< 2 Wafalme 1 >

1 Baada ya kifo cha Mfalme Ahabu, nchi ya Moabu iliasi dhidi ya Israeli.
Moab se révolta contre Israël, après la mort d'Achab.
2 Basi Ahazia alikuwa ameanguka huko Samaria kutoka baraza ya chumba chake cha juu, akaumia. Hivyo akatuma wajumbe, akiwaambia, “Nendeni mkaulize kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni, mkaone kama nitapona kutokana na kuumia huku.”
Ochozias tomba par la fenêtre en treillis de sa chambre haute à Samarie, et il fut malade. Il envoya des messagers et leur dit: « Allez consulter Béel-Zébub, dieu d'Accaron, pour savoir si je guérirai de cette maladie. »
3 Lakini malaika wa Bwana akamwambia Eliya, Mtishbi, “Panda ukakutane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, uwaulize, ‘Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana mnakwenda kumuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni?’
Mais l'ange de Yahweh dit à Elie, le Thesbite: « Lève-toi, monte à la rencontre des messagers du roi de Samarie, et dis-leur: “Est-ce parce qu'il n'y a point de Dieu en Israël que vous allez consulter Béel-Zébub, dieu d'Accaron?”
4 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana, ‘Hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!’” Hivyo Eliya akaenda.
C'est pourquoi ainsi dit Yahweh: “Du lit sur lequel tu es monté, tu ne descendras pas, tu mourras certainement.” » Et Elie s'en alla.
5 Wajumbe waliporudi kwa mfalme, akawauliza, “Kwa nini mmerudi?”
Les messagers retournèrent auprès d'Ochozias, et il leur dit: « Pourquoi revenez-vous? »
6 Wakamjibu, “Mtu fulani alikuja kukutana nasi, naye akatuambia, ‘Rudini kwa mfalme aliyewatuma na mkamwambie, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana unawatuma watu kwenda kuuliza kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa hiyo hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”’”
Ils lui répondirent: « Un homme est monté à notre rencontre et nous a dit: Allez, retournez vers le roi qui vous a envoyés, et dites-lui: Ainsi dit Yahweh: Est-ce parce qu'il n'y a point de Dieu en Israël que tu envoies consulter Béel-Zébub, dieu d'Accaron? C'est pourquoi du lit sur lequel tu es monté, tu ne descendras pas, mais tu mourras certainement. »
7 Mfalme akawauliza, “Alikuwa mtu wa namna gani ambaye mlikutana naye, akawaambia hili?”
Ochozias leur dit: « Quel était l'aspect de l'homme qui est monté à votre rencontre et qui vous a dit ces paroles? »
8 Wakamjibu, “Alikuwa mtu aliyekuwa na vazi la manyoya na mkanda wa ngozi kiunoni mwake.” Mfalme akasema, “Huyo alikuwa ni Eliya, Mtishbi.”
Ils lui répondirent: « C'était un homme velu, avec une ceinture de cuir autour des reins. » Et Ochozias dit: « C'est Elie, le Thesbite. »
9 Ndipo mfalme akamtuma mkuu mmoja wa kikosi pamoja na kikosi chake cha askari hamsini kwa nabii Eliya. Yule mkuu wa kikosi akamwendea Eliya, aliyekuwa ameketi juu ya kilima, na kumwambia, “Mtu wa Mungu, mfalme anasema, ‘Shuka chini!’”
Aussitôt il envoya vers lui un chef de cinquante avec ses cinquante hommes. Ce chef monta auprès d'Elie, et voici qu'il était assis sur le sommet de la montagne, et il lui dit: « Homme de Dieu, le roi a dit: Descends! »
10 Eliya akamjibu yule mkuu wa kikosi, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza yule mkuu wa kikosi pamoja na watu wake.
Elie répondit et dit au chef de cinquante: « Si je suis un homme de Dieu, que le feu descende du ciel et vous consume, toi et tes cinquante hommes? » Et le feu descendit du ciel et les consuma, lui et ses cinquante hommes.
11 Aliposikia hili, mfalme akatuma kwa Eliya mkuu wa kikosi mwingine na askari wake hamsini. Yule mkuu wa kikosi akamwambia Eliya, “Mtu wa Mungu, hili ndilo asemalo mfalme, ‘Shuka chini mara moja!’”
Ochozias envoya encore un autre chef de cinquante avec ses cinquante hommes. Ce chef, prenant la parole, dit à Elie: « Homme de Dieu, ainsi a dit le roi: Hâte-toi, descends! »
12 Eliya akajibu, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza yeye na watu wake hamsini.
Elie répondit et leur dit: « Si je suis un homme de Dieu, que le feu descende du ciel et vous consume, toi et tes cinquante hommes! » Et le feu de Dieu descendit du ciel, et les consuma, lui et ses cinquante hommes.
13 Hivyo mfalme akatuma mkuu wa kikosi wa tatu na watu wake hamsini. Huyu mkuu wa kikosi wa tatu akapanda na kupiga magoti mbele ya Eliya, akiomba, “Mtu wa Mungu, tafadhali niachie uhai wangu na uhai wa hawa watu hamsini, watumishi wako!
De nouveau Ochozias envoya un troisième chef de cinquante avec ses cinquante hommes. Le troisième chef de cinquante monta, et, étant arrivé, il fléchit les genoux devant Elie, et lui dit en suppliant: « Homme de Dieu, de grâce, que ma vie et que la vie de ces cinquante hommes, tes serviteurs, soit précieuse à tes yeux!
14 Tazama, moto umeshuka kutoka mbinguni na kuwateketeza wale wakuu wa vikosi viwili vya kwanza pamoja na watu wao. Lakini sasa niachie uhai wangu!”
Voici que le feu est descendu du ciel et a consumé les deux premiers chefs de cinquante et leur cinquante hommes; mais maintenant que ma vie soit précieuse à tes yeux! »
15 Malaika wa Bwana akamwambia Eliya, “Shuka pamoja naye, usimwogope.” Hivyo Eliya akainuka na kushuka pamoja naye kwa mfalme.
L'ange de Yahweh dit à Elie: « Descends avec lui, et ne crains pas devant lui. » Elie se leva et descendit avec lui vers le roi.
16 Akamwambia mfalme, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli wa kumuuliza habari, ndiyo maana ukatuma wajumbe kuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa sababu umefanya hili, kamwe hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”
Il lui dit: « Ainsi dit Yahweh: Parce que tu as envoyé des messagers consulter Béel-Zébub, dieu d'Accaron, — n'y a-t-il pas de Dieu en Israël dont on puisse consulter la parole? — à cause de cela, du lit sur lequel tu es monté tu ne descendras pas, mais tu mourras certainement. »
17 Hivyo akafa, sawasawa na lile neno la Bwana ambalo Eliya alikuwa amesema. Kwa kuwa Ahazia hakuwa na mwana, Yoramu akawa mfalme baada yake katika mwaka wa pili wa Yehoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda.
Ochozias mourut, selon la parole de Yahweh qu'Elie avait dite; et Joram devint roi à sa place, la seconde année de Joram, fils de Josaphat, roi de Juda; car il n'avait pas de fils.
18 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahazia na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Le reste des actes d'Ochozias, ce qu'il a fait, cela n'est-il pas écrit dans le livre des Chroniques des rois d'Israël?

< 2 Wafalme 1 >