< 2 Yohana 1 >
1 Mzee: Kwa bibi mteule na watoto wake, niwapendao katika kweli, wala si mimi tu, bali na wale wote waijuayo kweli:
The elder, to the elect lady and her children, whom I love in truth—and not I only, but also all who have known the Truth—
2 kwa sababu ya ile kweli ikaayo ndani yetu na ambayo itaendelea kukaa nasi milele: (aiōn )
because of the Truth, who abides in us and will be with us into the age: (aiōn )
3 Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo, Mwanawe Baba, itakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo.
Grace, mercy and peace from God the Father and from the Lord Jesus Christ, the Son of the Father, will be with you in truth and love.
4 Imenipa furaha kuu kuona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile Baba alivyotuagiza.
It has given me great joy to find some of your children walking in truth, just as we received commandment from the Father.
5 Sasa, bibi mpendwa, si kwamba ninakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo. Tupendane kila mmoja na mwenzake.
And now I put a request to you, lady (not as though writing a new commandment to you, but one that we have from the beginning): that we love one another.
6 Hili ndilo pendo, kwamba tuenende sawasawa na amri zake. Hii ndiyo amri yake kama vile mlivyosikia tangu mwanzo, kwamba mwenende katika upendo.
And this is the love, that we live according to His commandments—this is the commandment, just as you heard from the beginning, that you should live according to it.
7 Wadanganyifu wengi, wasiokubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili, wametokea ulimwenguni. Mtu wa namna hiyo ni mdanganyifu na mpinga Kristo.
Now many deceivers have come into the world, who do not acknowledge Jesus Christ as coming in flesh—this is the deceiver, even the Antichrist!
8 Jihadharini msije mkapoteza kile mlichokitenda, bali mpate kupewa thawabu kamilifu.
Look to yourselves, so that we not lose the things for which we worked but may receive a full reward.
9 Mtu yeyote asiyedumu katika mafundisho ya Kristo, bali akayaacha, yeye hana Mungu. Yeyote anayedumu katika mafundisho ana Baba na Mwana pia.
Anyone who turns aside and does not continue in the teaching of Christ does not have God; but whoever continues in Christ's teaching does have both the Father and the Son.
10 Msimpokee mtu yeyote anayewajia ambaye hawaletei mafundisho haya, wala msimkaribishe nyumbani mwenu.
If anyone comes to you and does not bring this teaching, do not receive him into your house; do not even tell him, “I wish you well,”
11 Yeyote amkaribishaye mtu wa namna hiyo anashiriki katika matendo maovu ya mtu huyo.
because whoever tells him, “I wish you well,” participates in his malignant works.
12 Ninayo mengi ya kuwaandikia, lakini sitaki kutumia karatasi na wino. Badala yake, nataraji kuja kwenu na kuongea nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.
Although I had many things to write to you, I did not wish to do so with paper and ink; instead I hope to come to you and speak face to face, so that our joy may be complete.
13 Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu. Amen.
The children of your elect sister greet you. Amen.