< 2 Wafalme 10 >

1 Wakati huu katika Samaria walikuwepo wana sabini wa nyumba ya Ahabu. Kwa hiyo Yehu akaandika barua na kuzituma Samaria: kwa maafisa wa Yezreeli, kwa wazee, na kwa walezi wa watoto wa Ahabu. Akasema,
Il y avait alors en Samarie soixante-dix fils d'Achab: Jéhu écrivit une lettre qu'il envoya dans Samarie aux chefs, aux anciens de la ville et aux gardiens des enfants d'Achab; il leur disait:
2 “Mara tu barua hii itakapokufikia, kwa kuwa wana wa bwana wako wapo pamoja nawe, nawe una magari ya vita na farasi, mji wenye ngome na silaha,
Aussitôt que cette lettre vous sera parvenue, vous qui avez avec vous les fils de votre maître, et des chars, et des forteresses, et des armes,
3 mchague mwenye uwezo zaidi kati ya wana wa bwana wako, na umweke juu ya kiti cha enzi cha baba yake. Kisha upigane kwa ajili ya nyumba ya bwana wako.”
Vous considèrerez quel est le meilleur et le plus droit des fils de votre maître, vous le placerez sur le trône de son père, et vous combattrez pour la maison de votre maître.
4 Lakini wakaogopa sana na kusema, “Ikiwa wafalme wawili hawakuweza kupambana na Yehu, sisi tutawezaje?”
Or, ils eurent crainte, et ils dirent: Si deux rois n'ont pu tenir devant lui, comment lui résisterons-nous?
5 Basi msimamizi wa jumba la mfalme, mtawala wa mji, na wazee na walezi wakatuma ujumbe huu kwa Yehu: “Sisi tu watumishi wako, na tutafanya kila kitu utakachosema. Hatutamteuwa mtu yeyote kuwa mfalme. Wewe fanya uonalo kuwa ni bora.”
Et les chefs du palais, ceux de la ville, ainsi que les anciens et les gardiens des enfants, envoyèrent des messagers à Jéhu, disant: Nous aussi nous sommes tes serviteurs; tout ce que tu nous diras nous le ferons; nous ne proclamerons point de roi, nous ferons ce que bon te semblera.
6 Kisha Yehu akawaandikia barua ya pili, akisema, “Ikiwa ninyi mko upande wangu na mtanitii mimi, twaeni vichwa vya wana wa bwana wenu, na mnijie huku Yezreeli kesho wakati kama huu.” Wakati huo wana sabini wa mfalme walikuwa wakiishi pamoja na viongozi wa mji wa Samaria, waliokuwa wakiwalea.
Jéhu leur écrivit une seconde lettre, où il disait: Si vous êtes à moi, si vous êtes dociles à mes ordres, prenez les têtes des hommes fils de votre maître, et apportez-les-moi demain, à pareille heure, en Jezraël. Or, les fils du roi étaient au nombre de soixante-dix, et les premiers de la ville les élevaient.
7 Hiyo barua ilipowafikia, watu hawa wakawachukua wale wana sabini wa mfalme na kuwachinja wote. Wakaweka vichwa vyao ndani ya makapu na kumpelekea Yehu huko Yezreeli.
Dès que la lettre leur fut parvenue, ils prirent les fils du roi et ils les égorgèrent au nombre de soixante-dix. Puis, ils mirent les têtes dans des paniers, et ils les envoyèrent à Jéhu en Jezraël.
8 Mjumbe alipofika, akamwambia Yehu, “Wameleta vichwa vya wana wa mfalme.” Ndipo Yehu akaagiza, “Viwekeni malundo mawili katika ingilio la lango la mji mpaka asubuhi.”
Et le messager de Jéhu revint, et il fit son rapport, disant: Ils ont apporté les têtes des fils du roi. Et Jéhu dit: Faites-en deux monceaux, et laissez-les jusqu'à demain matin des deux côtés de la porte de la ville.
9 Asubuhi yake, Yehu akatoka nje. Akasimama mbele ya watu wote na akasema, “Hamna hatia. Ni mimi niliyefanya shauri baya dhidi ya bwana wangu na kumuua, lakini ni nani aliyewaua wote hawa?
L'aurore parut, et il sortit; il s'arrêta, et il dit à tout le peuple: Vous êtes justes: voilà que je me suis révolté contre mon maître, je l'ai tué; mais qui donc à frappé tous ceux-ci?
10 Fahamuni basi kwamba, hakuna neno ambalo Bwana amesema dhidi ya nyumba ya Ahabu ambalo halitatimia. Bwana amefanya lile aliloahidi kupitia mtumishi wake Eliya.”
Vous le voyez, nulle des paroles que le Seigneur a dites contre la maison d'Achab ne devait tomber à terre; le Seigneur a exécuté tout ce qu'il nous avait dit par Elie, son serviteur.
11 Hivyo Yehu akaua kila mtu huko Yezreeli aliyekuwa amebaki wa nyumba ya Ahabu, ikiwa ni pamoja na wakuu wake, rafiki zake wa karibu, na makuhani wake. Hakuacha yeyote anusurike.
Et Jéhu extermina tout ce qu'il y avait encore de la maison d'Achab en Jezraël, et tous ses hommes éminents, tous ses amis et ses prêtres; pas un seul ne fut épargné.
12 Kisha Yehu akaondoka kuelekea Samaria. Alipokuwa njiani karibu na nyumba ya kukatia manyoya ya kondoo, yaani, Beth-Ekedi ya wachunga kondoo,
Puis, il se mit en marche pour Samarie; il était dans la maison des bergers, sur la route,
13 Yehu akakutana na watu wa jamaa ya Ahazia mfalme wa Yuda, akauliza, “Ninyi ni nani?” Wao wakasema, “Sisi ni jamaa ya Ahazia, nasi tumeshuka kuwasalimu jamaa ya mfalme na ya mama malkia.”
Quand il rencontra les frères d'Ochozias, roi de Juda, et il leur dit: Qui êtes-vous? Ils répondirent: Nous sommes les frères d'Ochozias, et nous sommes partis pour saluer les fils du roi et les fils de la reine.
14 Yehu akaagiza, “Wakamateni wakiwa hai!” Kwa hiyo wakawachukua wakiwa hai, watu arobaini na wawili, na kuwachinja kando ya kisima cha Beth-Ekedi. Hakuacha yeyote anusurike.
Aussitôt, il dit: Prenez-les vifs. On les prit, et on les égorgea dans la maison des bergers: quarante-deux hommes! il n'en resta pas un seul.
15 Baada ya kuondoka hapo, alimkuta Yehonadabu mwana wa Rekabu, aliyekuwa akienda kumlaki. Yehu akamsalimu na kusema, “Je, moyo wako ni mnyofu kwangu kama moyo wangu ulivyo kwako?” Yehonadabu akajibu, “Ndiyo.” Yehu akasema, “Kama ndivyo, nipe mkono wako.” Yeye akampa mkono, naye Yehu akampandisha kwenye gari lake la vita.
Et, s'étant éloigné de ce lieu, il rencontra Jonadab, fils de Rhéchab; celui-ci le bénit, et Jéhu lui dit: Ton cœur est-il sincèrement avec le mien, comme mon cœur est avec le tien? Jonadab répondit: Il l'est. Jéhu reprit: S'il l'est, donne-moi la main. Jonadab lui donna la main, et Jéhu le fit monter à côté de lui sur son char.
16 Yehu akasema, “Twende pamoja ukaone wivu wangu kwa ajili ya Bwana.” Hivyo wakasafiri pamoja kwenye gari lake.
Et il lui dit: Viens avec moi, tu verras mon zèle pour le Seigneur. Puis, il le fit asseoir sur le siège.
17 Yehu alipofika Samaria, akawaua wale wote waliokuwa wamesalia wa jamaa ya Ahabu, akawaangamiza, sawasawa na neno la Bwana alilosema kupitia Eliya.
Et il entra dans Samarie, et il extermina tout ce qui restait d'Achab, jusqu'à ce qu'il l'eût effacé, selon la parole que le Seigneur avait dite par la bouche d'Elie.
18 Kisha Yehu akawaleta watu wote pamoja na kuwaambia, “Ahabu alimtumikia Baali kidogo. Lakini Yehu atamtumikia zaidi.
Ensuite, Jéhu rassembla tout le peuple, et il leur dit: Achab a servi faiblement Baal, Jéhu le servira magnifiquement.
19 Sasa waiteni manabii wote wa Baali, watumishi wake wote na makuhani wake wote. Hakikisheni kwamba hakuna hata mmoja atakayekosekana, kwa sababu ninakwenda kutoa kafara kubwa sana kwa Baali. Yeyote atakayeshindwa kuja hataendelea kuishi.” Lakini Yehu alifanya hivyo kwa hila ili apate kuwaangamiza watumishi wote wa Baali.
Maintenant donc, vous tous prophètes de Baal, convoquez ici tous ses serviteurs et tous ses prêtres, sans qu'il manque un seul homme, car je vais faire un grand sacrifice à Baal; quiconque se cachera sera mis à mort. Or, Jéhu usait d'artifice pour détruire tous les serviteurs de Baal.
20 Yehu akasema, “Itisheni kusanyiko kwa heshima ya Baali.” Basi wakatangaza jambo hilo.
Il ajouta: Sanctifiez le sacerdoce de Baal. Et on fit une proclamation.
21 Kisha Yehu akapeleka ujumbe katika Israeli yote, nao watumishi wote wa Baali wakaja, hakuna hata mmoja ambaye hakufika. Wakasongana ndani ya hekalu la Baali hadi likajaa tangu mlango hadi mwisho wake.
Et Jéhu envoya des messagers en tout Israël, disant: Que de tous ses serviteurs, de tous ses prêtres, de tous ses prophètes, aucun ne fasse défaut, car je prépare un grand sacrifice. Celui qui ne viendra point ne restera pas en vie. Et tous les serviteurs de Baal vinrent, ainsi que tous ses prêtres et tous ses prophètes; il n'y eut pas un homme qui ne vînt. Et ils entrèrent dans le temple de Baal, et le temple de Baal fut rempli d'un bout à l'autre.
22 Naye Yehu akamwambia yule aliyekuwa mtunza chumba cha mavazi, “Leta majoho kwa ajili ya watumishi wote wa Baali.” Basi akawaletea majoho.
Et Jéhu dit au gardien des vêtements du temple: Apporte des robes pour tous les serviteurs de Baal. Et le gardien leur en donna.
23 Kisha Yehu na Yehonadabu mwana wa Rekabu wakaingia ndani ya hekalu la Baali. Yehu akawaambia watumishi wa Baali, “Tazameni kila mahali mhakikishe kwamba hakuna hata mtumishi mmoja wa Bwana aliye hapa pamoja nanyi, ila ni watumishi wa Baali tu.”
Et Jéhu, avec Jonadab, fils de Rhéchab, entra dans le temple de Baal, et il dit aux serviteurs de Baal: Cherchez, voyez s'il y a parmi vous des serviteurs du Seigneur, ou seulement des serviteurs de Baal.
24 Kwa hiyo wakaingia ndani ili kutoa kafara na sadaka ya kuteketezwa. Wakati huu, Yehu alikuwa amewaweka watu wake themanini akiwa amewapa onyo kwamba, “Ikiwa mmoja wenu atamwachia mtu yeyote ninayemweka mikononi mwake atoroke, itakuwa uhai wako kwa uhai wake.”
Puis, il pénétra plus loin pour offrir l'encens et les holocaustes. Or, il avait aposté dehors quatre-vingts de ses hommes, leur disant: Celui qui laissera échapper l'un de ceux que je livre entre vos mains, paiera de sa vie celle qu'il aura sauvée.
25 Mara baada ya Yehu kutoa sadaka ya kuteketezwa, akawaamuru walinzi na maafisa: “Ingieni ndani, waueni; asitoroke hata mmoja.” Basi wakawakatakata kwa upanga. Walinzi na maafisa wakazitupa zile maiti nje, kisha wakaingia mahali pa ndani pa kuabudia miungu katika hekalu la Baali.
Après qu'il eut consumé l'holocauste, Jéhu dit à ses gardes et à ses officiers: Entrez, frappez-les, n'en laissez pas sortir un seul. Et ils les passèrent an fil de l'épée; ils les jetèrent sur le chemin; et, du temple de Baal, ils retournèrent à la ville.
26 Wakaileta ile nguzo ya kuabudiwa nje ya hekalu la Baali, na wakaichoma moto.
Et ils emportèrent la colonne de Baal, et ils la brûlèrent.
27 Wakabomoa ile nguzo ya kuabudiwa ya Baali pamoja na hekalu la Baali, nao watu wakapafanya kuwa choo hadi leo.
Ils abattirent les colonnes de Baal, et, du temple, ils firent des latrines, qui existent encore de nos jours.
28 Kwa hiyo Yehu akaangamiza kuabudiwa kwa Baali katika Israeli.
Jéhu effaça Baal de la terre d'Israël.
29 Hata hivyo, Yehu hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, yaani kuabudu ndama za dhahabu huko Betheli ya Dani.
Seulement, il ne se retira pas du péché de Jéroboam, fils de Nabat, du péché où il avait fait tomber Israël; il conserva les génisses d'or de Béthel et de Dan.
30 Bwana akamwambia Yehu, “Kwa kuwa umefanya vyema kwa kutimiza yaliyo sawa machoni pangu, na umetenda kwa nyumba ya Ahabu yale yote niliyokuwa nimekusudia kutenda, wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
Le Seigneur dit à Jéhu: En récompense de ce que tu as fait d'agréable à mes yeux, de ce que tu as traité selon mon cœur la maison d'Achab, tes fils régneront sur Israël jusqu'à la quatrième génération.
31 Lakini Yehu hakuwa mwangalifu kushika sheria za Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
Mais Jéhu ne fut pas attentif à marcher de tout son cœur selon la loi du Seigneur Dieu d'Israël; il ne se retira pas du péché de Jéroboam, du péché où il avait fait tomber tout le peuple.
32 Katika siku hizo, Bwana akaanza kupunguza ukubwa wa Israeli. Hazaeli akawashinda Waisraeli sehemu zote za nchi yao
Et, en ces jours-là, le Seigneur commença de châtier Israël; Azaël le vainquit sur toutes ses frontières,
33 mashariki ya Yordani, katika nchi yote ya Gileadi (eneo la Gadi, Reubeni na Manase), kutoka Aroeri karibu na Bonde la Arnoni kupitia Gileadi hadi Bashani.
Jusqu'à la rive orientale du Jourdain; il envahit toute la terre de Galaad, savoir: les tribus de Gad et de Ruben, et le territoire de Manassé, à partir d'Aroer, qui est sur les bords du torrent d'Anion, et Galaad et Basan.
34 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehu, yote aliyofanya na mafanikio yake yote, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Quant au reste de l'histoire de Jéhu, aux actions qu'il fit en sa puissance et à ses combats, ne sont-ils pas écrits au livre des Faits et gestes des rois d'Israël?
35 Yehu akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa huko Samaria. Naye Yehoahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Jéhu s'endormit avec ses pères; on l'ensevelit en Samarie, et son fils Joachaz régna à sa place.
36 Muda Yehu aliotawala juu ya Israeli huko Samaria ilikuwa miaka ishirini na minane.
Jéhu avait régné vingt ans sur Israël en Samarie.

< 2 Wafalme 10 >