< 2 Yohana 1 >
1 Mzee: Kwa bibi mteule na watoto wake, niwapendao katika kweli, wala si mimi tu, bali na wale wote waijuayo kweli:
To an eminent Christian Lady, and to her Children, from the Officer of the Church. I sincerely love you all, and not I only, but also all those who have learned to know the Truth.
2 kwa sababu ya ile kweli ikaayo ndani yetu na ambayo itaendelea kukaa nasi milele: (aiōn )
We love you for the sake of that Truth which is always in our hearts; yes, and it will be ours for ever. (aiōn )
3 Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo, Mwanawe Baba, itakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo.
Blessing, mercy, and peace will be ours — the gift of God, the Father, and of Jesus Christ, the Father’s Son — in a life of truth and love.
4 Imenipa furaha kuu kuona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile Baba alivyotuagiza.
It was a great joy to me to find the lives of some of your children guided by the Truth, in obedience to the command that we received from the Father.
5 Sasa, bibi mpendwa, si kwamba ninakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo. Tupendane kila mmoja na mwenzake.
And now, I pray you, Lady — not as though I were writing a new command for you; no, it is the command which we had from the first — Let us love one another.
6 Hili ndilo pendo, kwamba tuenende sawasawa na amri zake. Hii ndiyo amri yake kama vile mlivyosikia tangu mwanzo, kwamba mwenende katika upendo.
And this is love — to live in obedience to the Father’s commands. This is the Command as you learned from the first, to live in a spirit of love.
7 Wadanganyifu wengi, wasiokubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili, wametokea ulimwenguni. Mtu wa namna hiyo ni mdanganyifu na mpinga Kristo.
I say this because many impostors have left us to go into the world — men who do not acknowledge Jesus as Christ come in our human nature. It is that which marks a man as an impostor and an anti-Christ.
8 Jihadharini msije mkapoteza kile mlichokitenda, bali mpate kupewa thawabu kamilifu.
Take care that you do not lose the fruit of all our work; rather, reap the benefit of it in full.
9 Mtu yeyote asiyedumu katika mafundisho ya Kristo, bali akayaacha, yeye hana Mungu. Yeyote anayedumu katika mafundisho ana Baba na Mwana pia.
Every one who goes beyond the limits of the Teaching of the Christ has failed to find God; the man who keeps to that Teaching — he has found both the Father and the Son.
10 Msimpokee mtu yeyote anayewajia ambaye hawaletei mafundisho haya, wala msimkaribishe nyumbani mwenu.
If any one comes to you and does not bring this Teaching, do not receive him into your house or welcome him;
11 Yeyote amkaribishaye mtu wa namna hiyo anashiriki katika matendo maovu ya mtu huyo.
for the man who welcomes him is sharing with him in his wicked work.
12 Ninayo mengi ya kuwaandikia, lakini sitaki kutumia karatasi na wino. Badala yake, nataraji kuja kwenu na kuongea nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.
Though I have a great deal to say to you, I would rather not trust it to paper and ink, but I am hoping to come and see you, and to speak with you face to face, so that your joy may be complete.
13 Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu. Amen.
The children of your eminent sister send you their greetings.