< 2 Wafalme 10 >

1 Wakati huu katika Samaria walikuwepo wana sabini wa nyumba ya Ahabu. Kwa hiyo Yehu akaandika barua na kuzituma Samaria: kwa maafisa wa Yezreeli, kwa wazee, na kwa walezi wa watoto wa Ahabu. Akasema,
Forsothe seuenti sones in Samarie weren to Achab. Therfor Hieu wroot lettris, and sente in to Samarie to the beste men of the citee, and to the gretter men in birthe, and to alle the nurschis of Achab, and seide,
2 “Mara tu barua hii itakapokufikia, kwa kuwa wana wa bwana wako wapo pamoja nawe, nawe una magari ya vita na farasi, mji wenye ngome na silaha,
Anoon as ye han take these lettris, ye that han the sones of youre lord, and the charis, and horsis, and stronge citees, and armeris,
3 mchague mwenye uwezo zaidi kati ya wana wa bwana wako, na umweke juu ya kiti cha enzi cha baba yake. Kisha upigane kwa ajili ya nyumba ya bwana wako.”
chese the beste, and hym that plesith to you of the sones of youre lord, and sette ye him on the trone of his fadir, and fiyte ye for the hows of youre lord.
4 Lakini wakaogopa sana na kusema, “Ikiwa wafalme wawili hawakuweza kupambana na Yehu, sisi tutawezaje?”
And thei dredden greetli, and seiden, Lo! twei kyngis myyten not stonde bifor hym, and how schulen we mowe ayenstonde hym?
5 Basi msimamizi wa jumba la mfalme, mtawala wa mji, na wazee na walezi wakatuma ujumbe huu kwa Yehu: “Sisi tu watumishi wako, na tutafanya kila kitu utakachosema. Hatutamteuwa mtu yeyote kuwa mfalme. Wewe fanya uonalo kuwa ni bora.”
Therfor the souereyns of the hows, and the prefect of the citee, and the grettere men in birthe, and the nurchis senten to Hieu, and seiden, We ben thi seruauntis; what euer thingis thou comaundist, we schulen do, and we schulen not make a kyng to vs; do thou what euer thing plesith thee.
6 Kisha Yehu akawaandikia barua ya pili, akisema, “Ikiwa ninyi mko upande wangu na mtanitii mimi, twaeni vichwa vya wana wa bwana wenu, na mnijie huku Yezreeli kesho wakati kama huu.” Wakati huo wana sabini wa mfalme walikuwa wakiishi pamoja na viongozi wa mji wa Samaria, waliokuwa wakiwalea.
Forsothe he wroot ayen to hem lettris the secunde tyme, and seide, If ye ben myne, and obeien to me, take ye the heedis of the sones of youre lord, and come ye to me in this same our to morewe in to Jezrael. Sotheli the sones of the kyng, seuenti men, weren nurschid at the beste men of the citee.
7 Hiyo barua ilipowafikia, watu hawa wakawachukua wale wana sabini wa mfalme na kuwachinja wote. Wakaweka vichwa vyao ndani ya makapu na kumpelekea Yehu huko Yezreeli.
And whanne the lettris hadden come to hem, thei token the sones of the kyng, and killiden seuenti men, and puttiden the heedis of hem in coffyns; and senten to hym in to Jezrael.
8 Mjumbe alipofika, akamwambia Yehu, “Wameleta vichwa vya wana wa mfalme.” Ndipo Yehu akaagiza, “Viwekeni malundo mawili katika ingilio la lango la mji mpaka asubuhi.”
Forsothe a messanger cam to hym, and schewide to hym, and seide, Thei han brouyt the heedis of the sones of the king. Which answeride, Putte ye tho heedis to tweyne hepis, bisidis the entring of the yate, til the morewtid.
9 Asubuhi yake, Yehu akatoka nje. Akasimama mbele ya watu wote na akasema, “Hamna hatia. Ni mimi niliyefanya shauri baya dhidi ya bwana wangu na kumuua, lakini ni nani aliyewaua wote hawa?
And whanne it was cleer dai, he yede out, and stood, and seide to al the puple, Ye ben iust men; if Y conspiride ayens my lord, and killide hym, who killide alle these?
10 Fahamuni basi kwamba, hakuna neno ambalo Bwana amesema dhidi ya nyumba ya Ahabu ambalo halitatimia. Bwana amefanya lile aliloahidi kupitia mtumishi wake Eliya.”
Therfor se ye now, that noon of the wordis of the Lord felde doun in to the erthe, whiche the Lord spak on the hows of Achab; and the Lord hath do that, that he spak in the hond of his seruaunt, Elie.
11 Hivyo Yehu akaua kila mtu huko Yezreeli aliyekuwa amebaki wa nyumba ya Ahabu, ikiwa ni pamoja na wakuu wake, rafiki zake wa karibu, na makuhani wake. Hakuacha yeyote anusurike.
Therfor Hieu smoot alle that weren residue of the hows of Achab in Jezrael, and alle the beste men of hym, and knowun men, and preestis, til no relikis of hym leften.
12 Kisha Yehu akaondoka kuelekea Samaria. Alipokuwa njiani karibu na nyumba ya kukatia manyoya ya kondoo, yaani, Beth-Ekedi ya wachunga kondoo,
And he roos, and cam in to Samarie; and whanne he hadde come to the chaumbir of schepherdis in the weie,
13 Yehu akakutana na watu wa jamaa ya Ahazia mfalme wa Yuda, akauliza, “Ninyi ni nani?” Wao wakasema, “Sisi ni jamaa ya Ahazia, nasi tumeshuka kuwasalimu jamaa ya mfalme na ya mama malkia.”
he foond the britheren of Ocozie, kyng of Juda; and he seide to hem, Who ben ye? And thei answeriden, We ben the britheren of Ocozie, and we comen doun to grete the sones of the kyng and the sones of the queen.
14 Yehu akaagiza, “Wakamateni wakiwa hai!” Kwa hiyo wakawachukua wakiwa hai, watu arobaini na wawili, na kuwachinja kando ya kisima cha Beth-Ekedi. Hakuacha yeyote anusurike.
Which Hieu seide, Take ye hem quyke. And whanne thei hadden take hem quyke, thei strangliden hem in the cisterne, bisidis the chaumbre, two and fourti men; and he lefte not ony of hem.
15 Baada ya kuondoka hapo, alimkuta Yehonadabu mwana wa Rekabu, aliyekuwa akienda kumlaki. Yehu akamsalimu na kusema, “Je, moyo wako ni mnyofu kwangu kama moyo wangu ulivyo kwako?” Yehonadabu akajibu, “Ndiyo.” Yehu akasema, “Kama ndivyo, nipe mkono wako.” Yeye akampa mkono, naye Yehu akampandisha kwenye gari lake la vita.
And whanne he hadde go fro thennus, he foond Jonadab, the sone of Rechab, in to meetyng of hym; and he blesside hym. And Hieu seide to hym, Whether thin herte is riytful with myn herte, as myn herte is with thin herte? And Jonadab seide, It is. Hieu seide, If `it is, yyue thin hond. Which yaf his hond to hym; and he reiside hym to hym silf in to the chare.
16 Yehu akasema, “Twende pamoja ukaone wivu wangu kwa ajili ya Bwana.” Hivyo wakasafiri pamoja kwenye gari lake.
And he seide to hym, Come thou with me, and se my feruent loue for the Lord.
17 Yehu alipofika Samaria, akawaua wale wote waliokuwa wamesalia wa jamaa ya Ahabu, akawaangamiza, sawasawa na neno la Bwana alilosema kupitia Eliya.
And he ledde hym, put in hys chare, in to Samarie. And he killide alle men that weren residue of Achab in Samarie `til to oon, bi the word of the Lord, which he spak bi Elie.
18 Kisha Yehu akawaleta watu wote pamoja na kuwaambia, “Ahabu alimtumikia Baali kidogo. Lakini Yehu atamtumikia zaidi.
Therfor Hieu gaderide to gidere alle the puple, and seide to hem, Achab worschipide Baal a litil, but Y schal worschipe hym more.
19 Sasa waiteni manabii wote wa Baali, watumishi wake wote na makuhani wake wote. Hakikisheni kwamba hakuna hata mmoja atakayekosekana, kwa sababu ninakwenda kutoa kafara kubwa sana kwa Baali. Yeyote atakayeshindwa kuja hataendelea kuishi.” Lakini Yehu alifanya hivyo kwa hila ili apate kuwaangamiza watumishi wote wa Baali.
Now therfor clepe ye to me alle the prophetis of Baal, and alle hise seruauntis, and alle hise preestis; `noon be that come not, for grete sacrifice is of me to Baal; who euer schal faile, he schal not lyue. Forsothe Hieu dide this bi tresoun, that he schulde distrie alle the worschipers of Baal.
20 Yehu akasema, “Itisheni kusanyiko kwa heshima ya Baali.” Basi wakatangaza jambo hilo.
And he seide, Halewe ye a solempne day to Baal.
21 Kisha Yehu akapeleka ujumbe katika Israeli yote, nao watumishi wote wa Baali wakaja, hakuna hata mmoja ambaye hakufika. Wakasongana ndani ya hekalu la Baali hadi likajaa tangu mlango hadi mwisho wake.
And he clepide, and sente in to alle the termes of Israel; and alle the seruauntis of Baal camen, `noon was residue, and sotheli `not oon was that cam not. And thei entriden in to the temple of Baal; and the hows of Baal was fillid, fro oon ende `til to `the tothir.
22 Naye Yehu akamwambia yule aliyekuwa mtunza chumba cha mavazi, “Leta majoho kwa ajili ya watumishi wote wa Baali.” Basi akawaletea majoho.
And he seide to hem that weren souereyns ouer the clothis, Bringe ye forth clothis to alle the seruauntis of Baal; and thei brouyten forth clothis to hem.
23 Kisha Yehu na Yehonadabu mwana wa Rekabu wakaingia ndani ya hekalu la Baali. Yehu akawaambia watumishi wa Baali, “Tazameni kila mahali mhakikishe kwamba hakuna hata mtumishi mmoja wa Bwana aliye hapa pamoja nanyi, ila ni watumishi wa Baali tu.”
And Hieu entride, and Jonadab, the sone of Rechab, in to the temple of Baal. And Hieu seide to the worschiperis of Baal, Enquere ye, and se, lest perauenture ony of the seruauntis of the Lord be with you; but that the seruauntis be aloone of Baal.
24 Kwa hiyo wakaingia ndani ili kutoa kafara na sadaka ya kuteketezwa. Wakati huu, Yehu alikuwa amewaweka watu wake themanini akiwa amewapa onyo kwamba, “Ikiwa mmoja wenu atamwachia mtu yeyote ninayemweka mikononi mwake atoroke, itakuwa uhai wako kwa uhai wake.”
Therfor thei entriden, to make slayn sacrifices, and brent sacrifices. Sotheli Hieu hadde maad redi to hym with outforth foure scoore men, and hadde seid to hem, Who euer schal fle of alle these, whiche Y schal brynge in to youre hondis, the lijf of hym schal be for the lijf of hym that ascapith.
25 Mara baada ya Yehu kutoa sadaka ya kuteketezwa, akawaamuru walinzi na maafisa: “Ingieni ndani, waueni; asitoroke hata mmoja.” Basi wakawakatakata kwa upanga. Walinzi na maafisa wakazitupa zile maiti nje, kisha wakaingia mahali pa ndani pa kuabudia miungu katika hekalu la Baali.
Forsothe it was don, whanne the brent sacrifice was fillid, Hieu comaundide to hise knyytis and duykis, Entre ye, and sle hem, that noon ascape. And the knyytis and duykis smytiden `hem bi the scharpnesse of swerd, and castiden forth. And `thei yeden into the citee of the temple of Baal,
26 Wakaileta ile nguzo ya kuabudiwa nje ya hekalu la Baali, na wakaichoma moto.
and thei brouyten forth the ymage fro the temple of Baal,
27 Wakabomoa ile nguzo ya kuabudiwa ya Baali pamoja na hekalu la Baali, nao watu wakapafanya kuwa choo hadi leo.
and brenten it, and al to braken it. Also thei destrieden the hows of Baal, and maden priuyes for it `til in to this dai.
28 Kwa hiyo Yehu akaangamiza kuabudiwa kwa Baali katika Israeli.
Therfor Hieu dide awei Baal fro Israel;
29 Hata hivyo, Yehu hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, yaani kuabudu ndama za dhahabu huko Betheli ya Dani.
netheles he yede not awei fro the synnes of Jeroboam, sone of Nabath, that made Israel to do synne, nether he forsook the goldun caluys, that weren in Bethel and in Dan.
30 Bwana akamwambia Yehu, “Kwa kuwa umefanya vyema kwa kutimiza yaliyo sawa machoni pangu, na umetenda kwa nyumba ya Ahabu yale yote niliyokuwa nimekusudia kutenda, wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
Forsothe the Lord seide to Hieu, For thou didist bisili that that was riytful, and pleside in myn yyen, and hast do ayens the hows of Achab alle thingis that weren in myn herte, thi sones `til to the fourthe generacioun schulen sitte on the trone of Israel.
31 Lakini Yehu hakuwa mwangalifu kushika sheria za Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
Forsothe Hieu kepte not, that he yede in the lawe of the Lord God of Israel in al his herte; for he yede not awei fro the synnes of Jeroboam, that made Israel to do synne.
32 Katika siku hizo, Bwana akaanza kupunguza ukubwa wa Israeli. Hazaeli akawashinda Waisraeli sehemu zote za nchi yao
In tho daies the Lord bigan to be anoyed on Israel; and Asahel smoot hem in alle the coostis of Israel,
33 mashariki ya Yordani, katika nchi yote ya Gileadi (eneo la Gadi, Reubeni na Manase), kutoka Aroeri karibu na Bonde la Arnoni kupitia Gileadi hadi Bashani.
fro Jordan ayens the eest coost, al the lond of Galaad, and of Gad, and of Ruben, and of Manasses, fro Aroer which is on the stronde of Arnon, and Galaad, and Baasan.
34 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehu, yote aliyofanya na mafanikio yake yote, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Forsothe the residue of wordis of Hieu, and alle thingis whiche he dide, and his strengthe, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel?
35 Yehu akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa huko Samaria. Naye Yehoahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Hieu slepte with hise fadris; and thei birieden hym in Samarie; and Joachaz, his sone, regnyde for hym.
36 Muda Yehu aliotawala juu ya Israeli huko Samaria ilikuwa miaka ishirini na minane.
Forsothe the daies, in whiche Hieu regnede on Israel in Samarie, ben eiyte and twenti yeer.

< 2 Wafalme 10 >