< 2 Wafalme 1 >

1 Baada ya kifo cha Mfalme Ahabu, nchi ya Moabu iliasi dhidi ya Israeli.
And Moab transgresseth against Israel after the death of Ahab,
2 Basi Ahazia alikuwa ameanguka huko Samaria kutoka baraza ya chumba chake cha juu, akaumia. Hivyo akatuma wajumbe, akiwaambia, “Nendeni mkaulize kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni, mkaone kama nitapona kutokana na kuumia huku.”
and Ahaziah falleth through the lattice in his upper chamber that [is] in Samaria, and is sick, and sendeth messengers, and saith unto them, 'Go ye, inquire of Baal-Zebub god of Ekron if I recover from this sickness.'
3 Lakini malaika wa Bwana akamwambia Eliya, Mtishbi, “Panda ukakutane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, uwaulize, ‘Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana mnakwenda kumuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni?’
And a messenger of Jehovah hath spoken unto Elijah the Tishbite, 'Rise, go up to meet the messengers of the king of Samaria, and speak unto them, Is it because there is not a God in Israel — ye are going to inquire of Baal Zebub god of Ekron?
4 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana, ‘Hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!’” Hivyo Eliya akaenda.
and therefore, thus said Jehovah, The bed whither thou hast gone up, thou dost not come down from it, for thou dost certainly die;' and Elijah goeth on.
5 Wajumbe waliporudi kwa mfalme, akawauliza, “Kwa nini mmerudi?”
And the messengers turn back unto him, and he saith unto them, 'What [is] this — ye have turned back!'
6 Wakamjibu, “Mtu fulani alikuja kukutana nasi, naye akatuambia, ‘Rudini kwa mfalme aliyewatuma na mkamwambie, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana unawatuma watu kwenda kuuliza kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa hiyo hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”’”
And they say unto him, 'A man hath come up to meet us, and saith unto us, Go, turn back unto the king who sent you, and ye have said unto him, Thus said Jehovah, Is it because there is not a God in Israel — thou art sending to inquire of Baal-Zebub god of Ekron? therefore, the bed whither thou hast gone up, thou dost not come down from it, for thou dost certainly die.'
7 Mfalme akawauliza, “Alikuwa mtu wa namna gani ambaye mlikutana naye, akawaambia hili?”
And he saith unto them, 'What [is] the fashion of the man who hath come up to meet you, and speaketh unto you these words?'
8 Wakamjibu, “Alikuwa mtu aliyekuwa na vazi la manyoya na mkanda wa ngozi kiunoni mwake.” Mfalme akasema, “Huyo alikuwa ni Eliya, Mtishbi.”
And they say unto him, 'A man — hairy, and a girdle of skin girt about his loins;' and he saith, 'He [is] Elijah the Tishbite.'
9 Ndipo mfalme akamtuma mkuu mmoja wa kikosi pamoja na kikosi chake cha askari hamsini kwa nabii Eliya. Yule mkuu wa kikosi akamwendea Eliya, aliyekuwa ameketi juu ya kilima, na kumwambia, “Mtu wa Mungu, mfalme anasema, ‘Shuka chini!’”
And he sendeth unto him a head of fifty and his fifty, and he goeth up unto him (and lo, he is sitting on the top of the hill), and he speaketh unto him, 'O man of God, the king hath spoken, Come down.'
10 Eliya akamjibu yule mkuu wa kikosi, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza yule mkuu wa kikosi pamoja na watu wake.
And Elijah answereth and speaketh unto the head of the fifty, 'And if I [am] a man of God, fire doth come down from the heavens, and consume thee and thy fifty;' and fire cometh down from the heavens, and consumeth him and his fifty.
11 Aliposikia hili, mfalme akatuma kwa Eliya mkuu wa kikosi mwingine na askari wake hamsini. Yule mkuu wa kikosi akamwambia Eliya, “Mtu wa Mungu, hili ndilo asemalo mfalme, ‘Shuka chini mara moja!’”
And he turneth and sendeth unto him another head of fifty and his fifty, and he answereth and speaketh unto him, 'O man of God, thus said the king, Haste, come down.'
12 Eliya akajibu, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza yeye na watu wake hamsini.
And Elijah answereth and speaketh unto them, 'If I [am] a man of God, fire doth come down from the heavens, and consume thee and thy fifty;' and fire of God cometh down from the heavens, and consumeth him and his fifty.
13 Hivyo mfalme akatuma mkuu wa kikosi wa tatu na watu wake hamsini. Huyu mkuu wa kikosi wa tatu akapanda na kupiga magoti mbele ya Eliya, akiomba, “Mtu wa Mungu, tafadhali niachie uhai wangu na uhai wa hawa watu hamsini, watumishi wako!
And he turneth and sendeth a third head of fifty and his fifty, and the third head of fifty goeth up, and cometh in, and boweth on his knees over-against Elijah, and maketh supplication unto him, and speaketh unto him, 'O man of God, let be precious, I pray thee, my soul and the soul of thy servants — these fifty — in thine eyes.
14 Tazama, moto umeshuka kutoka mbinguni na kuwateketeza wale wakuu wa vikosi viwili vya kwanza pamoja na watu wao. Lakini sasa niachie uhai wangu!”
Lo, come down hath fire from the heavens, and consumeth the two heads of the former fifties and their fifties; and, now, let my soul be precious in thine eyes.'
15 Malaika wa Bwana akamwambia Eliya, “Shuka pamoja naye, usimwogope.” Hivyo Eliya akainuka na kushuka pamoja naye kwa mfalme.
And a messenger of Jehovah speaketh unto Elijah, 'Go down with him, be not afraid of him;' and he riseth and goeth down with him unto the king,
16 Akamwambia mfalme, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli wa kumuuliza habari, ndiyo maana ukatuma wajumbe kuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa sababu umefanya hili, kamwe hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”
and speaketh unto him, 'Thus said Jehovah, Because that thou hast sent messengers to inquire of Baal-Zebub god of Ekron — is it because there is not a God in Israel to inquire of His word? therefore, the bed whither thou hast gone up — thou dost not come down from it, for thou dost certainly die.'
17 Hivyo akafa, sawasawa na lile neno la Bwana ambalo Eliya alikuwa amesema. Kwa kuwa Ahazia hakuwa na mwana, Yoramu akawa mfalme baada yake katika mwaka wa pili wa Yehoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda.
And he dieth, according to the word of Jehovah that Elijah spake, and Jehoram reigneth in his stead, in the second year of Jehoram son of Jehoshaphat king of Judah, for he had no son.
18 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahazia na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
And the rest of the matters of Ahaziah that he did, are they not written on the book of the Chronicles of the kings of Israel?

< 2 Wafalme 1 >