< 2 Yohana 1 >
1 Mzee: Kwa bibi mteule na watoto wake, niwapendao katika kweli, wala si mimi tu, bali na wale wote waijuayo kweli:
The elder unto the excellent Lady, and her children, whom I love in truth: and not I only, but also all they that have known the truth;
2 kwa sababu ya ile kweli ikaayo ndani yetu na ambayo itaendelea kukaa nasi milele: (aiōn )
for the sake of the truth which dwelleth in us, and will be with us for ever: (aiōn )
3 Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo, Mwanawe Baba, itakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo.
grace, mercy, and peace be with you from God the Father, and from the Lord Jesus Christ, the Son of the Father, in truth and love.
4 Imenipa furaha kuu kuona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile Baba alivyotuagiza.
I rejoiced greatly that I found among thy children such as walked in truth, as we received commandment from the Father.
5 Sasa, bibi mpendwa, si kwamba ninakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo. Tupendane kila mmoja na mwenzake.
And now I beseech thee, Lady, not as writing to thee a new commandment, but that which we had from the beginning, that we may love one another.
6 Hili ndilo pendo, kwamba tuenende sawasawa na amri zake. Hii ndiyo amri yake kama vile mlivyosikia tangu mwanzo, kwamba mwenende katika upendo.
And this is love, that we walk according to his commandments. This is the commandment, as ye heard from the beginning, that ye should walk in it.
7 Wadanganyifu wengi, wasiokubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili, wametokea ulimwenguni. Mtu wa namna hiyo ni mdanganyifu na mpinga Kristo.
For many deceivers are come out into the world, who disown that Jesus Christ is come in the flesh. Such a one is a deceiver and an antichrist.
8 Jihadharini msije mkapoteza kile mlichokitenda, bali mpate kupewa thawabu kamilifu.
Look to yourselves, that ye lose not the things which ye have wrought, but that ye may receive a full reward.
9 Mtu yeyote asiyedumu katika mafundisho ya Kristo, bali akayaacha, yeye hana Mungu. Yeyote anayedumu katika mafundisho ana Baba na Mwana pia.
Whosoever transgresseth, and abideth not in the doctrine of Christ, hath not God: but he, that abideth in the doctrine of Christ, hath both the Father and the Son.
10 Msimpokee mtu yeyote anayewajia ambaye hawaletei mafundisho haya, wala msimkaribishe nyumbani mwenu.
Now if any one come unto you, and bringeth not this doctrine, receive him not into your house, nor wish him success: for he,
11 Yeyote amkaribishaye mtu wa namna hiyo anashiriki katika matendo maovu ya mtu huyo.
that biddeth him welcome, is partaker of his evil deeds.
12 Ninayo mengi ya kuwaandikia, lakini sitaki kutumia karatasi na wino. Badala yake, nataraji kuja kwenu na kuongea nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.
Having many things to write unto you, I would not with paper and ink: but I hope to come unto you, and speak mouth to mouth, that our joy may be full.
13 Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu. Amen.
The children of thy elect sister salute thee. Amen.