjesti napolju osamdeset ljudi, i reèe: ako uteèe koji od ovijeh ljudi koje vam dajem u ruke, duša æe vaša biti za dušu njegovu.
25 Mara baada ya Yehu kutoa sadaka ya kuteketezwa, akawaamuru walinzi na maafisa: “Ingieni ndani, waueni; asitoroke hata mmoja.” Basi wakawakatakata kwa upanga. Walinzi na maafisa wakazitupa zile maiti nje, kisha wakaingia mahali pa ndani pa kuabudia miungu katika hekalu la Baali.
A kad se svrši žrtva paljenica, zapovjedi Juj vojnicima i vojvodama: uðite, pobijte ih, da ne izaðe nijedan. I tako ih pobiše oštrijem maèem i pobacaše ih vojnici i vojvode; potom otidoše u svaki grad gdje bješe kuæa Valova.
26 Wakaileta ile nguzo ya kuabudiwa nje ya hekalu la Baali, na wakaichoma moto.
I izbaciše likove iz kuæe Valove, i spališe ih.
27 Wakabomoa ile nguzo ya kuabudiwa ya Baali pamoja na hekalu la Baali, nao watu wakapafanya kuwa choo hadi leo.
I izlomiše lik Valov i raskopaše kuæu Valovu, i od nje naèiniše prohode do današnjega dana.
28 Kwa hiyo Yehu akaangamiza kuabudiwa kwa Baali katika Israeli.
Tako Juj istrijebi Vala iz Izrailja.
29 Hata hivyo, Yehu hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, yaani kuabudu ndama za dhahabu huko Betheli ya Dani.
Ali ne otstupi Juj od grijehova Jerovoama sina Navatova, kojima navede na grijeh Izrailja, od zlatnijeh telaca, koji bijahu u Vetilju i u Danu.
30 Bwana akamwambia Yehu, “Kwa kuwa umefanya vyema kwa kutimiza yaliyo sawa machoni pangu, na umetenda kwa nyumba ya Ahabu yale yote niliyokuwa nimekusudia kutenda, wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
A Gospod reèe Juju: što si dobro svršio što je pravo preda mnom, i što si uèinio domu Ahavovu sve što mi je bilo u srcu, zato æe sinovi tvoji sjedjeti na prijestolu Izrailjevu do èetvrtoga koljena.
31 Lakini Yehu hakuwa mwangalifu kushika sheria za Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
Ali Juj ne pažaše da hodi po zakonu Gospoda Boga Izrailjeva svijem srcem svojim, ne otstupi od grijehova Jerovoamovijeh, kojima navede na grijeh Izrailja.
32 Katika siku hizo, Bwana akaanza kupunguza ukubwa wa Israeli. Hazaeli akawashinda Waisraeli sehemu zote za nchi yao
U to vrijeme poèe Gospod krnjiti Izrailja, jer ih pobi Azailo po svijem meðama Izrailjevim.
33 mashariki ya Yordani, katika nchi yote ya Gileadi (eneo la Gadi, Reubeni na Manase), kutoka Aroeri karibu na Bonde la Arnoni kupitia Gileadi hadi Bashani.
Od Jordana k istoku sunèanom, svu zemlju Galadsku, Gadovu i Ruvimovu i Manasijinu, od Aroira na potoku Arnonu, i Galad i Vasan.
34 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehu, yote aliyofanya na mafanikio yake yote, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
A ostala djela Jujeva i sve što je èinio, i sva junaštva njegova, nijesu li zapisana u dnevniku careva Izrailjevijeh?
35 Yehu akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa huko Samaria. Naye Yehoahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
I poèinu Juj kod otaca svojih, i pogreboše ga u Samariji; a na njegovo se mjesto zacari Joahaz sin njegov.
36 Muda Yehu aliotawala juu ya Israeli huko Samaria ilikuwa miaka ishirini na minane.
A carova Juj nad Izrailjem u Samariji dvadeset i osam godina.

< 2 Wafalme 10 >