< 2 Yohana 1 >
1 Mzee: Kwa bibi mteule na watoto wake, niwapendao katika kweli, wala si mimi tu, bali na wale wote waijuayo kweli:
The Elder to the Elect Lady, and those born of her, whom I love in the truth: and not I alone, but also all those who have known the truth,
2 kwa sababu ya ile kweli ikaayo ndani yetu na ambayo itaendelea kukaa nasi milele: (aiōn )
because the truth which dwells in us shall be with us for eternity. (aiōn )
3 Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo, Mwanawe Baba, itakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo.
May grace, mercy, and peace be with you from God the Father, and from Christ Jesus, the Son of the Father, in truth and in love.
4 Imenipa furaha kuu kuona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile Baba alivyotuagiza.
I was very glad because I discovered some of your sons walking in the truth, just as we received the commandment from the Father.
5 Sasa, bibi mpendwa, si kwamba ninakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo. Tupendane kila mmoja na mwenzake.
And now I petition you, Lady, not as if writing a new commandment to you, but instead that commandment which we have had from the beginning: that we love one another.
6 Hili ndilo pendo, kwamba tuenende sawasawa na amri zake. Hii ndiyo amri yake kama vile mlivyosikia tangu mwanzo, kwamba mwenende katika upendo.
And this is love: that we walk according to his commandments. For this is the commandment that you have heard in the same way from the beginning, and in which you should walk.
7 Wadanganyifu wengi, wasiokubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili, wametokea ulimwenguni. Mtu wa namna hiyo ni mdanganyifu na mpinga Kristo.
For many deceivers have gone out into the world, those who do not confess that Jesus Christ has arrived in the flesh. Such a one as this is a deceiver and an antichrist.
8 Jihadharini msije mkapoteza kile mlichokitenda, bali mpate kupewa thawabu kamilifu.
Be cautious for yourselves, lest you lose what you have accomplished, and so that, instead, you may receive a full reward.
9 Mtu yeyote asiyedumu katika mafundisho ya Kristo, bali akayaacha, yeye hana Mungu. Yeyote anayedumu katika mafundisho ana Baba na Mwana pia.
Everyone who withdraws and does not remain in the doctrine of Christ, does not have God. Whoever remains in the doctrine, such a one as this has both the Father and the Son.
10 Msimpokee mtu yeyote anayewajia ambaye hawaletei mafundisho haya, wala msimkaribishe nyumbani mwenu.
If anyone comes to you, and does not bring this doctrine, do not be willing to receive him into the house, and do not speak a greeting to him.
11 Yeyote amkaribishaye mtu wa namna hiyo anashiriki katika matendo maovu ya mtu huyo.
For whoever speaks a greeting to him, is speaking with his evil works.
12 Ninayo mengi ya kuwaandikia, lakini sitaki kutumia karatasi na wino. Badala yake, nataraji kuja kwenu na kuongea nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.
I have much more to write to you, but I am not willing to do so through paper and ink. For I hope that I may be with you in the future, and that I may speak face to face, so that your joy may be full.
13 Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu. Amen.
The sons of your Elect Sister greet you.