< 2 Yohana 1 >
1 Mzee: Kwa bibi mteule na watoto wake, niwapendao katika kweli, wala si mimi tu, bali na wale wote waijuayo kweli:
The Elder to the elect lady and her children. Truly I love you all, and not I alone, but also all who know the truth,
2 kwa sababu ya ile kweli ikaayo ndani yetu na ambayo itaendelea kukaa nasi milele: (aiōn )
for the sake of the truth which is continually in our hearts and will be with us for ever. (aiōn )
3 Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo, Mwanawe Baba, itakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo.
Grace, mercy and peace will be with us from God the Father, and from Jesus Christ the Son of the Father, in truth and love.
4 Imenipa furaha kuu kuona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile Baba alivyotuagiza.
It is an intense joy to me to have found some of your children living true Christian lives, in obedience to the command which we have received from the Father.
5 Sasa, bibi mpendwa, si kwamba ninakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo. Tupendane kila mmoja na mwenzake.
And now, dear lady, I pray you--writing to you, as I do, not a new command, but the one which we have had from the very beginning--let us love one another.
6 Hili ndilo pendo, kwamba tuenende sawasawa na amri zake. Hii ndiyo amri yake kama vile mlivyosikia tangu mwanzo, kwamba mwenende katika upendo.
The love of which I am speaking consists in our living in obedience to God's commands. God's command is that you should live in obedience to what you all heard from the very beginning.
7 Wadanganyifu wengi, wasiokubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili, wametokea ulimwenguni. Mtu wa namna hiyo ni mdanganyifu na mpinga Kristo.
For many deceivers have gone out into the world--men who do not acknowledge Jesus as Christ who has come in human nature. Such a one is 'the deceiver' and 'the anti-Christ.'
8 Jihadharini msije mkapoteza kile mlichokitenda, bali mpate kupewa thawabu kamilifu.
Keep guard over yourselves, so that you may not lose the results of your good deeds, but may receive back a full reward.
9 Mtu yeyote asiyedumu katika mafundisho ya Kristo, bali akayaacha, yeye hana Mungu. Yeyote anayedumu katika mafundisho ana Baba na Mwana pia.
No one has God, who instead of remaining true to the teaching of Christ, presses on in advance: but he who remains true to that teaching has both the Father and the Son.
10 Msimpokee mtu yeyote anayewajia ambaye hawaletei mafundisho haya, wala msimkaribishe nyumbani mwenu.
If any one who comes to you does not bring this teaching, do not receive him under your roof nor bid him Farewell.
11 Yeyote amkaribishaye mtu wa namna hiyo anashiriki katika matendo maovu ya mtu huyo.
He who bids him Farewell is a sharer in his evil deeds.
12 Ninayo mengi ya kuwaandikia, lakini sitaki kutumia karatasi na wino. Badala yake, nataraji kuja kwenu na kuongea nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.
I have a great deal to say to you all, but will not write it with paper and ink. Yet I hope to come to see you and speak face to face, so that your happiness may be complete.
13 Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu. Amen.
The children of your elect sister send greetings to you.