< 2 Yohana 1 >
1 Mzee: Kwa bibi mteule na watoto wake, niwapendao katika kweli, wala si mimi tu, bali na wale wote waijuayo kweli:
The elder to the chosen lady, and to her children, whom I love in truth, and not only I, but also all those having known the truth,
2 kwa sababu ya ile kweli ikaayo ndani yetu na ambayo itaendelea kukaa nasi milele: (aiōn )
because of the truth that is remaining in us, and will be with us throughout the age, (aiōn )
3 Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo, Mwanawe Baba, itakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo.
there will be with you grace, mercy, [and] peace from God the Father, and from the Lord Jesus Christ, the Son of the Father, in truth and love.
4 Imenipa furaha kuu kuona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile Baba alivyotuagiza.
I rejoiced exceedingly that I have found of your children walking in truth, even as we received a command from the Father;
5 Sasa, bibi mpendwa, si kwamba ninakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo. Tupendane kila mmoja na mwenzake.
and now I implore you, lady, not as writing to you a new command, but which we had from the beginning, that we may love one another,
6 Hili ndilo pendo, kwamba tuenende sawasawa na amri zake. Hii ndiyo amri yake kama vile mlivyosikia tangu mwanzo, kwamba mwenende katika upendo.
and this is love, that we may walk according to His commands; this is the command, even as you heard from the beginning, that you may walk in it,
7 Wadanganyifu wengi, wasiokubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili, wametokea ulimwenguni. Mtu wa namna hiyo ni mdanganyifu na mpinga Kristo.
because many deceivers entered into the world, who are not confessing Jesus Christ coming in flesh; this one is he who is leading astray, and the antichrist.
8 Jihadharini msije mkapoteza kile mlichokitenda, bali mpate kupewa thawabu kamilifu.
See to yourselves that you may not lose the things that we worked for, but may receive a full reward;
9 Mtu yeyote asiyedumu katika mafundisho ya Kristo, bali akayaacha, yeye hana Mungu. Yeyote anayedumu katika mafundisho ana Baba na Mwana pia.
everyone who is transgressing, and is not remaining in the teaching of the Christ, does not have God; he who is remaining in the teaching of the Christ, this one has both the Father and the Son;
10 Msimpokee mtu yeyote anayewajia ambaye hawaletei mafundisho haya, wala msimkaribishe nyumbani mwenu.
if anyone comes to you, and does not bear this teaching, do not receive him into the house, and do not say to him, “Greetings!”
11 Yeyote amkaribishaye mtu wa namna hiyo anashiriki katika matendo maovu ya mtu huyo.
For he who is saying to him, “Greetings,” has fellowship with his evil works.
12 Ninayo mengi ya kuwaandikia, lakini sitaki kutumia karatasi na wino. Badala yake, nataraji kuja kwenu na kuongea nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.
Having many things to write to you, I did not intend [it] with paper and ink, but I hope to come to you, and speak mouth to mouth, that our joy may be full.
13 Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu. Amen.
The children of your chosen sister greet you. Amen.